Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 12/1 kur. 14-15
  • Yesu Kristo—Tumkumbuke kwa Njia Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Kristo—Tumkumbuke kwa Njia Gani?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • “Huyu Ni Mwanangu”
    Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu
  • “Huyu ni Mwanangu”
    Kumsikiliza Mwalimu Mkuu
  • Yesu Anazaliwa Katika Boma la Ng’ombe
    Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia
  • Alikata “Kauli Moyoni Mwake”
    Igeni Imani Yao
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 12/1 kur. 14-15

WAFUNDISHE WATOTO WAKO

Yesu Kristo TUMKUMBUKE JINSI GANI?

Mwezi wa Desemba watu wengi ulimwenguni pote huona picha za Yesu akiwa mtoto. Akiwa amelazwa kwenye hori, yaani, sanduku kubwa linalotumiwa kulishia wanyama. Lakini je, tunapaswa kumkumbuka Yesu akiwa mtoto tu?—a Acheni tuzungumzie njia muhimu zaidi ya kumkumbuka. Tunaweza kujifunza kutokana na jambo lililowapata wachungaji waliokuwa malishoni karibu na Bethlehemu usiku mmoja.

Ghafula malaika anawatokea wachungaji hao. Anawaambia hivi: “Mwokozi ambaye ni Kristo Bwana, amezaliwa kwenu.” Pia, malaika anawaambia watampata Yesu “akiwa amefungwa vitambaa na akiwa amelala katika hori.” Papo hapo, malaika wengine wengi wanatokea na kuanza ‘kumsifu Mungu.’

Ungehisije kama ungewasikia malaika wakimsifu Mungu?— Wachungaji wanafurahi sana! Wanasema: “Na twende moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukaone jambo hili ambalo limetendeka.” Wanapofika huko wanamkuta “Maria na vilevile Yosefu, na yule mtoto mchanga akiwa amelala katika hori.”

Baadaye watu wengine wanakuja Bethlehemu ambako Maria na Yosefu wanakaa. Wachungaji wanapowaambia kuhusu kilichotukia, wote wanashangaa. Je, unafurahi kujua mambo hayo yenye kustaajabisha?— Watu wanaompenda Mungu wanafurahi kuyajua. Sasa acheni tuone ni kwa nini watu wanafurahi sana baada ya Yesu kuzaliwa. Ili tuelewe jambo hilo, tutachunguza mambo yaliyotukia kabla Maria hajaolewa.

Siku moja malaika anayeitwa Gabrieli anamtembelea Maria. Anamwahidi kwamba atazaa mtoto ambaye “atakuwa mkuu naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Zaidi.” Pia, Gabrieli anasema: “Atatawala akiwa mfalme . . . na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

Maria anataka kujua hilo litawezekanaje kwa kuwa hajawahi kulala na mwanamume. Basi, Gabrieli anamfafanulia: “Nguvu za Aliye Juu Zaidi zitakufunika,” na “kile kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.” Huo ungekuwa muujiza mkubwa! Kuuhamisha uhai wa Mwana wa Mungu kutoka mbinguni na kuuweka ndani ya tumbo la uzazi la Maria.

Je, umewahi kuona picha zinazoonyesha wanaume watatu wenye hekima pamoja na wachungaji wakimtembelea mtoto Yesu?— Ni jambo la kawaida kuona picha hizo wakati wa Krismasi. Lakini hazionyeshi jambo sahihi. Wanaume hao watatu walikuwa wanajimu, walizoea kufanya jambo ambalo Mungu alikataza. Acheni tuone kilichotukia walipofika. Biblia inasema: “Walipoingia ndani ya ile nyumba wakamwona huyo mtoto mchanga pamoja na Maria mama yake.” Wakati huo Yesu hakuwa mtoto aliyetoka tu kuzaliwa ndani ya hori; bali alikuwa akiishi pamoja na Yosefu na Maria katika nyumba!

Wanajimu walimpataje Yesu?— Ile “nyota” haikuwaongoza kwenda Bethlehemu kwanza, bali iliwaelekeza kwa Mfalme Herode huko Yerusalemu. Biblia inasema Herode alitaka kumpata Yesu ili amuue. Sasa fikiria jambo hili. Unafikiri ni nani aliyetumia kitu kilichofanana na nyota kuwaongoza wale wanajimu kwa Herode?— Si Yehova, Mungu wa kweli, bali ni mpinzani na adui yake, Shetani Ibilisi!

Leo, Shetani anawafanya watu wamfikirie Yesu kuwa mtoto aliyetoka tu kuzaliwa. Lakini Malaika Gabrieli alimwambia hivi Maria: “[Yesu] atatawala akiwa mfalme . . . , na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” Sasa anatawala akiwa Mfalme huko mbinguni, na hivi karibuni atawaangamiza adui wote wa Mungu. Hilo ndilo jambo tunalopaswa kukumbuka kumhusu Yesu, na tunapaswa kuwaambia wengine kulihusu.

Soma Katika Bibilia Yako

  • Luka 1:26-35; 2:8-18

  • Mathayo 2:7-12; 1 Petro 5:8

  • Ufunuo 19:19-21; 1 Yohana 2:17

a Kama unasoma sehemu hii pamoja na mtoto, unapoona kistari kama hiki (—), tua na umtie moyo atoe maoni yake.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki