Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 8/88 uku. 4
  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Broshua

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutangaza Habari Njema—Kwa Broshua
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MADOKEZO FULANI
  • Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tumia Broshua Mbalimbali Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1988
km 8/88 uku. 4

Kutangaza Habari Njema—Kwa Broshua

1 Ni shangwe iliyoje kuzungumza ukweli pamoja na watu na kushiriki habari njema za Ufalme pamoja nao! (Mdo. 15:3) Lakini wakati wetu wa kufanya hivi umewekewa mpaka. Kwa hekima, Yehova kupitia tengenezo lake anaandaa vifaa bora sana vya kujifunza Biblia ambavyo tunaweza kuwaachia watu wanaopendezwa ili viwasaidie kufanya maendeleo zaidi. Tunataka kutoa vifaa hivyo kwa njia yenye matokeo.

2 Wakati wa Agosti tutakuwa tukitumia Kichwa cha Mazungumzo kipya, “Ufunguo wa Kupata Furaha,” na tutakuwa tukitoa mojapo ya broshua hizi: Furahia Maisha Milele Duniani!, Serikali Itakayoleta Paradiso au Jina la Mungu Litakaloendelea Milele. Kabla ya kwenda shambani, tunapaswa kuzungumzia jinsi tutakavyotoa vifaa hivyo vya Biblia kwa njia yenye matokeo mazuri na kupatana na Kichwa cha Mazungumzo chetu kuhusu furaha.

MADOKEZO FULANI

3 Furahia Maisha Milele Duniani!: Broshua hii inavutia macho ya vijana sana na pia wale ambao wanaweza kusoma kidogo tu. Picha na maandiko yametiwa namba ili yaweza kurejezewa kwa urahisi. Wewe unaweza kuitoa jinsi gani? Ili kumalizia mazungumzo kuhusu furaha, unaweza kusema: “Je! wewe ungependa kushangilia furaha ya kweli siku fulani, sivyo? [Ruhusu itikio.] Angalia picha hii yenye kupendeza ya watu wenye furaha humu katika kifaa hiki cha kujifunzia Biblia. [Fungua picha 49, na soma maelezo yaliyo juu ya picha.] Broshua hii itakusaidia wewe kujifunza jinsi Biblia inaweza kukusaidia uishi miongoni mwa watu wenye furaha kama hawa na kushangilia maisha milele duniani. Itakuwa yako kwa mchango wa—.” (Sema kiasi cha mchango.)

4 Baada ya utangulizi mfupi, mhubiri kijana au mpya anaweza kutoa broshua kwa kusema: “Tunatoa broshua hii ambayo inaonyesha jinsi Mungu atawaletea watu wote duniani pote furaha. Angalia jalada linaloonyesha watu wenye furaha wakishangilia maisha kweli kweli. Nina uhakika utapenda kusoma mengi kuhusu jambo hili na kuchunguza picha na marejezo ya maandiko katika broshua hii. Itakuwa yako kwa mchango wa—.” (Sema kiasi cha mchango.)

5 Serikali Itakayoleta Paradiso: Broshua hii inaelekeza fikira kwenye Ufalme wa Mungu—kichwa cha ujumbe wa Yesu na wetu. Hapa pana njia mbili ambazo unaweza kutumia kuunganisha broshua hii na mazungumzo yako kuhusu furaha:

6 “Wale ambao wanathamini na kushika Neno la Mungu kweli kweli wanaweza kutazamia maisha yenye furaha chini ya serikali ya Mungu. Hiyo ndiyo serikali itakayoleta hali za Paradiso duniani pote. Inaelezwa vizuri katika broshua hii ambayo unaweza kuchukua kwa— tu. Angalia yale yanayosemwa kuhusu serikali hiyo kwenye ukurasa 3.” Kisha soma fungu.

7 Au, “Wale wanaoshika Neno la Mungu wana furaha sasa na pia wanatazama mbele kwenye furaha kubwa zaidi. Kifaa hiki cha kujifunzia Biblia kinaonyesha kwenye ukurasa 29 kwa nini wale wanaoshika Neno la Mungu watakuwa na furaha. [Onyesha mwenye nyumba mambo yanayofaa kwenye ukurasa 29.] Nina uhakika utashangilia kusoma mengi zaidi kuhusu jambo hili. Unaweza kupata broshua hii yenye maagizo kwa—.”

8 Jina la Mungu Litakaloendelea Milele: Kwa kweli watafutaji wa furaha lazima wafahamiane na Mungu mwenye furaha, Yehova. Kwa hiyo unaweza kutoa broshua hiyo kwa njia hii: “Ili kujua na kushika Neno la Mungu, lazima mmoja afahamiane vizuri sana na Mungu mwenyewe. Hiyo ndiyo sababu moja tunawatolea watu kifaa hiki cha kujifunzia Biblia chenye kufundisha. [Onyesha broshua.] Haielezi tu jina la Mungu ni nani lakini pia inaonyesha hapa kwenye ukurasa 31 thamani ya kujua jina la Mungu. [Soma fungu 1.] Nakala hii itakuwa yako kwa mchango wa—.”

9 Huenda ukapata njia nyingine zenye matokeo za kutoa broshua katika utumishi wa shambani mwezi huu. Tayarisha vizuri, na Yehova akupe shangwe katika kutangaza habari njema kwa kutumia broshua.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki