Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 3/15 uku. 30
  • Baki Thabiti Katika Imani!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Baki Thabiti Katika Imani!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mwenendo Ulio na Msingi wa Kanuni za Kimungu
  • Uvumilivu Huleta Mibaraka
  • Kitabu cha Biblia Namba 60—1 Petro
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Je, Wanawake Wanapaswa Kuficha Urembo Wao?
    Amkeni!—2005
  • Acheni Tuishike Sana Imani Yetu Yenye Thamani!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Mwongozo Wenye Hekima kwa Wenzi wa Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 3/15 uku. 30

Baki Thabiti Katika Imani!

Mambo Makuu Kutoka Petro ya Kwanza

MASHAHIDI WA YEHOVA hukabili majaribu au mitihani ya namna mbalimbali ya imani yao. Katika mabara fulani, kazi yao ya kuhubiri Ufalme inafanywa kwa kukabili mnyanyaso mkubwa. Aliye nyuma ya juhudi hizi na nyingine za kuharibu uhusiano wao pamoja na Mungu ni Shetani Ibilisi. Lakini yeye hatafaulu kwa kuwa Yehova afanya watumishi wake imara—ndiyo, thabiti katika imani.

Mtume Petro alipewa pendeleo la ‘kuimarisha ndugu zake’ ambao walikuwa ‘wamehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali.’ (Luka 22:32; 1 Petro 1:6, 7) Yeye alifanya hivyo katika barua yake ya kwanza, iliyoandikwa 62-64 W.K. hivi kutoka Babuloni. Katika hiyo Petro alishauri, akafariji na kutia moyo Wakristo Wayahudi na Wasio Wayahudi, akiwasaidia washindane na mashambulio ya Shetani na wabaki “thabiti katika imani.” (1 Petro 1:1, 2; 5:8, 9) Sasa kwa kuwa wakati wa Ibilisi ni mfupi na mashambulio yake ni makali sana, kwa kweli watu wa Yehova wanaweza kufaidika kutokana na maneno ya Petro yenye pumzi ya Mungu.

Mwenendo Ulio na Msingi wa Kanuni za Kimungu

Kama tumaini letu ni la kimbingu au la kidunia, linapasa kutusaidia kuvumilia majaribu na kutenda katika njia ya kimungu. (1:1–2:12) Tumaini la urithi wa kimbingu linafanya wapakwa mafuta washangilie katika kukabili majaribu, ambayo hasa hutakasa imani yao. Wakiwa nyumba ya kiroho iliyojengwa juu ya msingi wa Kristo, wao hutoa dhabihu za kiroho zinazokubalika kwa Mungu na hujiendesha katika njia nzuri inayomletea Yeye utukufu.

Shughuli zetu pamoja na binadamu wenzetu zapasa kuongozwa na kanuni za kimungu. (2:13–3:12) Petro alionyesha kwamba tunapaswa kujitiisha kwa watawala wa kibinadamu. Watumishi wa nyumbani wangejitiisha kwa mabwana wao, na wake kwa waume wao. Mwenendo wa kimungu wa mke Mkristo waweza kuvuta mume wake asiyeamini upande wa imani ya kweli. Na mume anayeamini anapaswa ‘kumpa mke wake heshima, kama chombo kisicho na nguvu.’ Wakristo wote wapaswa kuonyesha maoni ya kujitia katika hali za wengine, kuwa na shauku ya kidugu, kufanya mema, na kufuata sana amani.

Uvumilivu Huleta Mibaraka

Kuvumilia mateso kwa uaminifu kwa Wakristo wa kweli kutatokeza mibaraka. (3:13–4:19) Ikiwa tunateseka kwa sababu ya uadilifu, tunapaswa kufurahi. Tena, kwa kuwa Kristo aliteseka katika mnofu ili kutuongoza kwa Mungu, hatupaswi kuishi zaidi kulingana na tamaa za kimnofu. Tukivumilia majaribu kwa uaminifu, tutashiriki katika shangwe kubwa kwenye ufunuo wa Kristo. Kustahimili shutumu kwa ajili ya jina la Kristo, au tukiwa wanafunzi wake, kwapasa kutufurahishe kwa sababu kwathibitisha ya kwamba tunayo roho ya Yehova. Kwa hiyo tunapoteseka kulingana na mapenzi ya Mungu, na tujiweke katika utunzi wake na kuendelea kufanya mema.

Tukiwa Wakristo, tunahitaji kutimiza wajibu wetu kwa uaminifu na kujinyenyekeza chini ya mkono wa Mungu wenye uwezo. (5:1-14) Ni lazima wazee wachunge kundi la Mungu kwa nia, na sisi sote twapaswa kumtupia Yehova mahangaiko yetu, tukitambua kuwa anatujali kweli kweli. Twapaswa pia kuchukua msimamo wetu dhidi ya Ibilisi na tusivunjike moyo kamwe, kwa sababu ndugu zetu hupatwa na mateso yale yale kama sisi. Sikuzote kumbuka kwamba Yehova Mungu atatufanya imara na atatuwezesha kubaki thabiti katika imani.

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 30]

Mapambo ya Kike: Katika kushauri wanawake Wakristo, Petro alisema: “Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi; bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.” (1 Petro 3:3, 4) Wakati wa karne ya kwanza W.K., wanawake wa kipagani mara nyingi walikuwa na mitindo ya nywele yenye madoido mengi, wakisuka nywele zao kwa namna mbalimbali zenye majivuno na kuweka mapambo ya dhahabu katika masuko. Yaelekea, wengi walifanya hivyo kama wonyesho mshaufu—kitu kisichofaa Wakristo. (1 Timotheo 2:9, 10) Hata hivyo, si mapambo yote yaliyo mabaya, kwa kuwa Petro atia ndani “kuvalia mavazi”—kwa wazi ni ya lazima. Vito vilitumiwa pia na watumishi wa Mungu wa nyakati za kale. (Mwanzo 24:53; Kutoka 3:22; 2 Samweli 1:24; Yeremia 2:32; Luka 15:22) Hata hivyo, mwanamke Mkristo huepuka kwa hekima mapambo mashaufu na mavazi yenye kuamsha nyege na apaswa kuwa mwangalifu kwamba utumizi wowote wa marashi uwe mzuri. Lengo la shauri hilo la kimtume ni kwamba yeye apaswa kuweka mkazo, si juu ya mapambo ya nje, bali ya ndani. Ili avutie kikweli, ni lazima ajivike kwa kiasi na kuwa na mwelekeo wa mmoja anayemhofu Mungu.—Mithali 31:30; Mika 6:8.

[Hisani]

Israel Department of Antiques and Museums: Israel Museum/David Harris

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki