Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 9/15 kur. 5-7
  • Jinsi Unavyoweza Kuwa na Rafiki za Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Unavyoweza Kuwa na Rafiki za Kweli
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kile Kitabu cha Urafiki wa Kweli
  • Urafiki Katika Kiwango cha Juu Zaidi
  • Rafiki Zetu Walio Bora Zaidi
  • “Uendako Nitaenda”
    Igeni Imani Yao
  • Ruthu na Naomi
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • “Uendako Nitaenda”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Ruthu na Naomi
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 9/15 kur. 5-7

Jinsi Unavyoweza Kuwa na Rafiki za Kweli

“NJIA moja peke yake ya kuwa na rafiki ni kuwa rafiki wewe mwenyewe,” akaandika Emerson, mshairi wa Amerika. Urafiki ni jambo la pande zote mbili linalohusu roho ya kutoa. Watu wanaofikiria mambo yao tu na wale walio na maelekeo ya ubinafsi wanaona ni vigumu kuwa na rafiki za kweli. Hata hivyo, wanaweza kufanikiwa, kama tutakavyoona.

Urafiki wa kweli unakua kutokana na upendo kwa sababu upendo unavuta watu. Hata hivyo watu fulani wanaona ugumu wa kuwa na rafiki. Mtu anaweza kushindaje jambo hilo?

“Uwe msikilizaji mwema. Tia wengine moyo waseme juu yao wenyewe” akashauri Dale Carnegie. Wakati watu wasiojuana wanapokutana, labda kwenye kikusanyiko cha kujifurahisha, ni akina nani wanaopata rafiki? Si wenye kupiga mdomo sana bali ni wale wanaopendezwa na wengine kwa uchangamfu, wakiwavuta watoe maoni yao ya moyoni na kusikiliza kweli kweli. Kukumbuka majina na mambo ya kupendeza juu ya wazoeani wapya kunaweza pia kusaidia kukuza urafiki.

Katika kichapo Fundamentals of Interpersonal Communication, Kim Giffin na Bobby R. Patton wanapendekeza mtu ajifunue wazi aonekane alivyo na kuonyesha hali yake ya kweli. “Ili mtu fulani awe wa maana kwako,” wao wanasema, “ni lazima wewe ujue jambo fulani juu yake ambalo ni la maana kwako wewe . . . [Uwe] mkunjufu na mnyofu katika usemi nyakati zote . . . Maitikio yako kwa yule mtu mwingine lazima yafanywe kwa moyo mweupe.”

Rafiki za kweli si wanyofu tu bali pia wenye kufikiria wenzao, wasiotumia kamwe wenzao kwa faida yao wenyewe au wasioshikilia mno haki zao wenyewe. Wao wanafahamiana, wanaweza kuhisi maoni ya mwenzao juu ya mambo, na hivyo wanaweza kuonyesha hisia-mwenzi. Kadiri uhusiano ule unavyozidi kukua, wao wanafunguliana mioyo yao, hivyo wakiwa si rafiki za kweli tu bali pia rafiki za karibu. Si rafiki za kweli wote walio rafiki za karibu. Yesu Kristo, mtu mwenye urafiki zaidi aliyepata kuwa duniani, alikuja kuwa na rafiki wengi, lakini ni wachache tu waliokuwa rafiki za karibu kweli kweli.​—Marko 9:1-10; Luka 8:51.

Kile Kitabu cha Urafiki wa Kweli

Biblia, ambacho ndicho kitabu bora zaidi kuhusiana na habari ya urafiki, inasema: “Mwandamani wa kweli anapenda wakati wote, na ni ndugu ambaye amezaliwa kwa ajili ya wakati ambapo pana taabu kubwa.” (Mithali 17:17, NW) Rafiki za kweli wanasikitikia watu na wanakuwa tayari kuandaa msaada wakati matatizo yanapotokea. Huu ni mfano mzuri sana wa jambo hilo—hadithi inayotokana na siku za Israeli wa kale.

Kwa sababu ya njaa, mwanamume mmoja wa Yuda alihamia Moabu pamoja na Naomi, mke wake. Baada ya muda fulani akafa. Ulipopita muda, wanaye wawili walioa wasichana Wamoabi Ruthu na Orpa. Ndipo wana wale wakafa, wakiacha wajane watatu wale peke yao. Naomi, yule mama, akaamua kurudi Yuda, na binti-wakweze wawili wakaondoka pamoja naye. Hata hivyo, walipokuwa njiani Naomi aliwahimiza vijana wale wanawake warudi wakatafute waume wengine miongoni mwa watu wao wenyewe. Orpa alifanya hivyo, lakini Ruthu akasisitiza kwenda pamoja na Naomi. Kwa sababu gani? Kwa sababu yeye hakuwa binti-mkwe tu; yeye alikuwa rafiki ya kweli pia. Kwanza, hali yake ya kusikitikia haingemruhusu aache mjane yule mzee-mzee, aliyefiwa na jamaa yake, aende peke yake.—Ruthu 1:1-17.

Ruthu alionyesha hisia-mwenzi, fadhili, ushikamanifu, na upendo wa kweli kweli. Sifa hizo zinafanyiza msingi mgumu wa urafiki wa kweli. Hata hivyo, kulikuwa na jambo jingine lililokuwa katika uhusiano wa Ruthu pamoja na Naomi.

Urafiki Katika Kiwango cha Juu Zaidi

Wakati Naomi alipomhimiza arudi, Ruthu alisema: “Usinisihi nikuache, . . . maana wewe uendako nitakwenda . . . Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.” (Ruthu 1:16) Naomi alikuwa amesaidia Ruthu, aliyekuwa mpagani hapo kwanza, amjue na kumpenda Mungu wa kweli, Yehova. Imani yao waliyoishiriki pamoja ikawa kifungo cha kiroho chenye nguvu nyingi kilichovuta wanawake wale wawili pamoja wakiwa rafiki za kweli. Na Yehova aliwabariki kwa kuwapa jamaa nyingine. Baada ya muda Ruthu aliolewa na Boazi, mwenye shamba; aliyekuwa tajiri katika Yuda, na akawa na mwana jina lake Obedi, ambaye akawa babu ya Mfalme Daudi. —Ruthu 4:15-22; Mathayo 1:5, 6

Jambo hilo la kiroho linaweka urafiki katika kiwango cha juu zaidi. Jinsi gani? Katika kisa cha Ruthu na Naomi, wote wawili waliabudu Yehova, “Mungu mwenye rehema na neema, asiye mwepesi wa hasira na mwingi wa fadhili za upendo na ukweli.” (Kutoka 34:6, NW) “Mungu ni upendo,” na ikiwa sisi tunamwabudu yeye kwa moyo mweupe tukiwa na roho na ukweli, tuna uhakika tutakua katika kumpenda yeye na viumbe wenzetu. (1 Yohana 4:8; Yohana 4:24) Hivyo, tunabadilika. Tunakuza hali ya kupendezwa na wengine kwa urafiki, hasa watu wapole wanaotaabika wa makabila yote. Hivyo watu wanaofikiria mambo yao wenyewe tu wanaendelea kuacha kujifikiria sana. Watu wenye ubinafsi wanakuza hali ya kujali wengine. Tunaanza kuonyesha tunda la roho ya Mungu​—“upendo, furaha, amani, ustahimilivu, fadhili, wema, imani, upole, kujiweza.”—Wagalatia 5:22, 23, NW.

Sifa hizo zinatusaidia tukuze ule uwezo muhimu wa kusamehe mambo ya udhaifu na makosa yaliyo katika wengine—“si, Mpaka mara saba, bali, Mpaka mara sabini na saba,” kama Yesu alivyosema. (Mathayo 18:21, 22, NW) Urafiki mwingi unashindwa hapa. Lakini Yesu Kristo alilihubiri na hata akalizoea. Ni mara nyingi kama nini yeye alisamehe wanafunzi wake wasiokamilika wenye makosa kwa kasoro zao, kutia ndani tendo lenye aibu la Petro kumkana Bwana!—Mathayo 26:69-75.

Kama matokeo ya ukuzi huo wote wa kiroho, hesabu yetu ya rafiki inaongezeka. Hatimaye, tunakuta kwamba sisi ni wa jamaa kubwa sana ya rafiki duniani pote! Tunakuta pia kwamba kiwango cha ujumla cha rafiki zetu kinakuwa juu zaidi. Kwa mfano, Brian, mwaabudu mpya-mpya wa Yehova, anakumbuka kwamba waliokuwa rafiki zake walimwingiza katika kunywa na kutokujali mke na watoto wake. Lakini sasa yeye amejitolea sana jamaa yake. Kuhusu rafiki zake wapya walio wengi ambao wana imani ile ile katika Yehova, yeye anasema: “Mimi nikiwa na tatizo, najua kwamba naweza kuinua simu na kusema na ye yote wao, nao wangefurahi kusaidia.”

Alan alikuwa na rafiki ambao kwa kawaida maongezi yao yalikuwa juu ya magari na wasichana. Lakini yeye alikuta kwamba vichwa hivyo vya maongezi vlikuwa “vya bure tu na visivyofaa kitu” wakati alipopata rafiki wapya wengi, wapenda Yehova wenzake. Wao walimvuta sana Alan kwa “upendezi wa kujitakia wao wenyewe, ulio wa kweli na wenye upendo” ambao walimwonyesha yeye.

Rafiki Zetu Walio Bora Zaidi

Watu wote hao mmoja mmoja na mamilioni wengine wanakuwa jamaa isiyo ya kisiasa ya rafiki ulimwenguni pote, ambayo inavipita vipingamizi vyote vya kitaifa, kikabila, na kijamii—udugu wa kweli wa wanadamu, sawa na ule wa Wakristo wa kwanza-kwanza. (3 Yohana 14) Kifungo kile kile kilichovuta Ruthu na Naomi pamoja ndicho pia kinachounganisha jamaa hii, yaani, ibada safi ya Yehova Mungu. Wote wanatambua kwa unyenyekevu na shukrani kwamba Yehova na Yesu Kristo ndio rafiki zao walio bora zaidi.

‘Ati Mungu Mwenye Nguvu Zote na Mwanaye wawe rafiki?’ huenda wewe ukataka kujua. ‘Jambo hilo linawezekanaje? Je! hicho si kimbelembele?’ Basi, Biblia inasema: “Abrahamu alitia imani katika Yehova, . . . na yeye akaja kuitwa ‘rafiki ya Yehova.’” Kwa uhakika hizo zilikuwa fadhili zisizostahiliwa. Hata hivyo, Neno la Yehova linasema: “Mungu hupinga wenye kutakabari, lakini yeye anawapa fadhili zisizostahiliwa wale wanyenyekevu.”—Yakobo 2:23; 4:6, NW.

Labda watu fulani wanahisi wakiwa wenye dhambi mno wasistahili pendeleo hilo. Lakini Yakobo anaendelea kusema: “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili. Jidhilini mbele za Bwana [Yehova, NW], naye atawakuza.”—Yakobo 4:8, 10.

Yesu alisema: “Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.” Yeye alionyesha pia kwamba amri zilizo kubwa zaidi ni ‘kupenda Yehova Mungu kwa moyo wetu wote, nafsi yetu, na akili zote, na jirani yetu kama sisi wenyewe.’ (Yohana 15:14; Mathayo 22:37-40, NW) Tukifanya hivyo, tutakuwa na rafiki wengi wa kweli. Zaidi ya hilo, sisi tutastahili hivyo kupata pendeleo jingine kubwa—uzima wa milele katika dunia iliyosafishwa chini ya Ufalme wa Mungu. (Mathayo 6:9, 10) Kama vile Yesu alivyosema: “Amri yake [Yehova] inamaanisha uzima wa milele.”—Yohana 12:50, NW.

Je wewe utaruhusu Mashahidi wa Yehova wakusaidie? Kwa kuwa wao ni wenye urafiki kikweli, wana nia ya kukutembelea na kuzungumza jambo hili muhimu pamoja nawe bila malipo. Wao wanaweza kukusaidia uwe na rafiki wengi wa kweli.

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

Miongozo Fulani ya Urafiki wa Kweli

Uwe mchaguzi juu ya wale unaoshirikiana pamoja nao.

Pendezwa na wengine kwa uchangamfu, na uwe msikilizaji mwema.

Fanyeni mambo pamoja—mambo yenye kushirikiwa yanatia nguvu urafiki.

Uwe mnyofu, mkunjufu, na mwenye moyo mweupe nyakati zote.

Onyesha hisia-mwenzi na sikitikio wakati wengine wanapokuwa matatani.

Wakati rafiki wanapofanya makosa au kukuudhi wewe, uwe tayari kusamehe—hata “mpaka mara sabini na saba.”—Mathayo 18:22, NW.

Wakati rafiki wanapochongewa au kuchambuliwa bila sababu nzuri, uwe mshikamanifu na uwatetee.

Ibada ya Yehova inayoshirikiwa pamoja inatia urafiki nguvu kwa kadiri isiyopimika.

[Picha katika ukurasa wa 7]

Ruthu alikataa kumwacha Naomi kwa sababu urafiki wao ulikuwa na msingi imara wa kiroho. Je! wewe una rafiki za kweli za namna hiyo?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki