Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 1/15 kur. 15-20
  • “Ulimwengu Haukustahili Kuwa Nao”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Ulimwengu Haukustahili Kuwa Nao”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Imani ya Waamuzi, Wafalme, na Manabii
  • Wengine Wenye Imani Iliyo Mfano Mwema
  • Endelea Kumtazama Mkamilishaji wa Imani Yetu
  • Zoea Imani Yenye Msingi Wa Kweli
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Imani Yako Ni Yenye Nguvu Kadiri Gani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Je, Kweli Una Imani Katika Habari Njema?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • “Tupe Imani Zaidi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 1/15 kur. 15-20

“Ulimwengu Haukustahili Kuwa Nao”

Wao walipigwa kwa mawe, wao walijaribiwa . . . na ulimwengu haukustahili kuwa nao.”—WAEBRANIA 11:37,38, NW.

1, 2. Ni chini ya hali gani mashahidi wa Yehova wa nyakati za kale walidumisha ukamilifu, na ni jinsi gani vitendo vyao vinakuwa na matokeo juu ya watumishi wa Mungu leo?

MASHAHIDI WA YEHOVA wa nyakati za kale walidumisha ukamilifu kwa Mungu ijapokuwa majaribu mengi yaliletwa juu yao na jamii ya kibinadamu isiyo na uadilifu. Kwa mfano, watumishi wa Mungu walipigwa kwa mawe na kuchinjwa kwa upanga. Wao walitendwa vibaya na kupata dhiki. Hata hivyo hawakuyumba-yumba katika imani. Basi, ni “Ulimwengu haukustahili kuwa nao.”—Waebrania 11:37. 38. NW.

2 Vitendo vinavyotia imani nguvu vya watu wa kabla ya gharika wenye kujitoa kwa Mungu, wazee wa ukoo, na Musa vinawasukuma mashahidi wa Yehova wa kisasa watumikie Mungu kwa imani. Lakini namna gani wengine wanaotajwa katika Waebrania sura 11 na 12? Sisi tunaweza kufaidikaje kutokana na kufikiria nyuso za imani yao?

Imani ya Waamuzi, Wafalme, na Manabii

3. Vituko vilivyohusu Yeriko na Rahabu vinaonyeshaje kwamba ni lazima imani ithibitishwe kwa kazi?

3 Kwa kuwa imani si itikadi tupu tu, ni lazima ithibitishwe kwa kazi au vitendo. (Soma Waebrania 11:30, 31, NW.) Baada ya kifo cha Musa, imani iliwaletea Waisraeli ushindi mmoja baada ya mwingine katika Kanaani, lakini jambo hilo lilihitaji jitihada kwa upande wao. Kwa mfano kwa imani ya Yoshua na wengine “kuta za Yeriko zilianguka chini baada ya kuwa zimezungukwa kwa siku saba.” Lakini “kwa imani Rahabu yule kahaba hakuangamia pamoja na wale [wakaaji wa Yeriko wasio na imani] waliotenda bila kutii.” Kwa sababu gani? “Kwa sababu yeye aliwapokea wapelelezi [Waisraeli] kwa njia yenye kuamanika,” akithibitisha imani yake kwa kuwaficha wasionwe na Wakanaani. Imani ya Rahabu ilikuwa na msingi mgumu katika ripoti zilizosema kwamba “Yehova aliyakausha maji ya Bahari Nyekundu” yatoke mbele ya Waisraeli na akawapa ushindi juu ya wafalme Sihoni na Ogu wa Amori. Rahabu alifanya mabadiliko ya kiadili yanayofaa naye akabarikiwa kwa imani yake yenye matendo kwa kuhifadhiwa pamoja na watu wa nyumba yake wakati Yeriko ulipoanguka na kwa kuwa bibi wa ukoo wa Yesu Kristo.—Yoshua 2:1-11; 6:20-23; Mathayo 1:1, 5; Yakobo 2:24-26.

4. Mambo yaliyopata Gideoni na Baraki yanakazia nini juu ya kuonyesha imani katika kukabiliwa na hatari?

4 Imani inaonyeshwa na tegemeo kamili juu ya Yehova katika kukabili hatari. (Soma Waebrania 11:32, NW.) Paulo alikiri kwamba wakati ungemwishia kama angeendelea kueleza juu ya “Gideoni, Baraki, Samsoni, Yeftha, Daudi na pia Samweli na manabii wale wengine,” ambao matendo yao hodari yalitoa udhahiri mwingi wa imani na tegemeo juu ya Mungu katika hali yenye hatari. Hivyo, kwa imani na akiwa na kikundi cha wanaume 300 tu, Mwamuzi Gideoni alipewa nguvu na Mungu avunjilie mbali uwezo wa kijeshi wa Wamidiani waonevu. (Waamuzi 7:1-25) Kwa kutiwa moyo na Debora nabii wa kike, Mwamuzi Baraki na jeshi la askari-watembea-miguu 10,000 wasio na vifaa vya kutosha waliyashinda majeshi makubwa zaidi sana ya Mfalme Yabini yenye magari ya vita 900 yenye silaha, yaliyoamriwa na Sisera.—Waamuzi 4:1–5:31.

5. Ni kwa njia gani mbalimbali Samsoni na Yeftha walionyesha imani iliyotoa udhahiri wa kwamba walikuwa na tegemeo kamili juu ya Yehova?

5 Mfano mwingine wa imani kutokana na siku za waamuzi wa Israeli ni Samsoni, adui wa Wafilisti mwenye uwezo mwingi. Ni kweli kwamba hatimaye yeye alikuja kuwa mtekwa wao aliyepofushwa. Lakini Samsoni aliwaua wengi wao wakati alipozivuta na kuziangusha nguzo za nyumba ambamo wao walikuwa wakitoa dhabihu kubwa mbele ya Dagoni mungu wao wa uwongo. Ndiyo, Samsoni alikufa pamoja na Wafilisti hao lakini si kwa kujiua mwenyewe akiwa amekata tumaini. Kwa imani yeye alimtegemea Yehova na kumpelekea sala apate nguvu zilizohitajiwa ili apatilize kisasi juu ya adui hao wa Mungu na watu Wake. (Waamuzi 16:18-30) Yeftha, ambaye Yehova alimpa ushindi juu ya Waamoni, alionyesha pia imani iliyotoa udhahiri wa kwamba alikuwa na tegemeo kamili juu ya Yehova. Ni kwa kuwa na imani kama hiyo tu yeye angaliweza kutimiza nadhiri yake kwa Mungu kwa kutoa binti yake kwenye utumishi wa Yehova akiwa mwanamwali wa daima.—Waamuzi 11:29-40.

6. Daudi alionyeshaje imani yake?

6 Aliyestahili pia kuangaliwa kwa ajili ya imani yake alikuwa Daudi. Yeye alikuwa mwanamume kijana tu alipopigana na lile jitu Filisti Goliathi. ‘Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki,’ akasema Daudi, ‘bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Yehova wa majeshi.’ Ndiyo, Daudi alimtegemea Mungu, akamuua Mfilisti huyo aliyekuwa mnara wa mtu, naye akasonga mbele na kuwa mfalme aliye shujaa kivita mwenye kupigana kwa ajili watu wa Mungu. Na kwa sababu ya imani ya Daudi, yeye alikuwa mwanamume aliyekubalika kwenye moyo wa Mungu. (1 Samweli 17:4, 45-51; Matendo 13:22) Katika muda wote wa maisha, Samweli na manabii wengine walionyesha pia imani kubwa na tegemeo kamili juu ya Yehova. (1 Samweli 1:19-28; 7:15-17) Hiyo ilikuwa mifano mizuri kama nini kwa watumishi wa kisasa wa Yehova, vijana kwa wazee!

7. (a) Ni nani ambao “kupitia imani walishinda falme katika pambano”? (b) Ni nani ambao “walitekeleza uadilifu” kupitia imani?

7 Kwa imani sisi tunaweza kukabili kwa mafanikio kila jaribu la ukamilifu na tunaweza kufanya jambo lo lote linalopatana na mapenzi ya Mungu. (Soma Waebrania 11:33, 34, NW.) Kwa kutaja tu vitendo zaidi vya imani, inaonekana kwamba Paulo alikuwa akifikiria waamuzi, wafalme, na manabii Waebrania, kwa maana kitambo kidogo tu alikuwa ametoka kusema juu ya wanaume hao. “Kupitia imani” waamuzi hao kama Gideoni na Yeftha “walishinda falme katika pambano.” Ndivyo pia alivyofanya Mfalme Daudi, ambaye alitiisha Wafilisti, Wamoabi, Washami, Waedomi, na wengine. (2 Samweli 8:1-14) Pia kupitia imani, waamuzi wanyofu “walitekeleza uadilifu,” na mashauri yenye uadilifu ya Samweli na manabii wengine yalivuta mioyo ya angalau watu fulani waepuke au waache kutenda mabaya.—1 Samweli 12:20-25; Isaya 1:10-20.

8. Ni ahadi gani ambayo Daudi alipewa, nayo iliongoza kwenye nini?

8 Daudi ni mmoja ambaye kupitia imani ‘alipata ahadi.’ Yehova alimwahidi hivi: “Kiti cha ufalme chako chenyewe kitakuwa kimoja kilichothibitishwa imara mpaka wakati usiojulikana.” (2 Samweli 7:11-16, NW) Na Mungu alitimiza ahadi hiyo kwa kuusimamisha Ufalme wa Kimasihi katika 1914 W.K.—Isaya 9:6, 7; Danieli 7:13, 14.

9. Ni chini ya hali gani ‘vinywa vya simba vilifungwa kupitia imani’?

9 Nabii Danieli alikabili kwa mafanikio jaribu la ukamilifu wakati alipoendelea kupelekea Mungu sala kulingana na desturi yake ya kila siku kujapokuwa na katazo la kifalme. Hivyo akiwa na imani ya mshika-ukamilifu, Danieli ‘alifunga vinywa vya simba’ katika maana ya kwamba Yehova alimhifadhi hai katika tundu la simba ambamo alikuwa ametupwa.—Danieli 6:4-23.

10. Ni nani ambao ‘walizuia kani ya moto’ kupitia imani, na imani inayolinganika na hiyo itatuwezesha sisi tufanye nini?

10 Shadraka, Meshaki, na Abednego, Waebrania washika-ukamilifu washiriki wa Danieli, ni kama kweli “walizuia kani ya moto.” Walipotishwa na kifo katika tanuri iliyopashwa moto zaidi ya kawaida, wao walimwambia Mfalme Nebukadreza, kwamba Mungu wao angewaokoa au la, wao hawangetumikia miungu ya mfalme huyo Mbabuloni wala hawangeabudu mfano aliokuwa amesimamisha. Yehova hakuzima moto katika tanuri hiyo. lakini alihakikisha kwamba haukuwadhuru hata kidogo Waebrania hao watatu, (Danieli 3:1-30) Imani inayolinganika na hiyo inatuwezesha sisi tudumishe ukamilifu kwa Mungu kufikia hatua ya kuweza kuuawa mikononi mwa adui.—Ufunuo 2:10.

11. (a) Kupitia imani, ni nani ambao “waliokoka ncha ya upanga”? (b) Ni nani ambao “walifanywa wenye nyingi” kupitia imani (c) Ni nani ambao “wakawa wenye ushujaa katika vita” na ‘wakashinda na kukimbiza majeshi ya wageni’?

11 Daudi ‘aliokoka ncha ya upanga’ wa wanaume wa Mfalme Sauli. (1 Samweli 19:9-17) Manabii Eliya na Elisha pia waliokoka kifo cha upanga. (1 Wafalme 19:13; 2 Wafalme 6:11-23) Lakini ni nani ambao ‘kutoka hali ya udhaifu walifanywa wenye nguvu nyingi kupitia imani’? Basi, Gideoni alijihesabu yeye mwenyewe na wanaume wake kuwa dhaifu mno wasiweze kuokoa Israeli kutoka kwa Wamidiani. Lakini yeye ‘alifanywa mwenye nguvu nyingi’ na Mungu, ambaye alimpa ushindi—tena akiwa na wanaume 300 tu!—Waamuzi 6:14-16; 7:2-7, 22) Samsoni ‘alifanywa mwenye nguvu nyingi’ na Yehova ‘kutoka hali ya udhaifu’ wakati nywele zake zilipokatwa, naye akaua Wafilisti wengi. (Waamuzi 16:1921, 28-30; linganisha Waamuzi 15:13-19.) Huenda pia Paulo akawa alifikiri juu ya Mfalme Hezekia kuwa mmoja ‘aliyefanywa mwenye nguvu nyingi’ kutoka hali ya udhaifu kijeshi na hata kimwili. (Isaya 37:1–38:22) Miongoni mwa watumishi wa Mungu ambao “wakawa wenye ushujaa katika vita” walikuwa Mwamuzi Yeftha na Mfalme Daudi. (Waamuzi 11:32, 33; 2 Samweli 22:1, 2, 30-38) Na wale ambao ‘walishinda na kukimbiza majeshi ya kigeni’ ni kutia ndani mwamuzi Baraki. (Waamuzi 4:14-16) Matendo yote hayo hodari yanapasa yatusadikishe sisi kwamba kwa imani tunaweza kukabili kwa mafanikio kila jaribu la ukamilifu wetu na tunaweza kufanya jambo lo lote linalopatana na mapenzi ya Yehova.

Wengine Wenye Imani Iliyo Mfano Mwema

12. (a) Ni “wanawake [gani ambao] walipokea wafu wao kwa ufufuo“? (b) Ni kwa njia gani ufufuo wa watu fulani wenye imani utakuwa “bora“?

12 Imani inatia ndani kuamini, tumaini ambalo linatusaidia sisi tudumishe ukamilifu kwa Mungu. (Soma Waebrania 11:35, NW.) Kwa sababu ya imani, “wanawake walipokea wafu wao kwa ufufuo.” Kwa imani na nguvu za Mungu, Eliya alifufua mwana wa mjane katika Sarepta, na Elisha aliinua kwenye uzima mvulana wa mwanamke Mshunami. (1 Wafalme 17:17-24; 2 Wafalme 4:17-37) “Lakini watu wengine waliteswa-teswa [kwa uhalisi, “walipigwa kwa vijiti”] kwa sababu wao walikataa kukubali kufunguliwa kwa ukombozi wa namna fulani, ili kwamba wao waweze kupata ufufuo bora.” Inaonekana kwamba mashahidi hao wa Yehova wasiotambulishwa Kimaandiko walipigwa mpaka wakafa, wakikataa kukubali kukombolewa kulikotaka kwamba wao wakubali kuiacha imani yao. Ufufuo wao utakuwa “bora” kwa sababu utakuwa bila ule uhitaji usioepukika wa kufa tena (kama walivyokufa wale walioinuliwa na Eliya na Elisha) nao utatukia chini ya utawala wa Ufalme ulio mikononi mwa Yesu Kristo, yule “Baba wa Milele” ambaye ukombozi wake unaandaa nafasi ya kupata uzima usio na mwisho duniani.—Isaya 9:6; Yohana 5:28, 29.

13. (a) “Ni nani waliopatwa na dhihaka na mapigo ya mijeledi”? (b) Ni nani waliopatwa na “vifungo na magereza”?

13 Ikiwa sisi tuna imani tutaweza kuvumilia mateso. (Soma Waebrania 11:36-38, NW.) Tunapoteswa inasaidia kulikumbuka tumaini la ufufuo na kung’amua kwamba Mungu anaweza kututegemeza kama alivyofanyia “wengine [ambao] walipokea jaribu lao [au jaribu la imani] Kwa dhihaka na mapigo ya mijeledi. ndiyo, zaidi ya hilo, kwa vifungo na magereza.” wafanyia dhihaka manabii wake, mpaka hasira kali ya Yehova ikapanda dhidi ya watu wake.” (2 Nyakati 36:15.16, NW) Kwa imani, Mikaya. Elisha, na watumishi wengine wa Mungu walivumilia “dhihaka.” (1 Wafalme 22:24; Wafalme 2:23, 24; Zaburi 42:3) “Mapigo ya mijeledi” yalijulikana katika siku za wafalme na manabii wa Israeli, na. wapinzani ‘walimpiga dharuba’ Yeremia, si kumpiga kofi tu kwa uchokozi. “Vifungo na magereza” vinaweza kutukumbusha juu ya mambo yaliyompata na pia yaliyopata manabii Mikaya na Hanani. (Yeremia 20:1, 2; 37:15; 1 Wafalme 12:11; 22:26, 27; 2 Nyakati 16:7, 10) Kwa sababu ya kuwa na imani inayofanana na hiyo, mashahidi wa kisasa wa Yehova wameweza kuvumilia taabu zinazolinganika na hizo “kwa ajili ya uadilifu.”—1 Petro 3:14, NW.

14. (a) Ni nani aliyekuwa miongoni mwa wale ‘waliopigwa kwa mawe’? (b) Ni nani ambao huenda wakawa “walikatwa vipandevipande kwa msumeno”?

14 “Wao walipigwa kwa mawe,” akasema Paulo. Mmoja wa wanaume wenye imani waliotendwa hivyo alikuwa Zekaria, mwana wa kuhani Yehoyada. Kwa kufunikwa kabisa na roho ya Mungu, yeye alinena dhidi ya waasi-imani wa Yuda. Matokeo yakawa nini? Kwa agizo la Mfalme Yehoashi, watunga-njama walimpiga kwa mawe mpaka akafa katika ua wa nyumba ya Yehova. (2 Nyakati 24:20-22; Mathayo 23:33-35) Paulo aliongeza hivi: “Wao walijaribiwa, wao walikatwa vipandevipande kwa msumeno.” Huenda akawa alifikiri nabii Mikaya kuwa mmoja wa wale ambao “walijaribiwa,” na pokeo moja la Kiyahudi lisilo la uhakika linasema kwamba Isaya alikatwa kwa msumeno vipande viwili wakati wa utawala wa Mfalme Manase.—1 Wafalme 22:24-28.

15. Ni nani waliopatwa na “kutendwa vibaya” na “walitangatanga katika majangwa”?

15 Wengine “walikufa kwa kuchinjwa kwa upanga,” kwa mfano, manabii wa Mungu wenzi wa Eliya ‘waliuawa kwa upanga’ katika siku za Mfalme Ahabu mwovu. (1 Wafalme 19:9, 10) Eliya na Elisha walikuwa miongoni mwa wale wenye imani ambao “walienda huku na huku katika ngozi za kondoo, katika ngozi za mbuzi, wao walipokuwa katika uhitaji, katika dhiki, chini ya kutendwa vibaya.” (1 Wafalme 19:5-8, 19; 2 Wafalme 1:8; 2:13; linganisha Yeremia 38:6.) Wale ambao “walitangatanga katika majangwa na milima na mapango na matundu ya dunia” wakiwa vitu vya mateso lazima wawe ni kutia ndani si Eliya na Elisha tu bali pia wale manabii 100 ambao Obadia alificha katika pango wakiwa hamsini-hamsini, akiwapa mkate na maji wakati Malkia Yezebeli mwabudu sanamu alipoanza ‘kuua manabii wa Yehova.’ (1 Wafalme 18:4, 13; 2 Wafalme 2:13; 6:13, 30, 31) Lo, washika-ukamilifu walioje! Si ajabu Paulo alisema: “Ulimwengu [jamii ya kibinadamu isiyo na uadilifu] haukustahili kuwa nao”!

16. (a) Kwa sababu gani mashahidi wa Yehova wa nyakati zilizotangulia Ukristo hawajapokea bado “utimizo wa ile ahadi”? (b) Kwa mashahidi wa Yehova wa nyakati zilizotangulia Ukristo, ni lazima ‘kufanywa wakamilifu’ kuwe kunahusiana na nini?

16 Imani inatupa sisi usadikisho kwamba katika wakati wa Mungu unaofaa wote wanaompenda yeye ‘wataupata utimizo wa ile ahadi.’ (Soma Waebrania 11:39, 40, NW.) Washika-ukamilifu wa nyakati zilizotangulia Ukristo “walitolewa ushahidi kupitia imani yao,” sasa ni kumbukumbu la Kimaandiko. Lakini wao hawajapokea bado “utimizo wa ile ahadi” ya Mungu kwa kupata ufufuo wa kidunia wakiwa na tazamio la uzima wa milele chini ya utawala wa Ufalme. Kwa sababu gani? “Ili kwamba wao wasiweze kufanywa wakamilifu mbali na” wafuasi wapakwa-mafuta wa Yesu, ambao kwa ajili yao “Mungu alitangulia kuona kitu fulani kilicho bora”—uzima wa kimbingu usiokufa na mapendeleo ya kutawala pamoja na Kristo Yesu. Kwa ufufuo wao, ulioanza baada ya kusimamishwa kwa Ufalme katika 1914, Wakristo wapakwa-mafuta ‘wanafanywa wakamilifu’ katika mbingu kabla ya mashahidi wa Yehova wa nyakati zilizotangulia Ukristo kufufuliwa duniani. (1 Wakorintho 15:5057; Ufunuo 12:15) Kwa mashahidi hao wa kwanza zaidi, ‘kufanywa wakamilifu’ ni lazima kuwe kunahusiana na ufufuo wao wa kidunia, kuja kwao hatimaye ‘kuwekwa huru kutoka kwenye utumikisho wa uharibifu,’ na kufikia kwao ukamilifu wa kibinadamu kupitia huduma za Kuhani Mkuu Yesu Kristo na makuhani wake wadogo wa kimbingu 144,000 wakati wa Utawala wa Mileani wake.—Warumi 8:20, 21, NW; Waebrania 7:26; Ufunuo 14:1; 20:4-6.

Endelea Kumtazama Mkamilishaji wa Imani Yetu

17, 18. (a) Ili tufanikiwe katika shindano letu la mbio kwa ajili ya uzima wa milele, ni lazima tufanye nini? (b) Ni jinsi gani Yesu Kristo ndiye “Mkamilishaji wa imani yetu”?

17 Akiisha kuzungumza vitendo vya mashahidi wa Yehova wa nyakati zilizotangulia Ukristo, Paulo alielekeza kwenye mfano ulio mkuu zaidi wa imani. (Soma Waebrania 12:13, NW.) Ni chanzo cha kutia moyo kama nini kuwa na wingu kubwa sana la watoaji ushahidi linalotuzunguka sisi’! Jambo hilo linatutia bidii tuvue kila uzito ambao ungezuia maendeleo yetu ya kiroho. Linatusaidia tuepuke dhambi ya upotevu au ukosefu wa imani na kukimbia kwa uvumilivu katika shindano la mbio ya Kikristo ya uzima wa milele. Ijapokuwa hivyo, ili tuufikie mradi wetu ni lazima tufanye jambo fulani zaidi. Ni jambo gani hilo?

18 Ikiwa sisi tutafanikiwa katika shindano letu la mbio ya uzima wa milele katika mfumo mpya wa Mungu, tunahitaji ‘kutazama kwa mkazo sana Wakili Mkuu [au, Kiongozi Mkuu] na Mkamilishaji wa imani yetu, Yesu.” Imani ya Abrahamu na washika-ukamilifu wengine wenye kuishi kabla ya huduma ya kidunia ya Yesu Kristo ilikuwa isiyo kamilifu, isiyo kamili kwa sababu wao hawakufahamu wakati huo unabii usiokuwa umetimizwa kuhusu Masihi. (Linganisha 1 Petro 1:10-12.) Lakini kwa uzaliwa wa Yesu, huduma yake, kifo, na ufufuo, unabii mwingi wa Kimasihi ulitimizwa. Hivyo imani katika maana iliyokamilishwa ‘ilifika’ kupitia Yesu Kristo. (Wagalatia 3:24, 25, NW) Tena, akiwa kwenye cheo chake cha kimbingu Yesu aliendelea kuwa Mkamilishaji wa imani wa wafuasi wake, kama wakati alipokuwa akimimina juu yao roho takatifu kwenye Pentekoste ya 33 W.K. na kwa mafunuo yaliyokuza imani yao hatua kwa hatua. (Matendo 2:32, 33; Warumi 10:17; Ufunuo 1:1, 2; 22:16) Sisi ni wenye shukrani kama nini kwa kuwa na “Shahidi Mwaminifu” huyo, “Kiongozi Mkuu” huyo wa Mashahidi wa Yehova!—Mathayo 23:10; Ufunuo 1:5, NW.

19. Kwa sababu gani Yesu anapasa ‘afikiriwe kwa ukaribu’?

19 Kwa kuwa si jambo rahisi kuvumilia masuto ya watu wasio na imani, Paulo alihimiza hivi: “Mfikirieni kwa ukaribu [Yesu] ambaye amevumilia maongezi-kinyume kama hayo yenye kufanywa na watenda dhambi dhidi ya mapendezi yao wenyewe, kwamba ninyi msipate kuchoka na kuzimia katika nafsi zenu.” Kwa kweli, sisi tukiendelea kukaza macho yetu juu ya “Shahidi Mwaminifu,” Yesu Kristo, hatutachoka kamwe juu ya kutenda mapenzi ya Mungu.—Yohana 4:34.

20. Ni mengine gani ya mambo ambayo wewe umejifunza juu ya imani kwa kufikiria Waebrania 11:1–12:3?

20 Kutokana na ‘wingu kuu la mashahidi’ tunajifunza mambo mengi juu ya nyuso za imani. Kwa mfano, imani kama ile ya Abeli inaongeza uthamini wetu kwa dhabihu ya Yesu. Imani ya kweli inatufanya tuwe mashahidi wenye ushujaa, kama vile Enoki alivyonena kwa ujasiri ujumbe wa Yehova. Kama Noa, imani yetu inavuta mioyo yetu tufuate maagizo ya Mungu kwa ukaribu na tutumikie tukiwa wahubiri wa uadilifu. Imani ya Abrahamu inatukazia uhitaji wa kutii Mungu na kutumaini ahadi Zake, hata ingawa nyingine zazo hazijatimizwa bado. Mfano wa Musa unaonyesha kwamba imani inatuwezesha tuendelee bila kutiwa doa na ulimwengu huu na kusimama kishikamanifu upande wa watu wa Yehova. Matendo hodari ya waamuzi, wafalme, na manabii wa Israeli yanathibitisha kwamba imani katika Mungu inaweza kututegemeza katikati ya mateso na majaribu. Nasi tuna shukrani kama nini kwamba mfano ulio bora kabisa wa Yesu Kristo unaimarisha imani yetu na kuifanya isiyotikisika! Basi, Yesu akiwa ndiye Kiongozi wetu na kwa kupewa nguvu na Mungu wetu, acheni sisi tuendelee kuonyesha wazi imani inayovumilia tukiwa Mashahidi wa Yehova.

Majibu Yako Ni Nini?

◻ Ni vitendo gani vya mashahidi wa Yehova wa nyakati zilizotangulia Ukristo vinavyothibitisha kwamba imani inaonyeshwa kwa tegemeo kamili juu ya Mungu katika kukabili hatari?

◻ Kwa sababu gani inaweza kusemwa kwamba kwa imani sisi tunaweza kukabili kwa mafanikio kila jaribu la ukamilifu wetu?

◻ Kuna uthibitisho gani kwamba kupitia imani sisi tunaweza kuvumilia mateso?

◻ Kwa sababu gani Yesu anaitwa “Mkamilishaji wa imani yetu”?

◻ Ni nini nyinginezo za nyuso nyingi za imani?

[Picha katika ukurasa wa 16, 17]

Daudi alionyesha imani kwa kumtegemea Yehova kwa ukamili. Ni mfano mzuri sana kwa watu wa Yehova leo!

[Picha katika ukurasa wa 18]

“Wanawake walipokea wafu wao kwa ufufuo.” Imani katika ufufuo inatusaidia tudumishe ukamilifu kwa Yehova

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki