Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 11/1 kur. 20-21
  • Kumaliza Magumu kwa Upendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kumaliza Magumu kwa Upendo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Barnaba Yule “Mwana wa Faraja”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • “Kuyaimarisha Makutaniko”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • Marko Hakukata Tamaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • “Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 11/1 kur. 20-21

Neno la Mungu Li Hai

Kumaliza Magumu kwa Upendo

YOHANA MARKO anaenda zake nyumbani Yerusalemu, ambako Mariamu mama yake anaishi. Huu ni wakati wa safari ya kwanza ya umisionari ya Paulo na Barnaba.​—Matendo 13:13; 12:12, 25.

Sasa mwaka ule mwingine umefika. Paulo na Barnaba wanajitayarisha kufunga safari ya pili ya umisionari. Barnaba anataka waende tena na Marko binamu yake. Walakini, Paulo hataki Marko aende nao. Yeye anasema hivi: ‘Marko alienda zake akatuacha wakati ule mwingine tulipoambatana naye.’ Hata hivyo Barnaba anasisitiza kwamba Marko apewe nafasi nyingine.

Kwa sababu ya tofauti hiyo ya maoni “kukatokea mfoko mkali wa hasira, hivi kwamba wakatengana.” Barnaba alienda pamoja na Marko. Wakapanda merikebu na kusafiri mpaka kisiwa cha Kipro wahubiri huko. Kwa upande mwingine, Paulo alichagua Mkristo mwingine, Sila, halafu wakaanza safari ya kuhubiri ambayo kwanza iliwaingiza Shamu.​—Matendo 15:36-41, NW.

Namna gani juu ya tatizo hili lililo kati ya Paulo na Barnaba? Kama wewe ungalikuwa huko na kuuona huo “mfoko mkali wa hasira,” je! ungalikata maneno kwa kusema kwamba Paulo na Barnaba hawakuwa sehemu ya watu wa Mungu kwa sababu ya tabia zao wakati huo?

Kwa kweli, kukata maneno hivyo kusingalikuwa jambo la hekima. Inatupasa tutambue kwamba sisi sote tuna hali ya kutokamilika tuliyorithi kutoka kwa wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa. (Warumi 5:12) Kwa hiyo “twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi,” Biblia inasema. (Yakobo 3:2; Warumi 3:23) Hata hivyo Wakristo wa kweli hawaendelei kukaa katika hali ya kukasirikiana wala kufungia kinyongo moyoni. Wao wanatii amri hii ya Biblia: “Mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake . . . Jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.”​—Wakolosai 3:13, 14.

Basi, je! wale Wakristo wawili mashuhuri, Paulo na Barnaba, walimaliza magumu yao kwa upendo? Ebu watazame hapa. Wanashirikiana pamoja tena! (1 Wakorintho 9:5, 6) Na baadaye Paulo alimwandikia Timotheo hivi: “Umtwae Marko, umlete pamoja nawe, maana anifaa kwa utumishi.”​—2 Timotheo 4:11.

Ndiyo, ingawa nyakati nyingine Wakristo wa kwanza walikuwa na magumu kati yao, wao waliyamaliza kwa upendo. Kwa uhakika sisi tunaweza kuiga mfano wao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki