Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 4/1 kur. 4-7
  • Mpango wa Kujifunza Biblia kwa Ajili ya Watu Wote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mpango wa Kujifunza Biblia kwa Ajili ya Watu Wote
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MAJIBU YA MASWALI YANAYOULIZWA MARA NYINGI KUHUSU MPANGO WETU WA KUJIFUNZA BIBLIA
  • Mtaala wa Kujifunza Biblia Unaotolewa na Mashahidi wa Yehova Ni Nini?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
  • Tutapata Wapi Majibu ya Maswali Muhimu Maishani?
    Tutapata Wapi Majibu ya Maswali Muhimu Maishani?
  • Nifanye Nini ili Nifurahie Kujifunza Biblia?
    Amkeni!—2012
  • Je, umefurahia mambo uliyojifunza?
    Furahia Maisha Milele—Masomo ya Kwanza ya Biblia
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 4/1 kur. 4-7
Funzo la Biblia

HABARI KUU | JE, UNGEPENDA KUJIFUNZA BIBLIA?

Mpango Wa Kujifunza Biblia Kwa Ajili Ya Watu Wote

Mashahidi wa Yehova wanajulikana sana kwa sababu ya kazi yao ya kuhubiri hadharani. Hata hivyo, je, unajua kwamba sisi hujifunza na watu Biblia duniani pote?

Mwanamume akijifunza Biblia kazini

Katika mwaka wa 2014, zaidi ya Mashahidi 8,000,000 katika nchi 240, waliongoza mafunzo ya Biblia, 9,500,000 hivi kila mwezi.a Kwa kweli, idadi ya watu wanaojifunza Biblia pamoja nasi, inazidi idadi ya watu katika nchi 140 hivi!

Ili kufanya kazi hii ya kuelimisha watu, kila mwaka Mashahidi wa Yehova huchapisha Biblia, vitabu, magazeti na machapisho mengine ya Biblia, bilioni moja na nusu hivi katika lugha 700! Jitihada hizo kubwa za kuchapisha zinasaidia watu wajifunze Biblia katika lugha wanayopendelea.

“Sikufurahia masomo shuleni, lakini nimefurahia sana kujifunza Biblia. Mambo niliyojifunza yalinifariji sana!”—Katlego, Afrika Kusini.

“Mambo niliyojifunza yalijibu maswali yangu yote na zaidi.”—Bertha, Mexico.

“Nilifundishwa Biblia nyumbani kwangu kulingana na ratiba yangu. Na hilo ndilo nililotaka zaidi!” —Eziquiel, Brazili.

“Tulijifunza kwa muda wa dakika 15 hadi 30 hivi au zaidi ikitegemea ratiba yangu.”—Viniana, Australia.

“Sikuhitaji kulipa chochote ili kujifunza, hilo lilinishangaza sana!”—Aimé, Benin.

“Mwalimu wangu wa Biblia alikuwa mwenye subira na fadhili. Tukawa marafiki sana.”—Karen, Ireland Kaskazini.

“Watu wengi hujifunza Biblia bila kuwa Mashahidi baadaye.” —Denton, Uingereza.

MAJIBU YA MASWALI YANAYOULIZWA MARA NYINGI KUHUSU MPANGO WETU WA KUJIFUNZA BIBLIA

Utaratibu wa kujifunza umepangwa jinsi gani?

Sisi huchukua habari mbalimbali zinazopatikana katika Biblia na kuchunguza mistari ya Biblia inayohusiana na habari hizo. Kwa mfano, Biblia inatoa majibu ya maswali kama vile: Mungu ni nani? Ana utu wa aina gani? Je, ana jina? Anaishi wapi? Je, tunaweza kumkaribia? Watu wengi hupata changamoto ya kujua ni wapi katika Biblia wanaweza kupata majibu.

Ili kuwasaidia watu wapate majibu ya maswali ya Biblia, sisi hutumia kitabu chenye kurasa 224, kinachoitwa Biblia Inafundisha Nini Hasa?b Kitabu hicho kimetayarishwa ili kuwasaidia watu kuelewa mafundisho ya msingi ya Biblia. Mafundisho hayo yanatia ndani masomo kuhusu Mungu, Yesu Kristo, kwa nini wanadamu wanateseka, ufufuo, sala, na mengine mengi.

Funzo linaweza kufanywa wakati na mahali gani?

Funzo linaweza kufanywa wakati na mahali panapokufaa.

Vipindi vya kujifunza huchukua muda gani?

Watu wengi hutenga saa moja au zaidi kila juma ili kujifunza Biblia. Hata hivyo, urefu wa kujifunza wa kila kipindi unaweza kubadilika. Tutajifunza kulingana na ratiba yako. Wengine wamejifunza kwa dakika 10 au 15 tu kila juma.

Funzo hilo linagharimu pesa ngapi?

Funzo na machapisho ya kujifunzia hutolewa bila malipo. Hilo linapatana na agizo hili la Yesu alilowapa wanafunzi wake: “Mlipokea bure, toeni bure.”—Mathayo 10:8.

Funzo linachukua kipindi gani mpaka kumaliza?

Unaweza kujifunza kwa kipindi cha wakati unachopenda. Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? kina masomo 19. Unaweza kumaliza masomo hayo yote kulingana na nafasi yako.

Je, ni lazima niwe Shahidi wa Yehova baada ya kumaliza kujifunza?

Hapana. Tunatambua na tunaheshimu uhuru alionao kila mtu wa kuamua atakachoamini. Hata hivyo, watu waliopata ujuzi wa msingi wa Biblia wanaweza kufanya uamuzi kulingana na ujuzi huo.

Nitapata wapi habari zaidi?

Tovuti ya jw.org/sw inatoa habari sahihi kuhusu imani na utendaji wa Mashahidi wa Yehova.

Ninawezaje kuomba funzo la Biblia?

  • Watu wanatuma maombi ya funzo la Biblia kupitia: Intaneti, barua, na kwa kutafuta namba ya simu katika kitabu cha orodha ya namba za simu

    Tuma ombi kupitia www.jw.org/sw.

  • Tuma ombi lako ukitumia mojawapo ya anwani zinazopatikana katika ukurasa wa pili wa gazeti hili.

  • Wasiliana na Mashahidi wa Yehova walio karibu nawe. Unaweza pia kutafuta Mashahidi wa Yehova katika kitabu cha orodha ya simu.

a Kwa kawaida, mafunzo ya Biblia huongozwa pamoja na watu mmoja-mmoja au vikundi vya watu.

b Kimechapishwa na Mashahidi wa Yehova. Nakala zaidi ya milioni 230 za kitabu hicho zimechapishwa katika lugha zaidi ya 260.

MSAADA KWA FAMILIA

Eziquiel

“Mke wangu alipoanza kujifunza Biblia, niliona akifanya mabadiliko makubwa. Maisha ya familia yetu yaliboreka. Ili kujua ni nini alichokuwa akijifunza, nilianza pia kujifunza Biblia. Yale niliyojifunza yalinifanya nisitawishe sifa nzuri. Kujifunza Biblia kumefanya familia yetu iwe na umoja.”—Eziquiel.

Karen

“Nilipoanza kujifunza Biblia, niliacha zoea la kutumia madawa ya kulevya, ulevi, na nilijifunza kudhibiti hasira yangu. Sasa nyumba yangu ni safi na nadhifu. Naithamini familia yangu na ninafurahia kufanya mambo yanayochangia furaha yao. Nina furaha sana.”—Karen.

Viniana

“Baadhi ya watu walinidhihaki kwa sababu ya kujifunza Biblia. Lakini mume wangu aliunga mkono uamuzi wangu na kuniambia hivi: ‘Usijali maneno ya watu. Jambo muhimu kwangu ni kwamba unafanya mabadiliko mazuri sana. Endelea kujifunza Biblia.’ Maisha ya familia yetu hayajawahi kuwa mazuri kama yalivyo sasa!”—Viniana.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki