Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 2/1 uku. 6
  • Musa—Alionyesha Upendo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Musa—Alionyesha Upendo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Musa—Jinsi Maisha Yake Yanavyokuhusu
    Amkeni!—2004
  • Kuzijua Njia za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Iga Imani ya Musa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Yesu Kristo Alikuwaje Nabii Kama Musa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1991
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 2/1 uku. 6

Musa—Alionyesha Upendo

UPENDO NI NINI?

Upendo unahusisha kupendezwa sana na wengine. Mtu mwenye upendo huonyesha kupitia maneno na matendo jinsi anavyohisi kuhusu wale anaowapenda, hata ikiwa atahitaji kujidhabihu ili kufanya hivyo.

[Picha katika ukurasa wa 6]

MUSA ALIONYESHAJE UPENDO?

Musa alionyesha kwamba alimpenda Mungu. Katika njia gani? Kumbuka maneno haya yaliyorekodiwa kwenye 1 Yohana 5:3: “Kwa maana kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake.” Musa alifanya hivyo. Alitii mambo yote ambayo Mungu alimwamuru, kutia ndani mgawo mgumu wa kukutana na Farao mwenye nguvu hadi tendo lililoonekana kuwa dogo la kunyoosha fimbo yake juu ya Bahari Nyekundu. Iwe amri ilikuwa ngumu au rahisi, Musa alitii. “Alifanya vivyo hivyo.”—Kutoka 40:16.

Musa aliwapenda Waisraeli wenzake. Walitambua kwamba Yehova alikuwa akimtumia Musa kuwaongoza, hivyo walizungumza na Musa walipokabili matatizo mbalimbali. Tunasoma hivi: “Watu wakasimama mbele ya Musa tangu asubuhi mpaka jioni.” (Kutoka 18:13-16) Fikiria jinsi Musa alivyochoka baada ya kuwasikiliza Waisraeli kwa saa nyingi walipokuwa wakimweleza mahangaiko yao! Hata hivyo, Musa alifurahi kuwasaidia watu kwa sababu aliwapenda.

Mbali na kuwasikiliza, pia Musa alisali kwa ajili ya watu aliowapenda. Hata alisali kwa ajili ya wale waliomkosea! Kwa mfano, Miriamu dada ya Musa aliponung’unika kumhusu Musa, Yehova alimpiga kwa ukoma. Badala ya kushangilia kwa sababu ya adhabu hiyo, mara moja Musa alisali kwa ajili ya Miriamu: “Ee  Mungu, tafadhali! Mponye, tafadhali!” (Hesabu 12:13) Bila shaka, Musa alichochewa na upendo alipotoa sala hiyo isiyo na ubinafsi.

TUNAJIFUNZA NINI?

Tunaweza kumwiga Musa kwa kusitawisha upendo wenye nguvu kumwelekea Mungu. Upendo huo unatuchochea kutii amri zake “kutoka moyoni.” (Waroma 6:17) Tunapomtii Yehova kutoka moyoni tunaufurahisha moyo wake. (Methali 27:11) Sisi pia tunafaidika. Zaidi ya yote, tunapomtumikia Mungu kwa kuchochewa na upendo wa kweli, hatufanyi tu jambo linalofaa bali pia tunafurahia kulifanya!—Zaburi 100:2.

Pia, tunaweza kumwiga Musa kwa kusitawisha upendo wa kujidhabihu kwa ajili ya wengine. Rafiki au watu wa familia wanapokuwa na matatizo, upendo unatuchochea (1) kuwasikiliza kwa upendo; (2) kusikitika pamoja nao au kuhisi kama wanavyohisi; na (3) kuwahakikishia kwamba tunawajali.

Kama Musa, tunaweza kusali kwa ajili ya wale tunaowapenda. Wakati mwingine tunaweza kuhisi kwamba hatuwezi kuwasaidia wanapotueleza matatizo yao. Huenda hata tukasema, “Pole sana, ninachoweza tu kufanya ni kusali kwa ajili yako.” Lakini kumbuka: “Sala ya mtu mwema ina nguvu ya kutenda mengi.” (Yakobo 5:16, Biblia Habari Njema) Sala zetu zinaweza kumchochea Yehova amfanyie mtu huyo jambo ambalo labda hangefanya. Kwa kweli, jambo zuri zaidi ambalo tunaweza kuwafanyia wale tunaowapenda ni kusali kwa ajili yao.a

Bila shaka, unakubali kwamba tunaweza kujifunza mengi kutoka kwa Musa. Ingawa alikuwa mtu wa kawaida, aliweka mfano bora wa imani, unyenyekevu, na upendo. Kadiri tunavyoiga mfano wake, ndivyo tutakavyozidi kujifaidi wenyewe na wengine pia.—Waroma 15:4.

a Ili Mungu asikilize sala zetu, ni lazima tujitahidi kutii maagizo yake. Kwa habari zaidi, ona sura ya 17 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki