Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w90 8/15 kur. 10-15
  • Uaminifu-Mshikamanifu—Kwa Bei Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uaminifu-Mshikamanifu—Kwa Bei Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Uaminifu-Mshikamanifu Watolewa Kielelezo
  • Wazee wa Jadi Waonyesha Uaminifu-Mshikamanifu
  • Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo
  • Uaminifu-Mshikamanifu—Kwa Bei Gani?
  • Uaminifu-Mshikamanifu Usio na Bei
  • Watazame Wale Waaminifu-Washikamanifu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Kukabili Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • “Wewe Peke Yako Ni Mwaminifu-Mshikamanifu”
    Mkaribie Yehova
  • Unapaswa Kuwa Mwaminifu kwa Nani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2002
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
w90 8/15 kur. 10-15

Uaminifu-Mshikamanifu—Kwa Bei Gani?

“Kwa mtu mwaminifu-mshikamanifu wewe utatenda kwa uaminifu-mshikamanifu.”—ZABURI 18:25, NW.

UAMINIFU, wajibu, upendo, jukumu, utii-thabiti. Maneno hayo yana ufanani gani? Hayo ni sura tofauti-tofauti za uaminifu-mshikamanifu. Uaminifu-Mshikamanifu ni sifa ya kimungu inayotokana na ujitoaji wa kujihisi moyoni. Hata hivyo, kwa watu wengi leo, uaminifu-mshikamanifu hauna maana kubwa. Uaminifu kwa mwenzi wa ndoa, majukumu kwa washiriki waliozeeka wa familia, utii-thabiti wa mwajiriwa kwa mwajiri wake—yote hayo huchukuliwa kwa wepesi na mara nyingi matakwa yayo huachiliwa. Na hutokea nini wakati uaminifu-mshikamanifu wa mambo unapogongana? Hivi karibuni, katika Uingereza, wakati mhasibu mmoja alipowaambia wachunguza ushuru ukweli juu ya hesabu za fedha za kampuni yake, alifutwa kazi yake.

2 Ni rahisi kunena tu juu ya uaminifu-mshikamanifu, lakini uaminifu-mshikamanifu wa kweli lazima uungwe mkono na kitendo kisichotia ndani kuachilia matakwa kwa hofu. Tukiwa binadamu wasiokamilika, mara nyingi tunashindwa katika hilo. Kwa hiyo ni vizuri tufikirie kielelezo cha mmoja ambaye uaminifu-mshikamanifu wake hauwezi kutiliwa shaka kamwe, Yehova Mungu mwenyewe.

Uaminifu-Mshikamanifu Watolewa Kielelezo

3 Adamu alipofanya dhambi, Yehova alijulisha waziwazi kusudi lake la kukomboa familia ya kibinadamu ambayo ilikuwa bado kuzaliwa. Msingi wa kitendo hicho ulikuwa ni upendo kwa ajili ya uumbaji wake wa kibinadamu. (Yohana 3:16) Kwa wakati wake, Yesu Kristo, mbegu ya ahadi aliyetabiriwa katika Mwanzo 3:15, alithibitika kuwa dhabihu ya ukombozi, na halingekuwa jambo la kuwazika Yehova kubatilisha kusudi lake alilojulisha. Kwa kukubali dhabihu ya Yesu, imani yetu haitatamaushwa.—Rum. 9:33.

4 Uaminifu-Mshikamanifu wa Yehova kwa Yesu ulitia nguvu sana Mwana wakati alipokuwa duniani. Yesu alijua kwamba ni lazima akabili kifo, naye aliazimia kwa uthabiti kubaki mwaminifu-mshikamanifu kwa Mungu wake hadi mwisho. Maarifa kamili zaidi ya maisha yake kabla hajawa binadamu yalifunuliwa kwake wakati wa ubatizo wake na kupakwa mafuta kwa roho takatifu. Usiku ule aliosalitiwa, yeye alisali arudishwe kwa Babae wa kimbingu, ‘kwa utukufu ule aliokuwa amekuwa nao pamoja na Yehova kabla ya ulimwengu kuwako.’ (Yohana 17:5) Hilo lingewezekanaje? Ni kwa Yehova tu kutoacha Mwana wake mwaminifu-mshikamanifu katika kaburi aone ufisadi. Yehova alimwinua kutoka kifo hadi kwenye uhai usioweza kufa, hivyo akatimiza ahadi ya kiunabii iliyorekodiwa katika Zaburi 16:10, NW: “Wewe hutaacha nafsi yangu katika Sheoli.”—Matendo 2:24-31; 13:35; Ufunuo 1:18.

5 Kufuatia ufufuo wake, vivyo hivyo Yesu alijua kwamba angeweza kutegemea uneni wa Yehova wa ‘kuweka maadui wake kuwa kiti cha miguu yake.’ (Zaburi 110:1) Wakati huo uliwadia katika 1914, mwishoni mwa “nyakati zilizowekwa za mataifa,” kwa kusimamishwa kwa Ufalme katika mbingu. Kukwezwa kulikoahidiwa kwa Yesu juu ya maadui wake kulianza kwa kufukuzwa kwa Shetani na mashetani wake kutoka mbinguni. Kutafikia upeo wakati waingizwapo abiso kwa miaka elfu moja na “wafalme wa nchi, na majeshi yao” kuharibiwa.—Luka 21:24, NW; Ufunuo 12:7-12; 19:19; 20:1-3.

6 Mtunga zaburi alihimiza hivi: “Tumaini katika Yehova na kushika njia yake, na yeye atakweza wewe ili kuchukua miliki ya dunia.” (Zaburi 37:34, NW) Twaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova ataendelea kushikilia neno lake, na hadi mwisho wenyewe wa huu ulimwengu mbovu, yeye ataokoa wanaume, wanawake, na watoto ‘wanaotunza njia yake.’ Kifungu hicho katika Kiebrania cha awali chatoa wazo la jitihada na uaminifu katika kutumikia Yehova. Kwa hiyo, sasa sio wakati wa kuchoka wala kuacha mapendeleo ya utumishi yaliyotolewa kwetu. Huu ndio wakati wa kujikaza katika utumishi wa uaminifu-mshikamanifu wa Mungu wetu na Ufalme wake. (Isaya 35:3, 4) kuna vielelezo vizuri vya kututia moyo. Ebu tufikirie baadhi yavyo.

Wazee wa Jadi Waonyesha Uaminifu-Mshikamanifu

7 Yehova alipokusudia kuangamiza jamii ya binadamu waovu kwa gharika ya maji, yeye alifanya agano pamoja na kichwa cha familia ya mzee wa jadi (ukoo) Noa kwa ajili ya uhifadhi wa familia yake na kuendelezwa kwa uhai juu ya dunia hii. (Mwanzo 6:18) Noa alishukuru kwa ajili ya taraja la himaya ya kimungu, lakini yeye na familia yake walipaswa kutoa ithibati ya kustahili hilo. Jinsi gani? Kwa kufanya aliyoamuru Yehova. Kwanza walikabiliwa na kazi kubwa sana ya kujenga safina. Ilipokamilishwa, Noa alipaswa kuijaza na wawakilishi wa dola ya wanyama na kwa chakula cha kutosha kuwategemeza kwa kipindi kirefu. Lakini si hayo tu. Katika kipindi kirefu cha matayarisho, Noa alikuwa akifanya yote aliyoweza katika kazi ya kuhubiri isiyopata kuwa na kitangulizi, akionya juu ya hukumu ya kimungu ambayo ingekuja.—Mwanzo, sura za 6 na 7; 2 Petro 2:5.

8 Biblia yatuambia kwamba “ndivyo alivyofanya [Noa], sawasawa na vyote alivyomwamuru Mungu, hivyo ndivyo alivyofanya.” (Mwanzo 6:22; 7:5) Noa na familia yake walitoa ithibati ya kuwa waaminifu-washikamanifu katika kutimiza migawo yao. Roho yao ya kujidhabihu ilimaanisha kwamba wakati wao ulitumiwa kwa faida, lakini kazi hiyo ilikuwa ngumu na kuhubiri kulikuwa tatizo. Kwa wao kutozaa watoto kabla ya Mafuriko, wana wa Noa na wake wao walisaidiwa kukaza fikira kwenye kazi waliyogawiwa kwa wakati huo na kuratibu utendaji wao. Mafuriko hayo yenye msiba yalileta mwisho wenye haki kwa ulimwengu mbovu. Noa, mke wake, na wana wao watatu na mabinti-wakwe watatu tu ndio waliookolewa. Sisi twaweza kuterema kwamba wao walikuwa waaminifu-washikamanifu kwa Mungu na kwa mielekezo yake, kwa kuwa kila mmoja wetu ni mzao wa moja kwa moja wa Noa kupitia ama Shemu, Hamu, au Yafethi.—Mwanzo 5:32; 1 Petro 3:20.

9 Abrahamu alipotayarisha kumtoa Isaka kuwa dhabihu, yeye alikuwa akitenda kwa utiifu mwaminifu kwa amri ya Yehova. Jinsi huo ulivyokuwa mtihani wa uaminifu-mshikamanifu! Hata hivyo, Yehova alizuia mkono wa Abrahamu, akisema hivi: “Sasa ninajua ya kuwa unamcha Mungu, iwapo hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee.” Hata hivyo, sisi twafanya vema kutafakari yaliyotangulia hilo. Wakati wa safari ya siku tatu ya kukwea Mlima Moria, hakika Abrahamu alikuwa na wakati wa kutosha kufikiria uzito wa mambo na kubadili nia yake. Vipi juu ya Isaka, ambaye alibeba kuni za dhabihu na aliyejiruhusu afungwe mikono na miguu? Yeye hakuyumba-yumba katika utii-thabiti wake kwa babae, Abrahamu, wala yeye hakusaili (hakutilia shaka) fungu lake la kutimiza, hata ingawa ilionekana kwamba mwendo wake wa uaminifu-mshikamanifu ungemgharimu uhai wake.—Mwanzo 22:1-18; Waebrania 11:17.

Uaminifu-Mshikamanifu wa Kikristo

10 Sikuzote Yehova ametenda kwa uaminifu-mshikamanifu wa kweli. “Mfuateni Mungu,” ahimiza mtume Paulo. (Waefeso 5:1, 2) Sawa na wazee wa jadi walivyoitikia, ndivyo Wakristo wangepaswa kuitikia. Wakristo wa mapema waliweka vielelezo vizuri katika ibada ya uaminifu-mshikamanifu, kama ambavyo jambo lililoonwa lifuatalo linavyoonyesha.

11 Maliki Mroma Konstansio 1, baba ya Maliki Konstantino, yaelekea alikuwa na staha yenye kina kirefu kwa ajili ya wafuasi wa Yesu Kristo. Ili kutahini uaminifu-mshikamanifu wa Wakristo waliohusiana na ikulu yake, yeye aliwaambia wangeweza kubaki katika utumishi wake ikiwa tu wangekubali kutoa dhabihu kwa sanamu. Kukataa kungeongoza kwenye kufukuzwa na kupata kisasi mkononi mwake, wakaambiwa. Kwa mbinu hii sahili, Konstansio alitaka kutambua wale ambao hawangeweza kuachilia matakwa ya uaminifu-mshikamanifu wao. Wale waliotoa ithibati ya kuwa waaminifu-washikamanifu kwa Mungu na kanuni zake waliendelea katika huduma ya maliki huyo, wengine hata wakawa washauri wenye kutumainiwa. Wale wasiokuwa waaminifu-washikamanifu kwa amri ya Mungu walifukuzwa kwa aibu.

12 Ingawa uaminifu-mshikamanifu wapasa kuwa sehemu ya maisha za Wakristo wote, unatajwa hasa katika Tito 1:8 katika orodha ya sifa zilizo za lazima kwa mwanamume awe mwangalizi Mkristo. William Barclay asema kwamba hoʹsi·os, neno la Kigiriki linalotafsiriwa hapa kuwa “uaminifu-mshikamanifu,” hueleza “mtu anayetii sheria za milele ambazo zilikuwa na ni za kabla ya sheria zozote zilizofanywa na binadamu.” Ni muhimu kwamba wazee wachukue msimamo huo wa uaminifu-mshikamanifu kwa kutii sheria za Mungu. Kielelezo hicho kinachofaa kitasaidia kundi likue na liwe na nguvu za kutosha kukabili majaribu na misongo inayoweza kulitisha kwa ujumla au washiriki walo mmoja mmoja. (1 Petro 5:3) Wazee waliowekwa wana daraka kubwa kwa kundi la kutoachilia kamwe matakwa ya uaminifu-mshikamanifu wao kwa Yehova, kwa maana kundi lashauriwa ‘liige imani yao.’—Waebrania 13:7.

Uaminifu-Mshikamanifu—Kwa Bei Gani?

13 “Watu wote wana bei yao” huo ni uneni wa Sir Robert Walpole, waziri mkuu mmoja wa Uingereza wa karne ya 18. Unajumlisha vizuri uhakika wa kwamba katika historia yote uaminifu-mshikamanifu wa mambo mara nyingi umeachiliwa kwa ajili ya faida ya ubinafsi. Fikiria mtafsiri wa Biblia William Tyndale, ambaye kwa kosa alikubali Henry Phillips kuwa rafiki mwaminifu-mshikamanifu. Katika 1535 Phillips bila ya uaminifu-mshikamanifu alimsaliti Tyndale kwa maadui wake, hilo likaongoza kwenye kufungwa gerezani kwa Tyndale mara moja na kifo cha mapema. Mwanahistoria mmoja husema kwamba Phillips, yamkini akiwa wakili wa ama mfalme Mwingereza au Wakatoliki Waingereza, “alilipwa sana kwa ajili ya kazi yake ya Yuda.” Kwa wazi, mwanahistoria huyo alikuwa akigusia Yuda Iskariote, aliyekubali vipande 30 vya fedha kuwa bei ya kusaliti Yesu Kristo. Hata hivyo, hatupaswi kukata shauri kutokana na vielelezo hivyo kwamba “bei” ya uaminifu-mshikamanifu wa mtu sikuzote ni pesa. Sivyo.

14 Mke wa Potifa alipomwomba-omba Yusufu ‘alale naye,’ uaminifu-mshikamanifu wake kwa Yehova ulitahiniwa. Yeye angefanya nini? Kwa akili ambayo tayari ilitambua kanuni zilizohusika, Yusufu alikimbia kutoka kwenye nyumba hiyo, akiwa ameazimia hangeweza kamwe ‘kufanya ubaya huo mkubwa amkose Mungu.’ Taraja la raha ya kingono halingeweza kushinda uaminifu-mshikamanifu wa Yusufu kwa Mungu wake, Yehova.—Mwanzo 39:7-9.

15 Hata hivyo, kuna hatari nyingine; tamaa ya makuu yaweza kuharibu uaminifu-mshikamanifu. Hicho ndicho kilichokuwa kichocheo cha uasi wa Absalomu dhidi ya baba yake, Mfalme Daudi. Kwa kufanya hila na ujanja, Absalomu alitafuta kujipendekeza mwenyewe kwa watu. Hatimaye, alisimamisha jeshi la kukabili wategemeza baba yake walio waaminifu-washikamanifu. Kifo chake mkononi mwa Yoabu kilikomesha ukosefu wa uaminifu-mshikamanifu wa Absalomu kwa baba yake, Daudi, lakini jinsi hiyo ilivyokuwa bei kubwa ya kulipa kwa ajili ya kujaribu kupindua mpango wa kitheokrasi!—2 Samweli 15:1-12; 18:6-17.

Uaminifu-Mshikamanifu Usio na Bei

16 Ingawa Shetani hudai kwamba kila mtu ana bei yake, na ilikuwa kweli kwa Absalomu, haikuwa kweli kwa Yusufu, na haijapata ka-mwe kuwa kweli kwa waabudu wa Yehova waaminifu-washikamanifu. Hata hivyo, Shetani atatoa chochote ili atufanye tuvunje uaminifu-mshikamanifu wetu kwa Muumba wetu. Mtume Paulo alieleza hofu yake kwamba “kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa,” kufikiri kwetu kungeweza kupotoshwa, tuongozwe kwenye kuachilia matakwa ya uaminifu-mshikamanifu wetu kwa Yehova na ibada yake.—2 Wakorintho 11:3.

17 Inafaa tujiulize hivi: ‘Je! kuna bei yoyote ambayo mimi ningekubali ili niachilie pendeleo langu la kuabudu Muumba wangu kwa uaminifu-mshikamanifu?’ Ni uhakika wenye kusikitisha kwamba, tofauti na Yusufu, baadhi ya waliokuwa watumishi walio wakfu wa Yehova walidai kidogo sana ili waachilie. Hata baadhi ya wazee wameachilia mapendeleo yao ya utumishi mtakatifu yenye bei kubwa kwa ajili ya shangwe ya muda ya anasa zisizo za adili za kimwili. Wawe ni wazee au la, wengi wa wale wanaofanya hivyo wamepoteza kabisa umoja wa familia, upendo na staha ya kundi, na kibali cha Yehova—Yeye ambaye aweza kutoa nguvu za kudumisha uaminifu-mshikamanifu na kukinza kishawishi chochote kutoka kwa Shetani.—Isaya 12:2; Wafilipi 4:13.

18 Wengine, kwa kuazimia kupata makuu katika shughuli za kilimwengu, ‘wamejichoma kwa maumivu mengi,’ yajapokuwa maonyo ya Biblia yaliyo wazi. (1 Timotheo 6:9, 10) Dema, Mkristo aliyetajwa na Paulo, alishindwa kwa sababu hiyo, ama kwa muda au daima. (2 Timotheo 4:10) Matakwa ya uaminifu-mshikamanifu kwa Yehova hayawezi kamwe kuachiliwa bila ya matokeo kuwa yenye maafa. “Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa cho chote apandacho mtu, ndicho atakachovuna.”—Wagalatia 6:7.

19 Nyakati nyingine bei ya kujadiliana hutokea kwa njia ya hila sana. Kwa kielelezo, ripoti moja kutoka United States yasema kwamba familia nyingi hutumia karibu nusu ya saa zao za kuamka nyumbani kutazama televisheni, hasa vijana ambao wamekuwa ni wazoefu. Ikiwa Mkristo angelisha akili yake televisheni hasa, pamoja na ngono na jeuri yayo, muda si muda angeweza kuharibu kanuni zake za Kikristo. Hilo lingeweza kumwongoza kwa urahisi kwenye kukosa uaminifu-mshikamanifu, kujitenga na Yehova. Ushirika huo mbaya huharibu mazoea yenye mafaa. (1 Wakorintho 15:33) Hatupaswi kusahau kwamba Maandiko hutushauri tutumie wakati kujifunza na kutafakari Neno la Mungu. Je! wakati wa kupita kiasi unaotumiwa katika kustarehe mbele ya kiwambo cha televisheni ni badilishano halali la wakati ambao ungeweza kutumiwa kupata maarifa yenye kuongoza kwenye uhai wa milele ukiwa mwabudu wa Yehova aliye mwaminifu-mshikamanifu? Wengi wenye kuja kwenye maarifa ya ukweli leo wamelazimika kufanya marekebisho makubwa katika kufikiri kwao katika jambo hilo.—1 Timotheo 4:15, 16; 2 Timotheo 2:15.

20 Takashi ni mfanya biashara Mjapani anayeishi katika Uingereza. Yeye alikuwa akitumia saa tatu au nne jioni zilizo nyingi kutazama televisheni pamoja na familia yake. Baada ya yeye na mke wake kubatizwa miaka mitatu iliyopita, yeye aliazimia kwamba funzo la Biblia la kibinafsi na la familia lazima lichukue mahali pa kwanza. Kwa kupunguza utazamaji wake wa televisheni kuwa dakika 15 au 30 tu kwa wastani kila siku, yeye alichukua uongozi mzuri katika familia. Ingawa Takashi hulazimika kujifunza akitumia Biblia mbili, moja ya Kiingereza na ile nyingine ya Kijapani, ukuzi wake wa kiroho umekuwa wa haraka sana, na sasa yeye hutumika akiwa mtumishi wa huduma katika kundi linalozungumza Kiingereza. Mke wake ni painia msaidizi. “Ili kulinda salama hali ya kiroho ya wavulana wawili wetu wachanga,” yeye asema, “kila siku mimi pia huchunguza sana mambo ambayo mke wangu nami huwaruhusu kuona kwenye televisheni.” Nidhamu hiyo ya kujitia inathawabisha.

21 Twaweza kuwa na uhakika huu: Shetani ajua udhaifu wetu, labda vizuri zaidi yetu. Yeye hataacha lolote anapojaribu kutufanya tuache matakwa au kudhoofisha utii-thabiti wetu kwa Yehova. (Linganisha Mathayo 4:8, 9.) Basi, ni jinsi gani twaweza kujilinda salama? Kwa kuweka wakfu wetu daima mbele yetu na kwa kupendezwa kusitawisha stadi tunapohudumia mahitaji ya kiroho ya wengine. Tukiwa watumishi waaminifu-washikamanifu wa Yehova, ni lazima tujishughulishe sana katika utumishi wake na kuongozwa nyakati zote na Neno lake takatifu. Hayo yatatusaidia katika azimio letu imara kwamba hakuna bei yoyote anayoweza kutoa Shetani itakayotuondosha kutoka kwa uaminifu-mshikamanifu kwa Mungu.—Zaburi 119:14-16.

Wewe Wajibuje?

◻ Yehova na Yesu wamedhihirishaje uaminifu-mshikamanifu?

◻ Ni nini baadhi ya vielelezo vingine vya Biblia vya uaminifu-mshikamanifu?

◻ Huenda Shetani akatutolea au kujaribu kufanya nini?

◻ Twaweza kujitiaje nguvu ili tubaki waaminifu-washikamanifu katika ibada yetu kwa Yehova?

[Maswali ya Funzo]

 1, 2. (a) Uaminifu-Mshikamanifu ni nini, na sura zayo huathirije maisha zetu? (b) Kwa nini ni vizuri kugeukia Yehova kuwa Kielelezo chetu chenye kutokeza?

 3. Yehova amethibitikaje kuwa mwaminifu-mshikamanifu kwa kusudi lake lililotaarifiwa katika Mwanzo 3:15?

 4. Yehova alithibitikaje kuwa mwaminifu-mshikamanifu kwa Yesu, na tokeo likawa nini?

 5. Ni vitendo gani vingine vya uaminifu-mshikamanifu vinavyohusiana na ahadi za Yehova kwa Yesu?

 6. Mungu atutolea tumaini gani lililohakikishwa, nasi twaweza kuonyeshaje uthamini wetu kwa ajili yalo?

 7, 8. (a) Ni migawo gani ya kazi ambayo Yehova alimpa Noa na familia yake? (b) Watu wa nyumba ya Noa walitoaje ithibati kwamba walistahili himaya ya Mungu wakati wa gharika ya duniani pote?

 9. (a) Mtihani wa Yehova kwa Abrahamu ulikuwaje mtihani wa uaminifu-mshikamanifu wake? (b) Isaka alionyeshaje uaminifu-mshikamanifu katika hilo?

 10, 11. Wakristo wa mapema huandaa vielelezo gani vya uaminifu-mshikamanifu?

 12. Waangalizi Wakristo wapaswa kudhihirishaje uaminifu-mshikamanifu, na ni kwa nini hilo ni la muhimu kwa ajili ya hali njema ya kundi?

 13. Uneni “Watu wote wana bei yao” humaanisha nini, na ni vielelezo gani vinavyoelekea kuthibitisha hilo?

 14. Uaminifu-mshikamanifu wa Yusufu kwa Yehova ulitahiniwaje, na tokeo likawa nini?

 15. Absalomu alidhihirishaje ukosefu wa uaminifu-mshikamanifu, na tokeo likawa nini?

 16. 2 Wakorintho 11:3 lafunua nini juu ya madhumuni ya Shetani?

 17. Wengine wamebadilishana mapendeleo ya utumishi yenye bei kubwa na nini?

 18. Kwa nini ni jambo la maana kutii onyo katika 1 Timotheo 6:9, 10?

 19, 20. (a) Ni nini baadhi ya hatari zinazoshirikishwa na kutazama televisheni kupita kiasi? (b) Familia moja ya Mashahidi imeweka kielelezo gani?

 21. Twajua nini juu ya mbinu za Shetani, nasi twaweza kujilindaje salama?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki