Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/97 uku. 8
  • Fundisha Wengine Yale Ambayo Mungu Anataka

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Fundisha Wengine Yale Ambayo Mungu Anataka
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mtegemee Yehova Akuze Vitu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mwige Yehova kwa Kujali Wengine Kikweli
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Tangaza Habari Njema za Ufalme Ukitumia Broshua
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 4/97 uku. 8

Fundisha Wengine Yale Ambayo Mungu Anataka

1 Watu wengi ambao wamenyimwa kiroho “kuyasikia maneno ya BWANA” wanaweza kupatikana bado. (Amo. 8:11) Ingawa watu fulani wanaamini kwamba Mungu yuko, hawajui kusudi na matakwa yake. Hivyo, kuna uhitaji kwetu kuwafundisha kweli ya Ufalme yenye kuokoa uhai. Kwa kuandaliwa vifaa ifaavyo na kuwa tayari kutoa ushahidi katika kila fursa, twaweza kupata wale wanaotaka kujifunza yale ambayo Yehova anataka.

2 Wakati wa Aprili na Mei, tutakuwa na matoleo ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ya wakati ufaao ya kugawanya. Kwa kuongezea, kwa mara ya kwanza, tutatoa broshua Mungu Anataka Tufanye Nini? Picha zayo zenye kuvutia na maswali yenye kuamsha fikira yanaipa broshua hii uvutio mkubwa sana. Madokezo yafuatayo yanatolewa kutusaidia kutumia vichapo vyetu bora kabisa kwa matokeo.

3 Kutafuta Watu: Mahali ambapo watu wengi hawako nyumbani tunapoenda nyumba hadi nyumba, inanufaisha kutafuta na kuongea na watu popote wapatikanapo. Nyongeza ya Huduma ya Ufalme Yetu ya Septemba 1996 ilitutia moyo tuhubiri habari njema kila mahali—barabarani, kwenye magari ya umma, na katika bustani, kwenye maegesho ya magari, mashambani, na mahali pa biashara. Kuhusu kuhubiri katika ofisi, mwangalizi wa mzunguko mmoja aliandika hivi: “Ilisisimua kuona itikio chanya upande wa watangazaji. . . . Watu wanaofanya kazi kwenye ofisi walituonyesha hisani isiyotazamiwa na walitukaribisha kwa uchangamfu. . . . Wengi walionyesha uthamini kwa kuwa tulikuwa tunafanya jitihada ya ziada kuwafikia tukiwa na ujumbe wa Kibiblia hata katika ofisi yao.” Wewe umefurahia mafanikio gani kufikia sasa kwa kuhubiri habari njema kila mahali? Mnara wa Mlinzi na Amkeni! pamoja na broshua Anataka vinafaa hasa aina zote za utoaji wa ushahidi, kwa sababu vinatoa habari ambayo hugusa maisha ya watu na huchochea uwezo wa kufikiri.

4 Kuanzisha Mazungumzo: Ukurasa wa nyuma wa Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1996 yatoa mambo kuhusu jinsi ya kutayarisha utoaji wako mwenyewe wa magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Madokezo hayohayo yatakuwa yenye matokeo unapotayarisha utoaji wako wa broshua Anataka. Tunayosema yaweza kuwa mafupi kama vile sentensi chache au marefu vya kutosha kutia ndani wazo la Kimaandiko. Ni jambo la maana kuchagua maneno ya ufunguzi kwa uangalifu, kwa kuwa yataamua kama mtu unayemfikia ataendelea kusikiliza. Wengine wamefanikiwa kwa maelezo haya ya ufunguzi: “Nilisoma makala iliyonitia moyo, nami nataka kuishiriki pamoja nawe.” Au swali lenye kupendeza laweza kutokezwa ili kumvuta yule mtu mwingine kwenye mazungumzo.

5 Ikifaa katika eneo lenu, waweza kujaribu kuuliza maswali kama yafuatayo katika utoaji wako mwezi huu:

◼ “Leo twaona maandishi na michoro mingi kwenye kuta za umma, takataka, na uchafuzi. Kutahitajiwa nini kusafisha dunia na kuifanya iwe mahali bora pa kuishi?” Ruhusu itikio, kisha ueleze kwamba una habari ambayo yatuhakikishia jinsi na wakati dunia itakapokuwa bustani ya tufe lote. Shiriki maelezo hususa, andiko fupi, na picha yenye kupendeza kutoka gazeti la karibuni, kisha umpe mtu huyo alisome. Kabla hujamaliza mazungumzo, jaribu kupanga kuyaendeleza wakati mwingine.

◼ “Unafikiri Mungu alikusudia sisi tuishi tukizungukwa na taabu kama zile tunazokabili leo?” Baada ya mtu huyo kujibu, ungeweza kusema: “Yamkini unafahamu ile sala ambayo Yesu alifundisha wafuasi wake kuisali, wakiomba Ufalme wa Mungu uje. Je, umepata kufikiria Ufalme wa Mungu kwa kweli ni nini?” Fungua somo la 6 katika broshua Anataka, na usome maswali ambayo yako mwanzoni mwa hilo somo. Kisha, unaposoma fungu la 1, onyesha jibu kwa swali la kwanza. Elezea kwamba maswali yaliyobaki yanajibiwa kwa ufupi vivyo hivyo. Toa broshua hiyo, na ujitolee kukutana naye tena kushiriki habari zaidi kuhusu Ufalme.

◼ “Watu wengi wenye kufikiri wanaanza kuona dini za ulimwengu kuwa sababisho la matatizo ya wanadamu badala ya kuwa suluhisho. Wewe wafikirije kuhusu hilo?” Baada ya kusikiliza maoni ya mtu huyo, onyesha jambo fulani kutoka mojawapo magazeti ya karibuni liwezalo kunasa kupendezwa kwake juu ya kushindwa kwa dini isiyo ya kweli au kukaribia kwa kuangamia kwayo. Mwulize kama angependa kulisoma. Julishaneni majina, na ujitolee kuwasiliana naye tena ili uweze kueleza jinsi ambavyo dini ya kweli haikoseshi wanadamu.

◼ “Kukiwa na matatizo mengi sana katika maisha ya familia leo, je, umepata kujiuliza ni nini siri ya kupata furaha ya familia?” Ngoja itikio, ueleze kwamba katika Biblia, Mungu huonyesha wazi siri halisi ya kupata furaha ya familia. Labda ungeweza kusoma Isaya 48:17. Kisha fungua somo la 8 katika broshua Anataka, na uelekeze kwenye baadhi ya mistari ya Biblia iliyotajwa bila kunukuliwa ambayo huandaa mwongozo uwezao kutegemeka kwa kila mshiriki wa familia. Soma orodha ya maswali mwanzoni mwa somo. Uliza ikiwa mtu huyo angependa kusoma majibu. Ikiwa ndivyo, mtolee broshua kwa mchango wa kawaida. Jitolee kurudi wakati mwingine kushiriki mwongozo zaidi wenye kutumika ambao Biblia inao kwa maisha ya familia yenye furaha.

6 Nyongeza iliyo katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1997 ilitutia moyo tujipatie ujasiri wa kufanya ziara za kurudia. Ilipendekeza kutumia broshua Anataka ili kuanzisha mafunzo ya Biblia, ikiwa si katika ziara ya kwanza, basi kwenye ziara ya kurudia. Uhitaji mkubwa zaidi wa wanadamu ni kujifunza yale ambayo Mungu anataka kisha kuyatenda. (Kol. 1:9, 10) Tutanufaisha wengine sana wakati wa Aprili na Mei ikiwa twaweza kuanza kuwafundisha yale tunayojua kuhusu matakwa ya Yehova ya kufuatwa maishani.—1 Kor. 9:23.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki