Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • wp18 Na. 3 uku. 12
  • Nani wa Kulaumiwa?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nani wa Kulaumiwa?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Kuna Mateso Mengi Ulimwenguni?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kuteseka Kuteseka
    Amkeni!—2015
  • Biblia Inasema Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2017
  • Kwa Nini Mungu Anawaacha Watu Wateseke?
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2018
wp18 Na. 3 uku. 12
Waokoaji waliofika kwenye eneo la aksidenti

Nani wa Kulaumiwa?

Ikiwa si Mungu anayesababisha hali ngumu duniani, basi kwa nini kuna njaa kali, umaskini usioisha, vita, magonjwa, na misiba ya asili? Neno la Mungu, Biblia, linataja mambo matatu makuu yanayosababisha wanadamu wateseke:

  1. Ubinafsi, Pupa, na Chuki. “Mwanadamu amemtawala mwanadamu mwenzake kwa kumuumiza.” (Mhubiri 8:9) Mara nyingi, wanadamu huteseka kwa sababu ya matendo ya wanadamu wenzao wasio wakamilifu ambao ni wabinafsi na wakatili.

  2. Wakati na Matukio Yasiyotarajiwa. Mara nyingi wanadamu huteseka “kwa sababu wakati na matukio yasiyotarajiwa huwapata wote.” (Mhubiri 9:11) Mtu anaweza kuwa mahali pasipofaa wakati usiofaa, ama aksidenti ikatokea, au labda watu wakakosa kuwa waangalifu au wakafanya makosa.

  3. Mtawala Mwovu wa Ulimwengu. Biblia inataja wazi chanzo kikuu cha matatizo ambayo wanadamu wanakabili. Inasema: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” (1 Yohana 5:19) “Mwovu” huyo ni Shetani Ibilisi, kiumbe wa roho mwenye nguvu ambaye mwanzoni alikuwa malaika wa Mungu lakini “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Viumbe wengine wa roho walijiunga na Shetani na kumwasi Mungu ili watimize tamaa zao za kibinafsi na hivyo wakawa mashetani. (Mwanzo 6:1-5) Tangu walipoasi, Shetani na mashetani wake wamekuwa wakiongoza mambo duniani kwa njia ya kikatili. Hilo ni wazi hasa katika nyakati zetu. Sasa, Ibilisi ana hasira kali na “[anaipotosha] dunia nzima inayokaliwa,” na hilo limeleta ‘ole kwa dunia.’ (Ufunuo 12:9, 12) Kwa kweli, Shetani ni mtawala katili sana. Anapenda kuwaona wanadamu wakiteseka. Shetani ndiye anayewafanya wanadamu wateseke, na wala si Mungu.

FIKIRIA HILI: Bila shaka, mtu anayesababisha mateso kwa wanadamu wasio na hatia lazima awe mwovu, katili, na asiye na huruma. Kinyume na hilo, Biblia inasema: “Mungu ni upendo.” (1 Yohana 4:8) Kwa kuwa msingi wa utu wake ni upendo, “Mungu wa kweli hawezi kamwe kuwazia kutenda uovu, na Mweza-Yote hawezi kamwe kutenda kosa!”—Ayubu 34:10.

Hata hivyo, huenda ukajiuliza, ‘Mungu Mweza-Yote atamruhusu Shetani aendelee kutawala kikatili hivyo hadi lini?’ Kama ambavyo tumeona, Mungu anachukia uovu, na anapoona tukiteseka yeye huumia sana. Kwa kuongezea, Neno lake linatusihi hivi: “[Tupeni] mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.” (1 Petro 5:7) Mungu anatupenda na ana nguvu za kuondoa mateso yote na ukosefu wa haki tunaouona, kama makala inayofuata itakavyoonyesha.a

a Ili kupata habari zaidi kuhusu sababu zinazofanya wanadamu wateseke sana, soma somo la 26 kwenye kitabu Furahia Maisha Milele! kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova, na unachoweza kukipakua bila malipo yoyote kwenye tovuti ya www.jw.org/sw.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki