Je! Wakumbuka?
Je! wewe umepata matoleo ya karibuni ya Mnara wa Mlinzi yakiwa yenye thamani inayoweza kutumika kwako? Basi kwa nini usitahini kumbukumbu lako kwa yafuatayo:
▫ Ni nini lililokuwa kusudi kuu la maponyo ya Yesu?
Yalionyesha, kwa ajili ya kitia-moyo cha umati mkubwa wa watu wenye mfano wa kondoo leo, kwamba waokokaji wa Har–Magedoni wataponywa muda mfupi tu baada ya Har–Magedoni. (Isaya 33:24; 35:5, 6)—12/15, ukurasa 12.
▫ Ni kwa nini tunahitaji kile kikumbusho cha daima: “Katika sala, mkidumu”? (Warumi 12:12)
Mibano na madaraka ya maisha yaweza kutulemea sana nyakati nyingine hivi kwamba tungeweza kusahau kusali. Au huenda matatizo yakatushinda, yakitufanya tuache kushangilia katika tumaini la Ufalme, hata kukoma kusali. Hivyo, tunahitaji vikumbusho vinavyotutia moyo kusali na katika njia hiyo kumkaribia Yehova hata zaidi.—12/15, ukurasa 14.
▫ Ni nini kinachothibitisha kwamba lile Furiko la siku ya Noa liliacha kumbukumbu la ajabu lisilofutika akilini mwa jamii ya kibinadamu?
Imekadiriwa kwamba hekaya zaidi ya 500 kuhusu Furiko husimuliwa na makabila na jamii za watu zaidi ya 250. Baadhi ya mambo ya msingi yanayofanana hupatikana katika hekaya hizo zote.—1/15, ukurasa 5.
▫ Manabii wawongo leo wakoje kama wale wa wakati wa Yeremia?
Manabii wawongo wa leo hudai kumwakilisha Mungu, lakini wanaiba maneno ya Mungu kwa kuhubiri mambo yanayoondoa watu mbali na yale ambayo Biblia husema kweli kweli. Hilo ni kweli hasa kwa habari ya fundisho la Ufalme. (Yeremia 23:30)—2/1, ukurasa 4.
▫ Ni nini kinachodokezwa wakati mtu anapobatizwa kwa jina la roho takatifu?
Hilo hudokeza kwamba yule anayebatizwa anapiga moyo konde kushirikiana na roho, kutofanya jambo lolote liwezalo kuzuia utendaji wayo miongoni mwa watu wa Yehova. Kwa hiyo, ni lazima mtu huyo ashirikiane pamoja na mtumwa mwaminifu mwenye akili na pamoja na mpango wa wazee kundini. (Waebrania 13:7, 17; 1 Petro 5:1-4)—2/1, ukurasa 18.
▫ Ni kwa nini ibada ya sanamu ni yenye kumdhuru sana mwabudu?
Biblia huonyesha kwamba sanamu zinamchukiza Yehova Mungu na hazifai kitu katika kusaidia wachaji wazo kumkaribia Mungu zaidi. (Kumbukumbu la Torati 7:25; Zaburi 115:4-8) Shetani Ibilisi “amepofusha fikira” za watu ili kweli “isiwazukie.” (2 Wakorintho 4:4) Kwa hiyo mtu anapoipa sanamu heshima, kwa kweli anatumikia masilahi ya roho waovu. (1 Wakorintho 10:19, 20)—2/15, kurasa 6-7.
▫ Ni kwa nini kondoo walionwa kuwa mali yenye thamani katika nyakati za Biblia?
Sufu ilikuwa mali ilioendelea kutokea na ingeweza kutumiwa kutengenezea mavazi kwa ajili ya familia au ingeweza kuuzwa. Pembe za kondoo dume zilitumiwa kutangaza Yubile au zingeweza kutumiwa kuvumisha vionyo vya kamsa au kuelekeza vita. Kwa kuwa kondoo walikuwa mojawapo wanyama safi ambao Waisraeli wangeweza kula, kundi la kondoo lilihakikisha ugavi wa chakula, na liliandaa ugavi wa kawaida wa maziwa ya kunywewa au kutengenezea jibini.—3/1, kurasa 24-5.
▫ Wapendao Mungu huomba nini wanaposali Ufalme wa Mungu uje? (Mathayo 6:9)
Wanaomba kwamba Ufalme wa Mungu wa kimbingu uchukue hatua ya kukata maneno kwa kuharibu mifumo ya kiserikali iliyofanyizwa na mwanadamu ambayo imeshindwa kutimiza ahadi yayo ya kuleta amani na usalama. (Danieli 2:44)—3/15, ukurasa 6.
▫ Wateteaji-Ukristo walikuwa nani, na je, walifundisha Utatu?
Wateteaji-Ukristo walikuwa wanaume wa kanisa walioishi katika sehemu ya mwisho wa karne ya pili. Waliandika ili kuulinda Ukristo walioujua dhidi ya falsafa zilizoenea katika ulimwengu wa Roma. Hakuna mmoja wao aliyefundisha Utatu.—4/1, kurasa 24-9.
▫ Je! Zekaria, aliyekuwa baba wa Yohana Mbatizaji, alifanywa kiziwi na bubu, kama Luka 1:62 ionekanavyo kuonyesha?
Gabrieli alisema kwamba usemi wa Zekaria ungeathiriwa, si kusikia kwake. (Luka 1:18-20) Luka 1:64 hutaarifu hivi: “Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake pia, akaanza kunena.” Ona kwamba, hakuna lolote ambalo limetajwa hapa kuhusu kusikia kwake kuwa kulikuwa kumeathiriwa kwa njia yoyote. Mtajo wa ‘kumwashiria’ kwenye Luka 1:62 huenda ukamaanisha kwamba ishara fulani ilifanywa ili kutokeza uamuzi wa Zekaria.—4/1, ukurasa 31.