Sanduku la Swali
● Tunaweza kuonyeshaje adabu za Kikristo tunapohudhuria Funzo la Kitabu la Kundi?
Kwa kawaida tunaangaliwa na majirani wetu, na nyakati nyingine wataeleza na hata kuitikia kulingana na mwenendo wetu. (Linganisha 1 Wakorintho 4:9.) Tukiwa watumishi wa Yehova, tunataka maelezo na maitikio yao kwa ajili ya tabia yetu yawe mazuri. (1 Pet. 2:12) Hivyo ndivyo ilivyo kwa habari ya utendaji wetu kwenye Funzo la Kitabu la Kundi. Kwa kuwa yaliyo mengi yayo yanafanyiwa katika nyumba za faragha, uangalizi wa kipekee lazima utolewe ili adabu zetu ziangazie vizuri yote tufanyayo. Inapokuwa kuna mahali padogo pa kuegeshea magari, kwa nini msifanye mipango ya kuegesha magari pamoja ili kuzuia kuudhi isivyofaa wale walio katika ujirani wa funzo la kitabu? Upendo wetu kwa ajili ya jirani yetu utatufanya tuepuke kuegesha motokaa yetu kwa njia isiyo ya kufikiria mwingine ya kumsababisha atatizike au kumsononesha.
Tunaona shangwe wakati wowote tukutanapo, na mara nyingi matokeo ya hilo ni mazungumzo moto-moto kabla na baada ya mkutano. (Mika 2:12) Adabu nzuri na ufikirio kwa wengine zingeongoza kwamba kiwango cha sauti ya mazungumzo yetu kiwe cha kiasi. (Mt. 7:12; Gal. 6:10) Upendo wa Kikristo pia ungetusukuma tuzuie watoto wetu wasikimbie nje na wasiharibu mali za watu wengine. (Mit. 29:15; 1 Kor. 13:4, 5) Hiyo ingetia ndani mwenendo wa staha ndani ya nyumba ambamo funzo la kitabu linaongozewa. Mwenendo wowote usiofaa ukionekana, wazee hawapaswi kukawia kutoa shauri la upendo lililo imara ili matatizo yasitokee ambayo yangeweza kusababisha malalamiko kutoka kwa majirani, kutatiza mwenye nyumba ambaye kwa ukaribishaji amefungua nyumba yake kwa ajili ya funzo, au kutatiza wale wanaohudhuria funzo la kitabu mahali fulani.