Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w89 9/15 kur. 20-25
  • Watiini Wale Wanaotoa Uongozi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watiini Wale Wanaotoa Uongozi
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Kuwatii?
  • Kwa Nini Tuthamini Utumishi Wao?
  • Uwe Mwenye Haraka Kutumia Shauri
  • Staha Hata Katika Mambo Madogo
  • Endelea Kuitikia Uangalizi Wenye Upendo
  • “Mwendelee Kuwachukua Watu wa Namna Hiyo Kuwa Wapendwa Wanaothaminika”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • “Mwatilie Maanani Wale Wanaofanya Kazi kwa Bidii Kati Yenu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Jinsi Ambavyo Kutaniko Limepangwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Wazee Wanaosimamia Vema
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
w89 9/15 kur. 20-25

Watiini Wale Wanaotoa Uongozi

“Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu.”—WAEBRANIA 13:17.

1. Watu fulani walimwonaje mtume Paulo, lakini ni mtazamo gani unaofaa kuelekea wazee?

YEHOVA ameandalia tengenezo lake waangalizi katika huu “wakati wa mwisho.” (Danieli 12:4) Wao wanatoa uongozi katika kutunza watu walio kama kondoo, na usimamizi wao ni wenye kuburudisha. (Isaya 32:1, 2) Tena, uangalizi wenye upendo unaofanywa na wazee ambao wanalitendea kundi la kondoo za Mungu kwa wororo unatumikia kama ulinzi kutoka kwa Shetani na mfumo huu mbovu wa mambo.—Matendo 20:28-30; 1 Petro 5:8; 1 Yohana 5:19.

2. Tunanufaikaje na kazi ya waangalizi Wakristo?

2 Lakini wewe unawaonaje wazee? Katika moyo wako, je! wewe unasema: ‘Mimi sitamwendea kamwe mzee mwingine katika kundi hili ikiwa nina tatizo, kwa sababu situmaini yeyote kati yao’? Ikiwa hivyo ndivyo unavyohisi, je! ingeweza kuwa unakazia mno kutokamilika kwao? Katika Korintho ya kale, wengine walisema hivi kuhusu mtume Paulo: “Barua zake zina uzito na kani nyingi, lakini kuwapo kwake yeye mwenyewe ni dhaifu na uneni wake ni wa kudharaulika.” Hata hivyo, Mungu alimpa Paulo mgawo wa huduma na alimtumia yeye akiwa “mtume wa watu wa mataifa.” (2 Wakorintho 10:10, NW; Warumi 11:13; 1 Timotheo 1:12) Basi, inatumainiwa kwamba wewe unahisi kama dada aliyesema: “Sisi tuna baraza la wazee lililo bora zaidi ulimwenguni. Wapo hapa ili wasaidie wanapohitajiwa.”

Kwa Nini Kuwatii?

3. Ikiwa Bwana atakuwa pamoja na roho tunayoonyesha, tunapaswa tuwaoneje wachungaji-wa-chini walio Wakristo?

3 Kwa kuwa wachungaji-wa-chini walio Wakristo wameandaliwa na Mchungaji Mkubwa, Yehova Mungu, wewe unafikiri anataka tuwaoneje? Hakika, Mungu anatazamia tufuate mwelekezo unaotegemea Biblia ambao unapokewa kupitia waangalizi wenye upendo chini ya usimamizi wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Kisha ‘Bwana atakuwa pamoja na roho tunayoonyesha,’ tutaona shangwe ya kuwa na amani, nasi tutajengwa kiroho.—2 Timotheo 4:22; linganisha Matendo 9:31; 15:23-32.

4. Sisi binafsi tunaweza kutumiaje Waebrania 13:7?

4 Paulo alihimiza hivi: “Wakumbukeni wale waliokuwa wakiwaongoza, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa mwenendo wao, iigeni imani yao.” (Waebrania 13:7) Miongoni mwa Wakristo wa mapema, mitume walitoa uongozi kwanza. Leo, tunaweza kuangalia wale wanaofanyiza Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova, waangalizi wengine wapakwa-mafuta, na wanaume wa “umati mkubwa” wanaotoa uongozi miongoni mwetu. (Ufunuo 7:9, NW) Ijapokuwa hatuhimizwi tuige sifa zao za sauti, njia yao ya kusimama au kuketi, au vitabia vingine vya kibinadamu, tunapaswa tuwe na uwezo wa kufanya mwenendo wetu uwe mzuri kwa kuiga imani yao.

5. Duniani leo, ni nani wamekabidhiwa amana ya daraka kuu la kutunza kundi la Kikristo, nao wanastahili nini?

5 Leo duniani, daraka kuu la kutunza mahitaji yetu ya kiroho limekabidhiwa liwe amana ya “mtumwa mwaminifu na mwenye uangalifu.” Baraza Linaloongoza lenye kumwakilisha linatoa uongozi na kuratibu kazi ya ulimwenguni pote ya kuhubiri Ufalme. (Mathayo 24:14, 45-47) Hasa wazee hawa wenye kupakwa mafuta kwa roho wanaweza kuonwa kuwa magavana wa kiroho, kwa kuwa Waebrania 13:7 inaweza kufasiriwa hivi: “Nyinyi mwafikirie wale wanaogavana . . . nyinyi.” (Kingdom Interlinear) Kukiwa na makundi zaidi ya 60,000 na wapiga mbiu ya Ufalme zaidi ya 3,500,000, wazee 12 wanaofanyiza Baraza Linaloongoza wana ‘mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.’ (1 Wakorintho 15:58, NW) Kwa sababu ya mgawo wao waliopewa na Mungu, wanastahili ushirikiano kamili, sawa na baraza lililoongoza la karne ya kwanza lilivyopata ushirikiano wa Wakristo wa mapema.—Matendo 15:1, 2.

6. Ni baadhi ya mambo gani yanayofanywa na wazee kwa manufaa ya watu wa Yehova?

6 Waangalizi wamewekwa rasmi kwa roho ili watunze mahitaji ya kiroho ya kundi. (Matendo 20:28) Wao wanahakikisha kwamba ujumbe wa Ufalme unahubiriwa katika eneo la kundi la mahali. Wanaume hawa wenye sifa za Kimaandiko wanaandaa pia mwelekezo wa kiroho katika njia yenye upendo. Wao wanasihi, wanafariji, na wanawavumilia ndugu na dada zao wa kiroho, mpaka waendelee kutembea katika njia inayostahili Mungu. (1 Wathesalonike 2:7, 8, 11, 12) Hata mtu anapochukua hatua fulani isiyo sahihi kabla ya yeye kujua juu yayo, wanaume hawa wanatafuta kumrekebisha upya “kwa roho ya upole.”—Wagalatia 6:1.

7. Paulo alitoa shauri gani kwenye Waebrania 13:17?

7 Mioyo yetu inasukumwa kushirikiana na waangalizi hao wenye upendo. Hili ni jambo linalofaa, kama alivyoandika Paulo: “Watiini wenye kuwaongoza, na kuwanyenyekea; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho [nafsi, NW] zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.” (Waebrania 13:17) Tunapaswa kuelewaje shauri hili?

8, 9. (a) Kulingana na Waebrania 13:17, kwa nini tunapaswa kuwatii wale wanaotoa uongozi? (b) Utii na unyenyekevu wetu unaweza kuwa na matokeo gani mema?

8 Paulo anatusihi tuwatii wale wanaotugavana kiroho. Tunapaswa ‘kuwatii,’ kujitoa kwa wachungaji hawa wa chini. Kwa nini? Kwa sababu ‘wanakesha kwa ajili ya nafsi zetu,’ au maisha iliyotolewa wakfu kwa Mungu. Nao ‘wanakesha’ kwa njia gani? Hapa hali ya utendaji mwendelevu wa kitenzi cha Kigiriki a·gru·pneʹo yamaanisha kwa njia halisi kwamba wazee ‘wamo katika kuendelea kujinyima usingizi.’ Hili linatukumbusha juu ya mchungaji aliye peke yake anayekosa usingizi ili alinde zizi lake na hatari za usiku. Nyakati fulani wazee wanakosa usingizi usiku wakihangaikia kundi la kondoo za Mungu katika sala au wakitoa msaada wa kiroho kwa waamini wenzi. Lo, jinsi tunavyopaswa kuthamini utumishi wao wa uaminifu! Kwa uhakika, hatutaki kuwa kama “watu wasiomcha Mungu” wa siku za Yuda ambao ‘walipuuza ubwana na kunena kwa kutukana watukufu,’ wazee Wakristo wapakwa-mafuta wenye utukufu au heshima waliyopewa na Mungu.—Yuda 3, 4, 8, NW.

9 Yehova angekosa kufurahi kama sisi hatungewatii na hatungewanyenyekea waangalizi Wakristo. Hiyo pia ingewapa mzigo na kutudhuru sisi kiroho. Kama hatungeonyesha ushirikiano, wazee wangeweza kufanya kazi zao kwa kuugua, labda wakiwa na roho ya kuvunjika moyo ambayo ingeweza kutokeza kukosa shangwe katika utendaji wetu wa Kikristo. Lakini utii na unyenyekeo wetu unaendeleza mwenendo wa kumcha Mungu na kuimarisha imani yetu. ‘Bwana yu pamoja na roho tunayoonyesha,’ na shangwe inasitawi katika hali hiyo yenye ushirikiano, amani, na umoja.—2 Timotheo 4:22; Zaburi 133:1.

10. Kulingana na 1 Timotheo 5:17, kwa nini wale wanaosimamia katika njia nzuri wanastahili heshima?

10 Kuwatii na kuwanyenyekea wazee wa kundi na kujitiisha hakuonyeshi kwamba sisi ni wapendeza-wanadamu. Hilo lingekuwa jambo lisilopatana na Maandiko, kwa kuwa watumwa Wakristo wa karne ya kwanza waliambiwa wawatii mabwana-wakubwa wao, “si kwa utumwa wa macho, kama wajipendekezao kwa wanadamu, bali kwa unyofu wa moyo, mkimcha Bwana [Yehova, NW].” (Wakolosai 3; 22; Waefeso 6:5, 6) Waangalizi ‘wanaosimamia kwa njia nzuri na kujibidiisha katika kunena na kufundisha’ wanastahili heshima, hasa kwa sababu fundisho lao linategemea Neno la Mungu. Kama alivyoandika Paulo: “Wazee watawalao [wanaosimamia, NW] vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha. Kwa maana andiko lasema, usimfunge kinywa ng’ombe apurapo nafaka. Na tena, Mtenda kazi astahili ujira wake.” —1 Timotheo 5:17, 18.

11. “Heshima maradufu” inaweza kumwendeaje mzee, lakini ni lazima aepuke nini?

11 Maneno ya Paulo ambayo yamenukuliwa sasa hivi yanaonyesha kwamba kwa kufaa msaada wa kimwili unaweza kupewa wale wanaoangalia masilahi ya kiroho ya wengine. Hata hivyo, hii haimaanishi kwamba wazee wanapaswa kupokea mshahara, na hakika “heshima maradufu” si jambo ambalo mzee angeshurutisha kupata. Huenda ikatoka kwa washirika wa kundi kwa hiari, lakini asitumie kamwe mgawo wake kupata mamlaka au vitu vya kimwili. Asijitafutie utukufu wake mwenyewe au kushirikiana sana sana na wale ambao ni wenye ufanisi wa vitu vya kimwili na kuwaachilia wengine. (Mithali 25:27; 29:23; Yuda 16) Bali, lazima mwangalizi alichunge kundi la Mungu ‘kwa hiari si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.’—1 Petro 5:2.

12. Ni kwa kukumbuka nini tutasaidiwa tutii wale wanatoa uongozi miongoni mwetu?

12 Tutasaidiwa tutii na kuwaheshimu wale wanaotoa uongozi ikiwa tunakumbuka kwamba Mungu mwenyewe ameandaa wazee. (Waefeso 4:7-13) Kwa kuwa wanaume hawa wamewekwa rasmi kwa roho na tengenezo la Mungu lina mahali pa muhimu katika maisha za Mashahidi wa Yehova, hakika tunataka kuonyesha shukrani zetu na staha kwa mipango ya kitheokrasi. Tena, tunaweza kuwasaidia wapya wakuze mtazamo huu ikiwa tunaweka kielelezo kizuri cha utii na unyenyekeo kwa wale wanaotoa uongozi miongoni mwetu.

Kwa Nini Tuthamini Utumishi Wao?

13. (a) Ni maoni gani yanayotofautiana kuhusu uongozi katika ulimwengu na katika tengenezo la Mungu? (b) Tuna sababu gani timamu za kuwa na uhakika katika wanaume wanaotoa uongozi miongoni mwetu? (c) Badala ya kuongeza sana kutokamilika kwa wazee wanaofanya kazi kwa bidii, tunapaswa tufanye nini?

13 Katika ulimwengu, kuna mwelekeo wa kukataa uongozi. Kama alivyosema mhadhiri mmoja: “Kiwango cha elimu kinachoongezeka kimefanya kuwe na watu wengi walio stadi hata wafuasi wakawa wachambuzi sana hivi kwamba karibu iwe haiwezekani kuwaongoza.” Lakini roho ya kujitegemea haienei katika tengenezo la Mungu, nasi tuna sababu timamu za kuwatumaini wanaume wanaotoa uongozi miongoni mwetu. Kwa kielelezo, wale tu wanaotimiza matakwa ya Kimaandiko ndio wanaowekwa rasmi kuwa wazee. (1 Timotheo 3:1-7) Wanazoezwa kuwa wenye fadhili, wenye upendo, na wenye kutoa msaada, hata hivyo wenye uthabiti katika kushikilia viwango vyenye uadilifu vya Yehova. Wazee wanashikamana na ukweli wa Kimaandiko, ‘wakilishika imara lile neno aminifu ili wapate kuweza kuonya kwa fundisho lenye afya.’ (Tito 1:5-9, NW) Bila shaka, hatupaswi kuongeza sana kutokamilika kwao kwa kibinadamu, kwa kuwa sisi sote ni wasiokamilika. (1 Wafalme 8:46; Warumi 5:12) Badala ya kuhisi tukiwa tumevurugika akili kwa sababu ya mapungukiwa yao na kulipuuza shauri lao, acheni tuthamini na kukubali mwelekezo wa wazee unaotegemea Biblia kuwa wenye kutoka kwa Mungu.

14. Kulingana na 1 Timotheo 1:12, mzee anapaswa aioneje huduma aliyogawiwa?

14 Paulo, mwanamume mwenye uthamini alisema hivi: “Namshukuru Kristo Yesu Bwana wetu, aliyenitia nguvu kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu, akaniweka katika utumishi wake.” (1 Timotheo 1:12) Huduma hiyo, au utumishi, ilitia ndani kazi ya kuhubiri na kutumikia waamini wenzi. Ingawa mwangalizi amepewa na roho takatifu mgawo wa kutumikia akiwa mchungaji, hii haipasi kumfanya ahisi akiwa mkubwa kuliko wengine, kwa kuwa yeye mwenyewe ni sehemu ya kundi la Mungu la watu walio kama kondoo. (1 Petro 5:4) Badala ya hivyo, anapaswa kuwa mwenye shukrani kwamba Kichwa cha kundi, Yesu Kristo, alimhesabu kuwa anastahili kuhudumia washiriki wa kundi la kondoo na kwamba Mungu alimstahilisha kwa kumpa kiasi fulani cha maarifa, hekima, na uelewevu. (2 Wakorintho 3:5) Kwa kuwa mzee ana sababu za kuwa mwenye shukrani kwa sababu ya mapendeleo yake aliyopewa na Mungu, washiriki wengine wa kundi wanapaswa kuthamini huduma au utumishi huu.

15. Ni nini hasa maana ya shauri la Paulo kwenye 1 Wathesalonike 5:12, 13?

15 Mashahidi wa Yehova wanashukuru kwa ajili ya tengenezo ambalo Yehova amejenga katika hizi siku za mwisho, na uthamini huo unatusukuma kuwastahi wazee. Tunapaswa kuwa wenye furaha kushirikiana kikamili na mipango ambayo wanafanya kwa manufaa yetu. Paulo alisema: “Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao.” (1 Wathesalonike 5:12, 13) Kutumia shauri hili kunaleta shangwe na baraka ya Yehova.

Uwe Mwenye Haraka Kutumia Shauri

16, 17. Ni shauri gani ambalo wazee wangeweza kutoa kuhusu ndoa, na ni nini kingetokea kwa kulifuata?

16 Paulo alimsihi Tito ‘aendelee kuonya na kukaripia kwa mamlaka yote.’ (Tito 2:15) Vivyo hivyo, wawakilishi wa Mungu leo wanatuongoza sisi kwenye kanuni na sheria za Biblia. Kuna sababu timamu za kukubali ombi lililorudiwa la kutumia shauri na mwelekezo wa tengenezo la Yehova na wazee waliowekwa rasmi.

17 Ili kutoa kielezi: Huenda wazee wakamhimiza Mkristo afuate shauri la Biblia la kuoa au kuolewa “katika Bwana tu.” (1 Wakorintho 7:39; Kumbukumbu 7:3, 4) Wanaweza kuonyesha kwamba kuoa au kuolewa na mtu ambaye hajabatizwa kunaweza kuongoza kwenye matatizo mazito, sawa na vile Mfalme Sulemani alivyokosea sana kwa kuchukua wanawake wageni, ambao walielekeza moyo wake kwenye miungu bandia na kuuondoa kwa Yehova. (1 Wafalme 11:1-6) Huenda wazee wakaeleza pia kwamba Ezra aliwaamuru wanaume Wayahudi wawaondolee mbali wanawake wao wapagani, na Nehemia alisema kwamba wale wanaooa au kuolewa na wasioamini walikuwa ‘wakifanya ubaya mkubwa katika kutenda kwa kukosa uaminifu dhidi ya Mungu.’ (Nehemia 13:2327; Ezra 10:1014, NW; ona Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1983 kurasa 22; Novemba 15, 1986, kurasa 26-30.) Mibaraka na uradhi wa kumpendeza Yehova unatokea kwa kutumia shauri la Kimaandiko, kama hili linalotolewa na wazee wenye upendo.

18. Kwa kufikiria yale ambayo Paulo aliandika kwenye 1 Wakorintho 5:913, tunapaswa kuitikiaje ikiwa mshiriki wa jamaa anatengwa na ushirika?

18 Ni jambo linalofaa pia kustahi maamuzi ya hukumu ya wazee. Paulo aliwaambia Wakristo Wakorintho ‘wasichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii wasikubali hata kula naye.’ Walipaswa ‘kumwondoa yule mbaya miongoni mwao.’ (1 Wakorintho 5:913) Lakini wewe ungetendaje ikiwa mtu mmoja wa ukoo wako angetengwa na ushirika? Ingawa huenda kukawa na uhitaji wa kuwekea mipaka uhusiano wa kushughulikia mambo ya kijamaa, ushirika wowote wa kiroho pamoja na mtu huyo wa ukoo aliyetengwa na ushirika ungekatizwa. (Ona Mnara wa Mlinzi, Aprili 15, 1988, kurasa 2631.) Hakika, uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu na tengenezo lake unapaswa utusukume tustahi uamuzi wa hukumu wa waangalizi.

19. Tunapaswa kufanya nini ikiwa wazee wanatuonyesha kwamba tunaenda kwenye njia ambayo si sawa kiroho?

19 Si jambo rahisi kubaki katika njia nyembamba inayoongoza kwenye uhai. Ili kufanya hivyo, ni lazima tufuate mwelekezo unaotolewa na Neno la Mungu na wale ambao wamekabidhiwa madaraka ya uchungaji katika tengenezo lake. (Mathayo 7:13, 14) Ikiwa tungekuwa tunasafiri kutoka jiji moja kuelekea jingine kwa gari nasi tukageuka kufuata njia ambayo si sawa, tendo lingehitajiwa ili kurekebisha mwendo wetu. Au sivyo, hatungeweza kamwe kufika mahali tunapoenda. Vivyo hivyo, ikiwa wazee wanatuonyesha kwamba tunaenda kwenye njia ambayo si sawa kiroho, labda kwa kuchumbia mtu asiyeamini, twapaswa tutumie shauri lao la Kimaandiko upesi. Hii ingekuwa njia moja ya kuonyesha kwamba kweli kweli ‘tunamtumaini Yehova.’—Mithali 3:5, 6.

Staha Hata Katika Mambo Madogo

20. Ni kwa kujiuliza wenyewe maswali gani tunaweza kusaidiwa tuonyeshe staha kwa mwelekezo wa wazee hata katika mambo madogo?

20 Tunahitaji kuonyesha staha kwa mwelekezo wa wazee hata katika mambo madogo. Kwa hiyo tunaweza kujiuliza wenyewe: ‘Je! mimi naonyesha ushirikiano ikiwa wazee wanatuomba tuwatembelee wagonjwa na kuwazoeza wapya katika huduma ya shambani? Je! mimi nakubali kwa utayari migawo kwa ajili ya mikutano na kuitayarisha vizuri? Je! mimi nasikiliza wazee wanapotoa mwelekezo kuhusu kuweka viti kwenye mikusanyiko, njia yetu ya kuvaa, na kadhalika? Je! mimi naonyesha ushirikiano wakati wanaponiomba nisaidie katika kusafisha Jumba la Ufalme, kutoa ripoti ya utumishi wa shambani mara moja, au kufika kwenye mikutano kwa wakati?’

21. Kuwaonyesha kwetu wazee staha kunaweza kutukumbusha maneno gani ya Yesu?

21 Waangalizi wa kundi wanathamini ushirikiano wetu, nao unatokeza mema mengi. Kwa kweli, kuwa kwetu wenye staha na wenye ushirikiano hata katika mambo madogo kunaweza kukumbusha maneno ya Yesu: “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia.” (Luka 16:10) Hakika, tunataka kuonwa kuwa waaminifu.

Endelea Kuitikia Uangalizi Wenye Upendo

22. Ni nini baadhi ya manufaa ambazo zinatokana na uangalizi wenye upendo wa mtumwa mwaminifu na wazee wa kundi?

22 Manufaa zinazotokana na uangalizi wenye upendo wa mtumwa mwaminifu na wazee wa kundi zinathibitisha kwamba baraka yenye kutajirisha ya Yehova i juu ya tengenezo lake la kidunia. Tena, mwelekezo wenye ustadi wa wazee unapatana na uwezo wao na kuendeleza umoja miongoni mwetu. Pia unatokeza jitihada ya pamoja na yenye mafanikio ya kusongeza mbele masilahi ya Ufalme. Kweli kweli, tokeo moja zuri la itikio letu lenye uthamini kwa uangalizi wa wale ambao wanatoa uongozi ni kwamba Mungu anabariki kazi yetu ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:19, 20) Kushirikiana kwetu pamoja na wazee kunatutayarisha pia kwa ajili ya uhai wa milele katika mfumo mpya wa mambo.

23. Kwa kuongozwa na 1 Yohana 5:3, tunapaswa kusukumwa kufanya nini?

23 Kwa kuwa tunampenda Yehova, kumtii yeye si kazi isiyofurahisha. Mtume Yohana aliandika hivi: “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.” (1 Yohana 5:3) Wakristo washikamanifu wanatii amri za Yehova kwa nderemo na wanasukumwa kushirikiana pamoja na wale ambao yeye amekabidhi uangalizi wa kundi. Jinsi tulivyo wenye shukrani kuwa katika tengenezo la Mungu na kuwa na hizo “zawadi katika wanaume”! (Waefeso 4:8, NW) Tukiwa na uhakika kamili kwamba Mungu anaongoza watu wake, basi, acheni sisi sikuzote tuwatii wale walio na pendeleo la kutoa uongozi miongoni mwa Mashahidi wa Yehova.

◻ Kwa nini kuwatii wale wanaotoa uongozi miongoni mwetu?

◻ Ni mtazamo gani ambao tunapaswa kuwa nao kuhusu utumishi unaotolewa na wazee wanaofanya kazi kwa bidii?

◻ Kwa nini tuwe wenye haraka kutumia shauri tunalopewa na wazee?

◻ Ni manufaa gani zinazotokea kwa kuitikia uangalizi wenye upendo kwa uthamini?

[Maswali ya Funzo

[Blabu katika ukurasa wa 24]

Je! wewe unashirikiana na wazee kwa kukubali migawo kwa ajili ya mikutano, kwa kusaidia kutunza usafi wa Jumba la Ufalme, kwa kuripoti utendaji wako wa utumishi wa shambani bila kukawia, na katika njia nyinginezo?

[Picha katika ukurasa wa 23]

Paulo alifurahia kuhubiri habari njema na kutumikia waamini wenzi. Ukiwa mzee, je! wewe unashukuru kwa ajili ya mapendeleo yako ya utumishi uliyopewa na Mungu?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki