Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w92 8/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Ayubu Alilitukuza Jina la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Mambo Makuu Katika Kitabu cha Ayubu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Kitabu Cha Biblia Namba 18—Yobu
    “Kila Andiko, Lenye Pumzi ya Mungu, Lafaa”
  • Mtu Aliye Mfano Bora Ambaye Alikubali Kusahihishwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
w92 8/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je! tuelewe kutokana na Ayubu 1:8 kwamba katika kipindi alimoishi Ayubu, yeye alikuwa binadamu wa pekee aliyekuwa mwaminifu kwa Yehova?

La. Mkataa huo hauthibitishwi na Ayubu 1:8, ambalo husema hivi:

“Kisha BWANA [Yehova, NW] akamwuliza Shetani, Je! umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na uelekevu [mnyofu], mwenye kumcha Mungu na kuepukana uovu.” Mungu aliandaa kadirio hilo hilo kwenye Ayubu 2:3, akimwuliza Shetani hivi: “Je! umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na uelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.”

Kitabu cha Ayubu chenyewe huonyesha kwamba Ayubu hakuwa binadamu wa pekee aliyekuwa hai ambaye alikubaliwa na Mungu kuwa mwaminifu. Kuanzia katika sura 32, twasoma juu ya Elihu. Ingawa alikuwa mwanamume mwenye umri mdogo zaidi, Elihu alirekebisha maoni ya Ayubu yasiofaa na akamtukuza Mungu wa kweli.—Ayubu 32:6–33:6, 31-33; 35:1–36:2.

Kwa hiyo, ni lazima maneno ya Mungu kwamba ‘hapana mmoja aliye kama Ayubu duniani’ yamaanishe kwamba Ayubu alikuwa mwenye kutokeza hasa akiwa mtu mwenye unyofu. Yaelekea Ayubu aliishi katika kile kipindi kati ya kifo cha Yusufu katika Misri na mwanzoni mwa utumishi wa Musa akiwa nabii wa Mungu. Katika kipindi hicho idadi kubwa ya Waisraeli waliishi Misri. Hakuna sababu ya kufikiri kwamba wao wote hawakuwa waaminifu na hawakukubaliwa na Mungu; labda kulikuwako wengi waliomtumaini Yehova. (Kutoka 2:1-10; Waebrania 11:23) Hata hivyo, hakuna mmojawapo aliyekuwa na daraka mashuhuri, kama lile la Yusufu, wala waabudu hao hawakutokeza kwa habari ya ibada ya kweli, kama vile Musa angekuwa katika kuliongoza taifa la Israeli kutoka Misri.

Lakini, kwingineko aliishi mwanamume mwenye uaminifu-maadili wenye kutokeza. “Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na uelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.”—Ayubu 1:1.

Hivyo Yehova aliweza kumtaja Ayubu kuwa mfano wa imani na ujitoaji wenye kutazamisha au wenye kutokeza. Vivyo hivyo, waandishi wa Biblia Ezekieli na Yakobo kwa kukumbuka yaliyopita walikazia juu ya Ayubu kuwa mwenye kuweka kiolezo cha uadilifu na uvumilivu—Ezekieli 14:14; Yakobo 5:11.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki