Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 5/1 kur. 8-9
  • 4 Ondoa Shaka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 4 Ondoa Shaka
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • “Nisaidie Mahali Ambapo Nahitaji Imani!”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
  • Je, Kweli Una Imani Katika Habari Njema?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • “Simameni Imara Katika Imani”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 5/1 kur. 8-9

4 Ondoa Shaka

“Wewe mwenye imani kidogo, kwa nini umekuwa na shaka?”—Mathayo 14:31.

KWA NINI INAWEZA KUWA VIGUMU? Nyakati nyingine hata wanafunzi wa Yesu walikuwa na shaka. (Mathayo 14:30; Luka 24:36-39; Yohana 20:24, 25) Biblia inaeleza ukosefu wa imani kuwa “dhambi ambayo hututatanisha kwa urahisi.” (Waebrania 12:1) Mtume Paulo aliandika: “Imani si mali ya watu wote.” (2 Wathesalonike 3:2) Hiyo haimaanishi kwamba watu fulani hawawezi kuwa na imani, bali inamaanisha kuwa wengi hawajitahidi kuisitawisha. Mungu atawabariki wale wanaojitahidi kusitawisha imani.

UNAWEZA KUFAULU JINSI GANI? Tambua mambo yanayokufanya uwe na shaka. Kwa mfano, mwanafunzi Tomasi alikuwa na shaka kwamba Yesu alifufuliwa hata ingawa wanafunzi wengine walisema walikuwa wamemwona. Tomasi alitaka uthibitisho. Matokeo yakawa nini? Yesu alimpa uthibitisho aliohitaji ili awe na imani yenye nguvu.—Yohana 20:24-29.

Kupitia Biblia, Yehova Mungu anatupa majibu tunayohitaji ili kuondoa shaka. Kwa mfano, wengi wanaacha kumwamini Mungu kwa sababu kwa njia ya moja kwa moja au isiyo ya moja kwa moja wanamlaumu kwa vita, jeuri, na mateso yanayowapata wanadamu. Biblia inasema nini kuhusu jambo hilo?

Mungu hatawali kupitia serikali za wanadamu. Yesu alisema kwamba Shetani ambaye ni kiumbe wa roho asiyeonekana, ndiye “mtawala wa ulimwengu.” (Yohana 14:30) Shetani alimwambia Yesu atampa mamlaka juu ya falme zote za dunia ikiwa atamfanyia tendo moja tu la ibada. Alisema: “Hakika nitakupa mamlaka yote hii na utukufu wake, kwa sababu nimepewa, na yeyote ninayetaka mimi humpa.” Yesu hakukana kwamba Shetani ana mamlaka kama hiyo. Badala yake alisema: “Imeandikwa, ‘Yehova Mungu wako ndiye unayepaswa kumwabudu, na yeye peke yake ndiye unayepaswa kumtolea utumishi mtakatifu.’” (Luka 4:5-8) Shetani na serikali za wanadamu ndizo zinazopaswa kulaumiwa kwa mateso yanayowapata watu ulimwenguni, bali si Mungu.—Ufunuo 12:9, 12.

Hivi karibuni Yehova Mungu ataondoa mambo yote yanayosababisha kuteseka. Tayari amepanga kuwe na Ufalme, au serikali, chini ya Mwana wake Kristo Yesu, ambao utawatawala wanadamu. (Mathayo 6:9, 10; 1 Wakorintho 15:20-28) Kazi ya kuhubiri habari njema kuhusu Ufalme huo inaendelea duniani kote na hivyo kutimiza unabii wa Biblia. (Mathayo 24:14) Punde si punde, Ufalme huo utaondoa watu wote wanaoupinga na mambo yote yanayosababisha kuteseka.—Danieli 2:44; Mathayo 25:31-33, 46; Ufunuo 21:3, 4.

UTAPATA THAWABU GANI? Wale wanaoendelea kuwa na shaka wanakuwa kama mawimbi yanayorushwa huku na huku na “kila upepo wa fundisho kupitia udanganyifu wa watu.” (Waefeso 4:14; 2 Petro 2:1) Lakini wale wanaojibiwa maswali yao kwa njia yenye kuridhisha wanaweza ‘kusimama imara katika imani.’—1 Wakorintho 16:13.

Mashahidi wa Yehova ambao ni wachapishaji wa gazeti hili, wangependa kukusaidia kupata majibu kwa maswali ambayo huenda yanakufanya uwe na shaka. Wanakualika ushirikiane nao na ujichunguzie mwenyewe mafundisho yao. Kufanya hivyo kutaimarisha imani yako sana katika Mungu.

Ili kupata habari zaidi, ona sura ya 8, “Ufalme wa Mungu Ni Nini?,” na sura ya 11, “Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?,” katika kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?a

[Maelezo ya chini]

a Kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

[Picha katika ukurasa wa 9]

Imani ya wale wanaojibiwa maswali yao kwa njia yenye kuridhisha inakuwa na msingi imara

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki