Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 5/96 uku. 4
  • Endelea Kusema Kweli

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kusema Kweli
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari Zinazolingana
  • Rudi Ili Kuokoa Wengine
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • “Imani Hufuata Jambo Lililosikiwa”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kutoa Kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Ujuzi Kutoka kwa Mungu Hujibu Maswali Mengi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 5/96 uku. 4

Endelea Kusema Kweli

1 Mitume walitangaza hivi: “Hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.” (Mdo. 4:20) Leo lazima pia tuendelee kusema kweli. Ingawa ugawanyaji wa Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ni njia ya kupata wale watakaosikiliza, lazima turudi ikiwa tutafundisha watu wenye kupendezwa kweli zaidi.

2 Unapofuata angusho la “Amkeni!” la pekee la Aprili lenye habari “Wakati Vita Havitakuwapo Tena,” unaweza kuanzisha funzo la Biblia kwa kuuliza:

◼ “Wakati uliopita, tulizungumza juu ya vita vya mataifa na fungu la dini katika hivyo. Je, umepata kutambua kwamba matukio kama hayo huthibitisha waziwazi kwamba tunaishi katika zile ambazo Biblia huita siku za mwisho? [Onyesha kitabu Ujuzi. Soma fungu la kwanza la sura ya 11, na ukazie sanduku lililo kwenye ukurasa 102.] Kitabu hiki hueleza habari hii pamoja na habari nyingine 18 zilizoorodheshwa hapa katika yaliyomo. [Onyesha ukurasa 3.] Ukiniruhusu, ningependa kukuonyesha jinsi kitabu hiki kinavyoweza kukusaidia kupata uelewevu wa mambo haya ya maana ya Biblia.” Ukiruhusiwa, anzisha funzo kwenye ukurasa 6.

3 Ikiwa uliahidi kurudi ili ueleze jinsi inavyowezekana kufurahia maisha salama sasa, unaweza kusema jambo kama hili:

◼ “Tulipokutana mara ya kwanza, nilishiriki nawe fungu kutoka Biblia ambalo hutupa sababu ya kuwa na maoni mazuri kuhusu wakati ujao wa mwanadamu. Leo ningependa kuelekeza uangalifu wako kwa jambo linaloonyesha ni nani awezaye kutupa hisia ya usalama sasa hivi.” Soma Zaburi 4:8. Fungua kitabu Ujuzi kwenye ukurasa 168 na usome fungu 19. Kisha uulize: “Je, ungefurahia kuwa na funzo la Biblia nyumbani bila malipo linaloonyesha wazi jinsi wewe pia unavyoweza kupata usalama wa aina hii maishani mwako?” Ikiwa jibu ni ndiyo, fungua sura ya 1.

4 Ili kuongeza wale ulioangushia “Amkeni!” la Mei 22 kwenye orodha ya wale unaowapelekea magazeti kwa ukawaida, unaweza kujaribu mfikio huu:

◼ “Ulionekana ukitaka sana kusoma gazeti la Amkeni! nililokuachia lililokuwa na habari kuhusu kusumbuliwa kingono kazini. Je, uliona habari hiyo kuwa yenye kupendeza? [Ruhusu itikio.] Wasomaji wa kawaida wa Amkeni! mara nyingi husema kwamba wanathamini jinsi hilo hushughulikia habari za maana kwa njia ya haki na kikamili. Nafikiri utaona hilo kuwa kweli pia kuhusu toleo hili la karibuni zaidi. [Kazia kifupi simulizi la jalada.] Je, ungependa kulisoma?”

5 Unaweza kutoa funzo la Biblia moja kwa moja kwenye ziara ya kurudia kwa kusema:

◼ “Sisi hugawanya magazeti yetu ulimwenguni pote ili kujulisha watu kila mahali juu ya yale ambayo Biblia hufundisha. Watu mmoja-mmoja wakithamini yale wanayojifunza, sisi huwatolea funzo la Biblia nyumbani bila malipo. [Rejezea kwenye sanduku ‘Je, Wewe Ungekaribisha Ziara?’ kwenye ukurasa wa mwisho wa Mnara wa Mlinzi.] Sisi hutumia kitabu hiki, Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, kuwa mwongozo. Acha nikuonyeshe kifupi jinsi funzo huongozwa.”

6 Tukiendelea kusema kweli, twaweza kuwa na uhakika kwamba kutakuwa na watu kadhaa watakaosikiliza na kuitikia vizuri.—Mk. 4:20.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki