Fuatia Kupendezwa Ulikopata
1 Tunapohubiri nyumba kwa nyumba, kwa kawaida tunapungukiwa na kiasi cha wakati ambacho twaweza kutumia na mtu anayependezwa. Katika visa vingi kazi halisi ya kufundisha hufanywa tunapofanya ziara za kurudia na kuongoza mafunzo ya Biblia. (Mt. 28:19, 20) Ili kufundisha kwa matokeo kwenye ziara ya kurudia, twahitaji kupitia yale tuliyozungumzia kwenye ziara ya kwanza kisha kutayarishia mazungumzo ya ziada.
2 Ikiwa uliongea juu ya ukosefu wa uthabiti katika mpango wa familia, waweza kutumia habari iliyo katika sura ya 29 ya kitabu “Kuishi Milele.” Ungeweza kusema hivi:
◼ “Wakati uliopita tuliongea juu ya hekima ya kufuata shauri la Biblia ili kuwa na maisha ya familia yenye furaha. Je, wewe waona nini kuwa ufunguo wa kuungamanisha familia leo?” Ruhusu jibu. Rejezea fungu la 27 kwenye ukurasa 247, na usome Wakolosai 3:12-14. Toa maelezo zaidi ukionyesha jinsi upendo wa kweli uwezavyo kushikamanisha familia. Eleza jinsi funzo lenye utaratibu la kitabu Kuishi Milele liwezavyo kusaidia kusuluhisha matatizo.
3 Ikiwa ulizumgumzia hali za ulimwengu zenye kuzorota kwenye ziara yako ya kwanza, waweza kufuatia hilo kwa kusema hivi:
◼ “Nina hakika utakubaliana nami kwamba mabadiliko makubwa yanahitajiwa ikiwa tutaishi kwa amani wakati wowote ule. Biblia huonyesha kwamba Shetani ndiye kisababishi hasa cha matatizo yetu. Wengi hujiuliza ni kwa nini Mungu amemruhusu aendelee kwa muda mrefu sana. Wewe waonaje?” Ruhusu jibu. Fungua ukurasa 20, mafungu 14 na 15, katika kitabu Kuishi Milele, na ueleze ni kwa nini Shetani hajaharibiwa bado. Kisha soma Warumi 16:20, lionyeshalo yale tuwezayo kutazamia katika wakati ujao ulio karibu.
4 Ikiwa uliongea juu ya baraka zitakazotimizwa chini ya utawala wa Ufalme, ungeweza kusema hivi, kwenye ziara yako ya kurudia:
◼ “Ufalme wa Mungu utaletea dunia na wanadamu baraka za ajabu. Baraka hizo zimetolewa kielezi vizuri hapa kwenye kurasa 12 na 13. Wewe waona nini kinachokuvutia? [Ruhusu jibu.] Fikiria jinsi ingekuwa kuishi katika ulimwengu kama huu.” Soma fungu la 12. Ikiwa kuna kupendezwa, uliza swali katika fungu la 13, na uzungumzie jibu. Onyesha kwamba sura hiyo yajibu maswali zaidi juu ya baraka za Ufalme na kwamba utapendezwa kuyazungumzia kwenye ziara yako ifuatayo.
5 Labda waweza kuanzisha funzo kwa kusema hivi:
◼ “Watu wengi wamepata majibu kwa maswali yao ya Biblia kwa kutumia kitabu hiki.” Fungua ukurasa wa yaliyomo, na uulize: “Ni habari ipi inayokupendeza zaidi hapa?” Ruhusu jibu, fungua sura iliyowapendeza, na usome fungu la kwanza. Eleza jinsi maswali yaliyo chini ya kila ukurasa yanavyokazia mambo makuu katika kila fungu. Toa kielezi kwa kuzungumzia fungu moja au mawili zaidi, kisha fanya mipango ya kutembelea tena.
6 Kufuatia kupendezwa katika kitabu Kuishi Milele kwaonyesha tamaa yetu ya kutimiza huduma yetu kikamili. (2 Tim. 4:5) Huenda tukaweza kusaidia wasikiaji wetu wafikie uhai wa milele.—Yn. 17:3.