Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 10/1 uku. 15
  • Kusamehe kwa Hiari

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusamehe kwa Hiari
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • ‘Endeleeni Kusameheana kwa Hiari’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1997
  • Msameheane Kwa Hiari
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kusamehe Kunamaanisha Nini?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Kwa Nini Uwe Mwenye Kusamehe?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1994
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 10/1 uku. 15

HEKIMA YA KALE INAYOFAA LEO

Kusamehe kwa Hiari

KANUNI YA BIBLIA: “Endeleeni . . . kusameheana kwa hiari ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika juu ya mwingine. Kama vile Yehova alivyowasamehe ninyi kwa hiari, nanyi fanyeni vivyo hivyo pia.”—Wakolosai 3:13.

Mwanamke anagombana na mwenzake

Inamaanisha nini? Biblia inasema dhambi ni kama deni, na kuomba msamaha ni sawa na kufutwa kwa deni. (Luka 11:4) Kitabu kimoja cha marejeo kinasema kwamba katika Maandiko, neno la Kigiriki linalotafsiriwa “samehe” linamaanisha “kuachilia deni kwa kutodai.” Hivyo, tunapoamua kumsamehe mkosaji hatutazamii atulipe chochote. Kusamehe kwa hiari hakumaanishi kwamba tunakubaliana na tabia mbaya au maumivu tuliyopata baada ya kukosewa. Badala yake, tunaamua kutoweka kinyongo hata ikiwa tuna sababu nzuri ya “kulalamika.”

Je, hekima hiyo inafaa leo? Sote tunatenda dhambi kwa kuwa hatujakamilika. (Waroma 3:23) Hivyo, ni jambo la hekima kuwasamehe wengine kwa kuwa huenda sisi pia tukahitaji kuomba msamaha. Pia, tunanufaika tunapowasamehe wengine. Jinsi gani?

Wanawake wamekumbatiana

Tunajiumiza wenyewe tunapokasirika, tunapoweka kinyongo, na kukataa kuwasemehe wengine. Hisia hizo zisizofaa zinaweza kutukosesha furaha na tushindwe kufanya vizuri shughuli za kila siku za maisha. Pia, zinaweza kuhatarisha afya yetu. Ripoti moja ya gazeti linaloitwa Journal of the American College of Cardiology, iliyotolewa na Dakt. Yoichi Chida na Profesa wa Saikolojia, Andrew Steptoe, ilisema hivi: “Uchunguzi wa hivi karibuni unaonyesha kwamba kuna uhusiano kati ya hasira, chuki, na magonjwa ya moyo.”

Kwa upande mwingine, fikiria faida za kusamehe. Tunapowasamehe wengine kwa hiari, tunadumisha umoja, amani, na kuimarisha mahusiano. Jambo la muhimu hata zaidi ni kwamba tunapofanya hivyo, tunamwiga Mungu anayesamehe kwa hiari watenda dhambi wanaotubu, naye anatarajia sisi pia tuwasamehe wengine.—Marko 11:25; Waefeso 4:32; 5:1.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki