Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/88 uku. 3
  • Wasaidie Wapya Watoe Maelezo Mikutanoni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Wasaidie Wapya Watoe Maelezo Mikutanoni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Habari Zinazolingana
  • Tianeni Moyo Katika Mikutano ya Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2023
  • Msifu Yehova ‘Katikati ya Kutaniko’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Jenganeni kwa Kutoa Maelezo Mikutanoni
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Msifu Yehova Katika Kutaniko
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 7/88 uku. 3

Wasaidie Wapya Watoe Maelezo Mikutanoni

1 Jinsi inavyosisimua kusikia mwanafunzi mpya akitoa maelezo yake ya kwanza kwenye Jumba la Ufalme! Hakika hilo linatupa sisi hisi ya uradhi, kama kwamba ni uthibitisho kwamba mpya anashika ukweli hakika. Wapya wanahitaji kung’amua kwamba kusema peupe ni jambo linalohitajiwa kabisa. Ni uthibitisho wa imani inayoongoza kwenye wokovu.—Rum. 10:10.

2 Yesu alisema: “Kila mtu ambaye amehitimu hulingana na mwalimu wake.” (Luka 6:40) Jambo hilo lapasa kuingiza ndani yetu uhakika wa kwamba tunaweza kuwafundisha wapya watoe maelezo mikutanoni kwa kufanya hivyo sisi wenyewe. Tunaweza kuwasaidia wathamini kwamba ili kutoa maelezo sharti maarifa yawepo. Wafunze kwamba funzo lapaswa kufanywa kwa kusudi la kutumia maarifa mikutanoni na shambani na pia katika kuongoza maisha ya kibinafsi ya mtu mwenyewe.

3 Huenda wapya fulani fulani wakaogopa, wakihisi kwamba wao hawana uwezo wa kutoa maelezo vizuri kama wengine wanavyofanya. Hata hivyo, tunaweza kusaidia wapya wathamini kwamba urahisi ni jambo la maana katika kutoa maelezo mazuri. Ikiwa maelezo yetu sisi wenyewe yanafaa, ni mafupi, na yangonga kichwa cha msumari, wapya hawatahisi wakiwa na wajibu wa kutoa maelezo marefu. Wao wanaweza kusaidiwa wachanganue swali, watafute wazo katika fungu linalotoa jibu, kisha waweke wazo hilo katika maneno yao wenyewe. Pia ni jambo la maana kwao waone jinsi maandiko yaliyotajwa au yaliyodondolewa yanavyohusiana na jambo linalozungumziwa. Wasaidie waelewe jinsi wanavyoweza kutumia maandiko yaliyo katika fungu ili kuunga mkono maelezo yao. Wafunze kupiga mstari chini ya maneno ya msingi na pengine waandike maandishi mafupi pambizoni. Watie moyo waseme kwa sauti na waziwazi ili wote wanaohudhuria wanufaike kutokana na maelezo yao yaliyotayarishwa. Kujitayarisha vizuri kutawasaidia wasiwe waoga wasitoe maelezo.

4 Ni jambo gani jingine tunaloweza kufanya ili tuwasaidie wapya watoe maelezo? Bila shaka, kuketi pamoja nao kunaweza kuwaondolea mashaka na kuwe kwenye kufariji. Huenda ukataka kudokeza kwamba waketi mbele mahali ambapo vivuta akili ni vichache. Waonyeshe maswali yanayoweza kujibiwa kwa maneno mafupi sana.

5 Kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kundi anapofahamiana na mpya katika kikundi chake, anaweza kumwomba asome andiko. Baadaye, maneno ya kweli ya kuonyesha uthamini kwa jitihada zake huenda yakatia moyo mpya aendelee kutoa maelezo kwenye funzo la kitabu na baadaye aanze kushiriki kwa ukawaida katika mikutano mingine.

6 Ni pendeleo kushiriki kutoa maelezo mikutanoni. (Ebr. 10:24, 25) Tunataka kusaidia wapya wathamini jambo hilo. Linaweza kuandaa kitia-moyo zaidi na baraka kwa wote wanaohusika. Tuwe katika utumishi wa shambani au kwenye mikutano yetu ya kundi, tuna fursa za kufanya kama vile Waebrania 13:15 inavyotukumbusha: “Basi, kwa njia yake yeye, na tumpe Mungu dhabihu ya sifa daima, yaani, tunda la midomo iliungamayo jina lake.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki