Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w01 2/1 uku. 8
  • Latvia Yaitikia Habari Njema

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Latvia Yaitikia Habari Njema
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Habari Zinazolingana
  • Hakuwa Mzee Mno Asimtumikie Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
  • Mwalimu Abadili Maoni Yake
    Amkeni!—2009
  • Igeni Mtazamo wa Manabii
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Haijawa Kuchelewa Sana Kumtumikia Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
w01 2/1 uku. 8

Wapiga-mbiu wa Ufalme Waripoti

Latvia Yaitikia Habari Njema

BIBLIA yaonyesha wazi kwamba ni mapenzi ya Mungu kwamba “watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Timotheo 2:4) Wale ambao kwa miaka mingi walinyimwa fursa ya kusikia habari njema sasa wanazisikia! Nchini Latvia, kama sehemu nyinginezo za ulimwengu, watu wa umri wote na malezi mbalimbali wanaitikia ujumbe huo, kama mambo yaliyoonwa yafuatayo yaonyeshavyo.

• Huko Rēzekne, mji ulio mashariki mwa Latvia, mama na binti yake kijana walimwomba mwanamke fulani barabarani awaonyeshe njia. Baada ya kuwaonyesha, mwanamke huyo aliyekuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, aliwaalika kwenye mikutano ya Mashahidi.

Kwa kuwa mama na binti huyo walipendezwa na mambo ya dini, waliamua kwenda kwenye mkutano. Wakiwa njiani, walikubaliana kwamba wakiona jambo lisilofaa kwenye mkutano huo, wataondoka mara moja. Lakini mkutano huo ulikuwa wenye kupendeza sana hivi kwamba hawakufikiria kuondoka. Walikubali funzo la Biblia, na wakaanza kuhudhuria mikutano kwa ukawaida. Baada ya muda wa miezi mitatu tu, walitaka kuwa wahubiri na walitazamia ubatizo kwa hamu.

• Katika jiji fulani huko Latvia magharibi, Shahidi mmoja alikutana na Anna mwenye umri wa miaka 85, ambaye alipendezwa sana na kukubali funzo la Biblia. Binti yake na watu wengine wa familia yake walimpinga vikali. Lakini Anna hakuruhusu upinzani wala uzee na afya mbaya imzuie kuendelea kujifunza Biblia.

Siku moja, Anna alimwambia binti yake kwamba atabatizwa. “Ukibatizwa, nitakupeleka kwa makao ya kutunzia wazee,” binti yake akajibu. Hata hivyo, tisho hilo halikumvunja moyo Anna. Kwa sababu ya afya yake, alibatizwa nyumbani mwake.

Binti yake alifanyaje kuhusiana na jambo hilo? Alibadili msimamo wake, akatayarisha mlo wa pekee kwa ajili ya mama yake baada ya ubatizo. Kisha akamwuliza mama yake hivi, “Unahisije kwa kuwa sasa umebatizwa?” Anna alijibuje? “Kama mtoto aliyetoka tu kuzaliwa!”

• Mnamo Desemba 1998, Mashahidi wawili walikutana na ofisa wa jeshi aliyestaafu wa ule uliokuwa Muungano wa Sovieti. Kwa kuwa aliamini kuna Muumba, alikubali funzo la Biblia, na baadaye mke wake akajiunga naye. Walifanya maendeleo haraka na muda si muda wakawa wahubiri wasiobatizwa. Kufikia kiangazi kilichofuata, mtu huyo aliyekuwa ofisa alibatizwa. Upendo huo mkubwa wa wenzi hao kwa mambo ya kiroho umewatia moyo wote katika kutaniko lao. Isitoshe, walitumia nguvu zao katika kazi ya kurekebisha nyumba moja ya mahali hapo kuwa Jumba zuri la Ufalme.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki