Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 1/15 uku. 31
  • Tangazo Maalumu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tangazo Maalumu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi Baraza Linaloongoza Linavyotofautiana na Shirika la Kisheria
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Kushirikiana na Baraza Linaloongoza Leo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1990
  • Jukumu la “Mtumwa Mwaminifu na Mwenye Busara”
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Uwe Mshikamanifu kwa Kristo na kwa Mtumwa Wake Mwaminifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 1/15 uku. 31

Tangazo Maalumu

MWISHONI mwa mkutano wa kila mwaka wa shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania Oktoba 7, 2000, tangazo maalumu lilitolewa na mwenyekiti John E. Barr wa Baraza Linaloongoza. Tangazo hilo lilitegemea hotuba zilizotolewa hapo awali na Theodore Jaracz na Daniel Sydlik.—Ona ukurasa wa 12-16 na 28-31 wa gazeti hili.

Akizungumzia jambo fulani muhimu sana, Ndugu Barr alisema: “‘Mtumwa mwaminifu na mwenye busara’ na Baraza lake Linaloongoza wamekabidhiwa masilahi ya juu zaidi, yanayotia ndani mambo mengi kuliko yale ambayo yamekabidhiwa mashirika ya kisheria. Makusudi ya kila mojawapo ya mashirika hayo, kama yalivyoandikwa kwenye mkataba, yana mipaka. Hata hivyo, Bwana-Mkubwa wetu Yesu Kristo, ameiweka rasmi jamii ya mtumwa mwaminifu juu ya ‘mali’ yake yote, au masilahi ya Ufalme hapa duniani.”—Mathayo 24:45-47.

Kuhusu shirika la Pennsylvania, Ndugu Barr aliongeza: “Tangu lilipoanzishwa mwaka wa 1884, shirika la Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania limetimiza jukumu muhimu katika historia yetu ya sasa. Hata hivyo, hilo ni shirika la kisheria tu linaloweza kutumiwa na ‘mtumwa mwaminifu na mwenye busara’ inapohitajika.”

Katika hotuba zao, Ndugu Sydlik na Ndugu Jaracz walikuwa wameeleza kwamba ule ukweli kuwa “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” amekabidhiwa mali yote ya kidunia ya Bwana, hauzuii jamii ya mtumwa kuruhusu wanaume wenye sifa za kustahili kutoka miongoni mwa “kondoo wengine” kushughulikia majukumu fulani ya kawaida ya usimamizi. (Yohana 10:16) Wala hakuna sababu yoyote ya Kimaandiko inayowataka wote au wowote wa waelekezi wa mashirika ya kisheria yanayotumiwa na Mashahidi wa Yehova wawe Wakristo watiwa-mafuta.

Ndugu Barr aliwaambia wasikilizaji kwamba hivi majuzi washiriki fulani wa Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova ambao walikuwa wanatumikia wakiwa waelekezi na wasimamizi walijiuzulu bila kulazimishwa kutoka katika mabaraza ya waelekezi ya mashirika yote yanayotumiwa na “mtumwa mwaminifu na mwenye busara” huko Marekani. Ndugu wenye kutumainika wa jamii ya kondoo wengine walichaguliwa kuchukua mahali pao.

Uamuzi huo ni wenye manufaa kwelikweli. Unawawezesha washiriki wa Baraza Linaloongoza kutumia wakati mwingi zaidi wakitayarisha chakula cha kiroho na kushughulikia mahitaji ya kiroho ya ndugu ulimwenguni kote.

Kwa kumalizia, mwenyekiti aliwaambia hivi wasikilizaji wake wenye furaha: “Ingawa majukumu kadhaa ya kisheria na ya usimamizi yamepewa waangalizi wenye uzoefu, . . . wote wanatumikia chini ya mwelekezo wa Baraza Linaloongoza. . . . Sote tunamtegemea Yehova kwa sala ili abariki jitihada zetu za pamoja za kufanya mapenzi yake, kwa heshima na utukuzo wa jina lake kuu.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki