Je! Wakumbuka?
Je! wewe umepata matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi yakiwa yenye thamani inayoweza kutumika kwako? Basi kwa nini usitahini kumbukumbu lako kwa yafuatayo?
◻ Ni mambo gani ya hakika yanayotoa hoja dhidi ya kutukuza mahali panapodhaniwa kuwa pa kuzaliwa kwa Yesu?
Biblia haitaji kisehemu hususa cha mahali alipozaliwa Yesu. Masimulizi ya Gospeli ya Mathayo na Luka hutoa mambo yanayohitajiwa tu. (Mathayo 2:1, 5; Luka 2:4-7) Usomaji wa Yohana 7:40-42 unaonyesha kwamba watu kwa ujumla walikosa kujua mahali pake pa kuzaliwa, wengine wakifikiri kwamba yeye alizaliwa katika Galilaya. Pia, muda wa uhai wa Yesu wenyewe wa kidunia, yeye hakutangaza kamwe mambo madogo-madogo ya kuzaliwa kwake.—12/15, ukurasa 5.
◻ Mkristo awezaje kudumisha shangwe yake anapokabiliana na majaribu ya ugonjwa wa kimwili, mshuko wa moyo, na magumu ya kiuchumi?
Neno la Mungu linatoa faraja na uongozi unaohitajiwa. Kwa kusoma au kusikiliza zaburi, uburudisho mwingi unaohitajika waweza kuandaliwa. Daudi alitushauri hivi: “Umtwike BWANA [Yehova, NW] mzigo wako naye atakutegemeza.” Yeye alituhakikishia pia kwamba Yehova kwa kweli ni “Msikiaji wa sala.” (Zaburi 55:22, UV; 65:2, NW) Kupitia vichapo vyalo na wazee walo wa kundi, tengenezo la Yehova huwa tayari sikuzote kutusaidia tushindane na matatizo yetu.—1/1, kurasa 14-15.
◻ Wakati Yesu alipokuwa njiani kutundikwa alimaanisha nini aliposema hivi: “Kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?” (Luka 23:31)
Yesu alikuwa akirejezea mti wa taifa la Kiyahudi. Kwa sababu ya kuwapo kwa Yesu na mabaki wa Wayahudi waliomwamini, taifa hilo bado lilikuwa na umaji-maji wa uhai ndani yalo. Hata hivyo, wakati hao wote wangetwaliwa kutoka kwa taifa hilo, mti uliokufa kiroho tu ndio ungebaki, tengenezo la kitaifa lililokauka.—1/15, ukurasa 9.
◻ “Wenye moyo safi,” wanaosemwa katika Mathayo 5:8, wanawezaje ‘kumwona Mungu’?
“Wao watamwona Mungu” wanapomtazama akitenda kwa ajili ya wanaoshikilia uaminifu wa maadili. (Linganisha Kutoka 33:20; Ayubu 19:26; 42:5.) Hata hivyo, neno la Kigiriki kwenye Mathayo 5:8 linalofasiriwa ‘–ona’ lamaanisha pia “kuona kwa akili, kufahamu, kujua.” Kwa kuwa Yesu alionyesha utu wa Mungu kikamilifu, mwono-ndani katika utu huo uliwawezesha ‘wenye moyo safi’ ‘wamwone Mungu.’ (Yohana 14:7-9)—1/15, ukurasa 16.
◻ Kwa sababu gani tunakata maneno kwamba Yesu ndiye malaika mkuu Mikaeli?
Neno la Mungu lataja malaika mkuu mmoja tu, na linaongea juu ya malaika huyo katika kurejezea Bwana Yesu aliyefufuliwa hivi: “Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu.” (1 Wathesalonike 4:16) Katika Yuda 9 tunapata kwamba jina la malaika mkuu huyo ni Mikaeli.—2/1, ukurasa 17.
◻ Maeneo manne ambamo tunaweza kuonyesha heshima kwa watu wengine ni yapi?
Tunapaswa kuonyesha heshima kwa watawala wa kisiasa, kwa waajiri kazi, kwa washiriki wa familia zetu, na kwa wale walio katika kundi.—2/1, kurasa 20-2.
◻ Muda mfupi kabla ya kifo cha Yesu, aliwawekea mfano gani mzuri wale wenye wazazi waliozeeka?
Yesu alipokuwa bado ametundikwa juu ya mti wa mateso akiwa na uchungu mwingi, alifanya ufikirio kwa hali njema ya kimwili na ya kiroho ya mama yake kwa kumkabidhi kwenye uangalifu wa mtume wake mpendwa Yohana. (Yohana 19:25-27)—2/15, ukurasa 8.
◻ Kwa nini Yesu alipaswa kuteseka?
Mateso ya Yesu yalitumika kulijibu suala la uaminifu wa maadili wa watumishi wa Mungu. Pia yalimtayarisha kwa ajili ya daraka lake la kuwa Kuhani wa Juu mwenye rehema kwa ajili ya ainabinadamu. (Waebrania 4:15)—2/15, kurasa 14-15.
◻ Uasi katika Edeni ulizusha masuala gani ya maana?
Je! mwanadamu aweza kujitawala mwenyewe bila Mungu? Je, ilikuwa haki kwa Mungu kudai utii kwa enzi kuu yake? Katika maana ya urefusho, je, wanadamu wowote wangechagua kumtumikia Mungu bila ubinafsi kwa hiari yao yenyewe?—3/1, ukurasa 6.
◻ Ni kwa sababu gani wengine wameshiriki mifano ya Ukumbusho kwa makosa?
Huenda ikawa wengine wasiokomaa hawajawa na uthamini uliosawazika wa makusudi ya Mungu. Huenda ikawa hawakiri kwamba kupakwa mafuta “si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.” (Warumi 9:16) Si juu ya mtu binafsi kuamua kwamba yeye angependa kuingizwa katika agano jipya na kuwa mtawala mwenzi pamoja na Kristo. Chaguo la Yehova ndilo la maana, na roho yake inashuhudia chaguo hilo. (Warumi 8:16; 1 Wakorintho 12:18)—3/15, ukurasa 21.
◻ “Lugha iliyo safi” inayosemwa katika Sefania 3:9 ni gani?
Ni ufahamu unaofaa juu ya kweli ya Mungu na makusudi yake.—4/1, kurasa 21-2.