‘Twahitaji Watu Wenye Kufuatia Haki’
UFUATIAJI WA HAKI ni haba katika ulimwengu wa leo. Hata hivyo, ni takwa la msingi kwa Wakristo. Paulo aliandika hivi: “Twataka kujiendesha wenyewe kwa kufuata haki katika mambo yote.” (Waebrania 13:18) Ndivyo alivyotaka kufanya Wilma, mmojawapo wa Mashahidi wa Yehova katika Faenza, Italia.
Gazeti la habari Il Resto del Carlino lasimulia kwamba yeye alipopata kibeti chenye kiasi kikubwa cha fedha nje ya duka kubwa katika jiji lake, alimpa polisi kibeti hicho “bila kusita” ili kiweze kurudishwa kwa mwenyewe.
Meya aliposikia juu ya hilo, mara moja alimtumia Wilma barua fupi ya shukrani. “Katika jina la hili Jiji,” akaandika, “nakushukuru sana kwa hatua nzuri uliyochukua. Jiji letu lenye kutokeza la Faenza lahitaji watu wema na wenye kufuatia haki.”
Iwe matendo mema yapata kujulikana au la, twapaswa sikuzote kujitahidi kuwa wenye kufuatia haki. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu, “tunajaribu kufanya lililo sawa si machoni pa Mungu tu bali pia machoni pa wanadamu.”—2 Wakorintho 8:21, The Jerusalem Bible.