Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w05 8/1 kur. 3-4
  • Je, Hisia Zako Zinakusumbua?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Hisia Zako Zinakusumbua?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inaweza Kukusaidia Upate Shangwe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Jinsi Unavyoweza Kuzuia Hisia Zisizofaa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Changamoto: Hisia Zisizofaa
    Amkeni!—2015
  • Ninawezaje Kudhibiti Hisia Zangu?
    Amkeni!—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
w05 8/1 kur. 3-4

Je, Hisia Zako Zinakusumbua?

KWA miaka mingi, Lena amesumbuliwa sana na hisia zisizofaa. Anasema: “Nilijiona kuwa mtu asiye na maana kwa sababu ya kutendewa vibaya kingono kwa miaka mingi nilipokuwa mtoto. Nilihisi kuwa sifai kitu hata kidogo.” Simone pia anakumbuka hali yake alipokuwa kijana na kusema: “Nilijihisi kuwa bure na asiyefaa kitu.” Inaonekana huzuni inayotokana na hisia hizo inawaathiri watu wengi leo. Shirika moja linalotoa mashauri kwa vijana linasema kwamba karibu nusu ya wale wanaowapigia simu wanakiri kwamba wanasumbuliwa na “hisia za kudumu za kujiona hawafai.”

Kulingana na wataalamu fulani, mtu hujihisi hafai watu wengine wanapomfanya ahisi hivyo. Hali hiyo inaweza kutokea ikiwa mtu anakemewa mara kwa mara, anachambuliwa sana au kutendewa vibaya. Hata sababu iwe nini, matokeo yanaweza kudhoofisha na hata kuumiza. Kulingana na uchunguzi wa kitiba wa hivi karibuni, watu wanaohisi kuwa hawafai hukosa kujitumaini na kuwatumaini wengine na hivyo wao hukatisha urafiki bila kupenda. Kulingana na uchunguzi huo, “kwa njia fulani, watu hao hujitumbukiza katika matatizo makubwa.”

Mara nyingi watu wanaohisi hivyo huathiriwa na kile ambacho Biblia huita ‘fikira zinazofadhaisha.’ (Zaburi 94:19) Wanahisi kuwa hawafai hata kidogo. Mambo yanapoharibika, kwa kawaida wao hujilaumu. Ingawa watu wengine wanaweza kuwasifu kwa mafanikio yao, wao huhisi ni kana kwamba hawastahili kupata sifa hizo na kwamba utu wao halisi utajulikana baada ya muda mfupi. Kwa sababu ya kuamini kwamba hawastahili kufurahia maisha, wengi wao hujiingiza katika tabia za kujiumiza ambazo wanahisi hawawezi kurekebisha. Lena, aliyetajwa mwanzoni, alikuwa na tatizo baya sana la kula kwa sababu ya kukosa kujiheshimu, naye anasema: “Nilihisi siwezi kubadili jambo lolote.”

Je, wale wanaosumbuliwa na ‘fikira zinazofadhaisha’ wataendelea kuhisi hivyo maisha yao yote? Je, lolote laweza kufanywa ili kushinda hisia hizo? Biblia ina kanuni na mashauri ambayo yamewasaidia watu wengi kufanikiwa kupambana na hisia hizo. Baadhi ya kanuni hizo ni gani, nazo zimewasaidiaje wale wanaosumbuliwa na hisia kupata shangwe maishani? Makala inayofuata itazungumzia habari hiyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki