Ufunuo—Ufunguo wa Furaha ya Kweli
1 Maneno ya mtume Yohana kwenye Ufunuo 1:3 ni habari njema kwetu kwa sababu yeye hutuambia jinsi ya kupata furaha. Yeye aliandika: “Heri [“Mwenye furaha ni,” NW] asomaye na wao wayasikiao maneno ya unabii huu, na kuyashika yaliyoandikwa humo.” Kitabu Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! kimesaidia wengi kupata furaha nyingi sana. Tuna sababu nzuri ya kukitoa kwa wengine.
2 Unaweza kuanzisha mazungumzo kwa swali hili:
◼ “Je, wafikiri kitabu cha Biblia cha Ufunuo kilikusudiwa kueleweka, au sikuzote kilipaswa kubaki kikiwa fumbo? [Ruhusu itikio.] Wengi wana maoni kama yako. Ona yale Biblia husema kwenye Ufunuo 1:3. [Soma.] Kwa hiyo kitabu cha Ufunuo chaweza kueleweka, na ujuzi kilio nao waweza kutuletea furaha. Hilo lawezekanaje?” Pitia mawazo yaliyo katika fungu la 2 kwenye ukurasa wa 6, kisha useme: “Kichapo hiki hutoa mazungumzo ya mstari kwa mstari ya kitabu cha Ufunuo. Kinastahili sana wakati wako wa kukisoma. Nitafurahi kukuachia nakala hii.”
3 Kwa kuwa wengi wanahangaikia kuandaa mahitaji yao ya kimwili, huu waweza kutokeza upendezi fulani:
◼ “Wafikiri uhitaji wetu mkubwa ni upi? [Ruhusu itikio.] Kuna wengi wanaosadiki kwamba tunahitaji mambo mengi zaidi ya kimwili.” Fungua ukurasa wa 73 na upitie mambo makuu katika sanduku lenye kichwa “Ufuatiaji wa Vitu vya Kimwili Ukitofautishwa na Hekima.” Endelea kwa kusema: “Hii huonyesha kwamba mkazo zaidi umewekwa kwenye vitu vya kimwili; twapaswa kuhangaikia zaidi mahitaji yetu ya kiroho. Ujuzi wa kweli ndio tunaohitaji hasa. Lakini ujuzi juu ya nini?” Soma Yohana 17:3, na ueleze jinsi ujuzi kuhusu Mungu uwezavyo kuongoza kwenye uhai udumuo milele. Toa kitabu na upange kurudi ili kumwonyesha jinsi kinavyofunua habari yenye kupendeza ajabu juu ya kusudi la Mungu la kutosheleza mahitaji yote ya wanadamu.
4 Kwa kuwa wengi wanahangaishwa na taabu katika ulimwengu, unaweza kujaribu mfikio huu:
◼ “Kila mtu ninayeongea naye anahangaika juu ya wakati ujao. Baadhi ya viongozi wa ulimwengu wanahisi kwamba tuko ukingoni mwa enzi mpya ya amani. Wewe wahisije juu ya hilo? [Ruhusu itikio.] Zijapokuwa jitihada zote za mwanadamu, jeuri na taabu huendelea kuongezeka ulimwenguni pote. Biblia hufunua utatuzi pekee kwa matatizo haya. [Soma 2 Petro 3:13. Fungua kwenye picha ya ukurasa wa 302, na ueleze jinsi Ufalme wa kimbingu wa Mungu utakavyoleta amani na usalama wa kudumu kwenye dunia hii.] Kichapo hiki kitakusaidia uone jinsi unavyoweza kuwa sehemu ya jamii hii ya watu ambao watafurahia uhai udumuo milele chini ya Ufalme wa Mungu.”
5 Ikiwa unatoa kitabu “Maisha ya Jamaa” unaweza kusema hivi:
◼ “Nawatembelea ili kushiriki nanyi habari fulani kuhusu tatizo linaloathiri sehemu kubwa ya ulimwengu leo. Linahusu maisha ya familia. Sisi sote twataka familia yetu iwe yenye furaha lakini wengi huona ikiwa vigumu kupata utatuzi wa matatizo ya familia. Unafikiri ni nini kitakachosaidia watu wapate furaha zaidi katika maisha yao ya familia? [Acha wajibu.] Je, hukubali kwamba ingenufaisha kusikiliza yale ambayo Muumba wa familia husema? Yeye huweka uongozi uhitajiwao katika Biblia. Kanuni hizo zazungumzwa katika kitabu hiki, Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha.” Elekeza kwenye yaliyomo na utoe kichapo kwa mchango wa kawaida.
6 Vitabu vyote viwili Upeo wa Ufunuo! na Maisha ya Jamaa huandaa ufunguo wa furaha ya kweli. Toa mojawapo vichapo hivyo vizuri wakati wa mwezi wa Februari.—Mit. 3:13.