Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/90 uku. 4
  • Sanduku la Swali

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Sanduku la Swali
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Habari Zinazolingana
  • “Jiendesheni kwa Namna Inayozistahili Habari Njema”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kusitawisha Adabu za Kikristo Katika Ulimwengu Usio na Adabu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1989
  • Kuwa na Adabu Nzuri Ni Sifa ya Watu wa Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Kuonyesha Adabu Tukiwa Wahudumu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 2/90 uku. 4

Sanduku la Swali

● Tunaweza kuonyeshaje adabu za Kikristo tunapohudhuria Funzo la Kitabu la Kundi?

Kwa kawaida tunaangaliwa na majirani wetu, na nyakati nyingine wataeleza na hata kuitikia kulingana na mwenendo wetu. (Linganisha 1 Wakorintho 4:9.) Tukiwa watumishi wa Yehova, tunataka maelezo na maitikio yao kwa ajili ya tabia yetu yawe mazuri. (1 Pet. 2:12) Hivyo ndivyo ilivyo kwa habari ya utendaji wetu kwenye Funzo la Kitabu la Kundi. Kwa kuwa yaliyo mengi yayo yanafanyiwa katika nyumba za faragha, uangalizi wa kipekee lazima utolewe ili adabu zetu ziangazie vizuri yote tufanyayo. Inapokuwa kuna mahali padogo pa kuegeshea magari, kwa nini msifanye mipango ya kuegesha magari pamoja ili kuzuia kuudhi isivyofaa wale walio katika ujirani wa funzo la kitabu? Upendo wetu kwa ajili ya jirani yetu utatufanya tuepuke kuegesha motokaa yetu kwa njia isiyo ya kufikiria mwingine ya kumsababisha atatizike au kumsononesha.

Tunaona shangwe wakati wowote tukutanapo, na mara nyingi matokeo ya hilo ni mazungumzo moto-moto kabla na baada ya mkutano. (Mika 2:12) Adabu nzuri na ufikirio kwa wengine zingeongoza kwamba kiwango cha sauti ya mazungumzo yetu kiwe cha kiasi. (Mt. 7:12; Gal. 6:10) Upendo wa Kikristo pia ungetusukuma tuzuie watoto wetu wasikimbie nje na wasiharibu mali za watu wengine. (Mit. 29:15; 1 Kor. 13:4, 5) Hiyo ingetia ndani mwenendo wa staha ndani ya nyumba ambamo funzo la kitabu linaongozewa. Mwenendo wowote usiofaa ukionekana, wazee hawapaswi kukawia kutoa shauri la upendo lililo imara ili matatizo yasitokee ambayo yangeweza kusababisha malalamiko kutoka kwa majirani, kutatiza mwenye nyumba ambaye kwa ukaribishaji amefungua nyumba yake kwa ajili ya funzo, au kutatiza wale wanaohudhuria funzo la kitabu mahali fulani.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki