Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 9/1 kur. 5-6
  • Utawala wa Mungu Njia Bora Zaidi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utawala wa Mungu Njia Bora Zaidi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Badiliko Kubwa Lakaribia!
  • Ufalme wa Mungu—Utawala Mpya wa Dunia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Ufalme Ambao Utabadili Dunia Nzima
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Utawala wa Yehova Umethibitika Kuwa Bora!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 9/1 kur. 5-6

Utawala wa Mungu Njia Bora Zaidi

HISTORIA ya serikali mbalimbali inaonyesha wazi kwamba wanadamu wasiokamilika hawawezi kutumia uwezo juu ya watu wengine. Kama Bwana Acton wa Uingereza alivyosema: “Uwezo huelekea kufisidi, na uwezo kamili hufisidi kikamili.” Hivyo, kama Biblia inavyosema: “Mtu mmoja anayo mamlaka juu ya mwenziwe kwa hasara yake.”—Mhubiri 8:9.

Hapo mwanzoni, Yehova Mungu alimpa mwanadamu utawala juu ya wanyama, lakini si juu ya wanadamu wengine. Mungu alimwambia hivi Mwana wake aliyeumbwa kwanza katika mbingu: “Na tufanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.” (Mwanzo 1:26) Muumba wa mwanadamu ndiye aliyekuwa Mtawala wake. Basi, hilo lilibadilikaje?

Mwanadamu alipoasi katika shamba la Edeni, yeye alimkataa Mungu asiwe Mtawala wake naye ameendelea kufanya hivyo tangu wakati huo. (Mwanzo, sura 3) Hilo lilionekana wazi katika Israeli ya kale, taifa ambalo Mungu alikuwa amechagua liwe lake mwenyewe. Waisraeli walipodai wawe na mfalme mwanadamu, Yehova alimwambia mnabii wake Samweli: “Hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao.”—1 Samweli 8:7.

Utawala wa Mungu juu ya Waisraeli ulikuwa mwema. Kupitia mwakilishi wake Musa, Yehova aliwapa sheria zilizofikiria hali njema yao kwa upendo. Ziliwalinda na magonjwa mengi na kuendeleza ufikirio kwa wazee-wazee, wajane, na yatima. Sheria ilihitaji kuonyesha staha kwa mali ya wengine na ufuataji haki katika shughuli za kibiashara. Ilishutumu upendeleo, ushuhuda wa bandia, na hongo. Utawala wa Mungu ulikuwa wa haki na uadilifu kweli kweli.

Yehova aliahidi kutawala si Israeli tu bali aina yote ya binadamu. Yeye angenyakua uwezo wa kutawala wanadamu wengine utoke kwa wanadamu wenye dhambi na kumpa Mwana wake mzaliwa wa pekee. Akitabiri hivyo, Mungu alisema hivi katika unabii wa Ezekieli: “Hiki nacho hakitakuwa tena, hata atakapokuja yeye ambaye ni haki yake; nami nitampa.”—Ezekieli 21:27.

Mungu alimpa Yesu Kristo haki ya kutawala aina ya binadamu akiwa mwakilishi wa enzi kuu ya Yehova. Kwa kuwa Ufalme wa Mungu kupitia Kristo ndiyo njia bora ya kutawala aina yote ya binadamu, Yesu alifundisha wasikilizaji wake wasali kwa ajili yao. “Basi ninyi salini hivi,” akasema Kristo: “Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.”—Mathayo 6:9, 10.

Kwa njia aliyowatendea watu, Yesu alionyesha angekuwa mtawala wa namna gani. Hakika Kristo alikuwa na huruma, kwa kuwa “alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.” (Mathayo 9:36) Yesu alionyesha kina cha upendo wake kwa wafuasi wake aliposema hivi: “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo.” (Yohana 13:34) Aliwapenda watu vya kutosha kutoa uhai wake uwe ukombozi. Dhabihu hiyo inawezesha wale wanaoikubali kuwekwa huru na dhambi, magonjwa, na hata kifo.—1 Yohana 2:1, 2; Ufunuo 21:1-4.

Akitabiri jinsi utawala wa Mungu kupitia Yesu Kristo ungekuwa wa haki, wenye uadilifu, na wenye amani, mnabii Isaya alivuviwa aandike hivi: “Kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme [Mwana-Mfalme, NW] wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani hayatakuwa na mwisho kamwe, katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; kuuthibitisha na kuutegemeza kwa hukumu na kwa haki, tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana [Yehova, NW] wa majeshi ndio utakaotenda hayo.”—Isaya 9.6, 7.

Wawakilishi wa kidunia wa utawala wa Mungu watakuwa kama wanaume ambao sasa wanaonyesha sifa za upendo za Yesu wakiwa waangalizi katika makundi ya kweli ya Kikristo. Tofauti na makasisi wenye kupiga ubwana, wanaume hawa wanaonyesha kundi hangaiko la upendo, kama alivyofanya Yesu Kristo. Kuhusu wanaume hao wenye kumcha Mungu, mnabii Isaya aliandika: “Tazama, mfalme atamiliki kwa haki [uadilifu, NW], na wakuu watatawala kwa hukumu.” (Isaya 32:1) Wawakilishi hao wa utawala wa Mungu pia watatumikia masilahi ya kimungu katika ulimwengu mpya. —Zaburi 45:16.

Badiliko Kubwa Lakaribia!

Kabla Ufalme wa Mungu haujachukua mahali pa utawala wa aina ya binadamu, lazima badiliko kubwa litokee. Badiliko hilo litakomesha mipaka ya kitaifa. Badala ya kuwa na serikali nyingi za kibinadamu zenye kuhitilafiana, kutakuwa na serikali moja ya kimbingu yenye uadilifu ikileta aina ya binadamu katika umoja wakiwa kikundi kimoja cha watu wenye kuishi kwa amani. Akitabiri hili, mnabii Danieli aliandika: “Katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi [serikali za wanadamu] zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.”—Danieli 2:44.

Utawala wa Mungu ndio jibu kwa matatizo ya kiserikali yanayokabili aina ya binadamu leo. Hali ambamo wanadamu wanajikuta ndani sasa inatisha kuwapo kwao wenyewe! Na hakuna utatuzi wa wanadamu unaoweza kufaulu. Basi, lingekuwa jambo la hekima, kuelekezea fikira utatuzi wa Biblia na kutazama mbele kwa uhakika kwenye wakati usio mbali ambapo wanadamu wenye mioyo mizuri wataona shangwe chini ya utawala wa Mungu usioshindaniwa na uliobarikiwa.

[Picha katika ukurasa wa 6]

‘Mfalme atamiliki kwa uadilifu wenyewe’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki