“Mambo Makuu ya Biblia” ya Kutoa Ufahamu Mkubwa Zaidi
WAKATI Wayahudi waliporudi kutoka uhamisho Babuloni katika karne ya sita K.W.K., watu wenye madaraka miongoni mwao “wakamkusanyikia Ezra, mwandishi, ili wapate kuyasikiliza maneno ya torati.” Matokeo ya ongezeko lao la ufahamu yalikuwa nini? Watu walifanya Sherehe ya Vibanda isiyo ya kawaida kukawa na “furaha kubwa sana”!—Nehemia 8:13-18.
Kama ambavyo mfano huo unavyoonyesha vizuri sana, kupata ufahamu wa Maandiko kwaweza kuwa na matokeo mazuri sana juu ya watu wa Mungu. Kwa sababu hiyo, katika matoleo ya Januari 15, Februari 15, na Machi 15, 1986, gazeti Mnara wa Mlinzi litakuwa na makala yenye kichwa “Mambo Makuu ya Biblia.” Makala hizo zitawawezesha wasomaji wetu wapate ufahamu wa kina kirefu zaidi wa vitabu vya Biblia vya Ezra, Nehemia, na Esta.
Masomo hayo yatatusaidia tuhuishe tena matukio yenye kusisimua yanayoshirikishwa na kurudishwa kwa ibada ya kweli katika Yerusalemu, ujenzi wa hekalu la Yehova huko, na kuhifadhiwa kwa watu wa Mungu wajapokabili shambulio la adui. Kweli kweli, kwa kusoma vitabu hivyo kama inavyopendekezwa katika “Mambo Makuu ya Biblia,” Mashahidi wa Yehova na wenzi wao wataweza kupata faida kubwa zaidi kwa kuzungumzwa kwa habari iyo hiyo ya Kimaandiko katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya kila juma. Kuongezea hilo, akina ndugu waliopewa mgawo wa kutoa “Mambo Makuu ya Usomaji wa Biblia” katika programu ya Shule wanaweza kutumia makala “Mambo Makuu ya Biblia” kwa faida nzuri sana katika kujibu maswali ya Kimaandiko na kuonyesha masomo tunayopata.—Warumi 15:4.
[Chati katika ukurasa wa 7]
Wafalme wa Ajemi Wanaotajwa Katika Ezra, Nehemia, na Esta
Utawala (K.W.K) Jina la Kilimwengu Jina la Biblia Mrejezo
wa Bibilia
kama 550-529 Koreshi Mkuu Koreshi Ezra 1:1; 4:5
529-522 Kambisesi II Ahasuero Ezra 4:6
522 (miezi 8) Gaumata (Smerdi) Artasakse Ezra 4:7-23
521-486 Dario I Dario Ezra 4:5, 24; 6:1-15
486-474 Sakse I Ahasuero Kitabu cha Esta