Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 4/15 kur. 30-31
  • Maonyo ya Kimungu Yanayokuathiri Wewe

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maonyo ya Kimungu Yanayokuathiri Wewe
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Afa kwa Edomu
  • Nyumba ya Yakobo Yarudishwa
  • Masomo Kutokana na Maandiko: Yona 1:1–4:11
  • Yona Atoroka
  • Yona Aenda Ninawi
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Obadia, cha Yona, na cha Mika
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Kitabu Cha Biblia Namba 32—Yona
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Igeni Imani Yao
  • Alijifunza Kuwa Mwenye Rehema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 4/15 kur. 30-31

Masomo Kutokana na Maandiko: Obadia 1-21

Maonyo ya Kimungu Yanayokuathiri Wewe

“YEYE awagusaye ninyi aigusa mboni ya jicho lake [langu, NW].” (Zekaria 2:8) Maneno hayo ya kutisha ni ujumbe wa tahadhari kwa kila mmoja: Yehova huona jinsi mataifa yanavyotendea watu wake. Ingawa hivyo, inakuwaje kwa taifa linalokaidi onyo hilo la kimungu na kuwagusa watu wa Mungu kwa madhara? Kitabu kilicho kifupi zaidi katika Maandiko ya Kiebrania, Obadia, kinajibu.

Afa kwa Edomu

Hakuna mmoja anayeepuka hukumu ya Yehova. Unabii wa Obadia, uliotamkwa karibu 607 K.W.K., ulitabiri kuondoshwa kwa Waedomi katika bara lao wajapoonekana kuwa katika hali salama wakiwa juu “kati ya nyota.” Na ingawa maisha ya kibinafsi ya mwandikaji huyu wa Biblia hayafunuliwi, yeye anaishi kulingana na maana ya jina lake, “Mtumishi wa Yehova.” Jinsi gani? Kwa kutangaza hukumu ya kuhuzunisha sana. Edomu aangukapo, atatekwa nyara kabisa na marafiki walio katika agano pamoja naye. Hata wenye hekima na wenye uweza ndani yake hawataokoka.​Mistari ya —1-9.

Mungu analeta afa juu ya wale walio na hatia ya kutenda jeuri dhidi ya watu wake. Ni nini sababu ya afa la Waedomi? Ni kurudia-rudia vitendo vya jeuri dhidi ya wana wa Yakobo, ndugu zao. Wakiwa wazao wa Esau, Waedomi walikuwa wa ukoo mmoja na Waisraeli. Hata hivyo, wanashtakiwa kuwateka nyara watu wenye ujamaa wao, wakishangilia kikorofi juu ya anguko la Yerusalemu, na kufikia upeo kwa kuwatia waokokaji katika mikono ya adui. Hivyo, Edomu imejitilia muhuri wa kuangamizwa kwayo.​—Mistari ya 10-16.

Nyumba ya Yakobo Yarudishwa

Ahadi za Yehova zinategemeka sikuzote. Katika siku ya Obadia, Yehova alitoa uhakikisho thabiti kwamba watu Wake wangemiliki tena bara lao na hata zaidi ya hapo. Israeli hawangekuwa tena katika kugawanyika. Nyumba ya Yakobo, ule ufalme wa Yuda wenye makabila mawili, ungetiwa tena katika muungamano pamoja na nyumba ya Yusufu, ule ufalme wa kaskazini wenye makabila kumi, katika kumeza Edomu kama vile moto unavyokula mabua makavu na katika kulikaa eneo la Edomu. Akimalizia kwa maneno yenye kutia moyo, Obadia anajulisha wazi kwamba Waisraeli waliorudishwa makwao watamwabudu Mungu wao kwa muungamano na wawe raia zake. Kweli kweli, umaliki utakuwa wa Yehova.​—Mistari ya 17-21.

Somo kwa leo: Maonyo yenye kupuuzwa hutokeza tunda lenye madhara. Hivyo, onyo kali la Obadia kwa Edomu linapasa lirudishe mwangwi katika masikio ya wapinzani wa ki-siku-hizi wa Mungu: Wale wanaopigana dhidi ya Yehova na watu wake watakatiliwa mbali milele.

Masomo Kutokana na Maandiko: Yona 1:1–4:11

EPUKA afa! Pokea rehema! Jinsi gani? Kwa kutii somo la hadithi ya kweli ya miaka zaidi ya 2,800 iliyopita​—kitabu cha Yona. Kikiwa kiliandikwa karibu 844 K.W.K. na mnabii Yona wa Galilaya, kimejaa muono-ndani wa kiroho.

Yona Atoroka

Inatupasa sisi tuitibari katika Yehova ili atuunge mkono katika utumishi wake. Hata hivyo, Yona anakimbia kazi aliyopewa na Mungu badala ya kutegemea Yehova ili amtegemeze. Ni kweli, mgawo wake haukuwa rahisi. Yeye alipaswa kuionya Ninawi bila aibu juu ya afa la kimungu. Lakini Yona anaenda upande ule mwingine, akitweka kuelekea Tarshishi, ambayo sasa ni Hispania. Njiani, tufani inakuwa kali sana hivi kwamba inaonekana haiwezekani meli na waliomo kuokoka. Yona anaungama, mabaharia wanamtupa nje ya meli, na bahari inatulia. Samaki mkubwa anammeza mnabii.​—1:​1-17.

Watumishi wa Mungu wanaweza kuwa na uhakika kwamba yeye atajibu sala zao. Akiwa ndani ya samaki, Yona anamlilia Yehova kuomba msaada, kwa sala anamshukuru Mungu kwa kumkomboa kutoka kaburi la maji, na kuahidi kulipa alichonadhiri. Baada ya muda, anatapikwa nje katika bara.​—2:​1-10.

Yona Aenda Ninawi

Usiepe kamwe mgawo kutoka kwa Yehova. Yaonekana akiisha kujifunza somo hili, mnabii asiyekuwa na nia hapo kwanza anahubiri katika “mji ule mkubwa.” Yona anavumisha onyo rahisi lakini la kutoboa wazi: “Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.” Kwa badiliko la matukio ya kustaajabisha, Waninawi wanatubu na kuepuka afa.​—3:​1-10.

Mwanadamu hawezi kuiwekea mipaka rehema ya Mungu. Kasirani ya Yona inaongezeka kwa sababu Ninawi umeachiliwa. Lakini kupitia mmea, Yehova anafundisha Yona kwamba Yeye ataonyesha rehema kulingana na raha njema Yake mwenyewe.​—4:​1-11.

Somo kwa leo: Afa linaweza kuepushiwa kando kwa kutii unabii wa kimungu! Waige Waninawi. Msikilize kwa unyenyekevu Yesu Kristo, aliye mnabii mkubwa kuliko Yona. ​—Luka 11:32.

[Sanduku katika ukurasa wa 30]

MAANDIKO YA BIBLIA YACHUNGUZWA

○ Obadia Mstari 7​—Katika nyakati za Biblia, ‘kula mkate’ (chakula, NW) pamoja na mtu kulikaribia kabisa kuwa kama kufanya agano la urafiki. Ni jambo la kinyume kama nini! Wababuloni, ‘watu wa mapatano’ (“watu katika agano,” NW) pamoja na Waedomi, ndio wangethibitika kuwa waharabu wao. Ni kweli, Wababuloni wa siku ya Nebukadreza waliruhusu Edomu ishiriki vitu vilivyoporwa Yuda baada ya Yerusalemu kuachwa ukiwa. Lakini Nabonido mfalme Mbabuloni wa baadaye alizuilia kabisa kabisa makuu ya Edomu ya kujitakia ubiashara na bidhaa.

○ Mstari 10​—Edomu ilihukumiwa maangamizi ‘kukatiliwa mbali hata milele’ kwa sababu ya chuki yayo yenye kusimanga na kutojali kabisa shauku ya kiasili kwa taifa ndugu yayo, “wana wa Yuda.” (Mstari 12) Kutoweka huko kwa taifa kulimaanisha kwamba taifa la Kiedomi lenye serikali na idadi ya watu katika mahali hususa pa kijiografia lingetoweka kabisa usoni pa dunia. Leo, hakuna watu wanaotambulikana kuwa wenye utaifa wa Kiedomi; wao ‘wamekuwa kana kwamba hawakuwa kamwe.’​—Mstari 16.

[Sanduku katika ukurasa wa 31]

MAANDIKO YA BIBLIA YACHUNGUZWA

○ Yona 1:17​—Kwa sababu ya kichwa chake kikubwa na umio mkubwa, nyangumi wa mafuta anaweza kumeza mwanadamu. Ingawa nyangumi ni haba katika Mediterania, wakati mmoja wawinda nyangumi walikuwa wakiweka merikebu zao katika gudi ya Yafa. Samaki mmoja anayejulikana kuwa mwenye kufuata meli katika Mediterania na kula chochote kinachotupwa nje ni yule papa mkubwa mweupe. Yeye pia anaweza kumeza mwanadamu akiwa mzima-mzima. Hata hivyo, katika kisa cha Yona, Mungu alitumia “samaki mkubwa,” labda kiumbe fulani asiyejulikana na sayansi ya ki-siku-hizi.

○ 2:​1, 2​—Kwa uhakika Yona hakuwa na hali nzuri kabisa za kuweza kutunga shairi alipokuwa “katika tumbo la yule samaki.” Lakini baadaye aliandika yaliyompata. Katika kina cha moyo wake mlitoka maneno yaliyoeleza maoni yake ya ndani ambayo yanalingana na yale yaliyo katika Zaburi. ​—Linganisha 2:2 pamoja na Zaburi 120:1 na Zab 130:1; Yon 2:5 pamoja na Zaburi 69:1.

○ 3:3​—Ukubwa wa Ninawi haukutiliwa chumvi. Ingawa kuta zenye kuizunguka zilikuwa karibu kilometa 13 tu kwa mduara, yaonekana wazi kwamba jina la jiji hilo lilitia ndani viunga vyalo, ambavyo huenda vikawa vilikuwa na umbali wa kama kilometa 42.

○ 3:10​—Neno la Kiebrania lililofasiriwa ‘akaghairi’ linamaanisha “kugeuza akili ya mtu kuhusiana na kitendo cha wakati uliopita (au kinachokusudiwa).” Hivyo, Yehova anaweza ‘kughairi’ au kugeuza akili yake kuhusu kuleta adhabu juu ya wanadamu wakosaji wakati wanapotubu kikweli.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki