Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w91 12/1 kur. 15-20
  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Neno “Dini” Katika Biblia
  • “Safi na Isiyo na Hitilafu” kwa Maoni ya Mungu
  • “Kujilinda Mwenyewe Usichafuliwe na Ulimwengu Huu”
  • Alama Nyinginezo za Dini ya Kweli
  • Dini ya Kweli—Njia ya Maisha
  • Nguvu Yenye Kuunganisha, Inayofaa
  • Ushindi wa Dini Safi
  • Kujiweka Huru Na Dini Bandia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je! Umeipata Dini ya Kweli?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Ibada Ambayo Mungu Anakubali
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Biblia Inafundisha Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2016
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
w91 12/1 kur. 15-20

Kuzoea Dini Safi Kwa Ajili Ya Kuokolewa

“Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu Baba ni hii: . . . kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.”—YAKOBO 1:27, HNWW.

1. Dini imefafanuliwaje, na kwa kupatana na fikira nzuri ni nani aliye na haki ya kuamua tofauti kati ya dini bandia na ya kweli?

DINI imefafanuliwa kuwa “wonyesho wa imani ya mwanadamu na kicho chenye staha kwa mwenye uwezo unaopita ule wa kibinadamu anayetambuliwa kuwa muumba na mtawala wa ulimwengu wote mzima.” Kwa kupatana na akili, ni nani basi aliye na haki ya kuamua tofauti kati ya dini ya kweli na dini bandia? Kwa hakika ni lazima awe yule aaminiwaye na kupewa kicho chenye staha, Muumba. Yehova ameonyesha waziwazi katika Neno lake msimamo wake juu ya dini ya kweli na bandia.

Neno “Dini” Katika Biblia

2. Kamusi zinaelezaje neno la Kigiriki la awali linalotafsiriwa “namna ya ibada” au “dini,” na laweza kutumiwa kwa aina zipi za ibada?

2 Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “namna ya ibada,” au “dini,” ni thre·skeiʹa. A Greek-English Lexicon of the New Testament hulifafanua neno hilo kuwa “ibada ya Mungu, dini, hasa jinsi inavyojionyesha katika utumishi wa kidini au katika dhehebu.” Theological Dictionary of the New Testament huandaa maelezo mengine zaidi, ikitaarifu hivi: “Mwanzo wa neno hilo hupingwa; . . . wanachuo wa ki-siku-hizi hupendelea ulinganisho walo na therap- (‘kutumikia’). . . . Tofauti ya maana yaweza kuonwa pia. Maana nzuri ni ‘bidii ya kidini’ . . . , ‘ibada ya Mungu,’ ‘dini.’ . . . Lakini kuna maana mbaya pia, k.v., ‘ushupavu wa kidini,’ ‘ibada mbaya.’” Hivyo, thre·skeiʹa laweza kutafsiriwa kuwa ama “dini” au “namna ya ibada,” nzuri au mbaya.

3. Mtume Paulo alitumiaje neno lililotafsiriwa “namna ya ibada,” na ni elezo lipi lenye kupendeza linalotolewa kuhusu tafsiri ya Wakolosai 2:18?

3 Neno hilo hutokea mara nne tu katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Mtume Paulo alilitumia mara mbili kuonyesha dini bandia. Katika Matendo 26:5, NW, anarekodiwa akitaarifu kwamba kabla ya kupata kuwa Mkristo ‘kwa kulingana na farakano lenye kufuatilia mambo sana la namna yetu ya ibada [“dini,” Philips] mimi niliishi nikiwa Farisayo.’ Katika barua yake kwa Wakolosai, alionya hivi: “Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika.” (Wakolosai 2:18) Ibada ya malaika ya jinsi hiyo yaonekana ilikuwa imeenea katika Firgia siku hizo, lakini ilikuwa namna ya dini bandia.a Kwa kupendeza, ingawa tafsiri za Biblia hufasiri thre·skeiʹa “dini,” kwenye Wakolosai 2:18 zilizo nyingi hutumia neno “ibada.” New World Translation hutafsiri thre·skeiʹa kuwa “namna ya ibada” kwa upatano, kielezi-chini katika Reference Bible kikitaja kila mara tafsiri ya namna ile ya pili ya kusema “dini” itumiwapo katika tafsiri za Kilatini.

“Safi na Isiyo na Hitilafu” kwa Maoni ya Mungu

4, 5. (a) Kulingana na mwanafunzi Yakobo, ni maoni ya nani kuhusu dini yaliyo yenye maana zaidi? (b) Ni nini kiwezacho kufanya namna ya ibada ya mtu kuwa isiyofaa, na ni nini maana ya neno linalotafsiriwa “haifai”?

4 Mahali pengine pawili ambapo neno thre·skeiʹa hutokea pamo katika barua iliyoandikwa na mwanafunzi Yakobo, mshirika wa baraza linaloongoza la kundi la Kikristo la karne ya kwanza. Yeye aliandika hivi: “Kama mtu akijiona kuwa ni mtu mwenye dini, lakini hawezi kuutawala ulimi wake, dini [namna ya ibada, NW] yake haifai kitu, na anajidanganya [moyo wake, NW] mwenyewe. Dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu baba ni hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu huu.”—Yakobo 1:26, 27.

5 Naam, kufuata msimamo wa Yehova juu ya dini ni jambo la muhimu ikiwa twataka kupata kibali chake na kuokoka kuingia katika ulimwengu mpya ambao ameahidi. (2 Petro 3:13) Yakobo aonyesha kwamba mtu huenda akaonekana machoni pake mwenyewe kuwa mtu wa kidini kweli kweli na bado namna yake ya ibada ingeweza kuwa isiyofaa. Neno la Kigiriki lililotafsiriwa hapa “haifai” humaanisha pia “bure, -tupu, bila matokeo, -bovu, bila nguvu, -enye kukosa ukweli.” Hali ingeweza kuwa hivyo ikiwa mtu anayedai kuwa Mkristo hangezuia ulimi wake na kuutumia kumsifu Mungu na kuwajenga Wakristo wenzake. Angekuwa “akidanganya moyo wake mwenyewe,” na asingekuwa akizoea “dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu.” (HNWW) Maoni ya Yehova ndiyo yenye maana zaidi.

6. (a) Ni nini kichwa cha barua ya Yakobo? (b) Yakobo alikazia takwa lipi la dini safi, na Baraza Linaloongoza la ki-siku-hizi linataarifu nini kuhusu jambo hilo?

6 Yakobo hataji mambo yote moja moja ambayo Yehova ataka kuhusiana na ibada safi. Kwa kupatana na kichwa cha ujumla cha barua yake, ambacho ni imani inayothibitishwa kwa matendo na uhitaji wa kujiweka huru na urafiki pamoja na ulimwengu wa Shetani, yeye hukazia matakwa mawili tu. Moja ni “kuwasaidia yatima na wajane katika shida zao.” Hilo huhusisha upendo wa kweli wa Kikristo. Yehova sikuzote ameonyesha hangaiko lenye upendo kwa yatima na wajane. (Kumbukumbu la Torati 10:17, 18; Malaki 3:5) Mojawapo ya matendo ya mwanzo-mwanzo ya baraza linaloongoza la kundi la Kikristo la karne ya kwanza yalikuwa kwa niaba ya wajane Wakristo. (Matendo 6:1-6) Mtume Paulo alitoa maagizo yenye maelezo mengi ya kuandaa utunzi wenye upendo kwa wajane wazee-wazee maskini ambao walikuwa wamejithibitisha kuwa waaminifu kwa miaka mingi iliyopita na ambao hawakuwa na familia yoyote kuwasaidia. (1 Timotheo 5:3-16) Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova la ki-siku-hizi limetoa pia maagizo hususa juu ya “Kuwaangalia Maskini,” likitaarifu hivi: “Ibada ya kweli inatia ndani kuangalia waaminifu na washikamanifu ambao huenda wakahitaji msaada wa kimwili.” (Ona kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kurasa 122-3.) Mabaraza ya wazee au Wakristo mmoja mmoja wanaojionyesha wenyewe kutokuwa waangalifu katika habari hii wanaacha sehemu ya maana ya namna ya ibada safi na isiyo na taka kwa maoni ya Mungu na Baba yetu.

“Kujilinda Mwenyewe Usichafuliwe na Ulimwengu Huu”

7, 8. (a) Yakobo alitaja takwa lipi la pili la dini ya kweli? (b) Je! makasisi na mapadre hutimiza takwa hilo, lakini ni nini laweza kusemwa kuhusu Mashahidi wa Yehova?

7 Takwa la pili la dini ya kweli lililotajwa na Yakobo lilikuwa “kujilinda na dunia pasipo mawaa.” Yesu alitaarifu hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu”; kwa kupatana na hiyo, wafuasi wake wa kweli wasingekuwa “sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19; 18:36, NW) Je! hilo laweza kusemwa kuhusu makasisi na mapadre wowote wa dini za ulimwengu huu? Wanaunga mkono Umoja wa Mataifa. Wengi wa viongozi wao walikubali mwaliko wa papa wa kukutana Assisi, Italia, katika Oktoba 1986 kuunganisha sala zao kwa ajili ya kufanikiwa kwa “Mwaka wa Amani ya Kimataifa” uliodhaminiwa na UM (Umoja wa Mataifa). Hata hivyo, kwa kuamua kutokana na mamilioni waliouawa katika vita ya mwaka huo na katika miaka iliyofuata, jitihada zao zilikuwa za bure. Makasisi mara nyingi hushirikiana kirafiki pamoja na chama cha kisiasa kinachotawala, huku wakifanya kwa hila shughuli za kisiri pamoja na wapinzani ili kwamba yeyote atakayetawala atawaona kuwa “rafiki.”—Yakobo 4:4.

8 Mashahidi wa Yehova wamejipatia sifa ya kuwa Wakristo ambao hubaki wenye kutokuwamo katika mambo ya kisiasa na katika mapigano ya ulimwengu huu. Wao hudumisha msimamo huo katika bara kuu zote na katika mataifa yote, kama inavyoshuhudiwa na ripoti za watangazaji habari na rekodi za historia za ki-siku-hizi katika sehemu zote za ulimwengu. Kwa kweli wao ‘hawachafuliwi na ulimwengu huu.’ Yao ni ile “dini iliyo safi na isiyo na hitilafu mbele ya Mungu.”—Yakobo 1:27, HNWW.

Alama Nyinginezo za Dini ya Kweli

9. Takwa la tatu la dini ya kweli ni lipi, na kwa nini?

9 Ikiwa dini ni “kicho chenye staha kwa mwenye uwezo unaopita ule wa kibinadamu anayetambuliwa kuwa muumba na mtawala wa ulimwengu wote mzima,” kwa hakika ni lazima dini ya kweli ielekeze ibada kwa Mungu wa kweli wa pekee, Yehova. Haipasi kufumba uelewevu wa watu kuhusu Mungu kwa kufundisha mawazo ya kipagani kama vile mungu mmoja-katika-watatu ambaye ndani yake Baba hushiriki uweza-yote, utukufu, na umilele wake pamoja na watu wengine wawili katika Utatu wa kifumbo. (Kumbukumbu la Torati 6:4; 1 Wakorintho 8:6) Ni lazima pia ijulishe jina la Mungu, Yehova, lisilo na kifani, na kuliheshimu jina hilo, kwa kweli kulichukua jina la Mungu wakiwa watu waliofanywa tengenezo. (Zaburi 83:18; Matendo 15:14) Katika kufanya hivyo ni lazima wenye kuizoea wafuate mfano wa Kristo Yesu. (Yohana 17:6) Ni watu gani leo wanaofanya kulingana na takwa hilo isipokuwa Mashahidi Wakristo wa Yehova?

10. Ili dini itoe wokovu kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu, ni lazima ifanye nini, na kwa nini?

10 Mtume Petro alitaarifu hivi: “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine [Yesu Kristo] chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.” (Matendo 4:8-12) Kwa hiyo, ni lazima dini safi itakayotoa wokovu kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu itie imani katika Kristo na katika thamani ya dhabihu ya fidia. (Yohana 3:16, 36; 17:3; Waefeso 1:7) Isitoshe, ni lazima isaidie waabudu wa kweli wajitiishe kwa Kristo akiwa Mfalme anayetawala na Kuhani Mkuu mpakwa-mafuta wa Yehova.—Zaburi 2:6-8; Wafilipi 2:9-11; Waebrania 4:14, 15.

11. Ni lazima dini ya kweli itegemezwe na nini, na ni nini msimamo wa Mashahidi wa Yehova kuhusu hilo?

11 Ni lazima dini safi itegemezwe na mapenzi yaliyofunuliwa ya yule Mungu mmoja wa kweli, si na mapokeo au falsafa zilizofanywa na wanadamu. Hatungejua lolote juu ya Yehova na makusudi yake mazuri ajabu, wala juu ya Yesu na dhabihu ya fidia, kama isingekuwa kwa sababu ya Biblia. Mashahidi wa Yehova hukazia kikiki katika watu uhakika thabiti katika Biblia. Wao huthibitisha pia kwa maisha yao ya kila siku kwamba wanakubaliana na taarifa hii ya mtume Paulo: “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, . . . ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.”—2 Timotheo 3:16, 17.

Dini ya Kweli—Njia ya Maisha

12. Kuongezea imani, ni nini kinachohitajiwa kabisa ili ibada iwe ya kweli, na dini ya kweli ni njia ya maisha katika mambo gani?

12 Yesu alitangaza rasmi hivi: “Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.” (Yohana 4:24) Kwa hiyo, dini au namna ya ibada ya kweli si wonyesho wa nje wa kumcha Mungu unaofuata mfululizo wa vitendo vya kisherehe au kawaida za dini. Ibada safi ni ya kiroho, yenye msingi wa imani. (Waebrania 11:6) Hata hivyo, ni lazima imani hiyo iungwe mkono na matendo. (Yakobo 2:17) Dini ya kweli hukataa mitindo inayofuatwa na watu wote. Inashikamana na viwango vya Biblia vya adili na usemi ulio safi. (1 Wakorintho 6:9, 10; Waefeso 5:3-5) Wale wanaoizoea hujitahidi kwa mioyo myeupe kutokeza matunda ya roho ya Mungu katika maisha yao ya familia, kwenye kazi zao za kilimwengu, shuleni, na hata katika tafrija yao. (Wagalatia 5:22, 23) Mashahidi wa Yehova hujaribu kutosahau kamwe shauri la mtume Paulo: “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.” (1 Wakorintho 10:31) Dini yao si jambo la kufuatwa kidesturi tu; hiyo ni njia ya maisha.

13. Ibada ya kweli inahusisha nini, na ni kwa nini yaweza kusemwa kwamba Mashahidi wa Yehova ni watu wa kidini kweli kweli?

13 Bila shaka, dini ya kweli huhusisha utendaji mbalimbali wa kiroho. Huo hutia ndani sala ya kibinafsi na ya familia, funzo la kawaida la Neno la Mungu na la misaada ya kujifunza Biblia, na kuhudhuria mikutano ya kundi ya Wakristo wa kweli. Mikutano hiyo hufunguliwa na kufungwa kwa nyimbo za kumsifu Yehova na kwa sala. (Mathayo 26:30; Waefeso 5:19) Habari za kiroho zenye kujenga huchunguzwa kupitia hotuba mbalimbali na mazungumzo ya maswali na majibu ya habari zilizochapwa zipatikanazo kwa wote. Mikutano ya jinsi hiyo hufanywa kwa kawaida katika Majumba ya Ufalme yaliyo nadhifu lakini yasiyo na mapambo mengi, ambayo hutumiwa kwa makusudi ya kidini peke yake: mikutano ya kawaida, arusi, mikutano ya ukumbusho. Mashahidi wa Yehova hustahi Majumba ya Ufalme na Majumba ya Kusanyiko yao yaliyo makubwa zaidi kuwa mahali palipowekwa wakfu kwa ibada ya Yehova. Tofauti na makanisa mengi ya Jumuiya ya Wakristo, Majumba ya Ufalme si vilabu vya starehe za kijamii.

14. Ibada ilimaanisha nini kwa watu wenye kusema Kiebrania, na ni utendaji upi unaotofautisha Mashahidi wa Yehova leo?

14 Tuliona mapema kwamba wanachuo huhusianisha neno la Kigiriki linalotafsiriwa “namna ya ibada” au “dini” na kitenzi “kutumikia.” Kwa kupendeza, neno la Kiebrania linalolingana na hilo, ʼavo·dhahʹ, laweza kutafsiriwa kuwa “utumishi” au “ibada.” (Linganisha vielezi-chini vya Kutoka 3:12 na 10:26.) Kwa Waebrania, ibada ilimaanisha utumishi. Na hivyo ndivyo inavyomaanisha kwa waabudu wa kweli leo. Alama yenye maana sana katika kutofautisha dini ya kweli ni kwamba wote wanaoizoea hushiriki katika utumishi wa kimungu wa kuhubiri “habari njema ya ufalme . . . katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote.” (Mathayo 24:14; Matendo 1:8; 5:42) Ni dini gani inayojulikana ulimwenguni pote kwa ajili ya kutoa kwayo ushahidi wa peupe juu ya Ufalme wa Mungu ukiwa tumaini la pekee la ainabinadamu?

Nguvu Yenye Kuunganisha, Inayofaa

15. Ni sifa gani ya dini ya kweli iliyo yenye kutokeza?

15 Dini bandia hugawanya watu. Imesababisha, na ingali inasababisha, chuki na umwagaji damu. Tofauti na hilo, dini ya kweli huunganisha. Yesu alitaarifu hivi: “Hivyo watu wote watatambua ya kuwa ninyi mmekuwa wanafunzi wangu, mkiwa na upendo ninyi kwa ninyi.” (Yohana 13:35) Upendo unaowaunganisha Mashahidi wa Yehova huruka mipaka ya kitaifa, ya kijamii, ya kiuchumi, na ya rangi ambayo hugawanya wale wengine wa aina ya kibinadamu. Mashahidi wanasimama “imara katika roho moja, kwa moyo mmoja [waki]shindania imani ya Injili [habari njema, NW].”—Wafilipi 1:27.

16. (a) Mashahidi wa Yehova huhubiri “habari njema” gani? (b) Ni unabii gani mbalimbali unaotimizwa juu ya watu wa Yehova, na ni mibaraka gani ambayo imefuata?

16 “Habari njema” ambazo wanahubiri ni kwamba hivi karibuni kusudi la Mungu lisilobadilika litatimizwa. Kusudi lake litatekelezwa, “hapa duniani kama mbinguni.” (Mathayo 6:10) Jina tukufu la Yehova litatukuzwa, na dunia itakuwa paradiso, ambapo waabudu wa kweli wataweza kuishi milele. (Zaburi 37:29) Kwa halisi mamilioni ya watu katika nchi zote wanashiriki pamoja na Mashahidi wa Yehova, wakisema, kwa kutimiza unabii wa Biblia: “Tutakwenda pamoja nanyi, kwa maana tumesikia kwamba Mungu yu pamoja nanyi.” (Zekaria 8:23) Yehova anawabariki watu wake. “Mdogo” kwa kweli amekuwa “taifa hodari,” kundi la ulimwenguni pote lililounganishwa kikamili katika kila jambo—katika fikira, katika kazi, katika ibada. (Isaya 60:22) Hilo ni jambo ambalo dini bandia haijaweza kamwe kulitimiza.

Ushindi wa Dini Safi

17. Ni nini kinachokaribia kupata Babuloni Mkubwa, na hilo litatimizwaje?

17 Neno la Mungu lilitabiri uharibifu wa milki ya ulimwengu ya dini bandia, inayoitwa kwa ufananisho “Babuloni Mkubwa.” Biblia pia huwakilisha “wafalme,” au watawala wa kisiasa, wa dunia kwa mfano wa pembe za hayawani-mwitu. Inatuambia kwamba Mungu ataweka katika mioyo ya watawala hao kusudi la kupindua na kuharibu kabisa shirika hilo la Shetani Ibilisi lililo kama kahaba.—Ona Ufunuo 17:1, 2, 5, 6, 12, 13, 15-18, NW.b

18. Biblia inatoa sababu gani ya maana ya kuharibiwa kwa Babuloni Mkubwa, na dini bandia ilianza lini katika mwendo wayo huu wenye kuchukiza?

18 Ni kwa nini Babuloni Mkubwa anastahili uharibifu? Biblia hujibu hivi: “Ndani yake ilionekana damu ya manabii, na ya watakatifu, na ya wale wote waliouawa juu ya nchi.” (Ufunuo 18:24) Akionyesha kwamba hatia hiyo ya damu ambayo dini bandia imejiletea yarudi nyuma hata kupita mwanzo wa Babuloni, Yesu aliwalaumu viongozi wa kidini wa dini ya Kiyahudi, iliyokuwa imejiambatisha na Babuloni Mkubwa, aliposema hivi: “Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum [gehena, NW]? . . . Hivyo [itakuja] juu yenu damu yote ya haki iliyomwagika juu ya nchi, tangu damu ya Habili, yule mwenye haki.” (Mathayo 23:33-35) Naam, ni lazima dini bandia, iliyoanza duniani wakati wa uasi katika Edeni, ipate adhabu kwa ajili ya hatia yayo ya umwagaji damu wenye kuchukiza.

19, 20. (a) Waabudu wa kweli watafanya nini baada ya hukumu kutekelezwa juu ya Babuloni Mkubwa? (b) Kisha ni nini kitakachotukia, na ni tazamio gani litakalofunguliwa mbele ya waabudu wote wa kweli?

19 Baada ya uharibifu wa Babuloni Mkubwa, waabudu wa kweli duniani wataunganisha sauti zao pamoja na jamii ya waimbaji ya kimbingu inayoimba kwa sauti kubwa hivi: “Haleluya, [Msifuni Yah, NW]; . . . maana amemhukumu yule kahaba mkuu . . . na kuipatiliza damu ya watumwa wake mkononi mwake. . . . Na moshi wake hupaa juu hata milele na milele.”—Ufunuo 19:1-3.

20 Kisha sehemu nyinginezo zinazofanyiza tengenezo la Shetani linaloonekana zitaharibiwa. (Ufunuo 19:17-21) Baada ya hilo, Shetani, mwanzilishi wa dini zote bandia, na roho waovu wake watatiwa katika abiso. Hawatakuwa huru tena kuwanyanyasa waabudu wa kweli wa Yehova. (Ufunuo 20:1-3) Dini safi itakuwa imeshinda dini bandia. Wanaume na wanawake waaminifu wanaotii onyo la kimungu la kukimbia sasa kutoka katika Babuloni Mkubwa watakuwa na nafasi ya kuokoka na kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu. Huko, wataweza kuzoea dini ya kweli na kumtumikia Yehova kwa ibada, milele.

[Maelezo ya Chini]

a Kupata maelezo kuhusu ibada ya malaika inayotajwa kwenye Wakolosai 2:18, ona Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 1986, kurasa 25-26.

b Kwa maelezo kamili ya unabii huo, ona kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! kilichotangazwa na Watchtower Bible and Tract Society of New York, Inc., sura 33-6.

Jaribu Kumbukumbu Lako

◻ Ni msimamo wa nani juu ya dini ulio wa maana zaidi, na kwa nini?

◻ Yakobo alikazia matakwa gani mawili ya dini ya kweli?

◻ Matakwa mengine ya ibada safi ni gani?

◻ Mashahidi wa Yehova huhubiri “habari njema” gani?

◻ Dini ya kweli itashindaje dini bandia?

[Picha katika ukurasa wa 17]

Viongozi wa kidini walikusanyika Assisi, Italia, katika Oktoba 1986

[Picha katika ukurasa wa 19]

Dini ya kweli inahusisha kukutana pamoja kwa ajili ya ibada

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki