Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w00 9/1 kur. 17-18
  • “Nyakati za Kurudishwa” Zimekaribia!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Nyakati za Kurudishwa” Zimekaribia!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Wakati wa Kurudishwa Waanza
  • Kurudishwa Zaidi Kwakaribia!
  • Uwezo wa Kurudisha Hali Nzuri—Yehova ‘Anafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya’
    Mkaribie Yehova
  • “Nyakati za Kurudishwa kwa Mambo Yote”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • “Nitawapa Moyo Wenye Umoja”
    Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Kile Ambacho Kuja Kwa Kristo Kutatimiza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2000
w00 9/1 kur. 17-18

“Nyakati za Kurudishwa” Zimekaribia!

Muda mfupi kabla Yesu hajapaa mbinguni, baadhi ya wanafunzi wake waaminifu walimwuliza hivi: “Bwana, je, wakati huu unarudishia Israeli Ufalme?” Jibu la Yesu lilidokeza kwamba wakati fulani ungepita kabla ya Ufalme huo kuja. Katika wakati huo, wafuasi wake wangekuwa na kazi kubwa ya kufanya. Wangekuwa mashahidi wa Yesu “katika Yerusalemu na pia katika Yudea yote na Samaria na hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.”—Matendo 1:6-8.

MGAWO huo haungeweza kutimizwa kwa muda wa siku, majuma, au miezi michache. Hata hivyo, wanafunzi hao walianza kuhubiri bila kusita hata kidogo. Lakini hawakuacha kupendezwa na habari iliyohusu kurudishwa. Mtume Petro aliongea na umati mkubwa uliokusanyika Yerusalemu juu ya kurudishwa, akisema: “Tubuni na mgeuke kabisa ili mpate kufutiwa dhambi zenu, ili majira ya kuburudisha yapate kuja kutoka kwa utu wa Yehova na kwamba apate kumtuma Kristo aliyewekwa rasmi kwa ajili yenu, Yesu, ambaye mbingu, kwa kweli, lazima imweke ndani yayo yenyewe hadi nyakati za kurudishwa kwa mambo yote ambayo Mungu alisema kupitia kinywa cha manabii wake watakatifu wa wakati wa kale.”—Matendo 3:19-21.

Hizo “nyakati za kurudishwa” zingeleta “majira ya kuburudisha” kutoka kwa Yehova. Kurudishwa huko kulikotabiriwa kungefanyika katika hatua mbili. Kwanza, kungekuwa na kurudishwa kwa kiroho kwenye kuburudisha, ambako sasa kunaendelea. Pili, kungefuatwa na kusimamishwa kwa paradiso halisi duniani.

Wakati wa Kurudishwa Waanza

Kama ambavyo mtume Petro alivyotajia umati ule Yerusalemu, mbingu ‘ilimweka Yesu ndani yayo yenyewe.’ Ndivyo ilivyokuwa hadi mwaka 1914, Yesu alipochukua nguvu yake ya kifalme akaanza kutawala akiwa Mfalme aliyewekwa rasmi wa Mungu. Petro alitabiri kwamba wakati huo Yehova ‘angemtuma’ Mwana wake katika maana ya kwamba Yeye angemruhusu Yesu atimize fungu lake akiwa mhusika mkuu katika makusudi ya Mungu. Biblia hufafanua tukio hilo kwa lugha ya ufananisho: “Naye [tengenezo la kimbingu la Mungu] akazaa mwana, wa kiume, [Ufalme wa Mungu mikononi mwa Yesu Kristo] atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma.”—Ufunuo 12:5.

Lakini mataifa hayakuwa na nia ya kuukubali utawala wa Kristo. Kwa kweli, yalishambulia raia zake wa kidunia walio waaminifu-washikamanifu, waitwao leo Mashahidi wa Yehova. Kama mitume waliokuwa watangulizi wao, Mashahidi walikuwa wamechukua “kazi ya kutoa ushahidi kuhusu Yesu” bila kusita. (Ufunuo 12:17) Upinzani dhidi ya kazi waliyokuwa wakifanya Wakristo hawa wenye mioyo myeupe ulipamba moto nchi moja baada ya nyingine. Mwaka 1918, washiriki wenye daraka miongoni mwa wafanyakazi wa makao makuu ya Watch Tower Society katika Brooklyn, New York, waliburutwa mpaka mahakamani juu ya msingi wa mashtaka ya kutungwa na kuhukumiwa isivyo haki vifungo virefu gerezani. Kwa muda fulani ilionekana kwamba kazi ya kisasa ya kutoa ushahidi “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia” ingeshindwa.—Ufunuo 11:7-10.

Hata hivyo, mwaka 1919, washiriki waliofungwa gerezani wa wafanyakazi wa makao makuu waliachiliwa na baadaye wakaondolewa mashtaka hayo yote ya uwongo. Bila kupoteza wakati waliendeleza kazi ya kurudishwa kwa kiroho. Tangu wakati huo, watu wa Yehova wamekuwa wakionea shangwe ufanisi wa kiroho usio na kifani.

Kampeni kubwa ilianzishwa ya kufundisha watu wa mataifa yote washike mambo ambayo Kristo alikuwa amewaamuru wafuasi wake wafanye. (Mathayo 28:20) Iliburudisha kama nini kuona wengine waliokuwa hapo kwanza wameonyesha tabia za kinyama wakibadili mtazamo wao! Walivua kabisa utu wa zamani, ambao hutokeza tabia kama vile “hasira,” “usemi wenye kuudhi,” na “maongezi yenye aibu,” wakavaa utu mpya, “ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa kuwa mpya kulingana na mfano wa [Mungu] aliyeuumba.” Katika maana ya kiroho, maneno ya nabii Isaya yanatimizwa hata sasa: “Mbwa-mwitu [mtu ambaye hapo kwanza alionyesha tabia kama za mbwa-mwitu] atakaa pamoja na mwana-kondoo [mtu aonyeshaye mwelekeo wa upole], na chui atalala pamoja na mwana-mbuzi; ndama na mwana-simba na kinono watakuwa pamoja.”—Wakolosai 3:8-10; Isaya 11:6, 9.

Kurudishwa Zaidi Kwakaribia!

Kuongezea kurudishwa ambako kumetokeza paradiso ya kiroho leo, wakati unakaribia kwa haraka ambapo sayari yetu itakuwa paradiso halisi. Yehova alipoweka wazazi wetu wa kale, Adamu na Hawa, katika shamba la Edeni, sehemu ndogo ya dunia ilikuwa paradiso. (Mwanzo 1:29-31) Ndiyo sababu twaweza kuongea juu ya Paradiso kurudishwa. Lakini, kabla hilo halijatokea, lazima dunia iondolewe dini isiyo ya kweli inayomdharau Mungu. Sehemu za kisiasa za ulimwengu huu zitafanya hivyo. (Ufunuo 17:15-18) Kisha, sehemu za kisiasa na kibiashara, pamoja na wenye kuzitegemeza wataharibiwa. Hatimaye, wapinzani wa mwisho wa Mungu—Shetani Ibilisi na roho zake waovu—watafungiwa miaka elfu moja—kipindi kinacholingana na muda wa mradi wa kurudishwa. Wakati huo, “nyika na mahali palipo ukiwa patafurahi; jangwa litashangilia na kuchanua maua kama waridi.” (Isaya 35:1) Dunia yote itakuwa haina vurugu. (Isaya 14:7) Hata mamilioni waliokufa watarudishwa kwenye uhai duniani. Wote watapata manufaa za kurudishwa za dhabihu ya fidia. (Ufunuo 20:12-15; 22:1, 2) Hakutakuwako watu vipofu, viziwi, au vilema duniani. “Hapana mwenyeji atakayesema, Mimi mgonjwa.” (Isaya 33:24) Muda mfupi baada ya mwisho wa ile Miaka Elfu ya Utawala wa Kristo, Ibilisi na roho zake waovu wataachiliwa kwa kipindi kifupi na wataona jinsi ambavyo kusudi la Mungu kwa ajili ya dunia limetimizwa kufikia hapo. Mwishowe, wataharibiwa milele.—Ufunuo 20:1-3.

Dunia ifikiapo mwisho wa miaka elfu ya kurudishwa, “kila kiumbe hai” watamsifu Yehova nao watafanya hivyo kwa umilele wote. (Zaburi 150:6, Biblia Habari Njema) Je, wewe utakuwa mmoja kati yao? Yawezekana uwe.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki