Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 6/1 kur. 4-7
  • Har–Magedoni—Si Mambo Haya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Har–Magedoni—Si Mambo Haya
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Si Mahali Fulani pa Nchi
  • Si Vita Kati ya Mataifa ya Kidunia
  • Si Maangamizi Makubwa ya Nyukilia
  • Si Pigano Lenye Kuendelea Kati ya Wema na Uovu
  • Si Anguko Kubwa la Uchumi wa Ulimwengu
  • Si Vita Katika Mashariki ya Kati
  • Msingi wa Tumaini
  • Har-magedoni Lini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Har-magedoni—Mwanzo Wenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Vita vya Har-Magedoni Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Har-Magedoni Itaanzia Nchini Israel?​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 6/1 kur. 4-7

Har–Magedoni​—Si Mambo Haya

Unakoenda ni mwendo mfupi kwa motakaa kutoka Haifa. Chini ya mng’ao mkali wa jua la upande wa Mashariki ya Kati, motakaa yako inakimbia kushotoni mwa upande wa kusini wa Mto Kishoni wenye kupinda-pinda mpaka bonde linakuwa jembamba. Unapita mwanya huo mwembamba kati ya vilima vyenye kuinuka juu vya Karmeli na vilima vya Galilaya, mpaka bonde linapotandaa mbele yako kama sahani pana, tambarare​—Uwanda wa Esdraeloni. Unaendesha motakaa upande wa kusini wa uwanda huo macho yako yanapoona kilima kimoja chenye kilele tambarare isivyo kawaida. Hapo ndipo mahali unapotaka! Mwinuko wa Megido, ambao ni chanzo cha neno Har–Magedoni.

HAR-MAGEDONI ni neno lililofumbika na lililomo katika mawazo yaliyofahamika vibaya. Kuna mawazo mengi juu ya ni nini maana yake. Neno Har–Magedoni, hata hivyo, linatokana na Mlima Megido.a Ni neno la Biblia linalopatikana katika Ufunuo 16:16, ambapo panasema: “Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har–Magedoni.”

Ni nani wanaokusanywa kwenye Har–Magedoni na kwa nini wanakusanywa hapo? Andiko la Ufunuo 16:14 linajibu hivi: “Wafalme wa ulimwengu wote” wanakusanywa “kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.”

Majibu hayo yanatokeza maulizo mengi. “Wafalme” hao wanapigana na nani, na sababu ya kupigana ni nini? Watapigania wapi? Je! watatumia silaha za nyukilia? Je! vita hiyo inaweza kuzuiwa? Kwa halisi, Har–Magedoni ni nini?

Si Mahali Fulani pa Nchi

Har–Magedoni haiwezi ikawa mahali fulani pa nchi. Kwa kweli hakuna mlima wenye jina hilo​—ingawa mpaka leo hii kuna mwinuko unaoitwa Megido. Maana halisi ya Har–Magedoni inarudi nyuma katika historia kwenye vita vilivyopiganwa kwenye eneo hilo la Megido.

Megido ni mahali ambapo pamepiganiwa mapigano yaliyo makali zaidi na yenye kukata maneno kabisa katika historia ya Mashariki ya Kati. Mambo yalianza wakati wa mileani ya pili K.W.K. kwa ushindi mkubwa wa mtawala Mmisri Thutmose wa Tatu juu ya watawala wa Palestina na Siria, na mambo yaliendelea katika karne nyingi mpaka mwaka wa 1918 wakati jemadari mkuu Viskaunti Allenby aliposhinda vibaya sana Waturuki.

Lakini la maana zaidi kwa wanafunzi wa Biblia, katika Megido kulitokea ushindi mkubwa ajabu wa majeshi ya Israeli yakiwa chini ya amri ya Mwamuzi Baraka dhidi ya jeshi la Wakanaani lenye nguvu la Mfalme Yabini likiongozwa na mkuu wa vita Sisera. Yehova Mungu alijiingiza akawapa Waisraeli ushindi mkubwa sana.​—Waamuzi 4:7, 12-16, 23; 5:19-21.

Kwa hiyo, Har–Magedoni inaanza kuchukua maana ya pigano lenye kukata maneno, kukiwa mshindi mmoja tu asiyetiliwa shaka.

Si Vita Kati ya Mataifa ya Kidunia

Sababu ya pigano la Har–Magedoni​—utawala wa ulimwengu​—ndiyo sababu kubwa leo. Lakini, ingawa mataifa mawili yenye nguvu nyingi yanashindania sasa utawala wa ulimwengu, Har–Magedoni haitakuwa vita ya ulimwengu, yenye kupiganwa na moja la mataifa hayo dhidi la lile jingine. Ni kweli kwamba ulimwengu umo katika mashindano ya kuunda silaha zenye kugharimu zaidi na ya kiwazimu zaidi katika historia yote. Hayo yalisababisha elezo hili litolewe katika India Today: “Yote hayo ni kuisukuma sayari hii kwa kuogopesha kwenye ncha ya Har–Magedoni​—vita ya mwisho kati ya mataifa.” Lakini andiko la Ufunuo 16:14 linaonyesha kwamba “wafalme wa ulimwengu wote” wanaunganisha majeshi yao kwenye “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.”

Kwa hiyo, Har–Magedoni si vita ya wanadamu. Ni vita ya Mungu. Har–Magedoni itayakuta mataifa yote ya kidunia yakiwa yameungana kupigana na ‘majeshi ya kimbingu’ chini ya amri ya kijeshi ya ‘Mfalme wa wafalme na Bwana na mabwana,’ Kristo Yesu. Yeye ndiye mtawala wa ulimwengu mwenye haki kwa sababu Mungu pia ‘alitia vitu vyote chini ya miguu yake [Kristo].’​—Ufunuo 19:14, 16; Waefeso 1:22.

Si Maangamizi Makubwa ya Nyukilia

Kwa watu wengi, vita ya nyukilia ni yenye kuogopesha sana hata hawataki kuifikiria. Uchunguzi wa pamoja wa 1983 uliofanywa na wanasayansi 40 unakadiri kwamba katika vita kamili ya nyukilia theluthi moja kufikia nusu moja ya jumla yote ya watu ulimwenguni wangepatwa na kifo cha mara moja. Ripoti yao, iliyochapishwa katika gazeti Science, inatabiri wakati ujao wenye kuogopesha sana kwa waokokaji. Inaonya hivi: “Katika pigano lo lote kubwa kati ya mataifa yenye nguvu zaidi, inaelekea kutokea mabadiliko ya mazingira ya dunia yote yanayotosha kusababisha kumalizwa kwa sehemu kubwa ya mimea na jamii za wanyama Duniani. Ikiwa hivyo, uwezekano wa kumalizwa kwa wanadamu, upo.”

Je! Mungu Yehova Mweza Yote angeruhusu ogopesho hilo kubwa? Hata! Hakuiumba dunia ‘bila sababu tu,’ bali kama anavyotuhakikishia, ‘aliifanya ili ikaliwe na watu.’ (Isaya 45:18, NW) Kwenye Har–Magedoni Mungu ‘atawaharibu hao wanaoiharibu dunia,’ wala si kuiteketeza katika maangamizi makubwa ya nyukilia.​—Ufunuo 11:18.

Si Pigano Lenye Kuendelea Kati ya Wema na Uovu

Viongozi wa kidini fulani wanasadiki Har–Magedoni ni shindano lenye kuendelea kati ya majeshi ya wema na uovu, yawe ni ya ulimwenguni pote au iwe ni akilini. “Har–Magedoni inatokea katika sehemu fulani ya ulimwengu kila siku,” ndivyo kinavyosema kitabu kimoja chenye kutoa maelezo ya Biblia. Hilo lingeweza kuwaje hivyo wakati Biblia inapoahidi kwamba Har–Magedoni italeta uharibifu wa haraka kwa mataifa na watu wote waovu? Kristo, akiwa Mfalme mpakwa mafuta wa Mungu kwenye Har–Magedoni, ‘atawaponda kwa fimbo ya chuma, na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.’​—Zaburi 2:9; ona pia Mithali 2:21, 22; Ufunuo 19:11-21.

Si Anguko Kubwa la Uchumi wa Ulimwengu

Serikali zenye nguvu zaidi za ulimwengu zinaogopa kwamba kushindwa kwa Nchi Zinazositawi kulipa madeni kungeiendesha hali ya kiuchumi ya dunia kwenye ambacho gazeti Business Life linaita “Har–Magedoni ya Kiuchumi.” Kuanguka kwa mashirika ya benki za ulimwengu hakika kungekuwa ni msiba mkubwa, lakini hakungekuwa ndiyo Har–Magedoni. Har–Magedoni ya Biblia ni hali ya ulimwenguni pote inayohusu vita, wala si uchumi. Nabii Yeremia anaieleza kwa maneno haya yaliyo wazi sana: “[Yehova] ana mashindano na mataifa, atateta na watu wote wenye mwili; na waovu atawatoa wauawe kwa upanga; asema [Yehova].”​—Yeremia 25:31.

Si Vita Katika Mashariki ya Kati

“Wakati fulani, mteketeo mkubwa utatokea katika Mashariki ya Kati,” ndivyo anavyohubiri mwevanjeli mwenye kujulikana ulimwenguni pote Billy Graham. Kuhusu jambo hilo, yeye anawakilisha maoni ya wenzi wake wengi wa kidini. Pia Graham anasadiki kwamba Har–Magedoni inaweza kukawizwa. “Nafikiri kwamba ulimwengu unaelekea sasa kwenye Har–Magedoni,” ndivyo anavyosema, “na kwamba kusipokuwapo kuamka kwa kiroho na tumrudie Mungu, huenda ulimwengu ukakabili Har–Magedoni katika kumi hili la miaka.”

Eneo la Megido halingeweza kutoa nafasi ya kuwatosha “wafalme wa nchi, na majeshi yao” yote. (Ufunuo 19:19) Kwa hiyo, je! hilo halikanushi fundisho lo lote la kihalisi kwamba Har–Magedoni itakuwa vita ya ulimwengu itakayopiganiwa kwenye uwanda halisi wa Megido? Nabii Yeremia anadokeza kwamba Har–Magedoni itaenea “toka upande mmoja wa dunia hata upande wa pili.”​—Yeremia 25:32, 33.

Na kwa kuwa maana ya Har–Magedoni ni “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi,” hakuna anayeweza kuikawiza. Yehova ‘ameweka wakati’ wa pigano hilo kuanza. “Haitachelewa.”​—Ufunuo 16:14; 11:18; Habakuki 2:3, NW.

Msingi wa Tumaini

Har–Magedoni si ya kuogopwa na watu wanaopenda uadilifu. Tofauti yake, inaweza kuwa msingi wa tumaini. Biblia inasema: “Nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-Kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.” (Ufunuo 19:11) Pigano la Har–Magedoni litaisafisha dunia uovu wote na kutengeneza njia ya kurudishwa kwa hali za uadilifu.​—Isaya 11:4, 5.

Kwa miaka zaidi ya 100, sauti ya Mashahidi wa Yehova imesikiwa ikitangaza ushindi wa wakati ujao wa Mungu dhidi ya watawala wafisadi, wasiokubali kushindwa wa mfumo huu. Hasa tangu mwaka wa 1925 Mashahidi wamekuwa na maoni yaliyo wazi juu ya ni nini Har–Magedoni na wanakataa kukaa kimya juu ya hilo. Tamaa yao ni kuwasaidia watu wawe waokokaji wa Har–Magedoni, wala si wenye kuuawa. Kwa hiyo wanasihi wote wanaosikiliza wafuate shauri la Yoeli 2:31, 32 linalosema juu ya kuja kwa “siku ya [Yehova] iliyo kuu na itishayo,” na kuongeza hivi: ‘Mtu awaye yote anayeliitia jina la Yehova ataponywa.’

Hata hivyo, huenda wengine bado wakauliza hivi: Ingawa Har–Magedoni ni ya duniani pote kwa ukubwa, je, itaanzia Mashariki ya Kati? Mungu wa upendo angeweza kuruhusuje Har–Magedoni? Je! amani ya kweli itafuata baada ya Har–Magedoni? Soma matoleo matatu yanayofuata ya Mnara wa Mlinzi, kwa maana yatajibu maulizo hayo.

[Maelezo ya Chini]

a Kittel, pia McClintock na Strong, wanachuo wa lugha ya Kibiblia, hawana uhakika juu ya maana ya neno “Megiddo,” lakini wanataja uhakika wa kwamba neno hilo lingeweza kumaanisha “kusanyiko” au “mahali pa askari.”

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

Har–Magedoni Ni Nini?

Har–Magedoni SI . . .

◆ a sehemu fulani ya nchi

◆ pigano kati ya mataifa

◆ maangamizi makubwa ya nyukilia

◆ anguko kubwa la uchumi wa dunia

◆ pambano kati ya wema na uovu

◆ pigano la Mashariki ya Kati

Har–Magedoni NI . . .

◆ hali ya ulimwenguni pote ambapo mataifa yote ya kidunia yatapigana na Mwana wa Mungu, Kristo Yesu, na jeshi lake la kimalaika katika “vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi”

[Picha katika ukurasa wa 4]

[Picha katika ukurasa wa 7]

Kwenye Har–Magedoni Mfalme wa Mungu, Yesu Kristo, ‘ataponda mataifa yote kwa fimbo ya chuma, na kuwavunja kama chombo cha mfinyanzi.’​—Zaburi 2:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki