Itibari Katika Yehova Inaongoza Kwenye Wakfu na Ubatizo
“Itibari katika Yehova na utende mema; kaa katika dunia, na ushughulike kwa uaminifu.”—ZABURI 37:3, NW
1. Ni ushuhuda gani wa watu wenye hekima ya kilimwengu unaoonyesha kwamba ni upumbavu kuitibari katika viongozi wa kibinadamu?
NIKATIKA nani sisi tunaweza kuitibari? Je! ni katika viongozi wa kibinadamu? Kumbukumbu ya matendo yao inaonyesha kwamba ni upumbavu kuitibari katika wanadamu wasiokamilika. Naam, hata watu wenye hekima ya kilimwengu wanatambua uhakika huo! Hivyo, gazeti Vision la Ulaya lililo la kibiashara lilisema wakati mmoja kwamba jambo “lililo baya kabisa juu ya hali ya sasa ni kwamba hakuna mtu anayeweza kuona njia ya kutoka humo.” Na Robert Heilbroner aliye mwanahistoria wa kiuchumi alisema: “Kuna jambo jingine ambalo linataka kutumomonyoa. Ni ile tuhuma ya kwamba hakuna mtu anayeiweza hali, kwamba hakuna mtu aliyetayarika kushughulika na matatizo ambayo yanatukumba sisi.”
2. Ni nini linaloweza kusemwa juu ya manufaa za sayansi ya ki-siku-hizi?
2 Ni kweli, wanadamu wamefanya maendeleo mengi katika nyanja mbalimbali za sayansi Lakini je! yote hayo yamekuwa yenye manufaa? Sivyo, hayakuwa. Kama ilivyoonyeshwa wazi mtungaji Lewis Mumford: “Lile wazo la kwamba maendeleo ya uundaji-vitu na ya kisayansi yalitoa uhakikisho kamili kwamba wanadai wangekuwa na ulinganifu katika manufaa ambazo wangepata... sasa limekuwa lisiloweza kushikiliwa hata kidogo.” Kielelezo kimoja mvua ya asidi, ambayo inatia uchafuzi katika maji ya maziwa na mito na inasaidia kuharibu miti kwa mamilioni. Waaidha, ile hali ya kusikitisha ya ulimwengu—lile ongezeko katika uhalifu jeuri, na uvamizi-haramu, katika uzoelevu wa kutumia dawa za kulevya na kileo, na katika magonjwa yenye kuambukiza kingono, na ile hali ya kutia wasiwasi wa kiuchumi—yote yanashuhudiza kwamba ni kazi-bure kutia itibari yetu katika viongozi wa kibinadamu.
3. Neno la Mungu linatoa shauri gani juu ya mahali ambapo inatupasa sisi tuweke itibari yetu?
3 Kwa kufaa sana Neno la Mungu linatushauri hivi: “Msitie itibari yenu katika washarifu, wala katika mwana wa binadamu wa dunia, ambaye kwake hakuna wokovu. Roho yake hutoka yeye hurudi kwenye udongo wake; katika siku hiyo fikira zake hupotelea mbali.” (Zaburi 146:3, 4, NW) Ni katika nani sisi tunaweza kutia itibari yetu, ikiwa si katika wanadamu? Sisi tunaweza kutia itibari yetu katika Muumba wa mbingu na dunia, kama vile tunavyosoma: “Mbarikiwa ni mwanamume yule kakawana ambaye anatia itibari yake katika Yehova, na ambaye Yehova amekuwa uhakika wake.”—Yeremia 17:7, NW.
Kwa Sababu Gani Tuitibari Katika Yehova?
4. Ni zipi zilizo sifa kubwa zaidi za Yehova, na ni jinsi gani hizo zinatupa sisi sababu zinazofaa za kutia itibari yetu katika yeye?
4 Sisi tunaweza kuitibari katika Yehova kwa sababu zinazofaa. Kwanza kabisa, sisi tunaweza kutia itibari yetu katika yeye kwa sababu ya sifa zake zilizo kuu—upendo, hekima, haki, na nguvu—na sifa nyingine zilizo nzuri ajabu. Neno lake linatuhakikishia kwamba yeye ni mweza-yote, kimoja cha vyeo vyake kikiwa ni “Mungu Mweza Yote.” (Mwanzo 28:3, NW) Huo ni msingi mzuri kama nini wa kuwa na itibari! Hakuna mtu ambaye anaweza kufanikiwa kumzuilia Yehova, na hakuna mtu ambaye anaweza kusukuma kando makusudi yake. Yeye ndiye yule Mmoja Mjua-Yote. Si kwamba tu anaujua mwisho kutoka mwanzo, huku wakati ujao ukiwa kitabu kilichofunguka mbele zake, bali pia ndani yake mnakaa maarifa na hekima, kama inavyoonwa na kazi zake za uumbaji zilizo nzuri ajabu. Yeye hajapata kamwe kufanya hata kosa moja katika shughuli zake. (Isaya 46:10; Warumi 11:33-35) Zaidi ya hilo, Yehova anastahili kuitibariwa kwa ukamilifu, Mungu wa uadilifu na uaminifu. Haiwezekani yeye kusema uwongo. (Kumbukumbu 32:4; Tito 1:2; Waebrania 6:18) Juu ya yote, kwa kuwa upendo usio na ubinafsi ndiyo sifa yake kubwa zaidi, inasemwa hivi kwa kufaa: “Mungu ni upendo.”—1 Yohana 4:8,16.
5. Neno la Mungu lina kumbukumbu gani, lenye kushuhudiza ustahili wake wa itibari?
5 Shughuli za Yehova pamoja na aina ya binadamu zinashuhudiza zaidi kwamba ni Mungu wa uweza-yote, hekima, haki, na upendo ambaye anastahili kuitibariwa. Musa alihakikishia Waisraeli kwamba Yehova anatunza agano na fadhili za upendo kuhusiana na wale ambao wanampenda na kutunza amri zake. (Kumbukumbu 7:9) Mapema zaidi, Yehova alihifadhi Noa mwogopa-Mungu na jamaa yake wakapita ile Gharika kuu. Mungu alikomboa Loti mwadilifu na binti zake wawili kutoka uharibifu wenye moto wa Sodoma na Gomora. Baadaye, Mungu alitoa Waisraeli Misri na kuwapa nchi ya Kanaani kwa kupatana na ahadi yake kwa Abrahamu. (Mwanzo 7:23; 17:8; 19:15-26) Na je! Yehova hakukomboa wale Waebrania watatu waliotupwa ndani ya ile tanuri yenye moto, na pia akamkomboa Danieli kutoka tundu la simba?—Danieli 3:27; 6:23.
6. Ni ithibati gani ya ki-siku-hizi tuliyo nayo kwamba kuweka itibari katika Yehova si kuiweka mahali pasipofaa?
6 Jambo la kwamba sisi tunaweza kuweka itibari yetu katika Yehova limeshuhudizwa pia na mambo yaliyoonwa na Mashahidi wake wa ki-siku-hizi. Mathalani, Adolf Hitler alijisifu kwamba yeye angeangamiza kabisa wale “vinyangarika” Mashahidi wa Yehova katika Ujeremani. Lakini badala ya hivyo Hitler na chama chake cha Nazi ndio walioangamizwa kabisa, na leo kikosi hicho cha Mashahidi kimezidika mara nyingi kikawa zaidi ya 119,000. Waaidha, mamia halisi ya masimulizi ya kimaisha kuhusu Mashahidi wa Yehova, ambayo yanachapishwa katika Mnara wa Mlinzi na Amkeni! gazeti jenzi la hilo, yanatoa ushuhuda wa kutosha kwenye uhakika wa kwamba kweli kweli Yehova ndiye Mungu ambaye sisi tunaweza kuitibari.
Sababu Inayofanya Watu Fulani Wasiitibari Katika Yehova
7. Kwa sababu gani mtu mmoja alisema alikuwa “Mtazamaji Asiyeshiriki wa Yehova”?
7 Hata hivyo, ni watu wachache kama nini wanaoitibari katika Yehova leo! Hata wengi ambao wamepata kujua juu ya sifa na matendo yake hodari wanashindwa kuweka itibari yao katika yeye. Makala moja iliyotokea katika jarida U.S. Catholic (Januari 1979) inasema hivi juu ya mtu mmoja wa namna hiyo: “Wakati mchunguza maoni ya watu alipouliza mwanamume huyo ni dini gani anayopendelea zaidi, yeye alijibu, ‘Nafikiri mimi ni Mtazamaji Asiyeshiriki wa Yehova.’ Alipoalikwa aeleze kwa urefu alisema, ‘Mimi naitikadi sana mambo ambayo Mashahidi wa Yehova wanaitikadi —lakini mimi sitaki kuhusishwa ndani.’” Gazeti hilo lilieleza hivi: “Shahidi wa Yehova aliyejitoa wakfu hana uchaguzi mwingine ila kujihusisha ndani kwa kina kirefu.”
8. Ni tabia gani za msingi zinazofanya mtu atake kuhusika katika kutumikia Yehova?
8 Ni kwa sababu gani watu fulani hawataki kuhusishwa ndani? Kwa sababu wao hawana hali ya moyoni inayofaa. Ni lazima mtu awe ‘kwa kufaa ana mwelekeo kwa ajili ya uzima wa milele.’ (Matendo 13:48, NW) Kama vile Yesu alivyosema katika mfano wake wa maneno juu ya mpanda-mbegu, wale wanaotokeza matunda wanapokea lile neno la ukweli ndani ya ‘mioyo mizuri na myema.’ (Luka 8:15, NW) Ndiyo, ukweli hauvuti watu wasio na weupe wa moyo. Takwa moja la msingi ni kuwa na moyo wa ufuataji haki. Pia ukweli wa Neno la Mungu hauvuti wale walio na kiburi. Mwelekeo wa unyenyekevu unahitajiwa. (Yakobo 4:6) Waaidha, ukweli hauvuti wenye kukinai mambo, wenye kujiona kuwa waadilifu. Lakini unavuta wale ambao wanafahamu uhitaji wao wa kiroho, wanaohisi njaa na kiu kwa ajili ya uadilifu, na ambao wanatweta na kupiga kite juu ya makuruhi yote wanayoona yakitendeka katika ulimwengu leo.—Mathayo 5:3, 6; Ezekieli 9:4, NW.
Itibari Katika Yehova Inaongoza Kwenye Wakfu
9, 10. (a) Ni jambo gani linalohitajiwa kabisa kabla mtu hajaweza kutia itibari katika Yehova, na wale walio na hali ya moyoni inayofaa wanaitikia jinsi gani? (h) Watu hao wanajizoeza imani katika nani?
9 Kabla mtu hajaweza kutia itibari katika Yehova, ni lazima yeye asikie juu Yake. Lakini “ni jinsi gani wao wataita yeye ambaye wao hawakuwa wametia imani katika yeye? Ni jinsi gani, tena, wao watatia imani katika yeye ambaye wao hawakuwa wamesikia juu yake? Ni jinsi gani, tena, wao watasikia pasipo mtu fulani wa kuhubiri?” (Warumi 10:14, NW) Wakati watumishi wa Yehova wanapohubiri wale walio na hali ya moyoni inayofaa wanaitikia, kama walivyofanya wengi katika Thesalonike wa kale. Kuhusu hao, Paulo aliandika hivi: “Wakati ninyi mlipopokea neno la Mungu, ambalo ninyi mlisikia kutoka kwetu, ninyi mlikubali hilo, si kuwa neno la wanadamu bali, kuwa neno la Mungu, sawa na vile hilo lilivyo kwa ukweli, ambalo linafanya kazi pia katika ninyi waitikadi.”—1 Wathesalonike 2; 13, NW.
10 Wanapojifunza juu ya Yehova, watu hao wenye mioyo myema wanajizoeza imani katika yeye. Hilo ni jambo muhimu, kwa maana “pasipo imani haiwezekani kumpendeza yeye vizuri, kwa maana yeye ambaye hufikia Mungu lazima aitikadi kwamba yeye yupo na kwamba yeye huwa mthawabishaji wa wale wanaotafuta yeye kwa bidii nyingi.” (Waebrania 11:6, NW) Jambo la umaana mkubwa pia ni kule kujizoeza imani katika Mwana wa Mungu, “Hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”—ndiyo, hakuna jina jinginelo lote isipokuwa lile la Yesu Kristo.—Matendo 4:12.
11. Itibari katika Yehova itasababisha mtu afuate shauri gani lililotolewa na mtume Petro?
11 Kuitibari katika Neno la Mungu, katika Yehova, na katika Yesu Kristo Mwana wake kutasukuma mtu atii lile shauri la mtume Petro kwa Wayahudi wa siku yake: “Tubuni, basi, na kugeuka ili mpate kufutisha dhambi zenu, kwamba majira ya kuburudisha yapate kuja kutoka kwa utu wa Yehova.” (Matendo 3:19, NW) Kwa kutwaa ndani maarifa ya Yehova na matakwa Yake, mtu anajifunza kwamba mapenzi ya Mungu ni kwamba yeye awe mfuasi wa Yesu Kristo. Ni kama vile Petro alivyoeleza jambo hilo: “Kwenye mwendo huu ninyi mliitwa, kwa sababu hata Kristo aliteseka kwa ajili ya ninyi, akiachia ninyi kiolezo ili ninyi mfuate kwa ukaribu hatua zake.” (1 Petro 2:21, NW) Yesu alielewesha wazi ni mambo gani yaliyohusika wakati aliposema: “Ikiwa mtu ye yote anataka anifuate mimi, acheni yeye akane kuwa wa yeye mwenyewe na kuinua mti wa mateso wake na kuendelea kunifuata mimi.” (Mathayo 16:24, NW) Hiyo inamaanisha kujitoa wakfu kuelekea Yehova Mungu ili kufanya mapenzi yake na kufuata hatua za nyayo za Yesu Kristo.
Wakfu Si Kujitia Katika Wajibu Wo Wote Ule
12. Mara nyingi maneno “kujitia katika wajibu” yanatumiwa jinsi gani katika Jumuiya ya Wakristo?
12 Katika Jumuiya ya Wakristo maneno “kujitia katika wajibu” yanatumiwa-tumiwa kuhusu kuwa Mkristo. Hivyo tunaambiwa kwamba Waevanjeliko wa United States “wanakazia kujitia katika wajibu wa kibinafsi kumwelekea Yesu.” Kiongozi mmoja wa kidini aliye Mkatoliki alisema juu ya “kujitia katika wajibu wa dini ya Kikatoliki.” Katika kutetea uhusika wake wa kisiasa, padri mmoja wa Kikatoliki alisema: “Kuingia katika siasa kulikuwa hatua ya kupanua wajibu wangu (wa kipadri).” Na mashirika ya kibiashara yanatangaza “Wajibu Wetu Kuelekea Wateja Wetu.” Kwa kweli, basi, mtu anaweza kujitia katika wajibu wa kufanya mambo mengi sana wakati ule ule mmoja: wajibu wa kibiashara, wajibu wa kijamii, wajibu wa kisiasa, na wajibu wa kidini.
13. Ni nini linalohusika katika wakfu kwa Yehova?
13 Hata hivyo, wakfu kwa Yehova Mungu si kujitia katika wajibu wo wote ule. Kwa urahisi, kujitia katika wajibu ni “mwafaka au ahadi nzito ya kufanya jambo fulani katika wakati ujao.” Lakini kujitoa wakfu kunamaanisha ‘kujitoa mwenyewe kuelekea utumishi au ibada ya mungu fulani au kuelekea matumizi yenye utakato bila kujihusisha na mambo mengine yo yote.’ Watu walio wengi wanatosheka kujitia katika wajibu fulani badala ya kujitoa wakfu. Bila shaka hiyo inaonyesha ni kwa sababu gani wanafuata dini yao kwa kufifia kama muziki unaodunda kwa sauti isiyosikika sana. Kuusikiliza kunafurahisha, lakini huo hauvurugi shughuli yo yote ambayo mtu anataka kufanya.
14. Kwa sababu gani kujitia tu katika wajibu fulani si jambo linalokubalika kwa Yehova Mungu?
14 Wakfu kwa Mungu unafanya kutenda mapenzi yake kuwe jambo lililo la maana zaidi maishani. Huo unataka mtu ashike ile amri ya kwanza iliyo kubwa zaidi, ambayo Yesu alitaja aliposema: “Ni lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo mzima wako wote na kwa nafsi nzima yako yote na kwa akili nzima zako zote na kwa imara nzima yako yote.” Yesu alikazia ile hali ya kutohusisha mambo mengineyo yote katika kutumikia Mungu, aliposema: “Hakuna mtu ambaye anaweza kuwa mtumwa kwa ajili ya mabwana-wakubwa wawili; kwa maana ama yeye atachukia yule mmoja na kupenda yule mwingine, au yeye atashikamana na yule mmoja na kudharau yule mwingine. Ninyi hamwezi kuwa watumwa kwa ajili ya Mungu na kwa ajili ya Mali.” (Marko 12:30; Mathayo 6:24, NW) Kwa uwazi, basi, kujitia tu katika wajibu fulani si jambo linalokubalika kwa Yehova.
Kwa Sababu Gani Kuwe na Uzamisho Katika Maji?
15. Ni kielelezo gani ambacho Yesu aliweka juu ya kufanya wonyesho wa peupe wa imani katika Mungu?
15 Kwa sababu gani mtu aonyeshe wakfu kwa Mungu kupitia kubatizwa? Ikiwa mtu anataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, yeye hana budi kubatizwa. Hivyo ndivyo ilivyo ikiwa yeye anatamani kujulikana kuwa Mkristo, mfuasi wa Yesu Kristo. “Shahidi Mwaminifu” wa Yehova, Yesu, aliweka kigezo cha jambo hilo, kwa maana yeye alibatizwa katika Mto Yordani. Kwa kuwa Yohana alikuwa akibatiza watenda dhambi wenye kutubu, yeye hakuweza kuelewa ni kwa sababu gani Yesu alitaka kubatizwa, lakini Yesu alimwambia: “Acha iwe hivyo, wakati huu, kwa maana katika njia hiyo inafaa sisi tutekeleze yote yaliyo ya uadilifu.” (Ufunuo 1:5; Mathayo 3:13-17, NW) Hivyo Mwana wa Mungu alifanya wonyesho wa peupe wa imani yake kwa kujitokeza mwenyewe kwa Yehova, akiweka kielelezo kwa wote wale wanaotamani kufanya mapenzi ya kimungu.
16. Ni amri gani ambayo Yesu aliwapa wafuasi wake kuhusu ubatizo, na ni nini kinachoonyesha kwamba wanafunzi wake walitii amri hiyo?
16 Zaidi ya hilo, muda mfupi kabla ya kurudia Baba yake katika mbingu, Yesu aliamuru wafuasi wake: “Kwa hiyo nendeni mkafanye wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote, kuwabatiza katika jina la Baba na la Mwana na la roho takatifu, kuwafundisha kushika mambo yote ambayo nimewaamuru ninyi.” (Mathayo 28:19, 20, NW) Kumbukumbu ya maandishi yaliyo katika kitabu cha Matendo inaonyesha kwamba wanafunzi wa Yesu walitii amri hiyo kwa bidii.—Matendo 2:40, 41; 8:12; 9:17, 18; 19:5.
17. Kwa sababu gani mnyunyizo tu wa maji hauwezi kuwa ubatizo halali?
17 Hao walibatizwa jinsi gani? Je! ni kwa kunyunyiziwa maji, kama ilivyo desturi katika makanisa yaliyo mengi ya Jumuiya ya Wakristo? Hata kidogo! Yesu ‘alikuja juu kutoka ndani ya maji’ baada ya kubatizwa. Hiyo inaonyesha wazi kwamba yeye alizamishwa katika maji. (Marko 1:9, 10, NW) Kwa kweli, hakuna jambo jinginelo lingekuwa ni ubatizo, kwa maana neno la Kigiriki linalotafsiriwa “batiza” linamaanisha ‘kuchovya ndani, kutumbukiza.’ —Matendo 8:36-39.
18. Kwa sababu gani uzamisho ni ufananisho unaofaa sana wa wakfu wa mtu kwa Mungu?
18 Ubatizo huo ni ufananisho unaofaa sana wa wakfu. Kwenda chini ya maji kunafananisha vizuri kufa kwa mtu kuelekea mfuatio wa mwendo wake wa zamani. Kuinuliwa kwake juu kutoka ndani ya maji kunafananisha kuinuliwa aje kwenye njia mpya ya uhai. Hata kama vile sherehe ya arusi inavyosaidia kutia mkazo juu ya bibi-arusi na bwana-arusi kwamba wamo katika hali ya kufunga ndoa, ndivyo kuzamishwa katika maji mbele ya mashahidi kutakavyoelekea kuwa na umaana wa daima juu ya mtaka-ubatizo. Hakuna swali: Kwa kile kitendo cha kubatizwa, wakfu wa mtu kwa Yehova unapasa kukazwa kikiki katika akili na kumbukumbu ya mtu kuwa ndilo tukio la maana zaidi katika uhai wake. Hilo linakuwa alama ya mgeuko wa kuacha kujitumikia mwenyewe aanze kutumikia Yehova Mungu.
19. Ni nini sababu zaidi ya kubatizwa?
19 Na tusisahau uhakika wa kwamba ubatizo katika maji ni jambo linalotakwa kabla ya kupata dhamiri njema kuhusiana na Yehova. Jambo hilo linaeleweshwa wazi kwenye 1 Petro 3:21 (NW), ambayo inasomwa hivi: “Lile linalolingana na hili pia linaokoa ninyi sasa, yaani, ubatizo, (si kuondolewa kwa uchafu wa mwili, bali ombi linalotolewa kwa Mungu ili kupata dhamiri njema,) kupitia ufufuo wa Yesu Kristo.”
Wabatizwe Kwenye Umri Gani?
20. Kwa sababu gani vitoto vichanga havingefaa ubatizo?
20 Maneno ya Yesu kwenye Mathayo 28:19, 20 yanaonyesha kwamba ni wale ambao wamefanywa kuwa wanafunzi wake wanaopaswa kubatizwa. Kwa sababu hiyo, inakuwa kwamba hakuna kitoto kichanga au mtoto mdogo angeweza kutimiza yale matakwa ya Kimaandiko kuhusu ubatizo. Kitoto kichanga hakingeweza kujizoeza imani katika Neno la Mungu, katika Mungu Muumba, na katika Yesu Kristo Mwana wake. Kitoto kichanga hakingeweza kuelewa kwamba roho takatifu ni kani ya utendaji ya Mungu; wala hakingeweza kutubia dhambi za wakati uliopita na kufanya nadhiri nzito kutenda mapenzi ya Mungu.
21. Je! inafaa vijana wabatizwe?
21 Lakini inaonekana kwamba wengine miongoni mwa watu wa Yehova wamepita kiasi upande ule mwingine. Wazazi wengi Wakristo wanaacha watoto wao wangoje mpaka wanapoingia miaka ya mwisho-mwisho wa utineja kabla ya kuzungumzia ile habari ya ubatizo. Tena na tena, sisi tunasikia juu ya watoto wanaofanya wakfu halali kwa kujichukulia hatua wao wenyewe. Mathalani, mwana asiyefikia umri wa utineja, wa mzee mmoja, alitaka kubatizwa kwa weupe wa moyo. Kwa hiyo baba yake aliomba wazee wengine watatu wazungumze pamoja na mtoto huyo maswali yale yaliyokusudiwa wale wanaofikiria ubatizo.a Walikata shauri kwamba, ingawa alikuwa wa umri mdogo sana, yeye alistahili kubatizwa kuwa mhudumu mwagizwa-rasmi wa Yehova Mungu. Ala, hivi majuzi msichana wa miaka kumi alibatizwa alihudhuria Shule ya Utumishi wa painia katika Bahamas, akiwa ni binti ya wahudumu wawili wa wakati wote!
22. Wakati wazazi wanapojenga nyutu za Kikristo katika watoto wao, wao wanaweza kutazamia nini kwao?
22 Katika habari hii, inaonekana kwamba wazazi fulani wanapungukiwa. Ni kwa kadiri gani wao wanatumia ‘vifaa visivyoweza kushika moto’ ili kujenga nyutu za Kikristo katika watoto wao? (1 Wakorintho 3:10-15, NW) Kwanza kabisa, kufanya hivyo kunataka kwamba ibada safi ya Yehova iwe jambo lililo la maana zaidi katika maisha za wazazi. Kuongezea hilo, ni lazima wazazi wawe wanatii lile shauri zuri lililotolewa kwenye Kumbukumbu 6:6, 7 na Waefeso 6:4. Tokeo la kufanya hivyo huenda likawa kwamba wazazi hao watahitaji kuzuia watoto wao wasibatizwe mapema mno, badala ya kuja kuwa na uhitaji wa kuwafunza-funza baadaye.
23. Mtu akiisha kufikia hatua ya wakfu na ubatizo, ni jambo gani jingine linalotakwa?
23 Mtu akiisha kuonyesha itibari yake katika Yehova kupitia wakfu na ubatizo katika maji, ni lazima yeye aendelee kuonyesha itibari hiyo. Makala inayofuata, “Kutumikia Yehova Tukiwa Wafanya Kazi Wenzake Wenye Kuitibari,” itatusaidia tuthamini ni mambo gani yanayohusika.
Wewe Ungejibu Jinsi Gani?
◻ Ni mambo gani ya uhakika ambayo yanakazia upumbavu wa kutia itibari yetu katika wanadamu?
◻ Kwa sababu gani sifa na shughuli za Yehova zinatupa sisi sababu zinazofaa za kuitibari katika yeye?
◻ Kwa sababu gani kutia itibari katika Yehova kunataka wakfu wala si kujitia katika wajibu fulani tu?
◻ Ni jinsi gani wazazi wanaweza kukaza kikiki katika watoto wao ile tamaa ya kujiweka wakfu kwa Yehova wakiwa kwenye umri wa mapema?
[Maelezo ya Chini]
a Mfululizo wa maswali ya kujibiwa na wote wanaotaka kubatizwa kuwa Mashahidi wa Yehova yanapatikana katika kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu. Kinafanywa kiwepo kwa wale wanaojitayarishia ubatizo.
[Maswali ya Funzo]
[Picha katika ukurasa wa 10]
Sisi tunaweza kuweka itibari yetu katika Yehova akiwa ndiye Mkombozi Mkuu