Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w05 2/15 uku. 9
  • Biblia ya Berleburg

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia ya Berleburg
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Habari Zinazolingana
  • “New World Translation” ya Utaalamu na Yenye Kufuatia Haki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Hatua Muhimu kwa Wapendao Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Tafsiri ya New World Translation Inathaminiwa na Mamilioni ya Watu Ulimwenguni Pote
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2001
  • Tafsiri Bora ya Neno la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
w05 2/15 uku. 9

Biblia ya Berleburg

HARAKATI ya kidini iliyoitwa pietism (uchaji) ilitokea katika Kanisa la Kilutheri la Ujerumani katika karne ya 17 na 18. Baadhi ya wafuasi wa harakati hiyo walidhihakiwa au hata kuteswa kwa sababu ya imani yao. Wasomi kadhaa wa harakati hiyo walitorokea Berleburg, umbali wa kilometa 150 hivi kaskazini ya Frankfurt am Main. Walipewa hifadhi na mwenyeji fulani mwenye cheo kikubwa, Count Casimir von Wittgenstein Berleburg, ambaye aliheshimu sana dini. Kuwapo kwa wahubiri na wasomi hao huko Berleburg kulisaidia kutokeza tafsiri mpya ya Biblia inayojulikana leo kuwa Biblia ya Berleburg. Tafsiri hiyo ilitokezwaje?

Mmoja wa wale waliotafuta hifadhi alikuwa Johann Haug, ambaye alilazimika kuacha nyumba yake huko Strasbourg kwa sababu wanatheolojia wa huko hawakumvumilia. Haug alikuwa msomi mwenye elimu ya juu na mjuzi wa lugha kadhaa aliye stadi. Aliwaeleza wasomi wenzake huko Berleburg tamaa yake kubwa ya “kutoa tafsiri safi kabisa ya Biblia, kusahihisha tafsiri ya Luther, kutoa maana sahihi kulingana na barua ya Neno la Mungu na kulingana na maana halisi ya barua hiyo.” (Die Geschichte der Berlenburger Bibel [Historia ya Biblia ya Berleburg]) Kusudi lilikuwa kutokeza Biblia ambayo ingekuwa na maandishi ya ufafanuzi na maelezo, na ambayo watu wa kawaida wangeweza kuielewa. Haug aliomba msaada kutoka kwa wasomi wa nchi nyingine za Ulaya, naye alitumika kwenye mradi huo kwa miaka 20. Biblia ya Berleburg ilichapishwa kuanzia mwaka wa 1726. Kwa sababu ya maandishi yake mengi ya pambizoni, ilikuwa lazima kuichapisha katika mabuku manane.

Kwa kweli, Biblia ya Berleburg ina mambo fulani yenye kupendeza. Kwa mfano, kwenye Kutoka 6:2, 3 tunasoma hivi: “Zaidi ya hayo, Mungu akasema na Musa naye akamwambia: Mimi ni BWANA! Nami nilimtokea Abrahamu/Isaka na Yakobo/kama Mungu aliye na kila kitu: lakini kwa jina langu YEHOVA sikujulikana kwao.” Maandishi fulani yanafafanua hivi: “Jina YEHOVA . . . , jina lililotakaswa/au/jina lililotangazwa.” Maelezo kuhusu jina la kibinafsi la Mungu, Yehova, yanapatikana pia kwenye Kutoka 3:15 na Kutoka 34:6.

Hivyo, Biblia ya Berleburg imekuwa mojawapo ya Biblia nyingi za Kijerumani ambazo zimetumia jina Yehova katika maandishi yenyewe, maelezo ya chini, au katika fafanuzi. Mojawapo ya tafsiri za kisasa zaidi ambayo huliheshimu jina la kibinafsi la Mungu kama inavyostahili ni Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya, ambayo imechapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki