Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w85 7/1 kur. 4-7
  • Sababu Inayofanya Iwe Lazima Har–Magedoni Ipiganwe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu Inayofanya Iwe Lazima Har–Magedoni Ipiganwe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Ni Wonyesho wa Upendo wa Mungu
  • Suala la Enzi Kuu
  • Kutosheleza Mahitaji ya Mwanadamu
  • Har-magedoni—Mwanzo Wenye Furaha
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Vita vya Har-Magedoni Ni Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Har-magedoni Lini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Baada ya Har-Magedoni, Dunia-Paradiso
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
w85 7/1 kur. 4-7

Sababu Inayofanya Iwe Lazima Har–Magedoni Ipiganwe

“MUNGU NI UPENDO.” Si kwamba tu Mungu anaonyesha upendo, asema mtume Yohana, bali yeye ni upendo​—ndiye upendo wenyewe.​—1 Yohana 4:8.

Lakini, Mungu uyu huyu wa upendo mara nyingi anaonyeshwa kuwa mungu mwenye tamaa ya kulipa kisasi anayeleta adhabu ya kikatili juu ya wale wasio na kibali yake. Kwa hiyo, wengi ama wamepoteza imani yao katika Mungu au wakaidhihaki Biblia, wakidai haingaliweza kuwa ilitokana na Mungu wa namna hiyo. Sana sana visehemu vya kitabu cha Ufunuo vinalaumiwa sana mahali ambako hukumu za Mungu juu ya waovu zinaelezwa, zikifikia upeo katika pigano la Har–Magedoni.

Kwa mfano, Joseph Wheless anaandika hivi katika kitabu chake Is It God’s Word?: “Hakika msomi mpole hangevumilia njozi ya ufunuo inayofunua nafsi iliyotubu yenye kutaka huruma kati ya wakosaji maskini (ama wa dhambi ya awali au yenye kuua), ambao humo ‘wanateswa kwa moto na kibiriti mbele za malaika watakatifu, na mbele za Mwana-kondoo,’ wote wakitazama kwa ubaridi huku ‘moshi wa mateso ukipaa juu milele na milele: na hawana siku ya kupumzika mchana wala usiku’ kutokana na ukali wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi (Ufu. xiv, 10, 11). Huo ndio ufunuo ulioongozwa na roho ya Mungu wa upendo.”

Pia akilaumu masimulizi ya Ufunuo, Profesa Gerald A. Larue wa Chuo Kikuu cha California ya Kusini aliandika majuzi hivi katika gazeti Free Inquiry: “Wasioamini wanavurumishwa kwenye shimo la mateso lisilofikirika. Adhabu hiyo si lex talionis, hukumu ya jicho kwa jicho; wala si kama ile hukumu ya jamaa kulipizana kisasi, ambayo kikundi chote kinaweza kufagiliwa mbali (linganisha Mwa. 4:23, [24]; Yosh. 6; n.k.). Hapa adhabu ni ya milele. Hakuna rehema, adhabu haina mwisho. Hakuna msamaha, ila adhabu tu isiyomruhusu mtu kuwa na amani ya kumalizwa kabisa. Huo si mfano wa Yesu mnyenyekevu na mpole.” Kisha, akitaja maneno ya Ufunuo 14:9-11, anaendelea kusema hivi: “Hakuna cha kugeuza shavu lile jingine hapa​—ila tu malipizo makali, ya ghadhabu kwa unyama unaofanya mateso ya Nazi yaonekane mapole kwa kulinganishwa.”

Ni jambo linaloeleweka kwamba mawazo ya mateso ya kikatili wakosaji wanapoteswa milele yanaweza kutia mashaka juu ya ‘Mungu wa upendo.’ Lakini mawazo hayo yanategemea kutokuelewa Biblia na mifano inayotumiwa humo. Hakuna mahali po pote ambapo Biblia inafundisha kwamba nafsi haiwezi kufa. Badala yake, Maandiko yanataja kwamba “mshahara wa dhambi ni mauti”​—wala si mateso ya milele​—na baada ya kufa hisia za mtu, kutia uwezo wa kuona maumivu, zinakwisha.​—Warumi 6:23; Mhubiri 9:5, 10.

Adhabu yenyewe, si kupewa adhabu yenyewe, ndiko kunakodumu milele​—kwa kuwa waovu wanaangamizwa kabisa katika “ziwa la moto,” ambalo ni mfano wa uharibifu kamili. (Ufunuo 20:14, 15; 21:8) Hata hivyo, pigano la Har–Magedoni litaleta mateso na magumu makubwa sana kwa wanadamu na litakuwa ndiyo vita yenye umwagaji mkubwa zaidi wa damu iliyopata kupiganwa. (Mathayo 24:21, 22; Ufunuo 14:20; 19:17, 18) Je! vita hiyo inatokana na ‘Mungu wa upendo?’ Je! kweli kweli Mungu ataleta vita hiyo?

Ni Wonyesho wa Upendo wa Mungu

Kwa kweli, ni kwa sababu ya upendo wa Mungu kwamba pigano la Har–Magedoni ni lazima lipiganwe. Kusudi la Yehova Mungu kwa dunia ni kuirudisha katika hali yake ya kwanza ya Paradiso na wanadamu waishi juu yake katika amani na ukamilifu ‘bila mtu wa kuwatia hofu.’ (Ezekieli 34:28; Mika 4:3, 4; Ufunuo 21:4) Basi, watafanywa nini wale ambao, kwa uhalifu na jeuri yao, wangependa kuharibu usalama wa Paradiso iliyorudishwa? Kungali hakuna mfumo wo wote uliobuniwa na mwanadamu ambao umeshughulikia tatizo hilo kwa kufanikiwa. Njia pekee ya kuhakikisha amani kamilifu ni kuondolea mbali hata tisho la uovu. Ndiyo, ni lazima Mungu aharibu waovu wasioweza kunyooshwa kwa faida ya wale wanaotaka kufanya yaliyo haki. Kwa ajili ya upendo, yeye anachukua hatua ya kuisafisha dunia kutokana na wale ambao wangependa kuiharibu.​—Ufunuo 11:18.

Lakini hakuna ye yote anayehitaji kufa. “[Mungu] hutaka watu wote waokolewe,” ndivyo anavyoandika mtume Paulo. (1 Timotheo 2:4) Na Petro, pia akiandika chini ya uongozi wa roho ya Mungu, alisema: “Hapendi mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba.” (2 Petro 3:9) Mungu amepanga ‘habari njema za ufalme’ zitangazwe ili kila mtu mmoja mmoja apate nafasi ya kujifanyia wokovu wake mwenyewe. (Mathayo 24:14; Wafilipi 2:12; Wagalatia 6:5) Unaweza kuishi milele katika ukamilifu juu ya dunia paradiso. Uchaguzi ni wako. (Warumi 2:5-9; Ezekieli 18:23, 32) Je! hivyo sivyo ungetazamia kutoka kwa Mungu wa upendo?

Suala la Enzi Kuu

Ili kuhakikisha amani kamilifu na utulivu, kutakuwako serikali moja tu ikitawala juu ya dunia yote​—Ufalme wa Mungu. Je! si serikali nyingi za kibinadamu, zote zikijitahidi zifikie faida zao za choyo za kitaifa, ambazo zimesababisha ugomvi mwingi na umwagaji mwingi wa damu duniani pote? Ni lazima serikali hizo ziondolewe ili.kupatia nafasi utawala wa uadilifu wa Ufalme wa Mungu chini ya Kristo. (Danieli 2:44) Umeomba kwa ajili ya serikali hiyo ya kimbingu uliporudia sala ya kielelezo ambayo Yesu aliwapa wanafunzi wake: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.”​—Mathayo 6:9, 10.

Lakini ni serikali gani ujuayo ambayo ina nia ya kuacha enzi kuu yake na kujitiisha kikamili chini ya Ufalme wa Mungu? Je! badala yake serikali hazikamatani kabisa na enzi zao zenyewe, daima zikitaka kupanua kadiri ya uvutano wazo kwa kukaidi Ufalme wa Mungu uliosimamishwa? (Zaburi 2:1-9) Je! kumepata kuwa kidokezo cho chote kwamba mataifa yataachia Mungu na Kristo tawala zayo? Kushindwa kwa tengenezo la Umoja wa Mataifa kuwa chombo cha amani ya ulimwengu kunaonyesha kwamba faida za kichoyo za kitaifa zinapohusika mataifa hayataki kuacha tawala zayo ili yajitiishe chini ya mamlaka moja. Mataifa yameazimia kuendesha mambo ya dunia kwa njia yao. (Ufunuo 17:13, 14; 19:19) Kwa hiyo ni lazima pigano la Har–Magedoni lipiganwe ili kuondoa hali hiyo ya kutojishusha na kusuluhisha milele suala la ni nani aliye na haki ya kutawala dunia.

Kutosheleza Mahitaji ya Mwanadamu

Matendo ya Yehova katika Har–Magedoni yatafanywa kwa kukumbuka faida bora zaidi za wanadamu. Fikiria. Wewe unahisije juu ya hali za ulimwengu za sasa? Je! unahisi ukiwa salama chini ya tisho la kuangamizwa kwa silaha za nyukilia? Je! wewe unatetemeka kwa kuona jeuri ikiongezeka, ujirani wako mwenyewe ukizidi kukosa usalama: Je! wewe unaogopea watoto wako na wakati ujao wao? Unaona faraja gani? Je! serikali yoyote imepata kuonyesha kwamba inaweza kuletea wanadamu wote amani na ufanisi? Je! kuna yoyote ambayo imeweza kuondoa magonjwa au kifo kutoka dunia? Badala yake, je, hali ulimwenguni pote hazikuwa mbaya zaidi yajapokuwa mambo ya ufundi wa mwanadamu, na mara nyingi yakifanywa mabaya zaidi kwa sababu ya maendeleo hayo? Ni Ufalme wa Mungu wenye uadilifu peke yake utakaotosheleza kabisa mahitaji ya wanadamu. Ni kupitia huo peke yake kwamba amani ya kweli itaenea duniani pote. Ni lazima pigano la Har–Magedoni lipiganwe!

Lakini namna gani juu ya kuteseka na magumu ya kibinadamu yatakayoletwa wakati Mungu achukuapo hatua ya kuisafisha dunia? Siku zote hayo yamekuwa ni mazao ya vita. Yatatokea katika Har–Magedoni kwa sababu tu mataifa yamejikaza kupinga utawala wa kitheokrasi. Wameazimia kupigana na kupinga. (Zaburi 2:2, 3) Hilo si shauri la Mungu. Yeye anawapa onyo linalofaa: “Na sasa, 0 wafalme, sikilizeni; mwonyeke, enyi watawala wa dunia. Mtumikieni Bwana kwa woga, na kufurahi mbele zake; kwa kutetemeka msujudieni, asije kukasirika na ninyi mpotee njiani, wakati hasira yake iwakapo ghafula. Wenye furaha ni wote wanaomfanya kimbilio!”​—Zaburi 2:10, 11, The New American Bible.

Sasa fikiria. Hali za ulimwengu zingekuwaje kama Mungu angeepuka kujiingiza anyooshe mambo ya ulimwengu? Je! vita, jeuri, na chuki hazingeendelea bila kupungua kama ambavyo imekuwa katika karne zote za utawala wa mwanadamu? Je! hata sasa mambo hayo hayaongezeki kufikia kadiri ambayo wanadamu wote wanatishwa na maogopesho makubwa ya vita ya nyukilia na miale yake yenye sumu? Kwa kweli Har–Magedoni ndilo jambo bora zaidi ambalo lingeweza kuipata dunia yetu! Itakomesha mwendo wa kujiua wa choyo wa mataifa. Itaondolea mbali mifumo inayoleta huzuni nyingi kwa wanadamu na kutengeneza njia uje mfumo mpya wa mambo ulio mwadilifu kweli kweli ambamo huzuni yote yenye kufanywa na wanadamu, maumivu, na kifo yataondolewa milele. Kisha ‘mambo ya kwanza yatakuwa yamepita,’ kulingana na ahadi ya Mungu.​—Ufunuo 21:4; 2 Petro 3:13.

Ni lazima tukumbuke kwamba Mungu katika hekima yake anajua ni nini yaliyo bora zaidi kwa wanadamu na ni mambo gani yanayohitajiwa ili kuyatimiza. Hata serikali za kibinadamu zimependekeza na kushiriki vita ili kurekebisha yanayoonekana kuwa maonezi au kupigania lililodhaniwa kuwa kusudi zuri sana. Lakini ni Mungu peke yake aliye na hekima ya kupigana vita yenye kuchagua kweli kweli ambayo katika hiyo watu mmoja mmoja wenye mioyo yenye haki, hata wawe wapi duniani, watahifadhiwa. (Mathayo 24:40, 41; Ufunuo 7:9, 10, 13-17) Na ni Mungu peke yake aliye na haki ya kuiweka kwa lazima enzi kuu yake duniani pote, kwa kuwa hiyo ni uumbaji wake. Ndiyo, ili kuondoa alama zote za uovu milele, kumaliza uonezi, ibada ya uwongo kuonea, hata kisababishi cha dhambi, na kutakasa kwa ukamili jina takatifu la yenye Mungu​—ni lazima Har–Magedoni ipiganwe. Nayo itapiganwa, kwa sababu “Mungu ni upendo!”

[Picha katika ukurasa wa 6, 7]

HAR-MAGEDONI . . . yatengeneza njia ije amani

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki