Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w00 1/1 uku. 29
  • Washiriki Wapya wa Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Washiriki Wapya wa Baraza Linaloongoza
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Habari Zinazolingana
  • Washiriki Wapya wa Baraza Linaloongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • ‘Aliijua Njia’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mshiriki Mpya wa Baraza Linaloongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mshiriki Mpya wa Baraza Linaloongoza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
w00 1/1 uku. 29

Washiriki Wapya wa Baraza Linaloongoza

MNAMO Jumamosi, Oktoba 2, 1999, Mkutano wa Kila Mwaka wa Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania ulimalizika kwa tangazo ambalo halikutarajiwa. Watu 10,594 waliohudhuria au waliosikiliza kupitia simu walisisimka kusikia kwamba washiriki wapya wanne walikuwa wameongezwa kwenye Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova. Washiriki hao wapya, wote Wakristo watiwa-mafuta, ni Samuel F. Herd; M. Stephen Lett; Guy H. Pierce; na David H. Splane.

• Samuel Herd alianza upainia mwaka wa 1958, na tokea 1965 hadi 1997, alikuwa mwangalizi wa mzunguko na wa wilaya. Kisha, yeye na mke wake, Gloria, wakawa washiriki wa familia ya Betheli ya Marekani, ambako Ndugu Herd amekuwa akitumikia katika Idara ya Utumishi. Pia alikuwa akitumikia akiwa msaidizi wa Halmashauri ya Utumishi.

• Stephen Lett alianza upainia Desemba 1966, na tokea 1967 hadi 1971, alitumikia katika Betheli kule Marekani. Mnamo Oktoba 1971, alioa mke wake, Susan, wakaanza utumishi wa painia wa pekee. Akawa mwangalizi wa mzunguko tokea 1979 hadi 1998. Tangu Aprili 1998, yeye na Susan wamekuwa washiriki wa familia ya Betheli ya Marekani. Huko alitumikia katika Idara ya Utumishi na alikuwa msaidizi wa Halmashauri ya Kufundisha.

• Guy Pierce alilea watoto kisha yeye na mke wake wakaanza upainia Aprili 1982. Akatumikia akiwa mwangalizi wa mzunguko tokea 1986 hadi 1997, wakati ambapo yeye na mke wake, Penny, walijiunga na familia ya Betheli ya Brooklyn. Ndugu Pierce alikuwa akitumikia akiwa msaidizi wa Halmashauri ya Wafanyakazi.

• David Splane alianza upainia Septemba 1963. Alihitimu darasa la 42 la Gileadi, akatumikia akiwa mishonari nchini Senegal, Afrika, kisha akawa mwangalizi wa mzunguko nchini Kanada kwa miaka 19. Yeye pamoja na mke wake, Linda, wamekuwa washiriki wa Betheli ya Marekani tangu mwaka wa 1990, ambako Ndugu Splane ametumikia katika idara ya Utumishi na ya Uandikaji. Tangu mwaka wa 1998, amekuwa msaidizi wa Halmashauri ya Uandikaji.

Kuongezea hao washiriki wapya wanne, sasa Baraza Linaloongoza lina C. W. Barber, J. E. Barr, M. G. Henschel, G. Lösch, T. Jaracz, K. F. Klein, A. D. Schroeder, L. A. Swingle, na D. Sydlik. Sote tunasali kwamba Yehova ataendelea kubariki na kuimarisha Baraza Linaloongoza, ambalo sasa limeongezeka, linapoendelea kusimamia utendaji wa watu wa Mungu ulimwenguni kote na kutumikia masilahi yao ya kiroho.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki