Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 7/92 uku. 1
  • Toa Broshua Ili Ushiriki Tumaini Lako la Ufalme

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Toa Broshua Ili Ushiriki Tumaini Lako la Ufalme
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Kutoa Broshua Ili Kutafuta-tafuta Wenye Kupendezwa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Tumia Broshua Mbalimbali Katika Huduma Yako
    Huduma Yetu ya Ufalme—1995
  • Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kumbuka Kutumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 7/92 uku. 1

Toa Broshua Ili Ushiriki Tumaini Lako la Ufalme

1 Tunaposhuhudia utimizo wa unabii wa Biblia, tunashangilia katika tumaini letu la Ufalme, nasi tunasukumwa kusema juu yalo kwa yeyote atakayesikiliza. (Lk. 6:45; Rum. 12:12) Kutoa broshua katika huduma ya shambani wakati wa Julai ni njia moja tunayoweza kushiriki tumaini letu la Ufalme na wengine kama vile Yesu alivyoamuru.—Mt. 24:14.

2 Kwa kuwa tuna hesabu fulani ya broshua zenye rangi na zenye kuarifu tunazoweza kuchagua, ni zipi kati yazo zinazoweza kuridhisha mahitaji ya wale walio katika eneo letu na kuamsha kupendezwa kwao? Ili kutumia broshua hizo kwa njia bora zaidi iwezekanavyo, ni lazima tujue yaliyomo ndani yazo. Pitio fupi lifuatalo litatusaidia katika jambo hilo.

3 Serikali Itakayoleta Paradiso: Yesu alipokuwa duniani, Ufalme wa Mungu ulikuwa ndio kichwa cha mahubiri yake. Broshua hii inaonyesha kwamba Ufalme huo ni serikali halisi na jinsi utakavyotatua matatizo yanayofanya maisha yawe magumu sana leo.

4 Furahia Milele Maisha Duniani!: Inaeleza kwa nini Mungu alimfanya mwanadamu na jinsi sisi tunavyoweza kufurahia milele maisha duniani. Picha zenye kueleza mambo na maneno sahili katika broshua hii huwavutia watoto na wale wasio na uwezo mzuri wa kusoma. Inaweza pia kutumiwa kutoa mafundisho ya msingi ya Biblia kwa wale wasio na uwezo wa kusikia.

5 Jina la Mungu Litakaloendelea Milele: Broshua hii inazungumza kuhusu jina la Mungu kwa maoni ya Kimaandiko na ya kihistoria, ikionyesha kwa nini ni jambo la maana kwa Wakristo kujua jina hilo na kulitumia pia katika ibada yao.

6 “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”: Broshua hii inaonyesha paradiso na inajenga uthamini kwa ajili ya Biblia na Muumba wetu. Baada ya kuzungumzia sababu ya Mungu kuruhusu uovu, inakazia mafundisho ya Biblia matatu yaliyo ya msingi: fidia, ufufuo, na Ufalme. Broshua hii pia ina maswali katika sehemu za chini za kurasa zayo, hilo likifanya iwe rahisi kuongoza funzo la Biblia kwa kuitumia.

7 Je! Uamini Utatu?: Huenda watu wakasema kwamba wanaamini Utatu, na bado wao huuelewa kwa njia tofauti-tofauti. Broshua hii hujibu maswali kama vile: Utatu ni nini? Je! Biblia huufundisha? Je! Yesu Kristo ndiye Mungu mweza yote na pia sehemu ya Utatu? Roho takatifu ni nini, nayo hutendaje kazi?

8 Tukiisha chagua broshua ambazo tungependa kutumia katika huduma ya nyumba kwa nyumba au tunapotoa ushahidi wa kivivi-hivi, turudie makala zilizo kwenye ukurasa wa nyuma wa toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu. Humo Tutapata madokezo ya kutoa fasihi yetu na kufanya ziara za kurudia kwa kusudi la kuamsha kupendezwa na kuanzisha funzo la Biblia.

9 Katika pindi nyingi, iwe tunatoa ushahidi kwa njia rasmi au ya kivivi-hivi, broshua fulani hususa ndiyo tu inayohitajiwa kutoa ushahidi mzuri. Hata hivyo, ni lazima tujitayarishe, tuwe na ugavi wa broshua za kutosha, tujue yaliyomo ndani yazo, na tuwe wenye utambuzi. Baraka za Yehova juu ya huduma yetu ya bidii na zitokeze wengi zaidi washangilie pamoja nasi katika tumaini la Ufalme!—Mdo. 13:47, 48.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki