Sifu Yah kwa Njia ya Kupata Maandikisho
1 Ni shangwe iliyoje kupokea kila toleo jipya la Amkeni! Jarida hili zuri linatusaidia tujue habari za karibuni kuhusu matukio ya ulimwengu yanavyohusiana na unabii wa Biblia. Hivyo, tunaweza kuthamini kwa njia nzuri fursa zetu za kumsifu Yehova.—Amosi 3:7; Ebr. 13:15.
2 Kufikia sasa katika 1989, Amkeni! imeonyesha habari zenye kuvuta fikira kama vile “Nani Atarithi Dunia?” “Ni Nini Kinachotukia kwa Thamani za Kiadili?” na “Jeuri—Wewe Unaweza Kufanya Nini?” Habari hizo zinazidisha uthamini wetu kwa Mnara wa Mlinzi, ambao kwa zaidi ya miaka mia moja umetetea Ufalme wa Mungu kuwa suluhisho la kweli kwa matatizo ya aina ya wanadamu. Magazeti haya yote mawili yamewaweka chonjo wasomaji waone jinsi matukio ya siku iliyopo yanavyotia alama “siku za mwisho” za mfumo huu wa kale. (2 Tim. 3:1-5) Bila shaka, Aprili na Mei ya mwaka huu iliona matoleo yenye maana sana ya Mnara wa Mlinzi yakifunua kwa ujasiri Babuloni Mkubwa aliye mwovu.
MAANDIKISHO YATOA
CHAKULA CHA KIROHO
3 Wakati wa Oktoba tutakuwa na pendeleo la kutoa maandikisho ya Amkeni! na Mnara wa Mlinzi au yote mawili. Je! kila mshiriki wa jamaa yako ana andikisho la kibinafsi? Ikiwa ndivyo basi umejiandaa vizuri kupendekeza kwamba wengine wafanye andikisho pia. Ukiwa msomaji wa kawaida wa yote mawili Mnara wa Mlinzi na Amkeni! unaweza kuwa mwenye idili katika kutoa maandikisho kama ulivyo katika kutoa nakala moja moja siku ya magazeti.
4 Usitangulie kuhukumu kama mtu mmoja mmoja angependa kuandikisha, bali, acha mtu yule aitikie utoaji wako wa moyo mweupe, wenye idili. Dada mmoja alisaidia kukuza mtazamo chanya zaidi kwa kufikiria usemi: “Huwezi kuhukumu kitabu kwa jalada yacho.” Yeye alijifunza kuwa zaidi sana kama Yehova, ambaye hana upendeleo. (Mdo. 10:34) Zaidi ya huduma yako ya mlango kwa mlango, je! wewe umewatolea maandikisho mafunzo yako ya Biblia, wale unaopelekea magazeti kwa ukawaida, wafanya kazi wenzi, majirani, na watu wa ukoo na unapotoa ushahidi barabarani?
5 Wenye nyumba wamewaambia wengi kwamba hawana pesa za kuandikisha wakati huo. Au huenda wakasema kwamba hawamo katika hali nzuri ya kuandikisha kwa sababu fulani. Jambo hilo linapotukia na ikiwa mtu ana nia, jaza vikaratasi vya maandikisho papo hapo wakati wa ziara ya kwanza kisha urudie mchango baadaye. Hakikisha kwamba unarudia wakati mliokubaliana. Hili linakazia umuhimu wa kutunza rekodi za nyumba kwa nyumba zilizo sahihi.
USHAHIDI WA KIVIVI HIVI
6 Ingawa kazi ya mlango kwa mlango ingali tegemezo kuu la ushahidi wetu, tunajua kwamba ushahidi wa kivivi hivi unakaziwa zaidi siku hizi. Ni njia bora ya kuwafikia wengi wa wale wasio nyumbani tunapofanya kazi nyumba kwa nyumba. Na namna gani wale unaofanya kazi ya kimwili pamoja nao? Wakati wa mwezi mmoja wa kampeni ya maandikisho, ndugu mmoja aliamua kuwatolea ushahidi wafanya kazi wenzake kwa uangalifu. Mwanzoni yeye aliweka mradi wa kupata maandikisho kumi kwa mwezi huo. Hata hivyo, alishangaa sana alipofikia mradi huo katika siku mbili. Ebu wazia shangwe yake aliporipoti maandikisho 68 kwa mwezi huo!
7 Wakati wa Oktoba huenda tukatoa andikisho tunapoenda mlango kwa mlango, tunapofanya ziara za kurudia, na wakati tunapotoa ushahidi kivivi hivi. Andikisho linapokataliwa, huenda tukasema jambo linalofanana na hili: “Ingawa hupendi kuandikisha wakati huu, mimi nasadiki kwamba ungeonea shangwe toleo hili ambalo tumezungumzia sasa hivi. Tunaliacha pamoja na gazeti hili andamani kwa mchango wa ______.” Magazeti mengi yanaangushwa katika njia hii.
8 Mtunga zaburi anatusihi: “Sifuni Yah, enyi watu.” (Zab. 147:1, NW) Ni jambo linalofaa kama nini kwetu kumsifu Yehova wakati wa Oktoba kwa kutolea watu maandikisho ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni!