Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 8/1 kur. 27-29
  • Fadhili Zisizostahiliwa za Mungu Usikose Kusudi Lazo!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fadhili Zisizostahiliwa za Mungu Usikose Kusudi Lazo!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kusudi la Mungu Latambulishwa
  • Kielelezo cha Kale
  • Kusudi la Kukombolewa Kwetu
  • ‘Usikose Kusudi Lazo’
  • Tunathamini Kupokea Fadhili Zisizostahiliwa za Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Eneza Habari Njema za Fadhili Zisizostahiliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Mmewekwa Huru kwa Fadhili Zisizostahiliwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Pendeza Yehova kwa Kuonyesha Fadhili
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 8/1 kur. 27-29

Fadhili Zisizostahiliwa za Mungu Usikose Kusudi Lazo!

“KUONGEA juu ya dini. . . kwa kweli ni kazi ya mchungaji,” akataarifu mshiriki mmoja wa kanisa. (Italiki ni zetu.) Wengine wamekiri kwamba, “Kwa kulinganisha ni Wakristo wachache wanaofanya jitihada ya kushiriki imani yao pamoja na wengine.” (Italiki ni zetu.) Taarifa kama hizo zinakazia kwa uwazi kwamba kwa walio wengi wa waenda-kanisani, Ukristo ni kitu kinachozidi kidogo tu kuwa na itikadi isiyo na utendaji katika Mungu na katika Kristo kuwa ndiye Mesiya.

Rai yako wewe ni nini? Wanafunzi wa Yesu walishiriki imani yao pamoja na wengine. (Luka 8:1) Je! inawapasa Wakristo leo wafanye hivyo hivyo? Au ikiwa Mungu hatoi tena takwa la kwamba wenye kudai kuwa ni Wakristo wawe waeneza-evanjeli, yeye anatazamia nini kwao? Je! Mungu ana kusudi fulani kwa Wakristo leo? Ndiyo! Na kwa sababu hii, onyo la mtume Paulo kwa Wakristo Wakorintho ‘kutokubali fadhili zisizostahiliwa za Mungu na kukosa kusudi lazo’ lina maana kwetu. (2 Wakorintho 6:1, NW) Acheni tuone ni kwa nini.

Kusudi la Mungu Latambulishwa

Kama Paulo, Wakristo Wakorintho walikuwa wameikubali dhabihu ya ukombozi ya Yesu Kristo. Kwa sababu ya imani yao katika uandalizi huu, Yehova aliwatangaza kuwa waadilifu. Kukubali kwao kweli za Kimesiya walizopokea kupitia huduma ya Paulo kuliwakomboa kutoka kwenye utumikisho wa mazoea yale bandia, ya kipagani na yasiyo ya adili, ambayo yalifanya Korintho wa kale uwe na sifa mbaya. Hata hivyo, je! fadhili zisizostahiliwa hizo zilikuwa bila kusudi?

Sivyo. Bali, kusudi la Yehova la kuwakomboa lilikuwa kusudi lile lile lililofanya akomboe Paulo kutoka kwenye mapokeo yasiyo ya Kimaandiko ya baba za Paulo. Paulo mwenyewe anaelewesha wazi kusudi hilo: “Mimi nikawa mhudumu wa jambo hili kulingana na kipaji cha bure cha fadhili zisizostahiliwa za Mungu ambazo zilipewa kwa mimi . . . kwamba mimi nipaswe kutangaza kwa mataifa habari njema juu ya mautajiri yasiyopimika kina ya Kristo.” (Waefeso 3:7, 8; linganisha Wagalatia 1:15, 16, NW.) Ndiyo, kusudi la fadhili zisizostahiliwa za Mungu lilikuwa kwamba watumishi wake wapaswe kuinua juu ibada ya kweli​—wakikweza jina lake, Yehova, na kulijulisha katika huduma ya Kikristo, sawa na vile Paulo alivyofanya.​—Warumi 10:10.

Hata hivyo, wakati Paulo alipoandika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho, ilionekana wazi kwamba wengi wao walikuwa wamekosa kusudi la fadhili zisizostahiliwa za Mungu. Jinsi gani hivyo? Badala ya kudumisha namna fulani ya ibada iliyokuwa safi na yenye kukubalika katika mwono wa Mungu, wao walikuwa wameruhusu uvutano usio wa kiadili wa wakaaji wa Korintho utie utepetevu katika hisia zao za kufikiri. Mafarakano na uasherati pia yalikuwa yameripotiwa miongoni mwao. (1 Wakorintho 1:11; 5:1, 2) Walio wengi wa wale wenye kufanya ushirika pamoja na kundi walirekebishwa upya na shauri la Paulo. Hata hivyo, Paulo hakutaka vivuta-fikira zaidi viwavute kutoka kwenye huduma ya Kikristo. Kwa sababu hiyo, baadaye aliwakumbusha ‘wasikubali fadhili zisizostahiliwa za Mungu na kukosa kusudi lazo.’​—2 Wakorintho 6:1, NW.

Kielelezo cha Kale

Hali inayofanana na hii ilikuwa imetukia karne kadhaa mapema. Katika masika ya 537 K.W.K., Yehova Mungu alifungua taifa lake chaguliwa la Israeli kutoka kwenye utekwa wa Kibabuloni kwa kutumia Sairasi mfalme Mwajemi. Kusudi la kukombolewa kwao lilitambulishwa na Sairasi mwenyewe katika uamuzi-rasmi unaofuata: “Mtu ye yote aliye miongoni mwa ninyi kati ya watu wake wote, Mungu wake na athibitike kuwa pamoja naye. Kwa hiyo acheni huyo apande juu kwenda Yerusalemu, ulio katika Yuda, na kujenga upya ile nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli.”​—Ezra 1:1-3, NW.

Ndiyo, ulikuwa wakati uliowekwa rasmi wa Yehova kurudisha ibada ya kweli kwenye bara la Yuda. Kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa za Yehova, Wayahudi hao waliorudishwa kwenye nchi ya kwao walikuwa na pendeleo la kujenga upya hekalu katika Yerusalemu. Wakikubali mwito huo wa ushindani, wahamishwa waliorudishwa walitulia katika nchi ya maskani yao na wakaanza kazi ya kulirudisha hekalu.​—Ezra 1:5-11.

Hata hivyo, katika muda mfupi, taifa hili la Kiyahudi lililorudi liliruhusu upinzani wa nje uvuruge kazi yao. Badala ya kuweka kusudi la kukombolewa kwao likiwa limekazika wazi katika akili, wao walianza kusema: “Wakati haujaja, wakati wa nyumba ya Yehova, ili hiyo ijengwe.” (Hagai 1:2, NW) Kama tokeo, kazi ya kujenga upya iliachwa kabisa kwa karibu miaka 16.

Kwa wakati huo, wao walijishughulisha na mifuatio ya ubinafsi, wakitia mkazo zaidi juu ya vitu vya kimwili, starehe za kimnofu, kuliko juu ya kujenga upya nyumba takatifu ya Yehova. (Hagai 1:3-9) Kwenye Hagai 1:4 NW, tunasoma hivi: “Je! ni wakati wa ninyi wenyewe kukaa katika nyumba zenu zilizotiwa mapambo ya ukutani, hali nyumba hii ni ukiwa?” Nyumba ya Yehova ya ibada ilikuwa ikilala “ukiwa,” ikiwa na msingi tu, huku Wayahudi wakiwa wanaishi katika nyumba zao zilizotiwa paa nzuri pamoja na kuta zilizotiwa mapambo mazuri kwa mbao nzuri sana.

Kupitia Hagai na Zekaria wanabii wake, Yehova alikumbusha Wayahudi juu ya kusudi la kukombolewa kwao, na kazi ya kujenga upya ilikamilishwa mwishowe. Hata hivyo kwa uwazi watu wowote ambao waliendelea kuziona mali za kimwili kuwa za kustahiwa zaidi ya lile pendeleo la kuona ibada ya kweli ikirudishwa katika Yerusalemu walikosa kusudi la fadhili zisizostahiliwa za Mungu.

Kusudi la Kukombolewa Kwetu

Sisi tunaweza kujifunza nini leo kutokana na kielelezo cha Wayahudi waliorudishwa nchini mwao katika 537 K.W.K. na kutokana na Wakristo Wakorintho wa siku ya Paulo? Sisi tulio watumishi walio wakfu wa Yehova Mungu, tumepata pia ukombolewa fulani. Kupitia fadhili zisizostahiliwa zake, sisi hatutumikishwi tena kwenye mafundisho bandia na mapokeo ya Babuloni Mkuu au kwenye uovu wa mfumo huu wa kale wa mambo. (Yohana 8:32; 2 Wakorintho 4:4-6) Ukombolewa huo, na pia uhuru unaoletwa nao, unatupa sisi fursa ya kuonyesha Mungu uthamini kwa upendo wake kwetu. (1 Yohana 4:9) Jinsi gani?

Kwa kutokosa kwetu kusudi la fadhili zisizostahiliwa za Mungu. Iko kama vile tu ilivyokuwa kwa watumishi hao wa mapema wa Yehova, kwamba inatupasa kuinua juu ibada ya kweli. Leo, kama katika siku ya Paulo, hii inamaanisha kwamba inatupasa ‘kutangaza kwa mataifa habari njema juu ya yule Kristo.’ (Waefeso 3:8, NW) Kwa hiyo, wote wanaokubali fadhili zisizostahiliwa za Mungu ni lazima washiriki katika huduma ya Kikristo. Hii inamaanisha kwamba sisi tulio watumishi walio wakfu wa Yehova Mungu, tuna daraka la kufanya ukweli uwe dhahiri kwa wengine, kutukuza na kusifu jina la Mungu, na kumtumikia yeye katika ibada iliyo safi na takatifu.​—Mathayo 28:19, 20; Waebrania 13:15; Yakobo 1:27.

‘Usikose Kusudi Lazo’

Je! inawezekana kwamba yeyote kati yetu, kama wale Wakristo wa mapema, yumo katika hatari ya ‘kukosa kusudi’ la fadhili zisizostahiliwa za Mungu? Ndiyo. Kama wao, wengi kati yetu, kazini au shuleni, tunalazimika kukutana-kutana pamoja na watu mmoja mmoja ambao wanazoea ukosefu wa adili katika ngono, uibaji, kusema uwongo, na kuhadaa, na pia mambo mengine ambayo ni ya kukirihika kwa Yehova Mungu. (1 Wakorintho 6:9, 10; Wagalatia 5:19-21) Kwa hiyo ni jambo muhimu kwamba sisi tuepuke kufanya ushirika pamoja na watu kama hao, ama sivyo sisi tutaanza kukuza mwonjo wa yaliyo mabaya. (1 Wakorintho 15:33) Mashirika kama hayo yanaweza kuwa na athari yenye kudhoofisha tu imani yetu. Kwa kufaa, Paulo aliandikia Tito hivi: “Kwa maana fadhili zisizostahiliwa za Mungu ambazo zinaleta wokovu kwa namna zote za wanadamu zimedhihirishwa, zikituagiza tukatae katakata ukosefu wa kutii Mungu na tamaa za kilimwengu na kuishi kwa utimamu wa akili na uadilifu na kujitoa kwa ajili ya Mungu katikati ya huu mfumo uliopo wa mambo.”​—Tito 2:11, 12, NW.

Huenda watu fulani wakakata shauri kwamba wao wanatimiza huduma yao ikiwa wanahudhuria mikutano kwenye Jumba la Ufalme, wanashiriki kwa ukawaida katika kutangaza habari njema za Ufalme wa Mungu, na hawajitii katika aina yoyote ya mwenendo wa ukosefu wa adili. Hata hivyo, kuna jambo jingine la kufikiria. Yesu alisema: “Hakuna mmoja ambaye anaweza kuwa mtumwa kwa mabwana-wakubwa wawili.” (Mathayo 6:24, NW) Yeye alimaanisha nini? Kwamba hata ingawa sisi tunatoa kipimo fulani cha wakati wetu kwenye uendelezaji wa habari njema, inawezekana upendezi wetu mkuu katika maisha uwe ule wa kujitahidi kufuatia vitu vingi zaidi na zaidi vya kimwili. Ni kweli, huenda sisi tukaliona tazamio la mfumo mpya wa mambo chini ya Kristo Yesu kuwa lenye kuvutia kikweli, hata hivyo wakati ule ule huenda sisi tukataka kupata kadiri iliyo kubwa zaidi kutokana na mfumo huu maadamu upo. Mwelekeo kama huo unaweza tu kutuvuta kando kutoka kwenye lile kusudi halisi la kukombolewa kwetu. Je! si mwelekeo unaofanana na huo kuelekea mifuatio ya kimwili uliowaondosha kando Wayahudi waliorudishwa kwao, wakakosa kutimiza kusudi la kukombolewa kwao?

Je! kazi zetu zinaonyesha kwamba sisi tumekosa kusudi la kukombolewa kwetu kutoka kwenye mfumo huu wa kale ulio mwovu na dini bandia yao? Paulo aliambia Wakorintho kwamba “sasa hasa ndio wakati unaokubalika” ili kusaidia wengine wapate wokovu. (2 Wakorintho 6:2, NW) Leo, huku uharibifu wa huu mfumo mbovu ukiwa karibu sana, kuna uharaka mkubwa zaidi kuhusu maneno ya Paulo. Ingawa inaonekana wazi kwamba walio wengi wa waenda-kanisani wa leo wanachagua kutoshiriki imani yao pamoja na wengine, Wakristo wanaodhihirisha upendo wenye kuhisiwa moyoni kwa ajili ya Yehova Mungu watalihesabu kuwa pendeleo kushiriki kwa ukamili katika huduma ya Kikristo ambayo yeye amewagawia. Wote wale ambao wanatangaza habari njema kwa uaminifu katika wakati huu unaokubalika na kutumikia Yehova katika ibada iliyo safi na takatifu wanaweza kufanya hivyo wakiwa na uhakikishio wa kwamba wao ‘wamekubali fadhili zisizostahiliwa za Mungu na hawajakosa kusudi lazo.’​—2 Wakorintho 6:1, NW.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki