Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w07 8/1 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Habari Zinazolingana
  • Daudi na Sauli
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Sababu Yampasa Daudi Akimbie
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • 1 Samweli—Yaliyomo
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  • “Kutii Ni Bora Kuliko Dhabihu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
w07 8/1 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Kwa nini Mfalme Sauli alimuuliza Daudi, “Mvulana, wewe ni mwana wa nani?” baada ya Daudi kumuua Goliathi, hata ingawa mapema Sauli alikuwa ameagiza Daudi aitwe ili awe mtumishi wake?—1 Samweli 16:22; 17:58.

Labda jibu rahisi ni kwamba Sauli alimsahau Daudi kwa sababu walipokutana kwa mara ya kwanza ilikuwa ni kwa muda mfupi tu. Hata hivyo, hilo linaweza kuwa tofauti, kwa kuwa masimulizi kwenye 1 Samweli 16:18-23 yanaonyesha kwamba Mfalme Sauli mwenyewe ndiye aliyeagiza kwamba Daudi aitwe, naye akampenda sana na kumfanya kuwa mchukua-silaha wake. Inaelekea kwamba Sauli alimfahamu Daudi vizuri sana.

Wasomi fulani wa Biblia wanafikiri kwamba maandiko ya 1 Samweli 17:12-31 na 17:55–18:5 yaliongezwa baadaye kwa sababu mistari hiyo haipatikani katika nakala fulani za Septuajinti ya Kigiriki, tafsiri ya Maandiko ya Kiebrania yaliyokamilishwa katika karne ya pili K.W.K. Hata hivyo, si jambo la hekima kukata kauli kama hiyo kwa msingi tu wa nakala hizo za Septuajinti, kwa kuwa mistari hiyo inaonekana katika hati nyingine zinazokubalika za Maandiko ya Kiebrania.a

Inaelekea kwamba kwa kumuuliza kwanza Abneri na kisha Daudi mwenyewe, Sauli hakutaka tu kujua jina la baba ya Daudi. Baada ya kuona utu mwingine wa Daudi kwamba alikuwa mtu mwenye imani kubwa na ujasiri ambaye alikuwa ametoka kumshinda Goliathi, Sauli alitaka kujua ni mtu wa aina gani aliyemzaa kijana kama huyo. Huenda Sauli alifikiria kumwingiza Yese, baba ya Daudi, au watu wengine wa familia yake katika jeshi, kwa kuwa huenda watu wengine wa familia hiyo walikuwa pia na ujasiri na ushujaa kama wa Daudi.

Ingawa andiko la 1 Samweli 17:58 linatia ndani jibu fupi tu la Daudi, “mimi ni mwana wa mtumishi wako Yese Mbethlehemu,” maneno yanayofuata yanaonyesha kwamba huenda kulikuwa na mazungumzo marefu zaidi. Kuhusu wazo hilo, ona maelezo ya C. F. Keil na F. Delitzsch: “Ni wazi sana kwamba maneno ya [1 Samweli 18:1], ‘alipomaliza kusema na Sauli,’ yanaonyesha kwamba bado Sauli alizungumza zaidi naye kuhusu familia yake, kwa kuwa maneno hayo yanadokeza kwamba kulikuwa na mazungumzo marefu zaidi.”

Kutokana na yote hayo, tunaweza kukata kauli kwamba kwa kuuliza, “Mvulana, wewe ni mwana wa nani?” Sauli hakuwa akitaka kujua Daudi ni nani, jambo ambalo alikuwa tayari amejua, bali alitaka kujua malezi ya Daudi.

[Maelezo ya Chini]

a Kwa habari zaidi kuhusu usahihi wa mistari iliyoondolewa katika tafsiri ya Septuajinti, ona Insight on the Scriptures, buku la 2, ukurasa wa 855, au Étude Perspicace des Écritures, buku la 2, ukurasa 886, lilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Picha katika ukurasa wa 31]

Kwa nini Sauli alimuuliza Daudi alikuwa mwana wa nani?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki