Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 7/1 uku. 3
  • Je, Tunaweza Kuielewa Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Tunaweza Kuielewa Biblia?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mtungaji wa Biblia Anataka Tulielewe Neno Lake?
  • 3. Kubali Kusaidiwa na Wengine
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • 1. Mwombe Mtungaji wa Biblia Akusaidie
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kuelewa Maandiko Kimakosa, Je, Ni Tatizo Dogo?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 7/1 uku. 3

Je, Tunaweza Kuielewa Biblia?

“Familia yetu ilisoma Biblia kila Jumapili (Siku ya Yenga). Kwa kweli, sikufurahia sana kusoma Biblia. Niliamini kwamba Biblia ni Neno la Mungu, lakini mambo mengi niliyosoma yalikuwa magumu sana kueleweka.” —Steven, Uingereza.

“Nilipokuwa na umri wa miaka 17, nilijaribu kusoma Biblia. Nilishindwa kuielewa, hivyo nikaacha kuisoma.”—Valvanera, Hispania.

“Nilisoma Biblia nzima mara moja kwa kuwa nilihisi kwamba nikiwa Mkatoliki, ninapaswa kuisoma. Ilinichukua miaka mitatu kuimaliza! Hata hivyo, nilielewa mambo machache sana.”—Jo-Anne, Australia.

BIBLIA ndicho kitabu kinachopendwa zaidi ulimwenguni. Biblia inanunuliwa kwa wingi kuliko vitabu vingine vyote, watu wengi wanaweza kuipata, inapatikana katika lugha nyingi, na imechapishwa au kunakiliwa kwa njia nyingi zaidi kuliko wakati mwingine wowote. Hata hivyo, watu wengi walio na Biblia wanashindwa kuielewa. Je, wewe pia una tatizo hilo?

Je, Mtungaji wa Biblia Anataka Tulielewe Neno Lake?

Biblia inasema hivi: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Ndiyo, Yehova Mungu ndiye Mtungaji wa Biblia. Je, anataka tulielewe Neno lake? Au, je, alifanya kimakusudi iwe vigumu kwa watu wengi kuielewa Biblia ila tu viongozi wa dini na wasomi wa Biblia?

Chunguza mistari inayofuata kutoka kwenye Biblia yenyewe:

“Amri hii ninayokuamuru leo si ngumu mno kwako, wala haiko mbali.”—Kumbukumbu la Torati 30:11.

“Kufunuliwa kwa maneno yako hutoa nuru, kukiwafanya wasio na uzoefu waelewe.”—Zaburi 119:130.

“Katika saa ileile [Yesu] akawa na shangwe sana katika roho takatifu, akasema: ‘Ninakusifu hadharani wewe, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha kwa uangalifu wenye hekima na walio na akili mambo hayo, nawe umeyafunua kwa watoto.’”—Luka 10:21.

Kwa kweli, Mtungaji wa Biblia anataka uelewe Neno lake! Hata hivyo, ukweli ni kwamba bado watu wengi wanyoofu wanashindwa kukielewa kitabu hicho. Ni nini kinachoweza kuwasaidia? Habari zinazofuata zinatoa mapendekezo matatu yanayoweza kukusaidia kuielewa Biblia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki