Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w83 2/1 kur. 22-23
  • Maswali kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
  • Habari Zinazolingana
  • Heshimu “Kile Ambacho Mungu Ameunganisha”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Maoni Yako Juu ya Ngono—Yanafanyiza Tofauti Gani?
    Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
  • Ikiwa Ndoa Imo Katika Hatua ya Kuvunjika
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kwa Nini Ndoa Inapaswa Kuonwa Kuwa Takatifu?
    Amkeni!—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1983
w83 2/1 kur. 22-23

Maswali kutoka kwa Wasomaji

◼ Ikiwa mke Mkristo mwaminifu ametalikwa na mumewe, ijapokuwa hakuna mmoja wao aliye na hatia ya uzinzi, je! ingefaa kulingana na Maandiko mke ashiriki kitanda cha ndoa pamoja na mume wakati mume anapotembelea jamaa yake?

Neno la Mungu linaonyesha waziwazi kwamba ngono inafaa kati ya mume na mke, si kati ya watu wasiooana. Kwa hiyo, watu waliotalikana hawapaswi kufanya ngono na mtu mwingine, kwa maana hiyo ingekuwa uasherati, lakini usiwape uhuru wa kuoa au kuolewa upya.

Kwa wazi, Wakristo wanahangaikia kwanza maoni na miongozo ya Mungu. Neno lake linashauri waziwazi hivi: “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi, kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.’’ (Waebrania 13:4) Na tuchunguze tuone hilo lina uhusiano gani na hali inayotokezwa na ulizo la juu.

Katika sehemu nyingi za dunia ni kawaida ya mwanamume na mwanamke kufanya ngono pasipo kuoana. Wengine wanadai kwamba jambo hilo linafaa kiadili na pia linakubalika kwa Mungu mradi wawili ‘wanapendana’ au wamefungiana wajibu. Walakini, hayo siyo maoni ya Kikristo. Wakifahamu kwamba “waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu,” Wakristo wanataka kuepuka uzinzi na vilevile uasherati.

Mwanamume na mwanamke wanapooana wanathibitisha mbele ya wote kwamba wameungana wawe mume na mke. Mbele ya sheria, jamii na Mungu, wana haki ya kushiriki mapendeleo ya ndoa, kutia na ngono. Kwa kweli, Maandiko yanasihi wenzi wasinyimane haki ya ngono: “Imempasa mume atosheleze mke wake mahitaji ya ngono. Kwa njia iyo hiyo, mke naye amepaswa atosheleze mahitaji ya ngono ya mumewe.”​—1 Wakorintho 7:3, Simple English Bible.

Namna gani ikiwa waliooana wanatengana tu, jambo ambalo linawezekana kisheria katika nchi fulani? Kwa kuwa wangali ni mume na mke kisheria na Kimaandiko, haiwapasi kushiriki ngono na mtu mwingineyo yote, kwa maana kufanya hivyo kungekuwa uzinzi ambao ungekuwa ni ‘kuchafua malazi yao ya ndoa.’ Lakini watu waliotengana wana uhuru wa kupatana tena na kuishi pamoja wakiwa mume na mke kama walivyo, wakiisha kufuta kisheria kutengana kwao.​—1 Wakorintho 7:10, 11.

Halafu ifikirie ile hali ambayo mwenzi mmoja, kwa mfano mume, anapoyapeleka mambo mbele zaidi kuliko kutengana naye na anataka talaka. Mke Mkristo mwaminifu ambaye baadaye anapata habari ya kwamba (kabla au baada ya kumtaliki) mumewe alikuwa mzinzi angeweza kuolewa upya, akiifikiria ndoa yake ya zamani kuwa ilikoma kisheria na vilevile machoni pa Yehova Mungu. Kwa upande mwingine, ikiwa kulikuwako talaka ya kisheria lakini pasipo uzinzi, talaka hiyo peke yake haingekomesha ndoa kwa maoni ya Mungu, kwa maana Biblia inaonyesha kwamba uzinzi wa mwenzi mmoja ndio msingi halali peke yake wa talaka.​—Mathayo 19:6, 9.

Hivyo ndivyo ilivyo na kisa hicho cha ulizo la juu, kwa maana imeelezwa waziwazi kwamba uzinzi haukufanyika. Mume alimwacha mke wake akapata talaka isiyo ya Kimaandiko. Kwa sababu ya talaka hiyo hawawi mume na mke tena katika maana kamili. Kwa kuwa mume alikomesha ndoa hiyo kisheria. Basi namna gani ikiwa mume huyo angetembelea jamaa yake naye angetaka kutosheleza mahitaji yake ya ngono? Kulingana na sheria na maoni ya jamii ya wafu, kufanya kwao ngono kungekuwa kama vile watu wawili wasiooana wangefanya ngono. Huo ungekuwa uasherati.

Katika hali hiyo hakuna mtu wa tatu anayehusika, kama ambavyo ingehitajiwa ili kutoa uthibitisho wa Kimaandiko wa talaka ya kisheria; hivyo machoni pa Mungu wala mwanamume wala mwanamke hangekuwa na uhuru wa kuoa au kuolewa na watu wengine. (1 Wakorintho 6:16-18) Hata hivyo kufanya kwao ngono pamoja bila shaka kungekuwa ni kutokujali shauri la Mungu; kwa kiasi ambacho wangekuwa wakichafua malazi ya ndoa kwa kuwa ndoa yao ilikoma kwa talaka hiyo. Mwenendo huo ungeleta lawama juu yao na juu ya kundi la Kikristo ambalo mke huyo angekuwa sehemu yake. Basi, ili mke aendelee katika kundi, ingempasa aepuke kufanya ngono isipokuwa ndoa ingehalalishwa upya. Imempasa mke ashikamane na msimamo mnyofu wa Kimaandiko na kiadili wa kwamba ngono zimepaswa zifanywe pamoja na wenzi waliooana kihalali tu. Kwa njia hiyo wangeongeza heshima ile ambayo Biblia inaonyesha ndoa inastahili kuwa nayo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki