Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 7/1 kur. 4-6
  • Sababu za Ziada za Kuwa Mwenye Shukrani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sababu za Ziada za Kuwa Mwenye Shukrani
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Miponyoko Miwili Kutoka Kwenye Kifo
  • Mbinu za Mungu Zenye Kutazamisha za Kupigana
  • Ushukuru wa Muda Mfupi Tu
  • “Mjionyeshe Wenyewe Kuwa Wenye Shukrani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Kwa Nini Kuwa Mwenye Shukrani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • “Mjionyeshe Kuwa Wenye Shukrani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Kuvuka Bahari Nyekundu (ya Shamu)
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 7/1 kur. 4-6

Sababu za Ziada za Kuwa Mwenye Shukrani

WATU wa Israeli ya kale walikuwa na sababu zaidi ya wengineo za kuonyesha ushukuru kwa Muumba. Kwa nini tunaweza kusema hivi?

Basi, kama wanadamu wengine wote, Waisraeli walikuwa na sababu ya kuwa wenye shukrani kwa ajili ya vitu vyenye uzuri na vya ajabu vilivyoumbwa na Mungu. Lakini wao walikuwa na sababu ya ziada ya shukrani kwa sababu Mwenye Nguvu Zote alikuwa amewachagua wawe watu wake wa pekee na kuwafanyia utunzaji hususa. (Amosi 3:1, 2) Fikiria baadhi ya sababu zao za kutokeza za ushukuru.

Miponyoko Miwili Kutoka Kwenye Kifo

Ni lazima wazazi wote Waisraeli wawe walikuwa wenye shukrani kama nini usiku wa Nisani 14, 1513 K.W.K.! Katika usiku huo wa maana sana, malaika wa Mungu alileta kifo kwa “kila mzaliwa wa kwanza katika bara la Misri, kuanzia binadamu mpaka hayawani.” Lakini yeye alipita juu ya nyumba za Kiisraeli ambako damu ya wanyama wa Kupitwa ilikuwa imenyunyizwa kwenye miimo ya milango na vizingiti. Ule utulivu-tuli ulivurugwa kwa kuwa “kulianza kuinuka mpalizo mkuu wa kilio miongoni mwa Wamisri, kwa sababu hakukuwa na nyumba moja ambako hakukuwa na mtu mfu.” Hata hivyo, mzaliwa wa kwanza mwenye thamani kubwa wa kila nyumba ya Kiisraeli alikuwa hai na mzima.​—Kutoka 12:12, 21-24, 30, NW.

Si muda mrefu baada ya hapo, lazima ushukuru uwe ulijazana katika mioyo ya Waisraeli waliposhuhudia hatua ya Yehova kujiingiza kimwujiza wakati walipoonekana kama kwamba wamenaswa mtegoni katika fuo za Bahari Nyekundu, huku jeshi la Farao wa Misri likiwafuatia kweli kweli. Kwanza, wao waliona ile nguzo ya wingu iliyokuwa ikiwaongoza ikienda nyuma yao, ikifaulu kupunguza-punguza mwendo wa wafuatiaji. Ndipo Waisraeli walipoona Musa akinyoosha mkono wake juu ya bahari, na wakatazama kwa kustaajabu huku Mungu akisababisha upepo-mashariki wenye nguvu nyingi uvume usiku kucha, ukipasua yale maji na kugeuza bonde la bahari liwe udongo mkavu. Waisraeli hawakuhitaji himizo kubwa ili wafanye haraka kupita katika mpitio huu wa kuponyokea ulioandaliwa kwa njia ya kimungu.

Ingawa hivyo, sasa kukawa na kisababishi kipya cha kugutusha! Wamisri walimiminika ndani ya sakafu ya bahari, wakiwa na uhakika wa kufikilia Waisraeli. Lakini tazama! Wakati Wamisri wote walipokuwa katika kile kipitio chenye kuta za maji, magurudumu yalianza kutoka katika magari-farasi yao, na baada ya muda mfupi kukawa na machafuko makubwa. Ndipo, Waisraeli wote wakiwa salama kwenye ufuo ule mwingine, Yehova akaambia Musa tena anyooshe mkono wake, “na bahari ikaanza kurudi kwenye hali yayo ya kawaida kwenye ukaribio wa asubuhi.” Tokeo lilikuwa nini? Hakuna hata mmoja wa kani ya kijeshi ya Farao yenye kutunukwa sana aliyeponyoka asizame, wala mtawala huyo mwenyewe mwenye kiburi. (Kutoka 14:19-28, NW; Zaburi 136:15) Je! wewe unaweza kuwazia jinsi Waisraeli hao wakombolewa walivyokuwa wenye shukrani kwa Yehova?

Mbinu za Mungu Zenye Kutazamisha za Kupigana

Ingawa walikuwa wenye shukrani kwa ukombolewa wao kutoka Misri na kupita kwao kusikosahaulika katika Bahari Nyekundu, Waisraeli wangeelekeana na maono mengi ya kuwatoa jasho kabla ya kufika kwenye Nchi ya Ahadi. Lakini kila ono la ile safari yao ya mkokoteko wa miaka 40 katika jangwa lingalipasa kuwa sababu ya ziada ya kuwa na shukrani za pekee kwa Yehova.

Hatimaye, Waisraeli walivuka Mto Yordani na wakawa katika bara ambalo Mungu alikuwa amewapa. Baada ya muda mfupi wao walishuhudia kielelezo cha mbinu zenye kutazamisha za Yehova za kupigana. Jinsi gani? Ni kwa utekwa na uharibifu wa kustaajabisha wa jiji la kwanza la Kikanaani ambalo wao walikuta—Yeriko! (Yoshua, sura 6) Ile mbinu ya kivita iliyoelekezwa na Mungu ili wapige miguu kuzunguka Yeriko huku wakiwa wamebeba sanduku la agano ilikuwa isiyo ya kikawaida kama nini! Kwa siku sita mfululizo, wao walipiga miguu kuuzunguka ukuta mara moja-moja kila siku. Siku ya saba, walizunguka ukuta mara saba. Makuhani walipopuliza pembe zao, Waisraeli walijaza hewani “mlio mkuu wa vita,” na “ule ukuta ukaanza kuanguka chini tambarare”! (Mstari 20, NW) Ni nyumba ya Rahabu tu na kisehemu cha ukuta uliokuwa chini yayo iliyobaki imesimama. Ukuta wa jiji hili lenye kuonekana kama lisilopenyeka ulikuwa umeanguka bila uhitaji wa Yoshua na jeshi lake kutupa hata mshale mmoja! Kwa uhakika, ono hilo kule Yeriko lilikuwa sababu ya ziada yenye kutokeza, ya kuwa wenye shukrani kwa Mungu.

Katika pindi nyingine, kulikuwa na wonyesho mwingine wa kutokeza wa mbinu za Yehova zenye kutazamisha za kupigana. Wakati watu wa Gibeoni walipofanya amani pamoja na Waisraeli, wafalme watano Waamori walitangaza rasmi vita juu ya Wagibeoni. Yoshua alikuja kuwasaidia, na mkono wa kimwujiza wa Yehova ukaonyeshwa-onyeshwa katika pigano lililofuata. Mungu alitupa Waamori katika vuruguvurugu, na “wakati wao walipokuwa wakikimbia kutoka mbele ya Israeli na wakiwa katika mshukio wa Beth-horoni, Yehova alivurumisha kutoka kwenye mbingu mawe makubwa juu yao mpaka kule mbali Azeka, hivi kwamba wao walikufa.” Wengine zaidi walipatwa na kifo kutokana na hayo mawe-barafu kuliko wale waliouawa na Waisraeli kwa upanga.​—Yoshua 10:1-11.

“Mbele ya macho ya Israeli,” ndipo Yoshua aliponena kwa Yehova na kusema: “Jua, uwe bila kusonga juu ya Gibeoni, na, mwezi, juu ya uwanda wa chini ya Aijaloni.” Tokeo lilikuwa nini? “Kulingana na hilo,” unasema usimulizi huo, “jua liliendelea bila kusonga, na mwezi ulifanya kusimama tuli, mpaka taifa likawa lingeweza kufanya mlipizo-kisasi juu ya adui zalo.”​—Yoshua 10:12, 13, NW.

Ni matukio ya kushangaza kama nini! Na ni sababu zaidi za kutokeza kama nini za kuwa na ushukuru kwa upande wa watu wa Yehova!

Ushukuru wa Muda Mfupi Tu

Baada ya kila udhihirisho wa kujiingiza kwa Yehova, Waisraeli walijawa na ushukuru. Inaelekea kwamba, kila Mwisraeli alisema katika moyo wake kwamba hangesahau kamwe mambo aliyokuwa ameona. Hata hivyo, ushukuru huo ulikuwa wa muda mfupi kwa njia ya ajabu. Tena na tena, Waisraeli walionyesha mwelekeo wa kukosa ushukuru. Hivyo, Mungu “aliwapa-wapa ndani ya mkono wa mataifa, kwamba wale wanaowachukia waweze kutawala juu yao.”​—Zaburi 106:41, NW.

Hata hivyo, Yehova alionyesha roho yake ya ukarimu wa kusamehe wakati Waisraeli walipoingia katika shida kubwa, wakatubu juu ya mwendo wao usiofaa na usio wa shukrani, na kumwitia wapate msaada. “Yeye angeona taabu kubwa yao wakati yeye aliposikia kilio chao cha kunasihi. Na yeye angekumbuka kwa habari yao agano lake, na yeye angehisi majuto kulingana na wingi wa fadhili-upendo zake zilizo adhimu.” (Zaburi 106:44, 45, NW) Wakati baada ya wakati, Mungu wao mwenye kusamehe aliwafungua kutoka kwenye waonevu na kuwarudisha ndani ya upendeleo wake.

Ujapokuwako ustahimilivu wa Mungu na kutuma-tuma kwake wanabii ili wakarekebishe kufikiri kwao, Waisraeli walithibitika kuwa wasiorudika. Mwishowe, saburi ya Yehova iliisha, naye akaruhusu taifa la Yuda lishindwe na Wababuloni katika 607 K.W.K. Wale ambao hawakuuawa na kani za Mfalme Nebukadreza walichukuliwa mateka Babuloni.

Ulikuwa mwisho wenye msiba kama nini kwa sababu ya kukosa-kosa ushukuru na ushikamanifu kwa Mungu! Na jambo hili lilitukia ijapokuwa kulikuwa na wingi wa sababu za kuwa wenye shukrani.

Wakristo wanaweza jinsi gani kuepuka kosa hilo hilo la kutoonyesha ushukuru kwa ajili ya yote ambayo Yehova Mungu amewafanyia, kwa kadiri inayozidi sana vitendo vya wema ambavyo amefanyia aina ya binadamu kwa ujumla? Tunaacha jambo hili lifikiriwe katika makala inayofuata.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki