Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w87 10/15 kur. 4-7
  • Upendo kwa Mungu—Ile Kani ya Kuleta Mema ya Kiadili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upendo kwa Mungu—Ile Kani ya Kuleta Mema ya Kiadili
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Zile Amri Kumi—Kani ya Kuleta Mema
  • Upendo kwa Mungu Unamaanisha Nini?
  • Upendo kwa Mungu ni Kani ya Kuleta Mema
  • Upendo Haushindwi Kamwe
  • “Kumpenda Mungu Humaanisha Hivi”
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
  • Sheria ya Upendo Katika Mioyo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Mpende Mungu Anayekupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Maana ya Kumpenda Jirani Yetu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
w87 10/15 kur. 4-7

Upendo kwa Mungu​—Ile Kani ya Kuleta Mema ya Kiadili

WATU wenye kufikiri vizuri watakubali kwa utayari kwamba ukosefu wa adili unahitaji kuzuiwa. Kama vile mhudumu wa United Church of Canada alivyoeleza jambo hilo: “Matokeo yanakuwa ya kutisha sana wakati watu mmoja mmoja na jamii ya watu wanapopuuza sheria ya kiadili; vita, infleshoni, [kashifa], na machafuko ya utawala.” Kama ilivyoonyeshwa katika makala ambayo imetangulia, zile dini kubwa-kubwa za ulimwengu huu hazikuthibitika kuwa kani yenye nguvu ya kuleta mema ya kiadili. Kwa hiyo ikiwa sisi mmoja mmoja tunataka kuishi maisha za kiadili, lazima sisi tutegemea mamlaka nyingine kuandaa kani hiyo halafu tuwe na nia ya kuishi kwa kufuata mamlaka hiyo.

Mavutano ya mamlaka kuu hiyo yalionekana wazi katika kisa kimoja katika maisha ya Yusufu, msimamizi Mwebrania aliyeandikwa na mkuu mmoja wa makao ya kifalme katika Misri. Wakati aliposhawishwa na mke wa mkuu huyo kufanya ngono na yeye, Yusufu alipinga, akisema: “Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?” (Mwanzo 39:7-9) Kutambua mamlaka ya Mungu na kutamani kumpendeza yeye kulimpa Yusufu nguvu za kiadili kupinga utongozi wa mwanamke huyo.

Miaka mia mbili baadaye, taifa la Kiisraeli, wazao wa baba ya Yusufu, Yakobo, lilipokea zile Amri Kumi zikiwa sehemu ya Sheria waliyopewa kupitia Musa. Ijapokuwa kutotii kulileta uchukivu wa Yehova Mungu, kutii Sheria hiyo kulileta baraka za kimungu. Kwa hiyo amri hizo zilikuwa mwongozo wa kiadili kwa taifa hilo.

Zile Amri Kumi—Kani ya Kuleta Mema

Zile Amri Kumi zilikuwa kani yenye nguvu jinsi gani? Mavutano yazo yangali yakihisiwa hata katika karne hii ya 20. Katika 1962 aliyekuwa wakati huo gavana-mkuu wa New Zealand alisema: “Mimi nadhani watu fulani wanafikiri zile Amri Kumi zimekuwa kuukuu. Lakini huenda likawa ni jambo la maana sana kwamba kama sisi sote tungezishika kwa uaminifu leo, ile sheria ya kawaida ya nchi ingekuwa isiyohitajiwa.”

Hata hivyo, katika maongezi pamoja na mtawala mmoja kijana Myahudi, Yesu Kristo alionyesha kwamba jambo fulani zaidi ya kushika zile Amri Kumi lilihitajiwa. Mwanamume kijana huyu alikuwa ameuliza: “Ni wema gani ambao lazima mimi nifanye ili kupata uzima wa milele?” Wakati Yesu aliposema kwamba yeye anapaswa “kushika zile amri kwa kuendelea,” akiorodhesha amri fulani kati ya zile Kumi, mtawala huyo alijibu: “Mimi nimeshika zote hizo; ni nini bado ambacho mimi ninakosa?” Yesu alijibu: “Nenda uuze mali zako na uwape maskini na wewe utakuwa na hazina katika mbingu, na uje uwe mfuasi wangu.” Usimulizi unaendelea: “Wakati mwanamume kijana yule aliposikia usemi huo, yeye alienda zake akiwa na kihoro, kwa maana yeye alikuwa na milki nyingi.”—Mathayo 19:16-22, NW.

Ulinganisho wa usimulizi huo pamoja na mwingine unaofanana nao katika Luka 10:25-28 unatusaidia kutambua tatizo la msingi la mtawala kijana huyo. Tunasoma: “Mwanamume fulani mwenye ujuzi katika ile Sheria aliinuka, kujaribu yeye [ Yesu], na kusema: ‘Mwalimu, ni kwa kufanya nini mimi nitarithi uzima wa milele?’ “Yesu alimsaidia kusababu juu ya jambo hilo, na tokeo likawa kwamba, mwanamume huyo aliweza kujibu swali lake mwenyewe, akisema jambo linalofanana na hili: ‘Penda Yehova Mungu kwa moyo wako wote, nafsi, nguvu, na akili zote, na jirani yako kama wewe mwenyewe.’ Halafu Yesu alimalizia: “Endelea kufanya hilo na wewe utapata uzima.”

Je! wewe unaweza sasa kuona lile tatizo la mtawala kijana huyo aliyetangulia kutajwa? Upendo wake kwa Mungu na kwa jirani ulitiwa giza na upendo wake kwa milki za kimwili. Ilisikitisha kama nini! Ijapokuwa yeye alijaribu kushika zile Amri Kumi, yeye alikuwa katika hatari ya kupoteza uzima wa milele.

Upendo kwa Mungu Unamaanisha Nini?

Sisi tunaishi katika wakati ambapo upendo kwa Mungu na jirani umeng’olewa na mahali pao pakapandwa upendo kwa mtu binafsi, milki za kimwili, na ngono. Kwani, hata itikadi katika Mungu akiwa Muumba imeondolewa katika akili za wengi na mahali payo ikawekwa itikadi katika ile nadharia ya mageuzi isiyothibitishwa. Ni nini ambacho kimeleta yote hayo?

Kwa karne nyingi, viongozi wa kidini wa Jumuiya ya Wakristo walitumia lile fundisho lisilo la Kibiblia la moto wa mateso ambao unaogopesha sana katika jaribio la kutawala maadili ya watu. Encyclopedia International inasema: “Kani ambayo ni yenye nguvu zaidi ya watu wa kawaida kutenda mema katika muda wote wa zile Zamani za Kati bila shaka ilikuwa woga juu ya moto wa mateso, ambao ulifanya hata Wafalme na Watawala walitii mno Kanisa, na labda hicho tu ndicho kizuizi kilichokuwa juu ya tamaa kali zao zisizozuiwa.” Fundisho hilo la moto wa mateso lilifanyiza wazo la kwamba Mungu si mwenye upendo, si mwenye rehema, na anapenda kulipa kisasi. Hata ingawa fundisho hilo huenda likawa lilitenda kama kizuizi kwa watu fulani, liligeuza wengine wengi kutoka kwa Mungu, likiacha wao waweze kwa urahisi kushindwa na mafundisho na nadharia zisizo za Kimaandiko, kama ile ya mageuzi.

Hata hivyo, Biblia haifundishi kwamba Mungu anatesa-tesa nafsi katika moto wa mateso. Badala ya hivyo, mtume Yohana anatuambia: “Mungu ni upendo.” “Yeye ni mwaminifu na mwadilifu ili kusamehe sisi dhambi zetu.” Musa aliandika: “Yehova, Mungu mwenye rehema na mwenye neema, wa polepole kukasirika na mwingi katika fadhili za upendo na kweli.” (1 Yohana 4:8; 1:9, NW; Kutoka 34:6, NW) Hizo ni chache tu za sifa za ajabu za Mungu. Hizo zinavuta sisi kwake. Sifa hizo, hasa upendo wake, ndizo zinazofanya sisi tutake kupenda yeye. “Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.” (1 Yohana 4:19) Ni upendo huo kwa Mungu ambao ndio kani iliyo kubwa zaidi ya kuleta mema ya kiadili; huo unaweza kuongoza kwenye uzima wa milele!

Upendo wa kweli kwa Mungu si sifa tu isiyo na matokeo yenye kuonekana. Huu unasukuma mtu kutenda kwa masilahi ya mwingine. Mtume Paulo aliorodhesha njia nyingi ambazo upendo huo unaweza kuonyeshwa. kutaja chache tu: “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu.” (1 Wakorintho 13:4, 5) Kuonyesha kwetu upendo huo ni jaribio la kuiga Baba yetu wa kimbingu. Yesu alisema: “Amri mbili hizo [kupenda Mungu na jirani] zinajumlisha fungu zima la ile Sheria na wale Manabii.” (Mathayo 22:40, An American Translation) Kwa maneno mengine, ikiwa sisi tunaonyesha upendo huo, sisi hatutaiba kutoka kwa jirani yetu wala kuua yeye wala kufanya uzinzi pamoja na mke wake. Mtume Yohana alikubali akisema: “Huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake.”—1 Yohana 5:3.

Upendo kwa Mungu ni Kani ya Kuleta Mema

Angalia tokeo ambalo upendo kwa Mungu ulikuwa nalo juu ya Wakristo wa mapema, kama inavyoonyeshwa na Tertullian, wa karne ya pili. Yeye alitoa mwito wa ushindani kwa wapinzani wake waonyeshe Mkristo mmoja miongoni mwa wahalifu wao. Wakati wao waliposhindwa, yeye aliongeza: “Sisi, basi, ndio watu peke yetu ambao hatuna uhalifu.” Kitabu The Old Roman World kinaunga mkono maoni hayo, kikisema: “Sisi tuna ushuhuda kwamba maisha zao zilikuwa bila lawama, kwamba maadili yao yalikuwa yasiyoweza kusutwa.” Pia, Christianity Today kinataja Roland Bainton mwanahistoria wa kanisa kuwa akisema: “Kutoka mwisho wa kipindi kile cha Agano Jipya mpaka ule mwongo wa 170-180 hakuna ushuhuda wo wote wa Wakristo kuwa katika jeshi.” Upendo kwa Mungu ulisukuma hao kutii yeye kwa kuishi maisha za kiadili. Ingawa hivyo, huenda wewe ukataka kujua, ‘Je! kuna ushuhuda wa kani hiyo ya kiadili yenye mafaa leo?’

Kweli kweli ipo! Mchangia-habari za magazeti Mike McManus aliandika katika Herald & Review kwamba yeye hakuwa kamwe amesikia hata mara moja mahubiri dhidi ya ngono kabla ya ndoa. Mwezi mmoja baadaye yeye aliripoti kwamba miongoni mwa barua za majibu alizopokea ilikuwamo moja kutoka kwa kijana wa umri wa miaka 14, mmoja wa Mashahidi wa Yehova, ambaye aliandika: “Lile wazo tu la kupatwa na magonjwa hayo linapasa litoshe kuzuia watu walio wengi [wasifanye ngono kabla ya ndoa]. Lakini sababu inayofanya Mashahidi wajiepushe ni kwamba Yehova anatuamuru tukimbie uasherati.” (Italiki ni zetu.) Akieleza juu ya barua hiyo, McManus aliuliza: “Ni [vijana] wangapi wa miaka 14 katika kundi lenu ambao wangeweza kutaja maneno ya Mt. Paulo waziwazi hivyo (1 Kor. 6:18)?”

Kanuni ile ile ya kutii amri za Yehova, iliyotajwa na msichana huyo, inatumiwa na Mashahidi katika mambo mengine. Maana kuu ya amri fulani za Mungu zilizoandikwa katika Maandiko ni: ‘Uwe mnyofu katika mambo yote,’ ‘Epuka sanamu,’ ‘Jiepushe na damu na uasherati,’ ‘Uwe msema-ukweli,’ ‘Zoeza watoto wako katika njia za Mungu.’ (Waebrania 13:18; 1 Yohana 5:21; Matendo 15:29; Waefeso 4:25; 6:4) Je! wewe hujaona Mashahidi wa Yehova katika ujirani wako au mahali pa kazi wakijaribu kutii amri hizo? Je! wewe umepata kutaka kujua ni kwa sababu gani wao wanafanya hivyo, kwa sababu gani wao wanakataa kutiwa damu mishipani, kwa sababu gani wao wanakataa kwenda vitani, kwa sababu gani wao wanakutembelea wewe kwenye nyumba yako, kwa ufupi, kwa sababu gani wao ni tofauti? Upendo wao kwa Mungu ndilo jibu.

Upendo Haushindwi Kamwe

Wakitaka kupendeza Mungu, Mashahidi wa Yehova wanathamini moyoni shauri hili: “Mgeuzwe kwa kubadili akili zenu, ili mpate kujithibitishia wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.” (Warumi 12:2, NW) Wakati wao wanapojifunza “mapenzi ya Mungu” ni nini kwao, wao wanataka kufanya haya. Upendo wao kwa Mungu ndio kani inayosukuma tamaa hiyo. Je! wewe unahisi kwamba huo ni msisimuko usio wa akili nzuri, usio na mafaa kwa wakati wetu? Fikiri kidogo juu ya masimulizi ya kweli yanayofuata.

Kule nyuma katika 1963, José, wa São Paulo, Brazili, alianza kuishi pamoja na Eugênia, ambaye alikuwa tayari amefunga ndoa. Miaka miwili baadaye, wao walianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Kutokana na funzo hilo watu wawili hao walijifunza kwamba Mungu anataka kwamba “ndoa iheshimike miongoni mwa wote.” (Waebrania 13:4, NW) Wao waling’amua kwamba wao wanapaswa kufunga ndoa, lakini Brazili haikuwa na sheria ya talaka ambayo kwayo Eugênia angeweza kuwekwa huru kuolewa na José. Hata hivyo, katika 1977, wakati sheria ya talaka ilipopitishwa, mwanamke huyo alipeleka ombi la talaka, na katika 1980 wao wakaweza kufunga ndoa, wakitimiza matakwa ya Mungu. Upendo wao kwa Mungu ulipata thawabu.

Inire alikuwa amejaribu namna zote za dawa za kulevya katika New York. Mwanamume huyo aliishi pamoja na Ann, rafiki yake msichana. Akiwa katika uhitaji wa pesa, yeye aliagiza msichana huyo apeleke picha zake yeye mwenyewe kwa gazeti moja la wanaume linalojulikana sana. Msichana huyo alitolewa pesa nyingi sana ili akae akiwa uchi kabisa kwenye kipindi cha upigaji picha. Katika wakati uo huo, Inire alianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, na baadaye Ann akajiunga. Inire aliacha kutumia dawa za kulevya. Baada ya majuma matatu, wao, kwa kupenda kwao wenyewe, waliamua kufunga ndoa. Halafu, walipojifunza kutokana na Biblia kwamba ni lazima Mkristo avalie kwa kiasi, Ann aliamua kwamba kwa dhamiri yeye hangeweza kukubali kipindi kile cha upigaji picha, hata kama ni pesa ngapi zingetolewa. (1 Timotheo 2:9) Wewe unafikiri ni nini kilichosababisha mabadiliko hayo? Ann anasema kwamba wakati yeye alipong’amua kwamba kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova hakukuwa shauri la kujiunga tu na dini fulani bali kulitia ndani kuishi maisha ya kujitolea Mungu, yeye alijua ilimpasa kufanya mabadiliko kwa haraka. Kwa kweli, upendo kwa Mungu ni kani yenye nguvu ya kuleta mema.

Huenda mtu fulani akahisi, ‘Hivyo ni visa kimoja kimoja tu.’ Lakini sivyo. Mabadiliko yanayofanana na hayo yametukia mara nyingi katika mahali-mahali ambako Mashahidi wa Yehova ni watendaji. Kwa sababu gani usichungulie zaidi jambo hilo. Jithibitishie mwenyewe kwamba upendo kwa Mungu kama unavyoonyeshwa katika dini ya kweli ungali ndio ile kani ya kuleta mema ya kiadili.

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Kwa habari ya Wakristo wa mapema, kile kitabu “The Old Roman World” kinasema “Sisi tuna ushuhuda wa kwamba maisha zao zilikuwa bila lawama, kwamba maadili yao yalikuwa yasiyoweza kusutwa.”Ni nini ile kani iliyofanya wao wawe na “maadili yasiyoweza kusutuwa”?

[Picha katika ukurasa wa 7]

Upendo kwa Mungu unaweza kukusaidia wewe upinge usishawishwe na kuingia katika kufanya kosa

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki