Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w93 2/15 kur. 17-22
  • Kusitawisha Utu Mpya Katika Ndoa

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusitawisha Utu Mpya Katika Ndoa
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Kukabili Mikazo ya Ndoa
  • Imarisha ile Kani
  • Vielelezo Tofauti vya Mwenendo
  • Imarisha Kifungo cha Ndoa
  • Ndoa Inaweza Kufanikiwa Katika Ulimwengu wa Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Dumisha “Kamba Yenye Nyuzi Tatu” Katika Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Baada ya Siku ya Harusi
    Jinsi ya Kudumu Katika Upendo wa Mungu
  • Fanya Ndoa Yako Iwe Muungano Wenye Kudumu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
w93 2/15 kur. 17-22

Kusitawisha Utu Mpya Katika Ndoa

“Na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu [kani itendeshayo akili yenu, NW]; mkavae utu mpya.”—WAEFESO 4:23, 24.

1. Kwa nini ndoa haipasi ichukuliwe ki-vivi-hivi tu?

NDOA ni mojayapo hatua za maana zaidi ambazo mtu huchukua maishani, kwa hiyo haipasi kamwe kuchukuliwa ki-vivi-hivi tu. Kwa nini? Kwa sababu inahitaji kifungo pamoja na mtu mwingine chenye kudumu muda wa maisha yote. Inamaanisha kushiriki maisha yote pamoja na mtu mwingine. Uamuzi mkomavu unahitajiwa ikiwa kifungo hicho kitakuwa timamu. Inadai pia uvutano chanya ‘ukitendesha akili na hivyo kuunda utu mpya.’—Waefeso 4:23, 24, NW; linganisha Mwanzo 24:10-58; Mathayo 19:5, 6.

2, 3. (a) Ni nini kinachohitajiwa ili kuchagua mwenzi wa ndoa kwa hekima? (b) Ni nini kinachohusika katika ndoa?

2 Kuna sababu nzuri ya kutoingia katika ndoa kwa uharaka, kuvutwa upesi na tamaa zenye nguvu za mnofu. Wakati unahitajiwa ili utu na sifa za mtu mzima zisitawishwe. Ujuzi na maarifa yanayoweza kutumikia yakiwa msingi wa uamuzi timamu huja pia kwa wakati. Kisha, kuchagua mwenzi wa maisha anayefaa kwaweza kuwa na kadiri kubwa zaidi ya fanikio. Mithali ya Kihispania hutaarifu jambo hilo kwa wazi: “Ni afadhali kutembea ukiwa mseja kuliko kufunga ndoa mbaya.”—Mithali 21:9; Mhubiri 5:2.

3 Kumchagua mwenzi wa ndoa anayefaa kwa wazi ndio msingi wa ndoa yenye kufanikiwa. Ili hilo liwezekane ni lazima Mkristo atumie na kufuata miongozo ya Kibiblia, si kuongozwa na uvutio wa kimwili na mibano ya kihisiamoyo na ya kimahaba isiyofaa. Ndoa inahusisha mengi zaidi ya kuunganishwa pamoja kwa miili miwili. Ni kuunganishwa pamoja kwa nyutu mbili, malezi mawili ya familia na ya kielimu, labda tamaduni na lugha mbili. Kuunganishwa kwa watu wawili katika ndoa kwa hakika hutaka utumizi ufaao wa ulimi; kwa uwezo wa usemi twavunja au kujenga. Kutokana na hayo yote, twaona pia hekima ya shauri la Paulo la ‘kuolewa au kuoa katika Bwana tu,’ yaani, mwamini mwenzetu.—1 Wakorintho 7:39; Mwanzo 24:1-4; Mithali 12:18; 16:24.

Kukabili Mikazo ya Ndoa

4. Kwa nini mkwaruzano na uvutano hutokeo katika ndoa nyakati nyingine?

4 Hata kukiwa na msingi mzuri, kutakuwa na nyakati za mkwaruzano, mbano, na uvutano. Hayo ni ya kawaida kwa mtu yeyote iwe amefunga ndoa au la. Matatizo ya kiuchumi na ya afya yaweza kusababisha mkazo katika uhusiano wowote. Mabadiliko ya hali ya mtu yaweza kuongoza kwenye migongano ya kiutu katika ndoa zilizo bora zaidi. Jambo jingine ni kwamba hakuna yeyote awezaye kuudhibiti ulimi kikamilifu, kama Yakobo alivyotaarifu: “Twajikwaa sisi sote pia katika mambo mengi. Mtu asiyejikwaa katika kunena, huyo ni mtu mkamilifu, awezaye kuuzuia na mwili wake wote kama kwa lijamu. . . . Ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo sana uwashavyo msitu mkubwa sana.”—Yakobo 3:2, 5.

5, 6. (a) Ni nini kinachohitajiwa wakati kutoelewana kunapotokea? (b) Ni hatua gani huenda ikahitaji kuchukuliwa ili kuupoza mvunjiko katika uhusiano?

5 Wakati mibano inapotokea katika ndoa, tunaweza kudhibitije hali? Tunaweza kuzuiaje kutoelewana kusisitawi kuwa ugomvi na kisha kuwa uhusiano uliovunjika? Hapo ndipo kani itendeshayo akili inapohusika. Roho yenye kusukuma yaweza kuwa ama inayofaa ama isiyofaa, yenye kujenga na yenye mwelekeo wa kiroho au yenye kushusha heshima, yenye kutawalwa na mielekeo ya kimnofu. Ikiwa ni yenye kujenga, mtu atatenda ili kumaliza kutoelewana katika uhusiano huo, ili kuidumisha ndoa yake ikiwa kwenye mwendo ufaao. Magombano na kutokubaliana havipasi kukomesha ndoa. Tatizo laweza kusuluhishwa na kustahiana na kuelewana kwaweza kurudishwa kwa kutumia shauri la Biblia.—Warumi 14:19; Waefeso 4:23, 26, 27;

6 Chini ya hali hizo maneno haya ya Paulo yanafaa sana: “Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana [Yehova, NW] alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi. Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.”—Wakolosai 3:12-14.

7. Huenda wengine wakawa na tatizo gani katika ndoa yao?

7 Andiko hilo ni rahisi kusomwa, lakini chini ya mbano wa maisha ya ki-siku-hizi, si rahisi sana sikuzote kulitumia. Ni nini huenda likawa tatizo la msingi? Nyakati nyingine, bila kutambua, huenda ikawa Mkristo anaishi kulingana na viwango viwili tofauti. Kwenye Jumba la Ufalme, yumo miongoni mwa ndugu, na atenda kwa fadhili na ufikirio. Kisha, akiwa nyumbani, katika utaratibu wa kinyumbani, huenda akaelekea kusahau uhusiano wake wa kiroho. Humo mna mume na mke tu, “yeye” na “mke” wake. Na chini ya mbano huenda mume (au mke) akasema mambo yasiyo ya fadhili ambayo yasingetamkwa kamwe katika Jumba la Ufalme. Ni nini limetukia? Kwa muda mfupi, utu wake wa Kikristo umetoweka. Mtumishi wa Mungu amesahau kwamba yeye angali ni ndugu (au dada) Mkristo akiwa nyumbani. Kani itendeshayo akili imekuwa isiyofaa badala ya kuwa inayofaa.—Yakobo 1:22-25.

8. Tokeo laweza kuwa nini wakati kani itendeshayo akili inapokuwa haifai?

8 Tokeo ni nini? Huenda mume akaacha ‘kukaa na mke wake kwa akili, kumpa heshima, kama chombo kisicho na nguvu.’ Huenda mke asimstahi mume wake tena; “roho [yake] ya upole na utulivu” inapotea. Kani itendeshayo akili imekuwa ya kimwili badala ya kiroho. ‘Akili ya kimwili’ imeanza kudhibiti. Kwa hiyo, ni nini kiwezacho kufanywa ili kudumisha ile kani yenye kusukuma ikiwa ya kiroho na inayofaa? Ni lazima tuimarishe hali yetu ya kiroho.—1 Petro 3:1-4, 7; Wakolosai 2:18.

Imarisha ile Kani

9. Tunahitaji kufanya uchaguzi gani mbalimbali maishani?

9 Kani yenye kusukuma ni ule mwelekeo wa kiakili unaohusika wakati tunapohitaji kufanya maamuzi na uchaguzi mbalimbali. Maisha hutokeza mfululizo wa daima wa mambo ya kuchagua—mema au mabaya, yenye ubinafsi au yasiyo yenye ubinafsi, ya kiadili au yasiyo ya kiadili. Ni nini kitakachotusaidia tufanye maamuzi yafaayo? Ni ile kani itendeshayo akili ikiwa imekazwa juu ya kufanya mapenzi ya Yehova. Mtunga zaburi alisali hivi: “Ee BWANA [Yehova, NW], unifundishe njia ya amri zako, nami nitaishika hata mwisho.”—Zaburi 119:33; Ezekieli 18:31; Warumi 12:2.

10. Tunaweza kuiimarishaje kwa njia ifaayo ile kani itendeshayo akili?

10 Uhusiano wenye nguvu pamoja na Yehova utatusaidia tumpendeze na tugeuke kutoka kwa yale yaliyo mabaya, kutia na ukosefu wa uaminifu katika ndoa. Israeli walitiwa moyo ‘wafanye yaliyo mema na kuelekea machoni pa Yehova, Mungu wao.’ Lakini Mungu alishauri hivi pia: “Enyi mmpendao BWANA [Yehova, NW], uchukieni uovu.” Kulingana na amri ya saba kati ya zile Amri Kumi: “Usizini,” Waisraeli walipaswa wauchukie uzinzi. Amri hiyo ilionyesha maoni makali ya Mungu juu ya ukosefu wa uaminifu katika ndoa.—Kumbukumbu la torati 12:28; Zaburi 97:10; Kutoka 20:14; Mambo ya Walawi 20:10.

11. Tunaweza kuiimarishaje zaidi ile kani itendeshayo akili zetu?

11 Tunaweza kuiimarishaje zaidi ile kani itendeshayo akili? Kwa kuthamimi utendaji na thamani mbalimbali za kiroho. Hiyo inamaanisha ni lazima tuuridhishe uhitaji wa kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida na ni lazima tujifunze kufurahia kuzungumza pamoja mawazo na shauri la Yehova. Hisia zetu za moyoni zinapasa kuwa kama zile za mtunga zaburi: “Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, usiniache nipotee mbali na maagizo yako. Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, nisije nikakutenda dhambi. Ee BWANA [Yehova, NW], unifundishe njia ya amri zako, nami nitaishika hata mwisho. Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, naam, nitaitii kwa moyo wangu wote.”—Zaburi 119:10, 11, 33, 34.

12. Ni mambo gani yawezayo kutuunganisha katika kuonyesha akili ya Kristo?

12 Uthamini wa aina hiyo kwa ajili ya kanuni za Yehova zenye uadilifu hudumishwa si kwa kujifunza Biblia tu bali pia kwa kushiriki kwa ukawaida katika mikutano ya Kikristo na kwa kushiriki katika huduma ya Kikristo mkiwa pamoja. Mivutano hiyo miwili yenye nguvu inaweza kuiimarisha daima ile kani itendeshayo akili zetu ili sikuzote njia yetu ya maisha isiyo ya ubinafsi ionyeshe akili ya Kristo.—Warumi 15:5; 1 Wakorintho 2:16.

13. (a) Kwa nini sala ni jambo muhimu katika kuiimarisha ile kani itendeshayo akili? (b) Yesu aliweka kielelezo gani kuhusu hilo?

13 Jambo jingine ni lile ambalo Paulo anakazia katika barua yake kwa Waefeso: “Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho.” (Waefeso 6:18) Waume na wake wanahitaji kusali pamoja. Mara nyingi sala hizo huufungua moyo na kuongoza kwenye mazungumzo ya unyoofu yanayorekebisha mvunjiko wowote katika uhusiano. Katika nyakati za mkazo na kishawishi, tunahitaji kumgeukia Mungu katika sala, tukiomba msaada, na nguvu ya kiroho ya kufanya yale yanayokubaliana na akili ya Kristo. Hata Yesu aliyekuwa mkamilifu alimgeukia Baba yake katika sala kwenye pindi nyingi, akiomba nguvu. Sala zake zilikuwa zenye kuhisiwa moyoni na zenye bidii. Leo vilevile, katika nyakati za kishawishi, tunaweza kupata nguvu ya kufanya uamuzi ufaao kwa kumwitia Yehova atusaidie tukinze tamaa ya kushindwa na mnofu na kusaliti nadhiri ya ndoa.—Zaburi 119:101, 102.

Vielelezo Tofauti vya Mwenendo

14, 15. (a) Yusufu alitendaje aliposhawishwa? (b) Ni nini kilichomsaidia Yusufu akinze kishawishi?

14 Tunaweza kukabilije kishawishi? Kwa habari hiyo tuna tofauti ya wazi kati ya mwendo uliochukuliwa na Yusufu na ule wa Daudi. Wakati mke wa Potifa alipojaribu kwa udumifu kumtongoza Yusufu mwenye sura nzuri, ambaye yaonekana alikuwa mseja wakati huo, alimjibu hatimaye kwa kusema hivi: “Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala [mume wako] hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?”—Mwanzo 39:6-9.

15 Ni nini kilichomsaidia Yusufu afanye uamuzi ufaao hali ingalikuwa rahisi sana kushindwa? Alikuwa na kani yenye nguvu iliyotendesha akili yake. Alifikiria sana uhusiano wake pamoja na Yehova. Yeye alijua kwamba kufanya uasherati pamoja na mwanamke huyo mwenye mahaba kwa kweli kungalikuwa dhambi si dhidi ya mume wake tu, bali kwa umaana zaidi, dhidi ya Mungu.—Mwanzo 39:12.

16. Daudi alitendaji aliposhawishwa?

16 Tofauti na hilo, ni nini kilichompata Daudi? Alikuwa mwanamume aliyeoa, mwenye wake kadhaa kama ilivyoruhusiwa na Sheria. Jioni moja alimtazama mwanamke akioga kutoka kwa jumba lake la kifalme. Alikuwa ni yule Bath-sheba mrembo, mke wa Uria. Kwa wazi Daudi aliweza kuchagua jambo la kufanya—kuendelea kutazama huku uchu ukikua moyoni mwake au kugeuka na kukatalia mbali kishawishi hicho. Alichagua kufanya nini? Aliamuru Bath-sheba aletwe kwenye jumba lake la kifalme, akafanya uzinzi naye. Hata kwa ubaya zaidi, alichukua hatua zaidi ya kusababisha kifo cha mume wake.—2 Samweli 11:2-4, 12-27.

17. Twaweza kutambua mambo gani juu ya hali ya kiroho ya Daudi?

17 Tatizo la Daudi lilikuwa nini? Kutokana na ungamo lake lenye toba katika Zaburi 51, twaweza kutambua mambo fulani ya hakika. Alisema hivi: “Ee, Mungu, uniumbie moyo safi, uifanye upya roho iliyotulia ndani yangu.” Ni wazi kwamba katika pindi ya kishawishi chake, hakuwa na roho safi na iliyotulia. Labda alikuwa amepuuza kusoma kwake Sheria ya Yehova, na likiwa tokeo, hali yake ya kiroho ilidhoofika. Au huenda ikawa aliruhusu cheo na mamlaka yake akiwa Mfalme ifisidi kufikiri kwake hivi kwamba aliangukia mtego wa tamaa yenye uchu. Kwa hakika, kani iliyotendesha akili yake wakati huo ilikuwa yenye ubinafsi na yenye dhambi. Hivyo, alikuja kutambua uhitaji wake wa ‘roho mpya, iliyotulia.’—Zaburi 51:10; Kumbukumbu la Torati 17:18-20.

18. Yesu alitoa shauri gani juu ya uzinzi?

18 Baadhi ya ndoa za Kikristo zimeharibika kwa sababu mwenzi mmoja au wote wawili wamejiruhusu waangukie hali ya udhaifu wa kiroho kama ile ya Mfalme Daudi. Kielelezo chake chapasa kituonye dhidi ya kuendelea kumtazama mwanamke, au mwanamume mwingine kwa ashiki, kwani uzinzi waweza kufuata hatimaye. Yesu alionyesha kwamba alizielewa hisia-moyo za kibinadamu kuhusu hilo, kwani alisema hivi: “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini; lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.” Katika hali hiyo, kani itendeshayo akili ni yenye ubinafsi na ya kingono, si ya kiroho. Basi, Wakristo wanaweza kufanya nini ili kuepuka uzinzi na kudumisha ndoa zao zikiwa zenye furaha na zenye kuridhisha?—Mathayo 5:27, 28.

Imarisha Kifungo cha Ndoa

19. Ndoa inaweza kuimarishwaje?

19 Mfalme Sulemani aliandika hivi: “Ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi.” Kwa hakika, wawili katika ndoa yenye upatano wanaweza kusimama pamoja katika dhiki kuliko mmoja. Lakini kifungo chao kikiwa kama kamba ya nyuzi tatu kwa kuwa na Mungu ndani yacho, ndoa itakuwa imara. Na Mungu anaweza kuwaje katika ndoa? Kwa wenzi wa ndoa kutumia kanuni na shauri lake kwa ndoa.—Mhubiri 4:12.

20. Ni shauri gani la Biblia liwezalo kumsaidia mume?

20 Kwa hakika, mume akitumia shauri la maandiko yafuatayo ndoa yake itakuwa na msingi bora zaidi wa mafanikio:

“Ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.”—1 Petro 3:7.

“Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake. Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe.”—Waefeso 5:25, 28.

“Mumewe naye humsifu, na kusema, Binti za watu wengi wamefanya mema, lakini wewe umewapita wote.”—Mithali 31:28, 29.

“Je! mtu aweza kukanyaga makaa ya moto, na nyayo zake zisiungue? Ndivyo alivyo aingiaye kwa mke wa jirani yake; kila mtu amgusaye huyo atakuwa na hatia. Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.”—Mithali 6:28, 29, 32.

21. Ni shauri gani la Biblia liwezalo kumsaidia mke?

21 Mke akitoa uangalifu kwa mafundisho ya Biblia yafuatayo, hiyo itachangia udumifu wa ndoa yake:

“Ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno; wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu [na] roho [yako] ya upole na utulivu.”—1 Petro 3:1-4.

“Mume na ampe mkewe haki yake [ya kingono]; na vivyo hivyo mke na ampe mumewe haki yake. . . . Msinyimane isipokuwa mmepatana kwa muda.”—1 Wakorintho 7:3-5.

22. (a) Ni mambo gani mengine yawezayo kuwa na matokeo mazuri kwa ndoa? (b) Yehova huonaje talaka?

22 Biblia huonyesha pia kwamba upendo, fadhili, huruma, saburi, uelewevu, kitia-moyo, na pongezi ni mambo mengi ya muhimu ya ndoa. Ndoa bila mambo hayo ni kama mmea bila mwanga wa jua na maji—unachanuka mara chache. Kwa hiyo acheni kani itendeshayo akili zetu itusukume tutiane moyo na kuburudishana katika ndoa yetu. Kumbuka kwamba Yehova ‘huchukia kutaliki.’ Ikiwa upendo wa Kikristo unazoewa hakupasi kuwako uwezekano wa uzinzi na kuporomoka kwa ndoa. Kwa nini? “Kwa sababu upendo haushindwi kamwe.”—Malaki 2:16; 1 Wakorintho 13:4-8, NW; Waefeso 5:3-5.

Je! Waweza Kueleza?

◻ Ni nini jambo la msingi kwa ndoa yenye furaha?

◻ Kani itendeshayo akili inaweza kuathirije ndoa?

◻ Tunaweza kufanya nini ili kuiimarisha kani itendeshayo akili zetu?

◻ Yusufu na Daudi walitendaje kwa njia tofauti walipokuwa chini ya kishawishi?

◻ Ni shauri gani la Biblia litakalowasaidia waume na wake waimarishe kifungo cha ndoa?

[Picha katika ukurasa wa 18]

Je! sisi huishi kwa viwango viwili tofauti—tukiwa wenye fadhili kutanoni na wakali nyumbani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki