Saidia Watu Walio Mfano wa Kondoo Wajenge Juu ya Msingi Imara
1 Kujenga nyumba kwahitaji upangaji mzuri na jitihada nyingi. Baada ya nyumba kuchorwa, mahali pa ujenzi papaswa kutayarishwa na msingi imara uwekwe. Mradi huo husitawi hatua kwa hatua mpaka umalizike hatimaye. Vivyo hivyo, lazima tusaidie watu walio mfano wa kondoo wajifunze kweli hatua kwa hatua. Tunajitahidi kuchochea kupendezwa katika ziara ya kwanza. Baadaye, twafanya ziara za kurudia, tukiweka msingi kwa kufundisha kweli za msingi kuhusu Mungu na kusudi lake kwa ajili ya ainabinadamu.—Lk. 6:48.
2 Hata hivyo, kabla msingi haujawekwa, twahitaji kutayarisha mahali pa ujenzi, yaani, kuzifikiria hali za mwenye nyumba. Ni jambo gani ambalo lilifikiriwa wakati uliopita? Ni maandiko gani yaliyotumiwa? Itikio lilikuwa nini? Ni kichapo gani kilichoachwa? Unaporudi, uwe na mambo hususa akilini na ujenge msingi hatua kwa hatua. Katika kila ziara ujuzi wa mwenye nyumba hukua na imani yake kwa Mungu huongezeka.
3 Ikiwa kitabu “Kuishi Milele” kiliangushwa, waweza kusema:
◼ “Nina furaha kukupata nyumbani. Huenda ukakumbuka kwamba tulipokuwa na mazungumzo yetu ya mwisho, tuliangalia kushuka kwa maadili katika eneo letu. Biblia huonyesha wazi kwamba Mungu hupendezwa na ainabinadamu na kwamba waadilifu watabarikiwa kupitia Ufalme wake. [Soma Mathayo 6:9, 10.] Kupitia Ufalme huu, uadilifu na haki zitadumu.” Soma Isaya 11:3-5, kisha uvute uangalifu wa mwenye nyumba kwenye mafungu ya kwanza mawili ya sura ya 1 ya kitabu Kuishi Milele. Onyesha jinsi habari hiyo yaweza kusomwa.
4 Ikiwa trakti Ulimwengu Mpya Wenye Amani iliangushwa katika ziara ya kwanza, mambo makuu yaliyoangaliwa wakati uliopita, kuhusu uhitaji wa hali bora na ahadi za Biblia, yaweza kupitiwa. Kazia kwamba ili kuishi katika ulimwengu mpya, lazima tutwae ujuzi sahihi. Soma Yohana 17:3. Eleza kwamba baada ya kutwaa ujuzi huo, lazima tufanye mapenzi ya Mungu. Soma 1 Yohana 2:17. Vuta uangalifu wa mwenye nyumba kwenye mambo hususa kutoka ukurasa 5 wa trakti hiyo.
5 Ikiwa habari ya maisha ya familia ilikaziwa ulipoangusha kitabu “Kuishi Milele” katika ziara ya kwanza, waweza kusema:
◼ “Mara ya mwisho nilipozuru, tuliongea juu ya maisha ya familia. Tulikubaliana kwamba ili kuwa na maisha ya familia yenye furaha miongozo inayopatikana katika Biblia lazima ifuatwe. Unafikiri ni nini linalohitajiwa ili kufanikisha ndoa?” Ruhusu itikio. Tokeza mambo hususa kutoka kwa habari iliyo kwenye kurasa 243-6 katika kitabu Kuishi Milele. Mwulize mwenye nyumba atoe maelezo juu ya hvyo vielezi na mwangalie mambo ambayo umechagua kama ifaavyo. Kazia thamani inayotumika ya kanuni za Biblia.
6 Ikiwa trakti Furahia Maisha ya Familia iliachwa, pitia kanuni kuu za Biblia zinazoonyeshwa kwenye kurasa 4 na 5. Kupendezwa kukichochewa, toa kitabu Kuishi Milele. Onyesha sura 29, “Kufanikisha Maisha ya Jamaa,” na onyesha jinsi jambo hili linavyoweza kufikiriwa pamoja na mwenye nyumba na familia yake.
7 Sisi sote twapaswa kushiriki kwa kawaida katika kufanya ziara za kurudia. Fuatia kupendezwa kote kunakoonyeshwa kwa ziara za kurudia zenye matokeo katika Septemba.