Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w04 3/15 uku. 3
  • Mwadhimisho Unaokuhusu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mwadhimisho Unaokuhusu
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Mlo wa Jioni wa Bwana—Maadhimisho Yanayomletea Mungu Heshima
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • ‘Fanyeni Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kwa Nini Tuadhimishe Mlo wa Jioni wa Bwana?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Mlo wa Jioni wa Bwana Huadhimishwaje?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2004
w04 3/15 uku. 3

Mwadhimisho Unaokuhusu

YESU KRISTO alipokuwa duniani, alianzisha mwadhimisho unaomtukuza Mungu. Hii ndiyo sherehe pekee ya kidini ambayo aliwaagiza wafuasi wake moja kwa moja waiadhimishe, nayo ni Mlo wa Jioni wa Bwana.

Wazia kwamba wewe ni mtazamaji asiyeonekana wa matukio yaliyoongoza kwenye sherehe hiyo. Yesu na mitume wake wamekutanika pamoja katika chumba cha juu huko Yerusalemu ili waadhimishe Pasaka ya Wayahudi. Wamemaliza kula chakula kilicholiwa wakati wa Pasaka, yaani, mwana-kondoo aliyechomwa, mboga chungu, mkate usiotiwa chachu, na divai nyekundu. Mtume Yuda Iskariote, asiye mwaminifu, amefukuzwa na baada ya muda mfupi atamsaliti Bwana wake. (Mathayo 26:17-25; Yohana 13:21, 26-30) Yesu yuko peke yake pamoja na mitume wake waaminifu 11. Mathayo ni mmoja wao.

Kulingana na masimulizi ya Mathayo aliyejionea tukio hilo, hivi ndivyo Yesu anavyoanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana: “Yesu alichukua mkate [usiotiwa chachu] na, baada ya kutoa baraka, akaumega, akawapa wanafunzi, akasema: ‘Chukueni, mle. Huu unamaanisha mwili wangu.’ Pia, akachukua kikombe na, akiisha kushukuru, akawapa, akisema: ‘Kinyweeni, ninyi nyote; kwa maana hii inamaanisha ‘damu yangu ya agano,’ ambayo itamwagwa kwa ajili ya wengi kwa msamaha wa dhambi.’”—Mathayo 26:26-28.

Kwa nini Yesu alianzisha Mlo wa Jioni wa Bwana? Alipoanzisha mlo huo, kwa nini alitumia mkate usiotiwa chachu na divai nyekundu? Je, wafuasi wote wa Kristo wangekula na kunywa mifano hiyo? Mlo huo ulipaswa kuadhimishwa mara ngapi? Je, kweli una maana kwako?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki