Maswali Kutoka kwa Wasomaji
Nyakati nyingine sisi husikia ndugu wakisema au wakisali kwamba Ufalme wa Mungu uje duniani. Je, usemi huo ni sawa?
Tukisema kihalisi, hiyo si njia ya Kimaandiko ya kueleza jinsi ufalme utakavyokuja. Ufalme wa Mungu ni wa kimbingu. Hivyo, mtume Paulo aliweza kuandika hivi: “Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina.”—2 Timotheo 4:18; Mathayo 13:44; 1 Wakorintho 15:50.
Ufalme ulisimamishwa mbinguni katika 1914, nao hautahamishwa kamwe kwenye Paradiso itakayorudishwa ya kidunia wala hautahamishwa penginepo. Yesu Kristo ni Mfalme wa huo Ufalme. Akiwa Mfalme, Yesu ana mamlaka juu ya malaika. Hivyo, mahali pake pafaapo pa kutawala ni upande wa kuume wa Mungu mbinguni. Wakristo watiwa-mafuta wajiunga naye wakiwa wafalme na makuhani mbinguni.—Waefeso 1:19-21; Ufunuo 5:9, 10; 20:6.
Basi, je, hilo lamaanisha kwamba hatupaswi tena kumtajia Mungu dua zipatikanazo katika sehemu ya Sala ya Bwana isemayo: “Ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni?” (Mathayo 6:9, 10) Tofauti na hilo, sala hiyo yafaa nayo ingali imejaa maana.
Ufalme wa Mungu bado utatenda kwa njia ya kukata maneno kuhusu dunia, nasi hufikiria jambo hilo tunaposali na kutumia usemi mbalimbali unaofanana na yale maneno ya Sala ya Bwana. Kwa kielelezo, Danieli 2:44 hutabiri kwamba huo Ufalme ‘utakuja’ kuharibu mataifa yote nao utaanza kutawala dunia hii. Ufunuo 21:2 husema juu ya Yerusalemu Mpya ikishuka kutoka mbinguni. Yerusalemu Mpya imefanyizwa na Wakristo watiwa-mafuta 144,000 ambao watakuwa bibi-arusi wa Kristo. Wao pia ni warithi wenzi pamoja na Yesu katika huo Ufalme. Hivyo Ufunuo 21:2 hufafanua kuelekezea kwao fikira duniani, kwa baraka zilizo kubwa kwa wanadamu watiifu.—Ufunuo 21:3, 4.
Mpaka unabii huo na mwingine mbalimbali mzuri ajabu utakapotimizwa, ni sawa kuendelea kumwomba Yehova Mungu kwa kupatana na maneno ya Yesu, “Ufalme wako uje.” Lakini tukumbuke kwamba huo Ufalme hautakuja katika sayari Dunia kihalisi. Serikali ya Ufalme ipo mbinguni, wala si duniani.
[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 31]
Dunia: Kwa kutegemea picha ya NASA