Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w11 8/1 uku. 3
  • Je, Watoto Wanapaswa Kujifunza Kumhusu Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Watoto Wanapaswa Kujifunza Kumhusu Mungu?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Dini Inawaathiri Watoto?
  • Siri ya Kufanikiwa
  • Wazazi—Wazoezeni Watoto Wenu Kwa Upendo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Wazazi—Wasaidieni Watoto Wenu Wampende Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
  • Wafundishe Watoto Wako Kumpenda Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
  • Watoto Wetu Ni Urithi Wenye Thamani
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 8/1 uku. 3

Je, Watoto Wanapaswa Kujifunza Kumhusu Mungu?

“Dini zinatusaidia zaidi kuchukiana kuliko zinavyotusaidia kupendana.”—JONATHAN SWIFT, MWANDISHI MWINGEREZA.

SWIFT alisema maneno hayo karne ya 18, lakini watu wengi leo wangekubaliana naye. Hata wengine wanaamini kwamba wazazi hawapaswi kuwa na haki ya kuwafundisha watoto wao kumhusu Mungu. Wanahisi kwamba watoto wanaolelewa katika familia za kidini wanakosa mambo fulani.

Una maoni gani? Ni hoja gani kati ya hoja zinazofuata ambazo unafikiri zinafaa zaidi?

● Wazazi hawapaswi kuruhusiwa kuwafundisha watoto wao kumhusu Mungu.

● Wazazi wanapaswa kungoja mpaka watoto wao wawe watu wazima kabla ya kuanza kuzungumzia mambo ya dini pamoja nao.

● Wazazi wanapaswa kuwafundisha watoto wao wakiwa wangali wadogo yale wanayoamini kumhusu Mungu. Lakini watoto wanapokuwa watu wazima, wazazi wanapaswa kuwatia moyo wachanganue mafundisho hayo wao wenyewe.

● Watoto wanapaswa kukubali mafundisho ya wazazi wao kumhusu Mungu bila kujali kama ni ya kweli au la.

Je, Dini Inawaathiri Watoto?

Hakuna mzazi anayejali ambaye angependa kumdhuru, au kumuumiza, mtoto wake. Lakini je, mambo ya hakika yanaunga mkono madai ya wale ambao wangetaka kuwazuia wazazi wasiwafundishe watoto wao kumhusu Mungu? Kwa miaka mingi sasa, watafiti wamechunguza sana jinsi imani ya wazazi inavyoweza kuwaathiri watoto. Wamefikia mkataa gani?

Watafiti wametambua kwamba dini inaweza kuwa na matokeo mazuri katika ukuzi wa mtoto, badala ya kumdhuru. Katika mwaka wa 2008, ripoti iliyochapishwa kwenye gazeti la Social Science Researcha ilisema: “Imethibitika kwamba dini inaweza kuboresha uhusiano kati ya mtoto na kila mmoja wa wazazi wake.” Ripoti hiyo pia ilisema: “Inaonekana kwamba dini na kuzingatia mambo ya kiroho ni sehemu muhimu katika maisha ya watoto wengi na ni muhimu pia katika mahusiano ya kifamilia.” Ona jinsi matokeo ya utafiti huo yanavyopatana na yale ambayo Yesu Kristo alisema: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji wao wa kiroho.”—Mathayo 5:3.

Namna gani maoni kwamba watoto wanapaswa kufundishwa kumhusu Mungu na dini wanapokuwa watu wazima? Maoni hayo yanapuuza jambo hili la hakika: Ubongo wa mtoto ni kama ndoo isiyo na kitu ndani ambayo inangoja kujazwa. Kwa kweli, lazima wazazi waamue; ama kujaza “ndoo” hiyo kwa kuwafundisha watoto wao mambo yanayofaa, au wawaache wajifunze kutokana na yale wanayosikia kutoka kwa watu wengine.

Siri ya Kufanikiwa

Historia inathibitisha kwamba dini inaweza kuchochea chuki na ubaguzi. Hivyo, wazazi wanaweza kuepuka jinsi gani matokeo ambayo yalitajwa na Jonathan Swift? Wanawezaje kuwafundisha watoto wao mambo yanayowasaidia kuwapenda wengine?

Siri inapatikana katika majibu ya maswali haya matatu: (1) Watoto wanapaswa kujifunza nini? (2) Ni nani anayepaswa kuwafundisha? (3) Ni njia gani za kufundisha ambazo zinafaa zaidi?

[Maelezo ya Chini]

a Utafiti huu ulitegemea habari zilizokusanywa kutoka kwa watoto zaidi ya 21,000 wanaoishi Marekani, na pia kutoka kwa wazazi na walimu wao.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki