Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 6/15 kur. 15-19
  • Kujaribu na Kupepeta Nyakati za Kisasa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kujaribu na Kupepeta Nyakati za Kisasa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakati wa Majaribu Makali
  • Kusafishwa Kitengenezo
  • Huduma ya Shambani
  • Nuru Yenye Kuongezeka
  • Kuyaondoa Mazoea Machafu
  • Wakati wa Kujaribu na Kupepeta
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Bwana wa Kweli Aja kwa Ajili ya Hukumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Enda Sambamba na Tengenezo la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • “Baraka Hata Kusiwe na Uhitaji Tena”
    Izingatie Siku ya Yehova Maishani
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 6/15 kur. 15-19

Kujaribu na Kupepeta Nyakati za Kisasa

“Ni nani atakayestahimili siku ya kuja kwake? au ni nani atakayesimama atakapoonekana yeye?”​—MALAKI 3:2.

1. Yehova alipokuja kwenye hekalu la kiroho katika nyakati za kisasa, yeye alipata kuona nini, jambo hilo likitokeza swali gani?

WAKATI “Bwana [wa kweli]” alipokuja kwenye hekalu la kiroho akiwa pamoja na “mjumbe wa agano” wake muda mfupi baada ya Ufalme kusimamishwa katika mbingu katika 1914, Yehova alipata kuona nini? Watu wake walihitaji kusafishwa na kutakaswa. Je! wao wangejitiisha wenyewe kwa jambo hili na kuvumilia utakasaji wo wote uliohitajiwa wa tengenezo lao, utendaji, mafundisho, na mwenendo? Kama anavyosema Malaki: “Ni nani atakayestahimili siku ya kuja kwake? Au ni nani atakayesimama atakapoonekana yeye?”​—Malaki 3:1, 2.

2. Katika nyakati za kisasa, ni nani “wana wa Lawi” wa Malaki 3:3?

2 Yehova anakubali daraka la kutakasa na kusafisha “wana wa Lawi.” (Malaki 3:3) Katika Israeli wa kale, kabila la Lawi lilitoa makuhani na wasaidizi wa hekalu. “Wana wa Lawi” hawa wanalingana na baraza la wapakwa-mafuta kwa ujumla, wanaotumika wakiwa makuhani chini ya Yesu, Kuhani Mkuu. (1 Petro 2:7-9; Waebrania 3:1) Wao ndio waliokuwa wa kwanza kupitia kipindi cha kujaribiwa wakati Yehova alipokuja kwenye hekalu lake la kiroho akiambatana na “mjumbe wa agano” wake. Sasa, kuna ushuhuda gani kwamba kusafisha huko kulitukia kuanzia siku za kumalizia Vita ya Ulimwengu ya Kwanza na kuendelea?

Wakati wa Majaribu Makali

3. Kufikia kiangazi cha 1918, ni nini iliyokuwa hali ya mashahidi wa Mungu?

3 Yehova alipoambatana pamoja na “mjumbe wa agano” wake kwenye hekalu la kiroho, Yeye alipata mabaki wakiwa katika uhitaji wa kusafishwa na kutakaswa. Kwa mfano, Mnara wa Mlinzi, ulikuwa umewatia moyo wasomaji wao waweke kando siku ya Mei 30, 1918 kuwa siku ya sala kwa ajili ya ushindi wa mamlaka za kidemokrasi, kama ilivyokuwa imeagizwa na baraza kuu la U.S. na Rais Wilson. Jambo hili lilikuwa kuvunja kutokuwamo kwa Kikristo.​—Yohana 17:14, 16.

4. Ni jambo gani lililotokea kuhusu mateso ya watumishi wa Yehova?

4 Viongozi wa kidini na serikali mbalimbali ziliwaletea watumishi wapakwa-mafuta wa Yehova mkazo mkubwa. Wakishtakiwa kwa uwongo kuwa wafitini serikali, mabaki wapakwa-mafuta walijaribu kujulisha hali yao ya kutokuwa na hatia waziwazi. Hata hivyo, katika Mei 7, 1918, waranti zilitolewa ili kuwakamata washiriki wanane wa usimamizi ya Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti, na halmashauri ya uhariri, kutia ndani J. F. Rutherford akiwa msimamizi. Kujaribiwa kwao kulianza Jumatatu, Juni 3. Juni 20, baraza la mahakimu lilikata maneno ya kwamba walikuwa na hatia ya mashtaka manne. Halafu Juni 4, 1918, wanaume hao Wakristo waliojitoa wakfu walipelekwa kwa gari-moshi kwenye gereza katika Atlanta, Georgia, U.S.A.

5. Ilionekanaje wazi kwamba kulikuwa na uhitaji wa kupepeta miongoni mwa wale waliokuwa wakimtumikia Mungu, na ni kitu gani kinachoonyesha kwamba jambo hilo lilitukia?

5 Kufikia kiangazi cha 1918, ile sauti yenye nguvu ya wapakwa-mafuta iliyokuwa imepangwa kitengenezo kuhubiri peupe kuhusu Ufalme wa Yehova ilinyamazishwa. Ilikuwa kana kwamba walikuwa ‘wameuawa’ kuhusiana na utendaji wao wa waziwazi. (Ufunuo 11:3, 7) Wakati wa mikusanyiko ya Sosaiti katika kiangazi hicho, waasi-imani fulani waligeuka na kufanyiza vikundi vyao wenyewe vya kidini vyenye kupinga. Wakionyesha nyutu za ‘mtumwa mbaya’ wao ‘walipepetwa’ kama “makapi” ili watenganishwe na mabaki waaminifu wa Yehova. (Mathayo 3:12; 24:48-51) Ukumbusho wa kifo cha Kristo uliadhimishwa Jumapili, Aprili 13, 1919, watu 17,961 wakihudhuria katika nchi nyingi. Ulipolinganishwa na ripoti isiyo kamili ya 1917, hudhurio la Ukumbusho lilikuwa limepungua kwa zaidi ya 3,000 kuonyesha matokeo ya kupepeta.

6. Kuruhusu kwa Yehova majaribu hayo kulikuwaje na tazamio la kuwabariki watu wake hatimaye?

6 Hata hivyo, Yehova aliruhusu majaribu hayo makali yawapate watu wake ili wapate baraka hatimaye. Yeye hakuwaacha kabisa. Jumanne, Machi 25, 1919, J. F. Rutherford na wale wengine saba walifunguliwa kutoka gerezani kwa dhamana na baadaye wakaondolewa mashtaka kabisa. Lo! Kwa ghafula, kwa waokokaji waliosafishwa wa kipindi hiki cha kujaribiwa, kukaja uhuru kutoka utumwani! Ndiyo, “roho ya uhai itokayo kwa Mungu ikawaingia, wakasimama juu ya miguu yao,” wakiwa tayari kutenda.​—Ufunuo 11:11.

7. (a) Mashahidi hao waliorudishwa sasa walifanya nini? (b) Ni jambo gani lililotokana na kusafishwa na kutakaswa huku?

7 Wangefanya nini sasa? Wakiwa jamii ya Kikristo iliyorudishwa, mabaki walijichunguza kwa uangalifu. Wakasali wapate msamaha wa Yehova kwa dhambi zo zote za kuacha kutokuwamo. (Linganisha Zaburi 106:6; Isaya 42:24.) Walisonga mbele wakiwa watu waliosafishwa. Kama matokeo ya kusafishwa, mabaki wenye moyo mshikamanifu ‘wakamtolea Bwana [Yehova, NW] dhabihu katika [uadilifu].’ (Malaki 3:3) Dhabihu za kiroho za sifa walizozitoa zilimpendeza Mungu. (Waebrania 13:15) Wao walifurahi kwamba kile kipindi kifupi cha kukosa upendeleo wa Yehova kilikuwa kimekoma. Wao walikuwa wana uhakika kwamba utumishi wao katika wakati ujao ungekuwa wenye kukubalika kwake. (Isaya 12:1) Kuanzia Septemba 1 hadi 8, 1919, mkusanyiko wenye furaha ulifanywa kule Cedar Point, Ohio, watu 7,000 wakihudhuria na 200 wakabatizwa. Yote hayo yalionyesha kurudishwa na nia ya kutaka kutimiza kazi ya Yehova ya kuhubiri.

8. (a) Kazi ya kusafisha na kutakasa inatuhusuje sisi leo? (b) Kwa kuongezea “wana wa Lawi” wa kisasa, ni nani wengine ambao lazima wapitie katika hali ya kujaribiwa na kupepetwa?

8 Lakini mambo hayo yote yanawahusuje watu wa Yehova wanaoishi leo? Kulingana na unabii huo, Yehova, akiambatana pamoja na mjumbe wake, angekuja na ‘kuketi kama asafishaye fedha na kuitakasa.’ (Malaki 3:3) Ndiyo, kazi ya kusafisha na kutakasa ingeendelea, naye ‘angeketi’ na kutazama kwa makini. Uhakika wa kwamba mabaki washikamanifu walikuwa wamepitia wakati wa majaribu makali mapema katika karne hii hakukumaanisha kwamba Msafishaji Mkuu alikuwa amemaliza kuwasafisha kwake. Kujaribu na kupepeta kumeendelea mpaka siku yetu. Yehova angali katika hekalu lake, akiketi katika hukumu. Amekuwa akitakasa si “wana wa Lawi” tu, mabaki wapakwa mafuta. Unabii wa Malaki ulionyesha kuhangaishwa Kwake na “mgeni” anayefananishwa na “mkutano mkubwa” ambao tazamio lao ni uzima wa kidunia. (Malaki 3:5; Ufunuo 7:9, 10) Ndiyo, wakati wa miaka 69 iliyopita, kumekuwapo kusafisha kunakoendelea kwa watu wa Yehova katika njia za nne kubwa.

Kusafishwa Kitengenezo

9. Ni nini baadhi ya matukio mengine ya hatua kwa hatua katika muundo wa kitengenezo tangu 1919?

9 Kwanza, kusafisha kulitukia kwa kupatanisha kundi la ulimwenguni pote hatua kwa hatua na kanuni mpya za Kimaandiko zilizopatikana. Kulipasa kuwe kuachwa polepole kwa njia za kidemokrasi za kuongoza shughuli za kundi. Yafikirie mengine ya maendeleo yaliyopatanishwa katika jambo hili.

1919: Kuwekwa na Baraza Linaloongoza kulianza kwa kuwekwa kutoka makao makuu ya Sosaiti ya Mnara ya Mlinzi mkurugenzi wa kudumu wa utumishi katika kila kundi ili asimamie utendaji wa utumishi wa shambani.

1932: Kuchaguliwa kila mwaka kwa wazee na mashemasi kulikomeshwa; mahali pa uchaguzi wa kundi wa wanaume kwa ajili ya vyeo hivyo palichukuliwa na uchaguzi wa halmashauri ya utumishi yenye kumsaidia (na kumtia ndani pia) mkurugenzi wa utumishi aliyewekwa na Sosaiti.

1937: Ilitambuliwa kwamba “Wayonadabu” [wale wenye tumaini la kidunia] wangeshikilia vyeo vya madaraka katika kundi.

1938: Waangalizi wote na wasaidizi wao wangewekwa na Sosaiti katika njia ya kitheokrasi.

1972: Ilijulishwa wazi kwamba njia ya Kimaandiko ya kuongoza kila kundi si kupitia mwanamume Mkristo mmoja aliyekomaa bali kupitia baraza la wazee, kama walivyowekwa na Sosaiti.

1975: Kusimamishwa kwa halmashauri za Baraza Linaloongoza ili kutunza madaraka mbalimbali; hakuna mtu mmoja ambaye angeongoza mambo, hata ndani ya halmashauri, lakini wote wangekuwa na nafasi ya kutoa maoni, nao kwa umoja wangeutumainia uongozi wa Kristo Yesu.

10. (a) Ni jambo gani ambalo limetokea kwa sababu ya kusafishwa huku? (b) Wewe unahisije kuhusu marekebisho yote hayo?

10 Matokeo ya marekebisho hayo yamekuwa nini? Bila shaka baraka ya Yehova imekuwa nyingi, kama inavyoonyeshwa kwa ukuzi wa kiroho na hesabu za waabudu wake. (Linganisha Matendo 6:7; 16:5.) Kwa kweli, waangalizi wengine na watu wengine wamepepetwa kwa sababu hawakujinyenyekeza kwa ushikamanifu kwa njia iliyoongozwa na Mungu. Ingawaje, walio wengi zaidi wa watu wa Yehova wamejithibitisha kuwa wenye kutii na wenye kunyenyekea maendeleo ya kitengenezo. (Waebrania 13:17) Wao wanathamini kwamba kupitia marekebisho hayo Msafishaji Mkuu amewaleta katika upatano wa karibu zaidi na njia za Kimaandiko za kuongoza makundi.

Huduma ya Shambani

11. Ni namna zipi za hatua kwa hatua ambazo kazi ya kuhubiri inafuata katika miongo ya karibuni?

11 Pili, kusafisha kumefanywa kupitia majaribu kuhusu kushiriki utumishi wa shambani.

1922: Washiriki wote wa makundi walisihiwa washiriki utumishi wa shambani wa nyumba kwa nyumba. Bulletin (sasa Huduma ya Ufalme Yetu) ya kila mwezi yenye miongozo ya utumishi ikapatikana.

1927: Kuhubiri nyumba kwa nyumba kwa ukawaida kila Jumapili kukaanza. Vitabu na vijitabu viligawanywa kwa mchango.

1937: Kijitabu cha kwanza ya Funzo la Mfano kwa ajili ya mafunzo ya Biblia ya nyumbani.

1939: Kampeni ya kwanza ya uandikishaji wa mwaka wa Mnara wa Mlinzi, ilitokea; zaidi ya maandikisho mapya 93,000 yalipatikana.

1940: Kazi ya barabarani ya magazeti ikaanza.

Njia nyingine zenye maendeleo zilianzishwa katika kazi hii ya kuhubiri hadharani, kutia na kufanya ziara za kurudia na kuongoza mafunzo ya nyumbani ya Biblia.

12. (a) Matokeo ya usafishaji huo wa huduma ya shambani yamekuwa nini? (b) Tunawezaje kuonyesha ushikamanifu wetu kwa njia ambayo Yehova amewasafisha watu wake?

12 Matokeo yamekuwa nini? Muda wa miaka hiyo wengine wamepepetwa kwa sababu hawakuwa na nia ya kuwa Wakristo wenye kuzaa matunda. (Yohana 15:5) Hata hivyo kwa hakika wengi wa watu wa Yehova wameitikia mwito wa kuwa wahubiri wa Ufalme. Kwani, kikundi hicho kidogo cha wahubiri walio chini ya 8,000 huko nyuma 1919 kimeongezeka kufika kilele cha wahubiri wa Ufalme 3,229,022 katika 1986! Namna gani juu ya huduma ya wakati wote? Kwa kulinganisha makolpota (mapainia) wenye kutenda 150 huko nyuma katika masika ya 1919, mwaka uliopita kulikuwa na wastani wa mapainia wahubiri watendaji zaidi ya 391,000 kila mwezi​—hesabu ya juu sana katika historia ya Mashahidi wa Yehova wa kisasa. Kwa kushiriki sehemu katika kuhubiri habari njema, tunaonyesha tegemezo letu kwa ushikamanifu kwa njia ambayo katika hiyo Yehova ameendelea kusafisha watu wake.​—1 Wakorintho 9:16.

Nuru Yenye Kuongezeka

13. Ni ipi mingine ya mifano ambayo kupitia kwayo Yehova amewatia nuru ya elimu watu wake?

13 Tatu, kusafisha kulitukia wakati watu wa Mungu walipojaribiwa kuhusu kukubali nuru ya elimu ya kiroho yenye kuendelea kutoka katika Biblia. (Mithali 4:18) Kuanzia 1919 mpaka leo hii mfuriko halisi wa kweli mpya zilizofunuliwa umetiririka.

1925: Ilitambuliwa waziwazi kwamba kuna matengenezo mawili dhahiri yenye kupingana​—la Yehova na la Shetani.

1931: Jina jipya Mashahidi wa Yehova lilikubaliwa.

1935: “Mkutano mkubwa” wa Ufunuo 7:9-15 ulitambuliwa kuwa jamii ambayo itaishi duniani.

1941: Kufaa kwa enzi kuu ya Yehova ya ulimwengu wote mzima kulionyeshwa kuwa ndilo suala la msingi lililotokezwa na mwito wa ushindani wa Shetani.

1962: “Mamlaka iliyo kuu” ya Warumi 13:1 ilitambulishwa kwa kufaa kuwa mamlaka za kiserikali za ulimwengu, ambazo kwazo Wakristo wanapaswa kujitiisha kwa kadiri.

1986: Ilithaminiwa kwamba wote mabaki na wale wa mkutano mkubwa kwa njia ya mfano lazima wale mwili wa Yesu na kunywa damu yake kwa kukubali dhabihu yake ili wawe katika umoja naye.​—Yohana 6:53-56.

Kwa miongo iliyopita, Yehova alivyozidi kuwapa nuru ya elimu watu wake, ikawa wazi kwamba kuna uhitaji wa kundi kutenda ili kudumisha tengenezo safi, lisilokuwamo lenye kuheshimu utakatifu wa damu.​—1 Wakorintho 5:11-13; Yohana 17:14, 16; Matendo 15:28, 29.

14. (a) Watu wa Yehova wameitikiaje huku kutiwa nuru ya elimu kwa hatua kwa hatua? (b) Wewe mwenyewe umeazimia kufanya nini kuhusu njia ya Yehova ya kuwasiliana?

14 Watu wa Mungu wameitikiaje nuru ya elimu hiyo yenye kuendelea? Muda wote huo, kumekuwako wachache ambao hawakuweza kukubali marekebisho fulani. Hao walipepetwa. (Mathayo 3:12) Kwa upande mwingine, watumishi washikamanifu wa Yehova wamefurahia kama nini nuru ya elimu hiyo ya kiroho! Wakati ambapo Jumuiya ya Wakristo inapopapasa-papasa katika giza la kiroho, njia ya watu wa Yehova inang’aa zaidi na zaidi. Je! hatupasi kuazimia kushikamana karibu karibu na njia ya kuwasiliana ambayo Yehova anatumia, tukikubali nuru ya elimu yote hiyo ya hatua kwa hatua kuwa “chakula kwa wakati wake”?​—Mathayo 24:45.

Kuyaondoa Mazoea Machafu

15. Yehova amewasafishaje watu wake polepole kuhusu mazoea machafu au ya Kibabuloni?

15 Nne, kusafisha kulitukia wakati ilipokuwa lazima kuacha mazoea machafu au ya Kibabuloni. Kuanzia mwaka wa 1920 na kitu, watu wa Mungu waliacha kusherehekea Krismasi na sikukuu nyingine ambazo zilionyeshwa kuwa na chanzo cha kipagani. Katika 1945 msimamo wa Kikristo kuhusu kutiwa damu mishipani ulielezwa. Wakati wa mwaka 1960 na kitu na 1970 na kitu, hali ya kiadili ya ulimwengu ilipoendelea kuharibika, Mnara wa Mlinzi uliendelea kutoa shauri lililo wazi kwa watu wa Mungu kuhusu habari kama vile mwenendo unaofaa kati ya watu wa jinsia tofauti na uhitaji wa kuacha tumbaku na dawa nyingine zenye kulevya.

16. Marekebisho kama hayo kuhusu mazoea machafu yanapaswa kuonwaje?

16 Bila shaka, marekebisho kama hayo kuhusu mazoea machafu mara nyingi yametumika kuwa jaribu la ushikamanifu kwa watu wa Mungu. Hata hivyo, wale waliofanya mabadiliko yaliyohitajiwa waliyaona mabadiliko hayo kuwa usaidizi wa kulivua vazi chafu. (Wakolosai 3:9, 10) Wao walitambua kwamba ingawa desturi zinazohusianishwa na sikukuu fulani huenda zikaonekana kuwa zisizo na madhara, maoni ya Yehova ndiyo yanayopaswa kutuhangaisha sisi; yeye mwenyewe alichunguza kwanza mazoea ya kidini ya kipagani ambayo hayo yalitokana nayo. Kuhusu matakwa ya adili ya Mungu, wao waliyaona kuwa ulinzi badala ya kuwa kizuizi, hivyo walibarikiwa na Yehova kwa kuwa safi. Ikiwa rekebisho lilionekana kuwa gumu kuelewa, waliamini kwamba Yehova alikuwa ‘akiwafundisha ili wapate faida.’​—Isaya 48:17.

17, 18. (a) Sisi tukiwa mtu mmoja mmoja tunajaribiwaje na Msafishaji Mkuu? (b) Lazima tuazimie kufanya nini tunapoingojea siku ya Yehova

17 Mwaka baada ya mwaka Yehova anaendelea kutakasa na kusafisha watu wake. Wakiwa jamii, wao wamejitiisha wenyewe kwa kazi ya kusafisha kuhusu tengenezo lao, utendaji, mafundisho, na usafi wa kiadili. Lakini namna gani sisi kama mtu mmoja mmoja? Kupitia tengenezo lake Yehova anaendelea kutoa “chakula kigumu” kwa mwongozo unaosafisha moyo. Makusudi yetu yanajaribiwa na kuchunguzwa. (Waebrania 4:12; 5:14) Kwa kuuitikia usafishaji huo, kazi ya kutakasa ya Msafishaji Mkuu, tunaendelea kuwa safi tunapoingojea “Siku ile ya BWANA [Yehova, NW] iliyo kuu na kuogofya.”​—Malaki 4:5.

18 Shukrani kwa Yehova, “Bwana [wa kweli],” na “mjumbe wa agano,” wake Yesu Kristo, wanaotusafisha sisi na kutuokoa kutokana na uchafu wakati huu wa kujaribiwa na kupepetwa! Sisi sote na tuazimie kuendelea kutembea katika njia safi ya Yehova chini ya “Mwana-Mfalme wa Amani,” Kristo Yesu, na hivyo tuendelee kuwa na uhusiano wetu wenye furaha pamoja na Yehova.​—Isaya 9:6, NW; Zaburi 72:7.

Yehova amewasafishaje watu wake kuhusu—

◻ Marekebisho ya kitengenezo?

◻ Ushiriki katika utumishi wa shambani?

◻ Kukubali kutiwa nuru ya elimu hatua kwa hatua?

◻ Kuondoa mazoea machafu?

[Blabu katika ukurasa wa 16]

Kama matokeo ya kusafishwa na kutakaswa, mabaki wenye moyo mshikamanifu ‘wakawa kwa Yehova watu wenye kutoa dhabihu katika uadilifu’

[Blabu katika ukurasa wa 19]

Mwaka baada ya mwaka Yehova anaendelea kutakasa na kusafisha watu wake

[Picha katika ukurasa wa 17]

Msafishaji wa kale aliondoa uchafu, au takataka. Vivyo hivyo, Yehova anaruhusu kujaribiwa na kupepetwa ili kuwasafisha watu wake.

[Picha katika ukurasa wa 18]

Wachache ‘wamepepetwa’ kama “makapi,” Lakini watumishi washikamanifu wa Yehova wanapokea kwa furaha nuru ya elimu ya kiroho yenye kuendelea

[Credit Line]

Pictorial Archive (Near Eastern History) Est.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki